Topic outline

  • SURA YA KWANZA : MADA KUU 1: LUGHA NA MAZINGIRA

    MADA KUU 1: LUGHA NA MAZINGIRA

    MADA NDOGO: Utalii nchini Rwanda

    1.1 Mazungumzo kati ya Mpokeaji na Mtalii

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi sahihi kwa

    kueleza kinachoendelea au mnachokiona katika mchoro huu.



    Maswali ya ufahamu

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, someni tena kifungu cha mazungumzo
    kilicho hapo juu kati ya Mtalii na Mpokeaji, kisha mjibu maswali haya.

    1. Mtalii anatoka katika nchi gani? Yeye anataka nini?
    2. Taja vivutio vya utalii vilivyopo nchini Rwanda.
    3. Mtalii atatembelea vivutio gani?
    4. Mtalii atachukua muda gani nchini Rwanda?
    5. Umuhimu wa mwelekezaji wa watalii ni upi?
    6. Watu huruhusiwa kuingia katika mbuga za wanyama kuanzia saa ngapi
    na hutoka saa ngapi?
    7. Mtalii atatumia nambari za simu alizopewa kufanya nini?
    8. Mtalii ataanza shughuli yake ya kuzuru maeneo mbalimbali lini?
    9. Mtalii atatumia nini kusafiri hadi kwenye mbuga za wanyama?

    10. Huduma za hoteli kwa Mtalii ni zipi? 

    1.2 Msamiati kuhusu utalii

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tafuteni msamiati mpya katika
    kifungu cha mazungumzo mlichosoma hapo juu kisha muutolee maelezo.
    Zingatieni matumizi ya msamiati huo katika kifungu hicho na mtumie kamusi

    pale panapohitajika. 

    Kwa mfano:

    mbuga – sehemu maalum ya kuwahifadhia wanyamapori

    Zoezi la 1.1

    A. Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, elezeni maana ya msamiati
    uliopigiwa mistari katika sentensi hizi kisha mtunge sentensi zenu sahihi
    kwa kutumia msamiati huo.

    1. Mtalii huyu kutoka nchi ya Ujerumani anataka kujua maeneo
    mazuri ya kuzuru nchini.
    2. Maeneo mengi ya nchi yetu yanavutia watalii wengi.
    3. Mtalii huyu anataka kuzuru wilaya ya Korongi ili aweze kutazama
    ziwa Kivu.
    4. Simba wengi waliletwa katika mbuga ya wanyama ya Akagera.
    5. Mbuga ya Wanyama ya Akagera ni kivutio muhimu cha utalii

    nchini Rwanda. 

    6. Mtalii huyu aliamua kufanya ziara ya kitalii ya siku tano nchini
    mwetu.
    7. Nchi yetu inatarajia kupokea watalii elfu themanini na watano
    mwaka huu.
    8. Mimi ninaona heri niondoke katika sehemu hii; sitaki wanyama
    wakali wanipate hapa.
    9. Unaweza kufanya ziara yako ya kitalii mjini Kigali kwa bei nafuu.

    10. Watalii hufurahia mazingira ya Akagera.

    B. Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi sahihi kwa

    kutumia maneno yaliyopigiwa mistari katika Zoezi la 1A

    1.3 Matumizi ya lugha: Aina mbalimbali za pesa

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni pesa zifuatazo kisha

    mziambatanishe kwa usahihi na nchi zinakotumika.




    Zoezi la 1.2

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, ambatanisheni aina za pesa

    zilizo katika sehemu A na nchi zinakotumika katika sehemu B kwa usahihi.

    Kwa mfano: Faranga - Rwanda


    Zoezi la 1.3

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, onyesheni aina za pesa ambazo

    hutumiwa katika nchi zifuatazo kwa kutunga sentensi sahihi. 

    Kwa mfano: Tanzania


    Zoezi la utafiti

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, badilisheni pesa za kigeni zifuatazo
    ziwe katika faranga za Rwanda kama ilivyo sasa hivi.

    Kwa mfano:
    Shilingi elfu moja za Kenya = Faranga elfu saba na mia tano za Rwanda
    1. Dola hamsini za Marekani
    2. Shilingi mia mbili za Uganda
    3. Shilingi hamsini za Tanzania
    4. Yuro tano za Ulaya
    5. Naira mia moja za Naijeria
    1.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo
    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, igizeni mazungumzo mliyosoma
    hapo awali kati ya Mtalii na Mpokeaji. 

    1.5 Sarufi: Viulizi ‘nani’ na ‘nini’

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, someni sentensi zifuatazo kisha

    mfanye mazoezi yanayofuata.


    1. Nani atamaliza wiki mbili nchini Rwanda?
     Jibu: Mtalii.
    2. Nini kinavutia katika mbuga ya Akagera?
    Jibu: Wanyamapori kwa mfano: simba.
    3. Nani alimpa mtalii maelezo kuhusu hoteli ya kuishi?
    Jibu: Mpokeaji wa watalii.
    4. Nani atarudi mwaka ujao kwa shughuli za utalii?
    Jibu: Mtalii.
    5. Ni nini mtalii atalipa ili kuzuru mbuga ya wanyama?
    Jibu: Pesa za kiingilio

    Zoezi la 1.4

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, ulizeni maswali mliyosoma hapo
    juu kwa kuanza na kiulizi ‘je’.

    Kwa mfano: 
    Je, ni nani atamaliza wiki mbili nchini Rwanda? 

    Zoezi la 1.5

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jazeni nafasi zilizoachwa wazi
    katika sentensi hizi kwa jibu sahihi kutoka kwenye mabano. 



    Maelezo muhimu!
    Maneno yaliyopigiwa mistari huitwa viulizi. Haya ni maneno
    ambayo hutumiwa kuulizia maswali. 
    Kwa mfano:

    i) Nani alikulipia karo ya muhula uliopita?
    Neno ‘nani’ linauliza kuhusu mtu aliyetenda kitendo cha kulipa
    karo. 
    ii) Nini kimekuhuzunisha?

    Neno ‘nini’ linauliza kuhusu kitu au jambo ambalo limemhuzunisha
    anayehusika.
    • Maneno ‘nani’ na ‘nini’ hayaongezewi viambishi ngeli vyovyote. 

    Zoezi la 1.6

    Tunga sentensi tano sahihi kwa kutumia kiulizi ‘nani’ na sentensi nyingine

    tano sahihi kwa kutumia kiulizi ‘nini’.


  • Somo la 2: Mbuga za wanyama

    2.1 Kifungu kuhusu mbuga za wanyama nchini Rwanda

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jadilini kuhusu mnachokiona
    katika picha hizi kisha, mjitokeze mbele ya wanafunzi wenzenu ili muwaeleze.
    Baadaye, msome kifungu kinachofuata cha habari kuhusu mbuga za wanyama
    zinazopatikana nchini Rwanda.




       

    Maswali ya ufahamu

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, someni tena kifungu cha habari
    kuhusu mbuga za wanyama kisha mjibu maswali yafuatayo.
    1. Nchi ya Rwanda inapatikana wapi?
    2. Je, ni vivutio gani vya utalii vinavyopatikana nchini Rwanda?
    3. Mbuga ya wanyama ya Akagera inahifadhi wanyama gani?
    4. Eleza sifa za mbuga ya Akagera.
    5. Mbuga ya wanyama ya milima mirefu inapatikana katika sehemu gani?
    Taja milima mirefu minne inayopatikana hapo.
    6. Mbuga hii inasifiwa kwa sababu ya kuwa na wanyama gani? Kwa nini
    wanyama hao wanapendwa sana na watalii?
    7. Je, ni sherehe gani inayofanywa kila mwaka kuhusiana na wanyama hao?
    8. Mbuga ya wanyama ya msitu wa Nyungwe inajulikana kwa sifa gani?
    9. Je, ni faida gani tunazopata kutokana na shughuli ya utalii?
    10. Ni mambo gani yanayostahili kukomeshwa ili utalii uweze kuendelea na
    kustawi? 

    2.2 Msamiati kuhusu mbuga za wanyama

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tafuteni msamiati mpya katika
    kifungu cha habari mlichosoma kisha mueleze maana ya msamiati huo.
    Zingatieni matumizi ya msamiati huo katika kifungu hicho na mtumie kamusi
    pale panapohitajika. 

    Kwa mfano:

    msitu – eneo kubwa lisilokuwa na watu lenye mimea mingi

    Zoezi la 2.1

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, husisheni kwa usahihi maneno
    yaliyoandikwa katika sehemu A na maelezo yake katika sehemu B. Zingatieni
    mfano uliotolewa.


    Zoezi la 2.2

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, husisheni kwa usahihi sentensi
    zilizo hapo chini na picha zifuatazo.



    1. Mlima huu ni mrefu kuliko milima mingine nchini Rwanda.
    2. Mnyama huyu ana pembe ndefu.
    3. Ziwa hili lina kisiwa kimoja kilicho na vibanda vingi.
    4. Pundamilia na nyati huishi katika msitu huu.
    5. Ziwa hili lina samaki wengi.

    2.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jaribuni kujadiliana kuhusu
    sifa za vivutio vya utalii mlivyojadili katika kifungu cha habari mlichosoma
    hapo awali. Tajeni vivutio ambavyo mngependa kutembelea huku mkitoa
    sababu za chaguo lenu. 

    2.3.1 Kuandika ufupisho/ Muhtasari

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, elezeni mambo muhimu
    yaliyozungumziwa katika kifungu cha habari mlichosoma. Msinakili sentensi
    zilizotumiwa katika kifungu hicho, jaribuni kutumia maneno yenu na kuunda
    sentensi zenu zilizofupishwa. Tumieni maneno yasiyozidi mia moja (100). 

    Maelezo muhimu

    Kabla ya kuandika ufupisho wenu ni vyema: 

    1. Kusoma kwa makini kifungu kilichopo na kuandika mawazo muhimu.
    Soma mara tatu ili kuelewa vizuri.
    2. Kujibu maswali haya:
    • Kifungu cha habari kinahusu nini? (Andika sentensi moja)
    • Kifungu hiki kina aya ngapi? (Tambua aya zinazojenga kifungu hiki).
    • Andikeni wazo moja kutoka kwa kila aya.
    3. Kuunganisha mawazo mliyoorodhesha na kuandika habari kamili. Ili
    mwandike vizuri ni vyema:
    • Kutumia maneno yenu wenyewe (msitumie maneno pamoja na sentensi
    zilizotumiwa katika kifungu cha habari mlichokisoma)
    • Kutoa maelezo bila kupotosha ujumbe asilia.
    • Kuhakikisha kuwa mmerejelea mawazo yote muhimu yanayopatikana
    katika kifungu cha habari mlichokisoma.
    • Kuhakikisha kuwa hakuna makosa ya kisarufi.
    • Kuhakikisha kwamba mmezingatia urefu unaofaa.
    • Kuzingatia matumizi ya alama za uandishi.
    Habari hiyo mliyoandika kwa kuzingatia maelekezo hayo hapo juu ni
    muhtasari au ufupisho wa habari asilia mliyosoma. Neno ‘ufupisho’
    linatokana na kitenzi ‘fupisha’ lenye maana ya ‘kufanya maelezo kuwa
    mafupi au kupunguza urefu wake’. 

    Mfano wa ufupisho wa kifungu kuhusu mbuga za
    wanyama


    Rwanda ni nchi iliyo na vivutio vingi vya kitalii kama vile: mito
    mbalimbali, mbuga za wanyama, misitu ya kiasili, hoteli nzuri, maziwa,
    milima mirefu pamoja na nyumba za kuhifadhia vifaa vya utamaduni wetu.
    Mbuga ya wanyama ya Akagera inapendwa na watu wengi. Mbuga hii ina
    wanyama kama vile: pundamilia, swara, paa, twiga, vifaru, tembo, simba
    pamoja na wanyama wengine. Pia, mbuga hii ina savana ya kupendeza.
    Mbuga ya wanyama ya milima mirefu ya Virunga huvutia kwa milima yake
    mirefu kama vile: Kalisimbi, Muhabura, Bisoke, Sabyinyo, Nyamuragira na
    Nyiragongo. Mbuga hii pia inajulikana kwa wanyama wanaoitwa ‘sokwe
    watu’.

    Mbuga ya msitu wa Nyungwe inafahamika kwa miti yake mirefu sana
    pamoja na ndege wa aina nyingi wasiopatikana kwingi ulimwenguni. Vivutio
    hivi vina manufaa mengi ya kiuchumi kwa Wanyarwanda. Ni lengo la kila
    Mnyarwanda kuhakikisha kuwa anatunza vivutio hivi ili utalii uendelee
    kutufaidi. (Maneno 140 )

    2.4 Kusikiliza na kuzungumza: Majadiliano

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jadilini kuhusu mbuga za wanyama
    zinazopatikana nchini Rwanda na kuyaandika maelezo yenu kwa ufupi halafu
    mjitokeze mbele ya wanafunzi wenzenu na kuwasomea kuhusu mbuga hizo

    pamoja na sifa zao.

    2.5 Sarufi: Kiulizi ‘lini’

    Jigaweni katika makundi ya wanafunzi wawili wawili ili mchunguze sentensi
    zifuatazo katika umoja na wingi kisha mfanye zoezi linalofuata.



    Zoezi la 2.3

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili:

    1. Jadilini aina ya neno lililopigiwa mstari katika sentensi mlizopewa.
    2. Jadilini mabadiliko ya sentensi hizo yanayojitokeza katika umoja na wingi.
    3. Tungeni sentensi tano sahihi kwa kutumia neno lililopigiwa mstari.

    Zoezi la 2.4

    Katika makundi yenu ya wanafunzi wawili wawili, jazeni nafasi zilizo wazi

    katika sentensi hizi kwa jibu sahihi kutoka kwenye mabano.

    Maelezo muhimu!

    Neno ‘lini’ ni kiulizi cha wakati. Hutumika katika sentensi kuulizia

    wakati wa kutendeka kwa kitendo fulani. 

    Kwa mfano: Utasafisha chumba cha mgonjwa lini?
    Jibu:      Kesho jioni.
    Jibu linalotolewa kwa sentensi iliyo na neno ‘lini’ linaonyesha majira
    mbalimbali ya wakati kama vile: majira ya siku (asubuhi, usiku, alasiri,
    mchana, jioni), saa, siku, wiki, mwezi, mwaka miongoni mwa nyakati

    nyingine.

    Zoezi la 2.5

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, andikeni sentensi hizi upya

    katika hali ya kuuliza kwa kufuata maagizo yaliyo kwenye mabano.

    Kwa mfano: Mgeni ataondoka kesho jioni. (Tumia: lini)
    Jibu: Mgeni ataondoka lini?
    1. Mtalii alizuru mbuga ya wanyama. (Tumia: Nani)
    2. Chakula hiki kitaliwa kesho. (Tumia: Nini)
    3. Watalii kutoka Marekani watafika kesho asubuhi. (Tumia: lini)
    4. Mwelekezaji atawapeleka watalii mjini Kigali. (Tumia: Nani)
    5. Kisu kitanunuliwa sokoni. (Tumia: Nini)

    Zoezi la 2.6

    A. Tunga sentensi tano sahihi kwa kutumia kiulizi ‘lini’.

    B. Andika sentensi ulizotunga katika sehemu A katika umoja au wingi.

  • SOMO LA 3: Mwelekezaji na Mtalii

    3.1 Mazungumzo kati ya Mwelekezaji na Mtalii
    Tazameni mchoro huu katika makundi ya wanafunzi watatu watatu kisha
    mwelezane mnachokiona.





    

    

    Maswali ya ufahamu

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, someni tena kifungu cha
    mazungumzo kati ya Mwelekezaji na Mtalii, kisha mjibu maswali haya.

    1. Kwa nini wanyama hufurahia kuishi katika mazingira ya mbuga ya
    Akagera?
    2. Taja vitu vilivyomfurahisha mgeni wa kitalii.
    3. Mgeni huyu alifika lini nchini Rwanda?
    4. Mgeni huyu wa kitalii atarudi nchini kwao lini?
    5. Ni wanyama gani wanaopatikana katika mbuga ya wanyama ya Akagera?
    6. Ndovu mwenye umri mrefu kuliko wengine ana sifa gani?
    7. Sungura hupenda nini?
    8. Ili sungura wasitoroke mwelekezaji alifanya nini?
    9. Ni wakati gani wanyama hujificha?

    10. Waharibifu wa mazingira hufanya nini?

    3.2 Msamiati kuhusu ziara ya kitalii

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tafuteni msamiati mpya kutoka
    katika kifungu cha mazungumzo mlichosoma hapo juu na kuueleza. Zingatieni
    matumizi ya msamiati huo katika kifungu hicho na mtumie kamusi pale

    inapohitajika. 

    Zoezi la 3.1

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, husisheni kwa usahihi msamiati

    katika sehemu A na maelezo yake katika sehemu B. Zingatieni mfano uliopo.

    Zoezi la 3.2

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, husisheni kwa usahihi michoro

    na picha hizi na sentensi zinazofuata. 


    1. Watalii wanawatazama wanyama katika mbuga ya Akagera.
    2. Mtoto wa simba anaitwa shibli.
    3. Msitu wa Virunga una miti mingi na sokwe wengi.
    4. Walinzi wa mbuga za wanyama wamewashika wasasi waliokuwa
    wakiwinda ndovu kwa ajili ya pembe zao.

    5. Wanafunzi walienda kuzuru mbuga ya Wanyama.

    3.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jadilini kuhusu wanyamapori
    ambao mmewahi kuwaona kwa kuelezana:
    1. Majina ya wanyamapori hao.
    2. Sifa za wanyamapori hao.
    3. Chakula cha wanyamapori hao.
    4. Maumbile ya wanyamapori hao.
    5. Uliwaona wanyama hao wapi?

    6. Wanyamapori hao wanapenda kuishi katika mazingira ya aina gani?

    A. Chunguza picha za wanyama hawa na kuzihusisha na majina yao sahihi


    B. Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, onyesheni wanyama ambao
    hufugwa na wanyamapori (wanyama wasiofugwa) kati ya wanyama walio

    hapo juu.

    3.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, igizeni mazungumzo mliyosoma

    kati ya Mwelekezaji na Mtalii wa kigeni. 

    3.5 Sarufi

    Viulizi ‘wapi’ na ‘vipi’
    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni sentensi zifuatazo kisha
    mjibu maswali haya.

    Sentensi 1: Kila siku tunapokea watalii wengi kutoka Marekani.
    Swali: Kila siku tunapokea watalii wengi kutoka wapi?
    Sentensi 2: Mgeni alihudumiwa vizuri.
    Swali: Mgeni alihudumiwa vipi?
    Sentensi 3: Mgeni alifurahishwa na huduma ya hoteli.
    Swali: Mgeni alifurahishwa na huduma ya wapi?
    Sentensi 4: Ndovu alionekana mpole.
    Swali: Ndovu alionekana vipi?

    Je, mmegundua nini?

    Zoezi la 3.4

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tungeni sentensi tano kama hizo
    zilizoandikwa hapo juu. Kutokana na sentensi utakazotunga, tunga maswali

    yake kwa kutumia neno ‘wapi’

    Maelezo muhimu!


    Zoezi la 3.5

    Tunga maswali kuhusu maneno yaliyopigiwa mstari katika sentensi hizi kwa

    kutumia viulizi sahihi.

    Kwa mfano:
                                       1. Mwanafunzi huyu anasomea Uchina

    Jibu:                        Mwanafunzi huyu anasomea wapi?

    2.Mwanafunzi   huyu anaandika vizuri

    Jibu:                         Mwanafunzi huyu anaandika vipi?

    1. Dereva huyu anatoka Afrika Kusini.
    2. Sembare anaingia chumbani mwake haraka.
    3. Gari la mtalii limesimama nje ya nyumba yetu.
    4. Simba anajificha vichakani.

    5. Ndugu yangu anatembea polepole

    Zoezi la 3.6

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tungeni sentensi tano katika

    umoja na wingi kwa kutumia viulizi ‘wapi’ na ‘vipi

    Zoezi la 3.7

    Jaza nafasi zilizoachwa wazi kwa kutumia jibu sahihi kutoka kwa yaliyo
    kwenye mabano.
    1. Kijana mmoja alienda _________ ? (nani, nini, wapi)
    2. Waziri ataondoka _________ ? (nani, vipi, nini)
    3. Mtumishi amepoteza ufagio wake ___________? (lini, nani, wapi)
    4. Fundi hodari amejenga nyumba __________? (nani, vipi, nini)

    5. Mwalimu wetu ameenda __________? (nani, nini, wapi) 

    3.5.1 Kiulizi ‘kwa nini’

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni sentensi zifuatazo.
    Sentensi 1: Mtalii atatembelea mbuga ya wanyama ili kuwaona
     wanyamapori.
    Swali: Kwa nini mtalii atatembelea mbuga ya wanyama?
    Sentensi 2: Mgeni alifurahi kwa sababu alipewa huduma nzuri.
    Swali: Kwa nini mgeni alifurahi? 

    Zoezi la 3.8

    1. Katika makundi ya wanafunzi wawili, tungeni sentensi mbili mbili kama
    hizo zilizoandikwa hapo juu. (Sentensi 1 na 2)
    2. Tunga maswali kwa sentensi mlizotunga katika swali la 1 hapo juu.
    (Hakikisha kuwa mmetumia kwa nini katika maswali yenu).
    
    Maelezo muhimu!
     Maneno ‘kwa nini’ yanatumiwa kuulizia sababu ya kufanyika
     kwa jambo fulani
    .
    Kwa mfano:
    Sentensi 1: Mwanafunzi huyu alipewa zawadi kwa sababu
                             anathamini mazingira yake.
    • Swali: Kwa nini mwanafunzi huyu alipewa zawadi?
    (Maneno ‘kwa nini’ yametumiwa kuulizia sababu ya kupewa zawadi

    kwa mwanafunzi huyu).

    Sentensi 2: Waelekezaji walipewa mafundisho ili wajue namna
     ya kuwapokea wageni.
    Swali: Kwa nini waelekezaji walipewa mafundisho?
    (Maneno ‘kwa nini’ yametumiwa kuulizia sababu ya waelekezaji
    kupewa mafundisho). Maneno ya kuulizia maswali huitwa viulizi.

    Zoezi la 3.9
    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, ulizeni maswali kuhusu maneno
    na vifungu vya maneno vilivyopigiwa mstari katika sentensi hizi.

    Kwa mfano: Mtalii huyu hupenda kuja Rwanda kwa sababu Rwanda

    ni nchi nzuri.

    Jibu: Kwa nini mtalii huyu hupenda kuja Rwanda

    1. Mtoto huyu analia kwa sababu anataka chakula.
    2. Mkulima huyu alichinja mbuzi mmoja kwa sababu ana wageni.
    3. Mukandori anakaa katika nyumba hii kwa sababu alihamishwa kikazi.
    4. Mtu huyu amepelekwa jela kwa sababu alihukumiwa kifungo cha miaka
    miwili.
    5. Mama na baba wamekaa sebuleni kwa sababu wanazungumza na
    wageni wetu. 
    
    
    
    

    

  • SOMO LA 4: Utamaduni na utalii

    4.1 Kifungu kuhusu utamaduni na utalii

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni picha hizi kisha mjadili

    kuhusu mnachokiona na kuwaelezea wenzenu.


    Soma kifungu cha habari kinachofuata kuhusu utamaduni na utalii kisha mjibu
    maswali yanayofuata. Kifungu hiki kinaeleza jinsi utamaduni unavyoweza

    kutumiwa katika utalii na kuleta manufaa kwa nchi.

    Maswali ya ufahamu

    I. Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, someni tena kifungu cha
    ufahamu kilichotangulia kisha mjibu maswali yafuatayo.
    1. Kwa nini watu wengi hawaelewi umuhimu wa utamaduni?
    2. Utamaduni unahusu nini?
    3. Ni mambo gani yanayofanywa ili kuhifadhi utamaduni wetu?
    4. Taja maeneo ambapo tunaweza kupata nyumba za kuhifadhia
    utamaduni wetu?
    5. Taja vitu tunavyoweza kupata katika nyumba ya kuhifadhi utamaduni
    wetu iliyoko wilayani Huye.
    6. Nyumba iliyoko wilayani Nyanza ilikuwa makazi ya nani?
    7. Ni vitu gani vya kuvutia ambavyo tunaweza kukuta katika nyumba
    hiyo?

    8. Kwa nini tunafaa kujivunia utamaduni wetu?

    II. Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, andikeni kwa ufupi kifungu

    cha habari mlichosoma hapo juu. Tumieni maneno sabini (70). 

    4.2 Msamiati kuhusu utamaduni

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tafuteni msamiati mpya kutoka
    katika kifungu cha habari mlichosoma kilichotangulia na kuueleza. Zingatieni
    matumizi ya msamiati huo katika kifungu hicho na mtumie kamusi pale

    panapohitajika. 

    Zoezi la 4.1

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, husisheni maneno yaliyoandikwa

    katika sehemu A na maelezo yake katika sehemu B. Zingatieni mfano uliopo.


    Zoezi la 4.2

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili,
    husisheni mchoro na picha hizi na sentensi zifuatazo kwa usahihi.


    1. Wageni hupokelewa katika sebule hii nzuri kwa mazungumzo.
    2. Mama yangu huvaa taji la kitamaduni katika sherehe za harusi.
    3. Babu anawasimulia wajukuu wake hadithi ya kusisimua.
    4. Huu ni mtindo tofauti wa kukata nywele unaoitwa ‘Amasunzu’.

    5. Haya ni makazi yetu. Tuna nyumba nzuri ya kisasa.

    4.3 Matumizi ya lugha: Zoezi la msamiati

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jazeni herufi zilizoachwa wazi

    katika visanduku vifuatavyo ili kuunda neno kamili. 


    4.4 Kusikiliza na kuzungumza: Majadiliano

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jadilini kuhusu utamaduni na
    utalii halafu mjitokezee mbele ya wanafunzi wenzenu kuwaeleza kuhusu yale
    mliyoafikiana. Jaribuni kuhakikisha kwamba mmejibu maswali haya katika
    majadiliano yenu:
    1. Utamaduni unahusu nini?
    2. Utamaduni wa Wanyarwanda unatambulishwa na nini?
    3. Utamaduni unaweza kuvutia watalii?
    4. Ni faida gani tunaweza kupata kutokana na utamaduni?
    5. Tunaweza kufanya nini ili kuhifadhi utamaduni wetu?

    6. Ni hasara gani tunaweza kupata iwapo hatutathamini utamaduni wetu?

    4.5 Sarufi: Wakati wa mazoea, tungo yakinishi

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, someni sentensi zinazofuata katika

    umoja na wingi kisha mfanye zoezi lililo hapo chini.


    Zoezi la 4.3

    1. Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tungeni sentensi moja moja
    kwa kutumia neno kila siku na kitenzi pika katika nafsi zifuatazo: mimi,
    wewe, yeye, sisi, nyinyi na wao.
    2. Linganisheni sentensi zenu na zile ulizotolewa hapo juu kuhusu kitenzi

    enda, chota na cheza.