Section outline

  • Mada Ndogo: Midahalo na mijadala kuhusu shughuli
    za maendeleo na uzalishajimali dhidi ya
    umaskini nchini 

    SOMO LA 10: Mdahalo

    10.1 Mdahalo kuhusu ‘Elimu ni muhimu kwa maendeleo ya
     wananchi kuliko biashara’

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni mchoro ufuatao kisha
    mjadili kuhusu kinachoendelea katika mchoro wenyewe. Baada ya kujadiliana,
    someni kifungu cha mdahalo kinachofuata kisha mjibu maswali yanayofuata.



     


    Maswali ya ufahamu

    1. Mada ya mdahalo iliyokuwa ikizungumziwa ilikuwa ipi?
    2. Eleza tofauti kati ya watetezi na wapinzani.
    3. Bigirimana alitoa hoja zipi?
    4. Mukamwiza alitoa hoja zipi?
    5. Mukandayisenga alitoa hoja gani?
    6. Eleza hoja ambazo Msikilizaji mshiriki 1 alitoa.
    7. Msikilizaji mshiriki 2 alitoa hoja zipi?
    8. Taja jina jingine la ‘mdahalo’.
    9. Mwenyekiti hufanya kazi gani katika shughuli za mdahalo?

    10.2 Msamiati kuhusu mdahalo

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tafuteni msamiati mpya kutoka
    katika kifungu cha mazungumzo yaliyotangulia na kuueleza. Zingatieni
    matumizi ya msamiati huo katika kifungu hicho na mtumie kamusi pale
    inapohitajika. 

    Zoezi la 10.1

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, elezeni maana ya msamiati
    uliopigiwa mistari katika sentensi zifuatazo kisha mtunge sentensi sahihi kwa
    kutumia msamiati huo.
    1. Alitupatia fursa ya kueleza shughuli za maendeleo ya kijiji chetu.
    2. Mukeshimana alitoa hoja nzuri katika mazungumzo yetu.
    3. Sisi tulitetea mawazo yake kwa sababu alisema ukweli.
    4. Mimi ninapinga mawazo ya watu wanaotaka kuendelea kuishi kwa
    kutegemea misaada tu.
    5. Nyirahabineza alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chama cha
    Wanafunzi wa Kiswahili nchini Rwanda (CHAWAKIRWA).
    6. Wageni hawa walikuja kuwekeza nchini mwetu na wanaendelea
    kupata faida nyingi.
    7. Mafunzo ya rafiki yangu yalichukua gharama kubwa.
    8. Matokeo ya mtihani wetu ni mazuri kwa sababu tumefaulu.
    9. Tujiepushe na ulevi kwa sababu ni kikwazo kwa maisha mazuri ya
    watu.
    10. Tulianzisha biashara ya kufuga kondoo na pato letu linaongezeka kila
    mwaka.

    Zoezi la 10.2

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, kamilisheni sentensi zifuatazo
    kwa kutumia maneno yafuatayo: walipiga makofi, maarifa, mshiriki,
    kutambua, itatunufaisha, anafananisha.

    Kwa mfano: Baada ya ____________ kuwa Bwiza hakufaulu katika
     somo la Kiswahili niliamua kumsaidia.
    Jibu: Baada ya kutambua kuwa Bwiza hakufaulu katika somo la
     Kiswahili niliamua kumsaidia.
    1. Watu hawa wana ___________ mbalimbali ya kutekeleza miradi.
    2. Washiriki wote wa mkutano ____________ baada ya kusikia hoja
    nzuri za Kayisabe na wenzake.
    3. Mwenyekiti wa mkutano wetu anasema kuwa kila _____________
    anapaswa kutoa hoja zake.
    4. Mtu huyu _______________ elimu na utajiri.
    5. Kazi hii ___________ wote kwa kutuwezesha kupata pesa za kujisaidia.

    Zoezi la 10.3

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, husisheni maneno yaliyoandikwa
    katika sehemu A na maelezo yake katika sehemu B.
    Kwa mfano: 1           C
     Sehemu A                                   Sehemu B
    1. mwenyekiti                                       A. mazungumzo kati ya watu wenye mitazamo
                                                                            tofauti
    2. mdahalo                                            B. jambo muhimu
    3. msingi                                                 CH. mtu aliyechaguliwa kuongoza mdahalo
    4. wanatatua                                        D. ufupisho
    5. muhtasari                                         E. wanaondoa tatizo

    10.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jadilini maswali yafuatayo na
    mwelezane kuhusu:
    1. Mdahalo ni nini?
    2. Toa mifano ya mada mbili zinazoweza kuzungumziwa katika mdahalo.
    3. Ni watu gani ambao hushirikishwa katika mdahalo?
    4. Watu hao huwa na mawazo au misimamo tofauti. Eleza misimamo hiyo.
    5. Taja tabia za kujiepusha katika mdahalo.

    Zoezi la 10.4

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jazeni herufi zilizoachwa ili
    kuunda neno kamili.

    Kwa mfano:


    Maelezo muhimu!
    Mazungumzo au majadiliano kati ya watu wengi ambao
    huzungumzia jambo moja maalumu na huwa na mitazamo tofauti
    huitwa mdahalo.
    • Mtazamo wa kwanza hutoa hoja zinazotetea au kuunga mkono
    wazo kuu.
    • Mtazamo wa pili hutoa hoja za kupinga au kukataa wazo kuu.
    Washiriki wa mdahalo ni:
    1. Mwenyekiti:
     Huongoza mazungumzo au majadiliano.
    Hupanga muda utakaotumiwa na kila msemaji kutoa hoja.
     Huchagua wasemaji katika mdahalo.
     Hupigisha kura baada ya mazungumzo ili kutaka kujua upande
    ulioshinda kati ya upande wa watetezi na ule wa wapinzani.

    2. Katibu:
    Huandika na kusoma hoja za wasemaji wote.
     Hutangaza matokeo ya kura zilizopigwa baada ya mazungumzo.
    3. Watetezi:
     Hawa ni wasemaji wanaotetea mada au wazo kuu linalozungumziwa.
    4. Wapinzani:
    Hawa ni wasemaji wanaopinga mawazo yanayotetea wazo kuu la
    mada.
    5. Wasikilizaji washiriki:
     Hawa wanashiriki kwa kusikiliza hoja za pande mbili: upande wa
    utetezi na upande wa upinzani.
    Baadhi ya tabia za kuepuka katika mdahalo ni: matumizi ya lugha
    yenye matusi na uchochezi, kutohifadhi wakati uliotengewa, kupandwa na
    hasira upande wako unaposhindwa, n.k.

    10.4 Kusikiliza na kuzungumza: Kuandaa mdahalo
    Katika makundi ya wanafunzi wanane wanane chagueni moja kati ya mada
    zifuatazo kisha mwandae mdahalo wenu.
    1. Elimu ndio msingi wa maisha mazuri.
    2. Wazazi wana nafasi kubwa katika malezi ya watoto wao kuliko walimu.
    3. Ni lazima viongozi wa kidini washirikiane na wanasiasa katika mipango
    ya maendeleo ya wananchi.
    4. Vitabu ndivyo vifaa muhimu katika elimu. 
    Katika maandalizi yenu, zingatieni mambo yafuatayo:

    • Jadilini maana ya msamiati uliotumiwa katika mada mlizopewa ili muweze
    kuelewa mada hizo.
    • Hakikisheni kuwa mnaelewa jambo muhimu linalozungumziwa katika
    kila mada.
    • Hakikisheni kuwa mmechagua mwenyekiti, katibu, wasikilizaji washiriki,
    watetezi na wapinzani.
    • Kila mzungumzaji aandae na kupanga hoja zake vizuri.
    • Kila mzungumzaji anapaswa kuwa na nidhamu kwa kuheshimu maelekezo
    ya mwenyekiti.

    10.5 Sarufi: Wakati uliotimilika, tungo yakinishi
    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zinazofuata
    katika umoja na wingi kisha mwelezane ugunduzi wenu na baadaye mjibu zoezi
    linalofuata.

    Je, mmegundua nini?

    Zoezi la 10.5

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi moja moja kwa
    kutumia kitenzi zungumza kwa kutumia kiambishi ‘me’ kama kilivyotumiwa
    katika tungo zenye kitenzi toa zilizo hapo juu. Tumia nafsi: mimi, wewe, yeye,

    sisi, nyinyi na wao.

    Kwa mfano:

    Mimi nimezungumza na mwalimu wangu.

    Sisi tumezungumza na walimu wetu.

    Maelezo muhimu!

    Kiambishi ‘me’ kinarudiwarudiwa katika vitenzi vyote baada
    ya viambishi nafsi ni, u, a, tu, m na wa. Kiambishi ‘me’ ni
    kiambishi cha wakati uliotimilika, tungo yakinishi.
    • Wakati uliotimilika huonyesha kuwa tendo tayari limefanyika na
    kumalizika.
    Kwa mfano:
    • Mimi nimefanya zoezi langu. (zoezi tayari limeshafanywa)
    • Kageruka ameondoka leo. (tendo la kuondoka tayari

    limeshamalizika)

    Matumizi ya wakati uliotimilika katika sentensi

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zifuatazo kwa

    kuziambatisha pamoja na michoro iliyopo. Elezaneni mlichogundua. 




    Zoezi la 10.6

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jazeni nafasi zilizoachwa wazi
    kwa kutumia kitenzi kinachofaa katika wakati uliotimilika, tungo yakinishi.
    Kwa mfano: Mwalimu ______ (kueleza) vizuri mambo yote muhimu.
    Jibu:                              Mwalimu ameeleza vizuri mambo yote muhimu.
    1. Sisi na viongozi wetu _________(kujadiliana) kuhusu umuhimu wa
    Kiswahili.
    2. Wewe ________ (kutazama) mchezo wa kandanda kwenye runinga.
    3. Mama yangu ________ (kuagiza) bidhaa nyingi kutoka Uchina.
    4. Mtetezi huyu na wasikilizaji washiriki wote_________(kuzungumzia)
    mambo muhimu.
    5. Mlango wa nyumba hii ________ (kufunguliwa) ili wageni wote
    waingie.
    6. Kisu changu _________ (kupotea).
    7. Nyumba zile _______ (kupakwa) rangi na mafundi wawili.
    8. Vitabu vingi vya Kiswahili ________ (kuchapishwa).
    9. Midahalo miwili _________ (kushirikisha) wasemaji wenye hoja nzuri.
    10. Mimi _________ (kuimba) wimbo wa kumsifu Mungu katika ibada
    yetu. 

    10.5.1 Wakati uliotimilika, tungo kanushi

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni sentensi zinazofuata
    katika umoja na wingi kisha mtunge sentensi zinazofanana nazo katika nafsi

    zote.

    

    Zoezi la 10.7

    a) Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tungeni sentensi moja
    moja kwa kutumia kitenzi imba katika wakati uliotimilika, hali
    yakinishi. Tumia nafsi: mimi, wewe, yeye, sisi, nyinyi na wao.

    b) Andikeni sentensi zenu katika hali kanushi. 

    Maelezo muhimu!

    • Kiambishi ‘me’ kimetumika kuonyesha wakati uliotimilika
    katika tungo yakinishi.
    • Katika wakati uliotimilika, kiambishi ‘ja’ kinatumiwa katika

    tungo kanushi badala ya kiambishi ‘me’ cha tungo yakinishi. 

    Zoezi la 10.8

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, andikeni sentensi hizi katika
    tungo kanushi.
    Kwa mfano: Wewe umeimba wimbo mzuri sana.
    Jibu:                                      Wewe hujaimba wimbo mzuri sana.
    1. Yeye ameagiza bidhaa nyingi kutoka Kigali.
    2. Mimi nimezunguka mjini kwa gari.
    3. Mtoto wangu amefaulu mitihani yake.
    4. Nyumba yangu imesafishwa.

    5. Mgomba umechomwa.

    Zoezi la 10.9

    Baada ya kukanusha tungo katika zoezi la 10.8, ziandike katika wingi.
    Kwa mfano: Wewe hujaimba wimbo mzuri sana. (umoja, tungo kanushi)
    Jibu:              Nyinyi hamjaimba nyimbo nzuri sana. (wingi, tungo kanushi)
     

    SOMO LA 11: Mjadala

    11.1 Mjadala kuhusu ‘Nafasi ya ukulima katika

     uzalishajimali dhidi ya umaskini’

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jadilini kuhusu kinachoendelea
    katika michoro ifuatayo kisha msome kifungu cha mjadala kinachofuata kuhusu
    nafasi ya kilimo katika shughuli za uzalishajimali dhidi ya umaskini na hapo
    baadaye mjibu maswali yanayofuata. 
     
                    

      


    Maswali ya ufahamu

    1. Mada ya mjadala ilikuwa ipi?
    2. Eleza tofauti kati ya ukulima na ufugaji.
    3. Tatizo linaloathiri kilimo kulingana na Kawera ni lipi?
    4. Serikali inashauriwa kufanya nini ili kusuluhisha matatizo ya kilimo?
    5. Bagirishya alitoa hoja gani?
    6. Mukandayisenga alitoa hoja gani?

    7. Eleza hitimisho ambalo Mwenyekiti alitoa.

    11.2 Msamiati kuhusu ukulima
    Jipangeni katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, kisha mtafute maana ya
    msamiati mpya katika kifungu cha mjadala kilichotangulia. Tafuteni maana ya
    msamiati huo kulingana na matumizi yake katika kifungu hicho. Tumieni kamusi

    pale inapohitajika. 

    Zoezi la 11.1

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zifuatazo
    kisha mtunge sentensi zenu kwa kutumia maneno yaliyopigiwa mistari.

    1. Taasisi ya kilimo imewaletea wakulima mbegu nzuri za mahindi.
    2. Nyanya na vitunguu vinanunuliwa kwa bei nafuu mjini Kigali.
    3. Ni lazima kila mkulima aache uvivu na kufanya kazi kwa bidii.
    4. Mtaalamu mmoja wa kilimo ameonyesha namna nzuri ya kupanda
    migomba.
    5. Mkulima huyu ana bidii sana katika shughuli zake.
    6. Watu hawa wanatimiza wajibu wao wa kufundisha wakulima.
    7. Wadau wote wa kilimo wamekutania mjini Kigali.
    8. Serikali ya Rwanda inatenga faranga nyingi za kuendesha sekta za

    kilimo na ufugaji.

    Zoezi la 11.2


    11.3 Matumizi ya lugha: Zoezi la jedwali

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jazeni nafasi hizi kwa kuzingatia

    majibu ya maelezo yaliyo hapo chini:


    Kwenda kulia
    1 Mazungumzo kati ya watu wenye mitazamo tofauti kuhusu mada maalumu
    6 Uchaguzi wa kupata mshindi
    8 Maombi yanayoelekezwa kwa Mungu
    9 Neno lionyeshalo kuwa hakuna kingine
    10 Maelezo ya kupinga au kuunga mkono
    11 Kitu kilichotengenezwa kwa ajili ya kukalia
    12 Kinachotokana na mmea
    14 Anakataa kuunga mkono

    16 Mazungumzo ya kujenga hoja yanayofanywa kwa ajili ya kufafanua jambo

    Kwenda chini

    2 Jambo linalozungumzwa au kujadiliwa
    3 Anaunga mkono
    4 Chombo cha mawasiliano
    5 Mtu anayeandika mawazo ya wasemaji na washiriki wengine katika
    mdahalo
    7 Kuwa kwa wingi
    13 Kitu anachopata mtu baada ya kazi

    15 Isipokuwa

    Maelezo muhimu!

    Mjadala ni mazungumzo kuhusu jambo maalum.
    • Watu wanaoshiriki katika mazungumzo haya hutoa hoja zao
    kuhusu jambo hilo.
    • Jambo ambalo linazungumziwa huhitaji kufafanuliwa na kutolewa
    maelezo.
    • Katika mjadala kila mtu aliye na hoja huonyesha kuwa anataka
    kusema na hupewa muda wake ili atoe hoja zake.
    • Msemaji anaweza kutetea au kupinga mawazo ya wengine.
    • Katika mjadala kuna kiongozi anayeongoza mazungumzo.
    • Kiongozi huchagua anayezungumza na kuongoza mazungumzo na
    kuhifadhi nidhamu.
    • Washiriki nao hutoa hoja zao kuhusu mada iliyotolewa mpaka
    wafikie uamuzi wao wa mwisho.

    • Hakuna kura zinazopigwa kama ilivyo katika mdahalo.

    11.4 Kusikiliza na kuzungumza: Kuandaa mjadala
    Katika makundi ya wanafunzi watano watano, chagueni moja kati ya mada
    zifuatazo na kuandaa mdahalo wenu.
    1. Umuhimu wa biashara katika uzalishajimali nchini Rwanda.
    2. Umuhimu wa uongozi bora katika uzalishajimali dhidi ya umaskini.
    3. Vikwazo vya kufanikisha kazi miongoni mwa vijana.
    4. Nafasi ya shule za ufundi katika maendeleo na uzalishajimali nchini
    Rwanda.

    11.5 Sarufi: Kauli asili na kauli taarifa

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni sentensi zifuatazo kisha

    mjibu maswali yaliyo hapo chini. 



        Je, mmegundua nini?

    Zoezi la makundi

    1. Linganisheni sentensi katika sehemu A na sentensi katika sehemu B kwa
    kuonyesha sifa zake.
    2. Tungeni sentensi mbili zenye sifa kama za sentensi za sehemu A na

    kuziandika kwa kuzingatia sifa za sentensi katika sehemu B. 

    Maelezo muhimu!

    Sentensi katika kundi A zinarudia maneno yaliyotamkwa na mtu bila
    kubadilisha chochote katika kauli yake.
    • Kauli hiyo imeandikwa kwa kutumia alama za usemi (“ ” ) na kuanza
    kwa herufi kubwa.
    Kwa mfano: Mwalimu alisema, “Mimi nitafundisha somo la Kiswahili.”
    • Sentensi katika kundi B zinalenga kutuambia maneno ambayo
    yalizungumzwa na mtu mwingine bila kuyarudia kama yalivyokuwa
    katika kauli yake ya kwanza.
    Kwa mfano: Mwalimu alisema kwamba yeye atafundisha somo la
     Kiswahili.
    • Sentensi katika kundi A zinaonyesha kauli ya mtu katika hali yake ya
    kwanza na kauli hiyo inaitwa kauli asili.
    • Sentensi katika kundi B zinatoa taarifa au habari ya kauli au maneno
    yaliyosemwa na mtu mwingine bila kuongeza wala kupunguza maana
    ya jambo aliloeleza. Kauli hiyo inaitwa kauli taarifa.
    • Katika kauli ya taarifa mambo haya huzingatiwa:
    Nafsi hubadilika
    Mimi hubadilika na kuwa yeye

    Sisi hubadilika na kuwa wao

    Zoezi la 11.3

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, badilisheni sentensi hizi za kauli
    asili ziwe katika kauli taarifa.
    Kwa mfano: Mkulima mmoja anasema, “Mimi nitapata mavuno mengi
     sana.”
    Jibu:                           Mkulima mmoja anasema kwamba yeye atapata mavuno
     mengi sana.
    1. Wazungumzaji hawa wanasema, “Sisi tunapenda kutoa maoni yetu.”
    2. “Kabera atajijengea nyumba nzuri.” Mwanafunzi mmoja anasema.
    3. “Mimi nitaingia darasani saa nane kamili.” Ndayisaba anasema.
    4. Wakulima wanasema, “Mvua itanyesha na mimea yetu itastawi.”
    5. Baba yangu anasema, “Ni lazima watoto wote wasome kwa bidii.”
    6. “Sisi tutasaidia wakulima wetu kupata mbegu nzuri.” Mkuu wa wilaya
     anasema.
    7. “Mimi ninahitaji dereva mwenye ujuzi.”Mkuu wa kiwanda hiki anasema.
    8. Mama yangu anasema, “Kisu changu kimepotea.”
    9. “Kitanda changu ni kizuri.” Mgeni mmoja anasema.
    10. “Mimi sikubaliani na mawazo ya mtetezi wa pili.” Mpinzani huyu

     anasema.

    Zoezi la 11.4

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, badilisheni sentensi hizi kutoka
    kauli taarifa na kuziweka katika kauli asili.
    Kwa mfano: Mama alisema kuwa alitaka kwenda sokoni.
    Jibu: “Ninataka kwenda sokoni.” Mama alisema.
    1. Baba aliniambia kuwa nikifika Kigali ninunue sare mpya.
    2. Kaka alisema kuwa hakutaka kwenda shambani.
    3. Mwalimu alisema aende hapo.
    4. Kalisa alisema kuwa yeye aliandika barua hiyo.
    5. Birasa alishangaa kuwa yeye hawezi kubeba mzigo huo.

    6. Mwalimu mkuu aliuliza sababu yake ya kulia.

    SOMO LA 12: Mjadala

    12.1 Mjadala kuhusu ‘Ufugaji kama njia ya kupigana na

     umaskini nchini’

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni na mjadili kuhusu
    kinachoendelea katika michoro hii kisha msome kifungu kilicho hapo chini na

    baadaye mjibu maswali ya ufahamu yanayofuata.




    Maswali ya ufahamu

    1. Mjadala uliosoma ulihusu nini?
    2. Bwana Niyibizi alitoa maoni gani kuhusiana na mada husika?
    3. Nyiraneza alichangia mjadala kwa hoja zipi?
    4. Muhirwa alitoa hoja zipi kuhusiana na umuhimu wa ufugaji?
    5. Eleza hoja alizotoa Bwana Rwambibi.

    6. Mwenyekiti alihitimisha vipi mjadala huu?

    12.2 Msamiati wa mjadala kuhusu ufugaji

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tafuteni msamiati mpya katika
    kifungu cha mazungumzo hapo juu na kuueleza. Zingatieni matumizi ya msamiati

    huo katika kifungu hicho na mtumie kamusi pale inapohitajika. 

    Zoezi la 12.1

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni sentensi zifuatazo
    kisha mtunge sentensi zenu kwa kutumia maneno yaliyopigiwa mistari.

    1. Watoto wanapenda kunywa maziwa ya ng’ombe.
    2. Ni lazima sisi tupambane na umaskini kwa kufanya kazi kwa bidii.
    3. Mtoto huyu ana shida ya kukosa karo ya shule.
    4. Mfugaji huyu ametenga mnyama huyu mgonjwa ili asiambukize
    wanyama wengine.
    5. Kiwanda hiki kitafanya kazi kubwa ya kutengeneza nguo nyingi.
    6. Si vizuri kupuuza ushauri wa viongozi wetu.
    7. Mzungumzaji huyu amegusia umuhimu wa mifugo nchini Rwanda.
    8. Eneo hili lina mazao mazuri kwa sababu lina rutuba nyingi.
    9. Viwanda vyetu vinahitaji malighafi nyingi kutokana na kilimo.

    10. Mazungumzo yetu yamefikia kikomo kwa sasa.

    Zoezi la 12.2

    Chagueni neno kati ya yafuatayo ili kukamilisha sentensi hizi kwa usahihi:
    mjadala, hoja, umoja, umaskini, mifugo, mbolea, maziwa
    Kwa mfano: Ng’ombe wanatupatia ______________ ya kuweka katika
     mimea yetu.
    Jibu: Ng’ombe wanatupatia mbolea ya kuweka katika mimea
     yetu.
    1. Wizi wa ___________ unaweza kuleta hasara kubwa kwa wafugaji na
    kuwarudisha katika hali ya ___________.
    2. Watu wengi wanapenda kunywa ________ ili kupambana na magonjwa
    mbalimbali.
    3. Wafugaji hawa wamejiunga katika shirika kubwa kwa sababu wanajua
    kwamba _________ ni nguvu.
    4. __________ wetu umetufurahisha sana kwa sababu washiriki wote

    walitoa ________ nzuri. 

    12.3 Matumizi ya lugha: Kuunda maneno kamili

    Katika makundi ya mawafunzi wawili wawili, jaribuni kupanga sehemu za
    maneno zifuatazo ili kuunda maneno kamili.
    Kwa mfano: zi-te-m-te
    Jibu: mtetezi
    1. da-m-lo-ha
    2. ki-mwe-ti-nye
    3. zu-m-ngu-ji-za-m
    4. pi-u-ni-nza
    5. ja-la-da-m
    6. li-u-sha-ji-za li-ma
    7. fu-ji-u-ga
    8. ku-m-li-ma
    9. o-ma-ni

    10. li-ki-mo

    Zoezi la 12.3

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jaribuni kupanga maneno
    yafuatayo ili kuunda sentensi kamili na sahihi.
    1. kazi lazima zinakwamisha za uvivu na ulevi tabia kwa sababu ni na
    kujiepusha mbaya.
    2. ya na kazi ufugaji za kilimo zinaweza raia kupigana wengi kuwasaidia
    umaskini dhidi.
    3. waweze bidii kazi mazuri kwa wafanya ni lazima watu ili kuwa maisha
    na wote.
    4. hushiriki katika na wengi kwa mjadala zao kutoa mdahalo watu hoja.
    5. namna kuhusu sisi maendeleo kazi umuhimu na miradi wa tunajadiliana

    ya kuanzisha ya

    12.4 Kusikiliza na kuzungumza: Kuandaa mjadala

    Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watano watano kisha mwandae mjadala
    kuhusu mojawapo ya mada zifuatazo:
    1. Kazi muhimu za kuleta maendeleo kwa wananchi

    2. Tabia za kujiepusha ili kufanikisha kazi. 

    12.5 Sarufi: Mabadiliko ya kauli asili na kauli taarifa

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni kwa makini sentensi

    zifuatazo ili muweze kujibu maswali yaliyo hapo chini: 


    Zoezi la 12.4

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jibuni maswali yafuatayo:
    1. Linganisha sentensi katika A na sentensi katika B kwa kuonyesha sifa
    zake.
    2. Tunga sentensi sita kwa kuzingatia sentensi katika A na kuziandika

    tena kwa kuzingatia sifa za sentensi katika B.

    Maelezo muhimu!

    Sentensi katika A ni za kauli asili na sentensi katika B zimeandikwa
    katika kauli taarifa.
    • Kutokana na kitenzi sema au uliza katika wakati uliopita, sentensi za
    kauli asili zimetanguliwa na kitenzi ‘alisema’ au ‘aliuliza’.
    Kwa mfano:
    • Wafanyakazi walisema, “Leo tunafurahia matunda ya kazi yetu.”
    • Dereva aliuliza, “Nani anataka kufika mjini Kigali?”
    • Mwanafunzi mmoja aliuliza, “Mdahalo utafanyiwa wapi?”
    • Alama ya kuuliza (?) na alama za kufunga na kufungua (“ ”) huwa
    hazitumiwi katika kauli taarifa.
    Kwa mfano: Dereva aliuliza mtu ambaye alitaka kufika mjini Kigali.
    • Mambo yafuatayo hubadilika wakati wa kugeuza sentensi za kauli asili
    na kuziandika katika kauli taarifa: 


    Zoezi la 12.5

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, badilisheni sentensi zifuatazo
    ziwe katika kauli taarifa.
    Kwa mfano: Wanafunzi wote walisema, “Sisi tunatakiwa kufaulu katika
     mitihani yote ya muhula huu.”
    Jibu:                          Wanafunzi wote walisema kwamba wao walitakiwa kufaulu
     katika mitihani yote ya muhula huo.
    1. Seremala mmoja alisema, “Mimi ninaunda vitanda vikubwa.”
    2. Mfugaji alisema, “Wanyama wetu wanakosa maji.”
    3. Mwalimu alisema, “Wanafunzi hawa wanaenda kucheza.”
    4. Mtoto wake alisema, “Mimi nitaenda kuchota maji pamoja na ndugu
    yangu.”

    5. Bwana yule aliuliza, “Unataka nini hapa?” 

    Tathmini ya mada ya 3

     Zoezi la 1

    1. Katika makundi ya wanafunzi watano watano, andaeni mdahalo kuhusu:
     ‘Shule za umma ni bora kuliko shule za kibinafsi’.
    2. Katika makundi yenu, jadilini kuhusu majukumu ya wahusika hawa wa
     mdahalo:
    a) Mwenyekiti                            b) Katibu                                       ch) Wapinzani                    d) Watetezi
    Zoezi la 2
    Katika makundi ya wanafunzi watano watano, andaeni mjadala kuhusu:

     ‘Athari za mavazi ya kisasa kwa wanajamii’.

    Zoezi la 3

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, andikeni sentensi hizi katika
    tungo kanushi.
    Kwa mfano: Wewe umeimba wimbo mzuri sana
    Jibu:                             Wewe hujaimba wimbo mzuri sana
    1. Yeye ameagiza bidhaa nyingi kutoka Kigali.
    2. Mimi nimezunguka mjini kwa gari.
    3. Mtoto wangu amefaulu mitihani yake
    4. Nyumba yangu imesafishwa.
    5. Mgomba umechomwa.
    6. Kazi hii imefanywa vizuri.
    7. Kitabu chako kimeharibika.
    8. Utambi umekauka.
    9. Udevu mrefu umenyolewa.

    10. Barua imetumwa.

    Zoezi la 4

    Baada ya kukanusha sentensi zilizo katika zoezi la 3 lililo hapo juu, ziandike
    tena katika wingi.
    Kwa mfano:                                    Wewe hujaimba wimbo mzuri sana (umoja, tungo kanushi)
    Jibu: Nyinyi hamjaimba (wingi, tungo kanushi)

    Zoezi la 5

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, andikeni sentensi hizi katika
    wingi.
    Kwa mfano: Kisu kimeibiwa
    Jibu:                     Visu vimeibiwa.
    1. Kiti kimevunjika
    2. Mtu huyu ametuimbia vizuri.
    3. Mzee huyu amelewa.
    4. Mwanafunzi huyu ameelewa somo la Kiswahili.
    5. Ng’ombe wangu amezaa leo.
    6. Mto huu umefurika.
    7. Kiongozi amewasili mapema.
    8. Mbwa amekula chakula.
    9. Uso wake umeharibika.
    10. Mguu wangu umetibiwa vizuri.

    Zoezi la 6

    Baada ya kuandika wingi wa sentensi katika zoezi la 3 lililo hapo juu, ziandike
    upya katika tungo kanushi.
    Kwa mfano: Visu vimeibiwa. (wingi, tungo yakinishi)
    Jibu:                 Visu havijaibiwa. (wingi, tungo kanushi)

    Zoezi la 7
    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, kamilisheni sentensi zifuatazo
    kwa kutumia maneno yafuatayo:
    walipiga kura, wanatushawishi, uchumi, dhahiri, kuinua
    1. Kila mwananchi anapaswa kufanya kazi kwa bidii ili _______ kiwango
    cha maisha yake.
    2. _______________ wa nchi yetu utastawi baada ya kuanzisha miradi
    mingi mizuri.
    3. Viongozi hawa __________ kutumia mbinu za kisasa katika shughuli
    zetu za kilimo na ufugaji.
    4. Ni ________ kwamba raia wa Rwanda walipata maisha mazuri baada
    ya kuanzishwa kwa shughuli za ‘Gira inka Munyarwanda’.
    5. Juzi wanafunzi wote __________ kwa sababu Mkuu wa shule alitaka
    orodha ya viongozi wa madarasa yote. 
    

    Zoezi la 9

    Katika makundi yenu, badilisheni sentensi hizi ziwe katika kauli taarifa.
    1. Rais alisema, “Kila mwananchi anaweza kujitajirisha kwa kufanya kazi
    kwa bidii.”
    2. Mkuu wa shule alisema, “Wanafunzi wawili hawajui kusoma vizuri.”
    3. Wafanyakazi walisema, “Hatutaki kufanya kazi na watu wavivu.”
    4. Wazazi waliuliza, “Nani anaenda kununua mavazi ya watoto wetu?”

    5. Mkulima alisema, “Mvua hainyeshi sana siku hizi.”

    Zoezi la 10

    Katika makundi yenu, badilisheni sentensi hizi ziwe katika kauli asili.
    1. Kalisa alimwambia shangazi yake kuwa kesho yake angeenda Kigali.
    2. Bagirishya alisema huku akitetemeka kuwa chumbani mwake
    mlikuwa na nyoka.
    3. Kasisi alituambia kuwa ikiwa tungependa kuendelea vyema
    maishani, ingebidi tuwe na heshima.
    4. Daktari alituambia kuwa UKIMWI ni ugonjwa hatari sana.

    5. Baba aliniuliza idadi ya mabao tuliyofungwa mchezoni.