• Faharasa

    adimika           – kosa kupatikana kwa urahisi
    ambukiza        – enezea ugonjwa
    andaa          - tayarisha
    ankra           – orodha ya vitu vilivyouzwa pamoja na bei ya kila bidhaa
    anuani         – maelezo ya mahali mtu anapoishi ambayo huandikwa katika barua
    asali            – namna ya kitu kioevu na kitamu sana kitengenezwacho na nyuki
    azma          – lengo au shabaha
    bainisha     – tambua jambo
    bao            – mpira kuingia katika lango katika mchezo wa kandanda (goli)
    baridi kali  – hali isiyokuwa na joto na isisimuayo sana mwili
    bei            – kiasi cha pesa kinachotumiwa kununulia ama kuuzia bidhaa fulani
    burudani  - starehe
    burudisha – sababishia raha
    chai          – zao la mchai
    dumisha   – endeleza
    faranga    – pesa, fedha, dirhamu, senti, fulusi
    filisika      – ishiwa na mali
    fyeka       – kata nyasi
    gharamia – lipia gharama
    harage/haragwe– nafaka ya jamii ya kunde
    haramu     – -siyoruhusiwa, -siyokuwa halali
    Hisabati    – sayansi ya tarakimu ijumuishayo aljebra
    hitaji         – kuwa na haja ya kitu
    huzuni     – hisia za majonzi
    ibuka       – tokeza
    idadi        – hesabu au jumla ya vitu
    ilani         – tangazo la kuonya watu wasifanye jambo fulani hasa lenye
                       kuleta madhara
    ingawa    – hata ikiwa
    jadhba/jazba – hisia isababishayo kujisahau
    jamii       – watu wanaoishi pamoja
    jangili    – mwindaji haramu
    jedwali  – orodha ya maelezo kuhusu mambo fulani kwa namna
                      yatakavyofuatana
    jibini      – chakula kinachotengezwa kwa kuyagandisha maziwa na kuyatoa
                      maji
    jukumu  – wajibujumuiya– mkusanyiko wa watu
    kabuti    – koti zito la kuzuia baridi
    kagua    – chunguza kwa makini
    kahawa  – zao la mkahawa ama mbuni
    kandanda – mchezo wa miguu
    kauli         – usemi
    kiasili       – kienyeji
    kifaa        – chombo
    kikao       – mkutano
    kipindi     – muda
    kipusa    – pembe ndogo ya kifalu
    kivuna nafaka – mashine kama trekta ambayo huvuna ngano huku
                                ikiitoa wishwa
    kiwanda – mahali panapotengenezwa bidhaa
    kodi ya mapato – fedha zinazolipwa serikali kama ushuru wa mapato ya mtu
    kupanda– tia mbegu mchangani ili ziote
    limbikiza – weka vitu kidogo kidogo ili viwe vingi
    lishe bora – chakula kinachohitajika kwa afya nzuri ya mwili
    maabara – mahali mnamofanyiwa majaribio ya kisayansi
    maalumu – -enye sifa ya kipekee
    mada– kiini cha jambo linalozungumziwa
    majira– wakati au kipindi
    majira ya kiangazi – kipindi cha kiangazi
    majira ya kipupwe – kipindi cha baridi
    majira ya mvua– kipindi cha mvua
    majira ya vuli– kipindi cha mvua chache
    majivuno – hali ya kujiona
    manufaa  – faida
    mapato    – kitu kinachopatikana kama vile baada ya kufanya kilimo ama
                        kufanya biashara.
    masuala mtambuka – mambo muhimu yanayoiathiri jamii katika kipindi cha
                                         sasa
    matini          – kifungu cha habari iliyoandikwa
    mazingira    – mambo yanayotuzunguka mahali tunapoishi
    maziwa        – kitu kioevu kitokacho ndani ya titi la mnyama
    mbatata       – namna ya viazi vilivyo mviringo na visivyo na ladha
    mbinu          – njia au namna ya kufanyia jambo
    mbuga        – eneo lililotengewa wanyama wa porini
    mchele       – mpunga uliokobolewa,yaani kuondolewa mashuke
    mfawidhi    – mtu aliyepewa wajibu wa kuendesha shughuli fulani, kama vile
                           mkutano au sherehe fulani
    mfugaji tajiri – mfugaji ambaye ana mali nyingi
    mifugo          – wanyama wanaotunzwa nyumbani
    mikahawa     – mimea izaayo kahawa
    mkulima tajiri – mkulima ambaye ana mali nyingi
    mmomonyoko – kuchukuliwa kwa udongo wenye rutuba
    mori          – hasira kali
    mshinde   – aliyeshindwa
    mshindi    – aliyeshinda
    msimu      – majira
    mtama      – zao la mtama
    muhogo   – mzizi wa muhogo unapokuwa umekomaa tayari kwa kuliwa
    ndama     – mtoto wa ng’ombe
    ndizi        – tunda la mgomba linalomea kwenye mkungu.
    ngeli       – kikundi cha majina au nomino zinazofuata kanuni sawa za kisarufi
    njugu      – mbegu zitengenezewazo mafuta ya karanga
    nyama    – sehemu laini ya mwili ambayo ikikatwa hutoka damu
    pandwa  – ingiwa na
    pekee     – pweke; bila ya -ingine
    pesa       – noti na sarafu zinazotolewa na kuidhinishwa na serikali kuwa ni
                      fedha rasmi za kubadilishana na bidhaa.
    pori        – mahali palipo na miti mingi, nyasi na vichaka
    ratiba     – mpango wa mfululizo wa shughuli fulani
    refa        – mwamuzi katika mchezo wa mpira
    rejesta   – lugha inayotumiwa katika mahali maalum, kama vile hospitalini, hotelini, msikitini na kwingineko
    rutuba   – mbolea ya kukuzia mimea ardhini
    sajili      – rejesta
    shabiki  – apendaye sana timu
    sheria    – kanuni za kuongoza watu
    shime   – neno la kuhimizia mtu
    shiriki  – husika au kuungana na watu katika kufanya shughuli fulani
    soseji   – namna ya chakula kinachotengenezwa kutoka kwa nyama ya
                     nguruwe au ya ng’ombe
    suala       – jambo au hoja
    sufu        – manyoya ya kondoo
    takwimu – nambari zinazoeleza ukweli kuhusu matukio ya mambo, kwa
                       mfano idadi ya watu katika eneo fulani
    tambua   – fahamu au maizi
    tanbihi    – maelezo yanayotoa habari muhimu
    tathmini – pima
    tegemea– weka matumaini kupata kitu
    tia mdomoni– kumsema ama kumsengenya mtu
    ulinzi          – ulindaji, hali ya kulinda
    upanzi        – upandaji (uwekaji mbegu ardhini)
    utafiti          – uchunguzi wa kisayansi
    vanila          – kiungo kiyafanyayo maziwa yaliyoganda kuwa na ladha ya
                            kupendeza
    viazi vitamu– namna ya viazi vikubwa na vilivyo vitamu
    wadau          – mtu mwenye maslahi katika shughuli fulani
    wadhifa        – madaraka au cheo fulani
    waligonga ndipo – walisema ukweli
    wasifukazi     – maandishi yanayoeleza kuhitimu kwa mtu katika
                             kutekeleza kazi fulani, aghalabu, kimasomo, tajiriba ya kazi
                             na ujuzi wake
    wishwa        – takataka za nafaka kama vile mtama au ngano
    yakinishi     – hali ya kukubali
    zao               – kile kinachozaliwa na mmea
    zaraa           – kilimo
    Sura 4: Mazungumzo na mawasiliano katika shughuli mbalimbali za kijamii Vitabu vya rejea