Topic outline

  • General

  • Sura 1:Mazungumzo na majadiliano


    Mada ndogo: Msamiati na mawasiliano katika shughuli za kilimo na ufugaji


    A . Msamiati wa msingi kuhusu mazao na shughuli za kilimo na ufugaji nchini Rwanda.
    i) Msamiati wa mazao nchini Rwanda
    Tazama mazao yafuatayo na usome maneno chini yake.

    Bidhaa zilizopo kwenye michoro zinaitwa mazao. Mazao ni vitu tunavyovuna
    baada ya kupanda mbegu zake.Ni vitu vinavyozaliwa na mimea iliyopandwa. Hapa
    nchini Rwanda, udongo wetu ungali na rutuba ya kutoa mazao mema. Tunapanda
    mimea mbalimbali inayotupatia mazao.

    Tazama mifano zaidi ya mazao yanayopatikana hapa nchini Rwanda na
    usome vifungu kando yake.                                



                                 Kahawa ni zao la mkahawa au mbuni. Kahawa
                                hukaushwa na kusagwa ili kutoa ungaunga.
                                Ungaunga huo hutumiwa kwa kutengenezea
                                kinywaji cha kahawa. Kinywaji cha kahawa
                                kina ladha nzuri. Kahawa pia huuzwa katika
                                nchi za nje na kuletea nchi yetu pesa za kigeni.










                                                                                                                      
      Haya ni
      majani ya mchai. Majani ya mchai hukaushwa
      na kusagwa. Majani haya hutumiwa kutengenezea
      kinywaji cha chai. Nchi yetu huuza majani ya
      mchai katika nchi za kigeni. Majani ya mchai
      pia huletea nchi yetu pesa za kigeni.
                                                                                                   






             
      

                                                                                         
                                                                                                Hizi ni ndizi. Ndizi 
                                                                                                ni zao la mgomba.  
                                                                                                Ndizi humea kwenye      
                                                                                                mkungu. Ndizi
                                        inaweza kuivishwa na kuliwa moja kwa moja. Baadhi ya
                                       ndizi hupikwa na kuliwa.Ndizi pia huuzwa na kutuletea
                                       mapato.





                                                                     

    Haya ni maharagwe. Maharagwe ni zao la mharagwe.
    Nafaka hii ni muhimu sana kwa chakula chetu. Hii ni
    kwa kuwa virutubishi vyake vya protini huhitajika sana
    miilini mwetu. Wale ambao hawali nyama mara kwa mara
    huweza kupanda miharagwe na kupata protini zao kutoka
    kwayo.





             



    Huu ni mtama. Mtama huzaa punje ndogo ndogo. Punje  
    za mtama hukaushwa na kuchanganywa na mihogo au mahindi. Baadaye husagwa ili kupata unga. Unga huu hutengenezewa  uji au sima (ugali).




                                                                
                
    Haya ni mahindi.Mahindi ni mazao
    ya mhindi. Mahindi hukaushwa na
    kusagwa ili kutoa unga wa dona.
    Unga wa mahindi hutengenezewa
    sima au ugali.Mahindi pia yanaweza kupikwa pamoja na
    maharagwe kutengenezea pure au kande. Pure ni chakula kitamu kinachoshibisha vilivyo. Ama hindi linaweza kuchomwa au kuchemshwa na likawa chakula kwetu. Mafuta ya mahindi hutumiwa kutengenezea mafuta ya kupikia. Mbali na mahindi, njugu pia hutengenezewa mafuta ya kupaka kwenye mkate. Njugu ni zao la karanga. Njugu hukaangwa na kuliwa. Baadhi ya watu hutwanga njugu na kutengeneza borohoa ya kuungia kitoweo.


                
                              Haya ni mananasi. Nanasi ni zao la mnanasi.   
                              Nanasi huivishwa na kuliwa.
                              Nanasi hutoa maji matamu yanayomaliza kiu.
                              Maji hayo hutumiwa kutengenezea sharubati au soda.



                                                                                                         
                                   Hii ni mihogo. Muhogo ni mzizi wa muhogo.
                                   Muhogo huweza kuchemshwa au kukaangwa na kuliwa.
                                   Muhogo pia huweza kukaushwa, ukasagwa na kutengenezewa
                                   sima.


                                                                                       
                       

                                                                                                      Hizi ni mbatata. Mbatata  
                                                        ni viazi vya mviringo. Viazi hivi havina sukari. Mbatata
                                                        huweza kupikwa kama kiungo. Pia, huchemshwa na
                                                        kuliwa na vinywaji au vyakula vinginevyo. Mbatata pia
                                                        hukatwakatwa kwa vipande vyembamba na kutiwa ndani           
                                                        ya mafuta ili kutengenezea vibanzi au chipsi.




    Hivi ni viazi vitamu. Viazi hivi hupandwa katika matuta au sesa.
    Viazi vitamu huchemshwa na kunywewa kwa chai au kahawa.
    Viazi vitamu huwa na sukari kiasi cha haja.





    Zoezi

    1. Angalia maana ya maneno yaliyokolezwa kwa wino katika kamusi.
       Tunga sentensi sahihi kwa kila neno.
    2. Taja mazao zaidi yanayopatikana nchini Rwanda lakini hayajatajwa katika kifungu.
         Je, mazao hayo yana faida gani?
    3. Tunga sentensi sahihi ukitumia maneno yafuatayo:
        a) ndizi           b) mahindi           c) kahawa 
        d) mbatata     e) maharagwe     f ) chai
    4. Taja majina ya mazao haya na faida zake.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Jadilianeni kuhusu majina na faida ya mazao mbalimbali katika maeneo mnakoishi

    Kazi ya kikundi
    Katika vikundi, kila mwanafunzi ataje mazao yasiyopatikana katika eneo anamoishi.
    Jadilianeni kuhusu faida za mazao mliyoyataja.

    ii) Msamiati kuhusu shughuli za kilimo nchini Rwanda
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Jadilianeni kuhusu shughuli mbalimbali za kilimo kwenye michoro.
    Mfano
                   

    Soma kifungu kilichopo hapa chini na ujibu maswali chini yake.
    HABIMANA:  Habari za asubuhi wenzangu?
    KAREKEZI
    na ITUZE:       Nzuri sana Habimana.
    HABIMANA:   Wenzangu, naomba mnieleze maana ya kilimo.
    KAREKEZI:    Kilimo au zaraa ni kazi ya kulima shamba na kukuza mimea hadi
                            kufikia kiwango cha kuvunwa.
    HABIMANA:   Wenzangu, naomba mnitajie shughuli hizi za kilimo.
    KAREKEZI:    Kwanza, kuna kufyeka. Sisi hufyeka shamba letu kwa kutumia
                            upanga na fyekeo. Baadaye, kuna kulima shamba ili kuandaa konde.
                            Katika kijiji chetu, tunatumia jembe la mkono kuandalia konde.
    HABIMANA:   Kwa nini mnatumia jembe la mkono?
    KAREKEZI:    Kwa sababu mashamba katika kijiji chetu ni madogomadogo.
                            Vilevile, wakulima katika kijiji chetu hawawezi kumudu mbinu
                            nyinginezo za kulima. Je, Ituze, wakulima katika eneo lenu
                            hutumia mbinu zipi kuandaa mashamba yao?
    ITUZE:            Wakulima katika eneo letu hutumia plau inayovutwa na ng’ombe au punda.
                            Wakulima katika eneo jirani nao hutumia plau inayovutwa na trekta. Wakulima
                            hao wanamiliki mashamba makubwa. Pia wanaweza kulipia gharama za trekta.
                            Karekezi, hebu tueleze namna nyingine ya ukulima katika eneo lenu.
    KAREKEZI:    Sisi hulima sesa. Tunapojiandaa kupanda mbegu, huchanganya mbolea ya samadi
                            na udongo. Udongo wetu hauna rutuba ya kutosha. Baada ya kuweka mbolea,
                            tunapanda mbegu za mahindi na maharagwe ndani ya udongo na kuzifukia.
                            Mbegu zinapoota, tunapalilia miche ili kuondoa magugu au kwekwe. Baadhi ya
                            wakulima huweza kupiga dawa za kuwaua wadudu waharibifu.Wakati wa kiangazi,
                            kuna kunyunyizia mimea maji. Baada ya mimea kukua na kukomaa, tunavuna. Viazi
                            na mihogo yetu ndiyo hutuletea pesa za matumizi nyumbani kwetu. Tunakula baadhi
                            ya mazao hayo na kuyauza mengine.
    HABIMANA:   Kumbe kazi hii ya kilimo ni nzuri mno! Nilisoma juzi kuwa nchi yetu hupata pesa
                            za kigeni kwa kuuza chai na kahawa katika nchi za kigeni.
    ITUZE:            Kweli kabisa. Uchumi wa Rwanda umeimarika kwa sababu ya kilimo.
                            Maisha ya wakulima wengi yameimarika pia. Watu wengi
                            wameajiriwa kutokana na kilimo.
    HABIMANA:   Hata mimi nitaanza kufanya shughuli hizi za kilimo. Tuna shamba
                            dogo lakini lina rutuba nyingi. Nitapanda mboga na njugu.
                            Asanteni kwa kunifunza kuhusu kilimo. Kushauriana katika kazi
                            ya kilimo ni jambo lililo muhimu mno.
    KAREKEZI:     Pia, tusome kwa bidii hadi chuo kikuu ndipo tuwe wakulima bora zaidi.
                            Tukisoma kwa bidii, tutajifunza na kutumia mbinu za kisasa za kilimo.
                            Mbinu hizi zitatusaidia na kusaidia jamii. Kilimo kitaimarika.
    ITUZE:            Taibu! Pia tukisoma, tutabuni mbinu mpya za kurahisisha kilimona kujiongezea mazao.
                            Ni lazima tufanye juu chini kupata elimu na kufanya utafiti zaidi. Asanteni wenzangu.

    Maelezo ya msamiati
    kufyeka      – kusafisha shamba kwa kukata miti au majani
    kulima        – kutayarisha shamba kwa kutifua ardhi
    konde         – sehemu ya shamba iliyolimwa
    sesa           – ukulima usiokuwa wa matuta katika ardhi tambarare
    kuzifukia     – kuzificha mbegu ardhini
    zinaota        – zinachipuka kutoka ardhini
    kupalilia       – kulima kwa kuondoa magugu katikati ya mimea au miche
    kunyunyizia – kumwagilia maji au dawa ya maji
    kukua           – kuongezeka ukubwa au kimo
    kukomaa      – kuwa tayari kuvunwa/kutolewa shambani
    kuvuna         – kutoa mazao shambani

    Maswali
    1. Angalia maana ya maneno haya katika kamusi na uyatungie sentensi sahihi.
        a) upanga                    b) fyekeo                   c) plau                             d) trekta                                        e) mbolea    
        f ) samadi                     g) udongo                 h) rutuba                           i) kwekwe                                     j) mbegu
         k) mche                        l) pampu
    2. Andika manufaa ya kilimo yaliyotajwa kwenye kifungu. Ongezea manufaa matano zaidi.
    3. Karekezi na Ndoli hawapendi kilimo. Je, kauli hii ni kweli? Toa sababu zako.
    4. Je, masomo ya kilimo yana umuhimu gani?
    5. Tumia maneno uliyopewa kutaja shughuli kwenye michoro.
         (kufyeka, kulima, kupanda mbegu, kupalilia, kupiga dawa, kunyunyizia maji, kuvuna)
    6. a) Taja majina na matumizi ya vifaa vilivyopo hapa chini.
       
        b) Tunga sentensi sahihi kuhusu kilimo ukitumia jina la kila kifaa hapo juu.
    7. Andika maneno kumi ya shughuli na zana za kilimo kutoka kwenye mraba huu.
        Tunga sentensi sahihi ukitumia kila neno.
         
    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Jadilianeni kuhusu shughuli za kilimo katika nchi
    ya Rwanda na manufaa ya shughuli hizo.

    iii) Msamiati kuhusu shughuli za ufugaji nchini Rwanda
    Ufugaji hasa ni kazi ya kutunza wanyama, ndege na hata wadudu. Kazi hii ina faida
    kubwa sana kama kilivyo kilimo cha mimea. Mfugaji anaweza kufuga wanyama ama wadudu.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Kumbushaneni majina ya mifugo mbalimbali
    mliyosoma katika kidato cha kwanza na umuhimu wake.

    Tazama michoro iliyopo hapa chini na usome kifungu cha maneno kando yake.
     


    Huyu ni Ikirezi. Ikirezi ni mfugaji wa nyuki. Ikirezi
    anarina asali.Baada ya kurina, yeye husafisha
    asali yake na kuiuza. Asali hiyo hutumiwa kama
    chakula au hutengenezewa dawa.








                
    Huyu ni Gabiro. Gabiro anakata sufu. Sufu ya kondoo
    hutumiwa kutengenezea nyuzi za kufumia nguo.

                                                                   






    Huyu ni Ituze. Ituze anakama
    ng’ombe.Kabla ya kukama, aliosha chuchu kwa
    maji vuguvugu na kuzikausha kwa kitambaa safi.
    Anatumia mkebe safi kuwekea maziwa. Ituze
    huwapandisha mitamba kwa dume au mpira.













    Hili ni josho. Ng’ombe hawa wanaogeshwa kwa dawa ndani ya josho. Wafugaji huosha mifugo katika josho ili kuikinga dhidi ya kupe. Dawa huua viroboto wanaoishi kwenye ngozi za mifugo.






    Hawa ni Mudenge na Gatera.
    Mudenge anawalisha kuku kwa mahindi. Pia,
    huwapa kuku mtama, ugali, wadudu na vyakula
    vinavyopatikana kwa urahisi. Wakati mwingine,
    yeye huwapa kuku chakula maalumu
    kilichotengenezwa katika viwanda. Mudenge anawafuga
    kuku wa mayai na nyama. Yeye huuza baadhi ya mayai ili kujipatia riziki. Mudenge pia huwaatamisha baadhi ya kuku wake ili apate vifaranga wa kuuza na kufuga. Gatera naye anawalisha ng’ombe kwa nyasi. Gatera anawafuga ng’ombe wake ndani kwa ndani. Anawapa lishe, maji na dawa humohumo zizini. Gatera hukata pembe za ng’ombe wake. Ng’ombe hukatwa pembe ili kumzuia kumdhuru mtu au kuharibu vitu.





    Huyu ni Kaliza. Kaliza anapenda kuchunga punda. Anawachunga punda penye maji safi na nyasi nyingi. Kulisha mifugo ni shughuli muhimu ya ufugaji. Mifugo wanapolishwa vizuri hukua kwa haraka, huwa na afya nzuri na hutupatia mapato mazuri.









    Kaliza anafagia zizi la ng’ombe. Mkulima
    bora husafisha makao ya mifugo na vyombo
    vyao vya kulia na kulalia. Mifugo wanaolala
    katika mahali safi na kula katika vyombo safi
    huwa na afya njema.













    Daktari wa mifugo anamtibu kuku kwa kumdunga sindano. Kutibu mifugo ni muhimu kwa mkulima. Ni vizuri kutambua dalili ya ugonjwa ili watibiwe mapema.


    Msamiati
    kurina         – kufukuza nyuki kutoka kwenye mzinga na kukata masega ili kupakua asali.
    kukata sufu – kunyoa manyoya ya kondoo kutoka kwenye ngozi yake
    kukama       – kuminya chuchu za mnyama kama vile ng’ombe ili maziwa yatoke
    kupandisha mtamba                     – kumpa ng’ombe wa kike mbegu za kiume ili kuzalisha ndama
    kufuga ng’ombe ndani kwa ndani – kufuga ng’ombe ndani ya eneo au jengo fulani na
                                                             kuwapa mahitaji yote humo bila kuwatoa nje
    kuwapeleka ng’ombe katika josho – kuwapelekea ng’ombe katika dimbwi maalumu lililotiwa dawa ya kuulia kupe
    kuatamisha kuku – kumfanya kuku kulalia mayai
    kuchunga            – kuwapeleka wanyama malishoni na kuwalinda wasiibwe
    kukata pembe     – kutoa pembe kwa kutumia kisu au chuma moto
    kulisha   – kupea chakula na maji

    Maswali
    1. Andika majina yote ya mifugo waliotajwa katika ufahamu hapo juu.
        Taja umuhimu wao.
    2. Eleza faida za shughuli za ufugaji ulizosoma katika kifungu.
    3. Jaza mapengo haya kwa shughuli sahihi ya ufugaji.
       
     
     
    4. Tunga sentensi sahihi ukitumia maneno hapo chini.
        a) rina asali
        b) chunga
        c) kata pembe
        d) kama
        e) lisha
        f ) fagia zizi
        g) tibu ng’ombe
        h) pandisha mtamba
         i) atamisha

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako na mfanyeni zoezi hili:
    1) Kwa pamoja, andikeni shughuli mbalimbali za ufugaji na mifugo nchini Rwanda katika karatasi.
    2) Kunjeni karatasi hizo na kuziweka pamoja.
    3) Kila mwanafunzi achukue karatasi moja kwa zamu, asome shughuli ya ufugaji
        au mifugo katika karatasi aliyochukua na atunge sentensi sahihi kwa kutumia
        neno katika karatasi yake. Atakayekosea asahihishwe.

    Kazi ya kikundi
    Kama darasa zima, fanyeni mjadala kuhusu: Njia za kisasa za ufugaji zinaleta mapato
    makubwa zaidi kuliko njia za kienyeji.

    B . Majira ya mwaka nchini Rwanda
    Tazama michoro iliyopo hapa chini. Je, nini kinafanyika?
     

     Soma kifungu hiki na ujibu maswali yaliyoulizwa chini yake.
    Majira ni kipindi maalumu cha hali ya hewa. Majira haya ndiyo huelekeza upanzi
    wa mimea na uvunaji wa mazao hapa kwetu.
    Tupo na majira mbalimbali. Yapo majira ya mvua nyingi. Majira ya mvua nyingi ya
    mfululizo huitwa masika. Majira haya hutokea kuanzia mwezi wa Machi hadi Mei
    kila mwaka. Shughuli za kupanda mimea kama vile maharage, mtama, mbatata,
    mahindi,na kadhalika hutokea mwanzoni mwa majira ya masika. Mimea hiyo    
    huota na kupaliliwa katika majira haya ya masika.
    Vilevile, mimea mbalimbali kama vile mikahawa, mipareto, migomba, minanasi na
    kadhalika hustawishwa mnamo majira haya.
    Msimu huu wa masika hufuatwa na majira ya kiangazi au ukame. Huu ni wakati
    ambapo jua kali huwaka, mvua hukosa kunyesha na ardhi hukauka. Yapo majira
    mafupi ya kiangazi ambayo hutokea kuanzia Juni hadi Septemba. Mifugo na mimea
    hukosa chakula na maji ya kutosha na huanza kuwa na afya mbaya mnamo majira haya.
    Baadhi ya wakulima huanza kuvuna mazao yao katika majira ya kiangazi.
    Wengine hulima na kuandaa makonde yao mnamo majira haya kabla ya mvua
    kuanza kunyesha.
    Mbali na majira haya, yapo majira ya vuli. Huu ni wakati ambapo huwepo mvua
    ndogo ndogo tu. Majira haya hutokea kati ya mwezi wa Novemba na Februari.
    Wakati wa vuli, wakulima hupanda vyakula vinavyochukua muda mfupi kukua na kukomaa.
    Hata hivyo, shughuli nyingi za upanzi hazifanyiki kwa kuwa mvua inyeshayo huwa haitoshi
    kukuza baadhi ya mimea.
    Hali kadhalika, yapo majira ya kipupwe. Kipupwe ni majira ya baridi ambayo hutokea katika
    miezi ya Septemba na Novemba nchini Rwanda. Wakati huu wa mwaka huwepo baridi kali
    na hubidi watu kuvaa sweta, makoti na hata makabuti.
    Kwa ufupi, wakulima wengi nchini Rwanda huzingatia majira mbalimbali
    wanapofanya shughuli zao za kilimo. Wao hutegemea mvua na jua katika kukuza mimea.

    Msamiati
    masika               – majira ya mvua nyingi ya mfululizo
    kiangazi/ukame  – majira ya jua kali
    vuli                      – majira ya mvua ndogo ndogo
    kipupwe              – majira ya baridi kali

    Maswali
    1. Taja miezi na majira ambapo shughuli hizi za kilimo hufanywa hapa kwetu Rwanda.
        a) kulima shamba kavu
        b) kuandaa konde lenye unyevunyevu
        c) kupanda mimea mingi
        d) kupalilia
        e) kustawisha mimea
        f ) kuvuna
        g) kupanda mimea michache inayokua na kukomaa haraka
    2. Ipo tofauti gani kati ya vuli na kipupwe?3. Tazama mraba ufuatao na uandike maneno manne ya majira.
          

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwenzako. Chunguzeni michoro ifuatayo na mjaze mapengo kando yake.
     
     

    C . Msamiati wa msingi kuhusu wanyama wa porini na umuhimu wake

    i) Msamiati wa wanyama wa porini nchini Rwanda
    Tazama wanyama hawa. Je, hawa ni wanyama gani? Wanyama hawa
    wanapatikani katika mbuga na sehemu ipi ya Rwanda?

    Kisome kifungu kifuatacho ili kujifunza msamiati wa wanyama wa porini.
    Mnyama wa porini ni mnyama anayeishi katika pori. Pori ni mahali penye miti na nyasi nyingi.
    Mnyama wa porini hafugwi na binadamu. Wanyama wengi wa porini hupatikana katika mbuga
    za wanyama. Mbuga za wanyama ni sehemu zilizotengwa na serikali kuwa ndio makazi ya
    wanyama hao wa porini. Je, unafahamu mbuga gani za wanyama nchini Rwanda?
                                                                                                                              

    Nchi ya Rwanda ina wanyama wengi wa porini.
    Nchi yetu ya Rwanda inasifika sana kutokana
    na masokwe. Sokwe ni mnyama mkubwa zaidi
    katika jamii ya nyani. Mnyama huyu hana
    mkia. Sokwe ana akili nzuri inayokaribiana
    na ile ya binadamu. Wana uwezo wa
    kumwiga binadamu. Nchi yetu inajulikana
    sana kutokana na masokwe. Masokwe hawa
    wanapatikana katika mbuga zetu za wanyama.
    Masokwe wengi wanapatikana katika Mbuga
    ya Wanyama ya Volcanoes (Volkano).









    Nyani ni mnyama wa jamii ya sokwe na tumbiri.
    Nyani ni mdogo kuliko sokwe lakini ana akili nyingi zaidi.
    Ana masikio makubwa nao mwili wake una rangi ya kaki ya
    kijivu na ngoko nyekundu makalioni. Nyani huishi katika
    vikundi vya majike na madume. Wana uwezo wa kuishi
    kwa miaka zaidi ya arubaini.
     







                                                                                                                   

               Pia kuna tumbiri porini. Tumbiri ni mnyama mdogo
               zaidi katika jamii ya nyani. Tumbiri hupenda sana
               kukaa mitini. Hula vyakula mbalimbali kama vile
               matunda, mazao ya mimea mbalimbali na kadhalika.







    Simba ni mnyama mkubwa wa jamii ya paka.
    Simba hula nyama. Anaitwa mfalme wa wanyama
    au nyika. Simba huishi kwenye vikundi. Vikundi
    hivyo huongozwa na simba dume.



         
                   


                                 Ndovu ndiye mnyama mkubwa zaidi wa porini.
                                 Ndovu ana mkonga pamoja na pembe mbili
                                 kubwa zenye thamani. Ndovu wana masikio
                                 makubwa na miguu mifupi minene. Ndovu hula
                                 nyasi, mizizi, matunda na mashina ya miti. Pia,
                                 huishi katika vikundi. Kila kikundi huongozwa na
                                 ndovu jike ambaye ana umri mkubwa zaidi kuliko
                                 wote. Uwindaji wa ndovu na kuuza pembe
                                  zake ni hatia. Sisi sote tunafaa kuwatunza ndovu na wanyama wote wa porini.


    Chui pia hupatikana katika mbuga zetu. Chui ni
    mnyama wa jamii ya paka lakini aliye mkubwa na
    mkali na mwenye madoadoa ya manjano na meusi.
    Chui hula wanyama wadogo wadogo wanaoishi porini.
    Baada ya kuwinda, wao huficha nyama kwenye matawi
    ya mti. Wao hupenda sana kutembea na kuwinda wakati
    wa usiku na kupumzika wakati wa mchana.



    Pundamilia pia ni mnyama wa porini wa jamii ya farasi.
    Ana milia myeusi na myeupe katika mwili mzima.
    Inaaminika kuwa milia hiyo huwawezesha kujificha
    nyikani ili wasionekana na wanyama wanaowawinda.
    Pundamilia hutembea na kula nyasi katika vikundi vikubwa.



                                                                                                                                                      

                          Twiga naye ana shingo ndefu, rangi ya kahawia na madoadoa meusi.
                          Twiga  ndiye mnyama mrefu zaidi. Yeye hula majani ya miti.




    Kifaru pia hupatikana katika mbuga zetu. Ni mnyama
     mkubwa afananaye na kiboko na mwenye kipusa usoni.






                                                                       
                                          
                                  
     Nyati pia ni mnyama mkubwa sana. Hufanana na ng’ombe. Pembe zake zimepinda kwa mbele. Nyati hula nyasi. Wao pia huishi katika vikundi kutegemea jinsia. Nyati pia huitwa mbogo.                                    
     






    Swara ni mnyama mdogo anayefanana na mbuzi.
    Swara anaweza kukimbia haraka. Yeye hula nyasi.



    Wanyama hawa wa porini hupatikana katika mbuga zetu kama vile Akagera,
    Nyungwe na Volcanoes. Wanyama hawa ni vivutio vikubwa vya watalii wanaotoka
    ndani na nje ya nchi yetu.

    Maswali
    1. Andika orodha ya majina ya wanyama wa porini wanaokula:
        a) nyama
        b) nyasi
    2. Eleza tofauti zilizopo kati ya sokwe na nyani.
    3. Jaza kila pengo kwa jina sahihi la mnyama wa porini.
         a) Mwenye tamaa kama______________.
         b) _________ ana mkonga na pembe mbili.
         c) _______ haoni kundule.
         d) Ndovu pia huitwa_____________.
         e) Nimemwona mnyama mwenye milia myeusi na myeupe mwilini.
             Nimemwona__________.
    4. Tunga sentensi sahihi ukitumia majina haya ya wanyama wa porini.
         a) pundamilia             b) simba               c) tumbir
        id) swara                     e) nyati                  f ) ndovu
    5. Taja majina ya wanyama hawa:


    6. Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Fanyeni utafiti kuhusu majina na sifa
        za wanyama wa porini wanaopatikana ndani na nje ya Rwanda na ambao
        hawajatajwa katika ufahamu.

    ii) Umuhimu wa wanyama wa porini nchini Rwanda
    Kufikia sasa, umesoma mengi kuhusu wanyama wa porini. Wanyama hao wana
    umuhimu mbalimbali.
    Tazama mchoro huu na usome kifungu chini yake.
                                                  
    KANYANA:  Karibuni katika mbuga yetu ya Volcanoes.
    UWASE
    na HIRWA:   Asante.
    KANYANA: Hapa, mtaona wanyama wengi wa porini.
    UWASE:      Wanyama hao wana umuhimu gani?
    NGABO:     Wanyama hao wana umuhimu mkubwa sana kwa nchi hii yetu ya
                        Rwanda. Wanyama hao kama vile masokwe ni vitega uchumi. Kila
                        mwaka, watalii kutoka nchi za mbali huja hapa kwetu kuwaona
                        wanyama. Wajapo hivyo, huja na pesa za kigeni ambazo huinua sana
                        uchumi wetu.
    KANYANA: Nyinyi pia ni watalii wetu hapa. Pesa mnazolipa mkiingia hujenga
                        uchumi wetu. Pesa hizo pia hutumiwa kutulipia mshahara. Mimi na
                        wenzangu tumeajiriwa kwa sababu ya wanyama wa porini.
    HIRWA:       Je, nchi yetu hunufaika na pesa za kiingilio peke yake?
    NGABO:      Hapana. Wageni wanapokuja, wanaleta manufaa mengi zaidi. Wao
                         hulipia huduma mbalimbali. Kwanza kuna malazi yao. Sisi
                         huwakaribisha katika hoteli kubwa kubwa na nzuri nzuri. Hoteli
                         hizo zimepanuka na kuwaajiri watu wengi kwa sababu ya wageni
                         hao wanaokuja kuangalia wanyama wa porini. Wageni hao pia
                         hulipia usafiri wao uwe ni wa ndege au gari. Usafiri huo huwapeleka
                         huko wanakopenda kwenda kuwaona wanyama.
    KANYANA: Mbali na hayo, zipo bidhaa nyingi sana za hapa ambazo watalii hao
                        hununua kuwa ni ushahidi kwao kwamba kweli walikuwa hapa. Kwa
                        njia hiyo pia nchi hufaidika kiuchumi.
    UWASE:      Mbali na faida hizo za kifedha, zipo faida gani tena za wanyama hawa?
    NGABO:      Wanyama hawa hukuza elimu yetu. Wanafunzi, na hata watu wazima
                         huzuru mbuga zetu za wanyama ili kuwaona na kujifunza mengi
                         kuwahusu.
    KANYANA:  Isitoshe, wanyama wa porini ni hazina kwa vizazi vyetu vya baadaye.
                         Sisi sote tumewaona wanyama hawa. Vivyo hivyo, litakuwa jambo
                         zuri sana ikiwa wanetu, wajukuu, watukuu, vilembwe na hata
                         vilembwekeza wetu kuwaona wanyama wa porini pia. Hii ndiyo
                          sababu ya serikali yetu kuwatunza na kuwalinda wanyama wa porini.
    UWASE
    na HIRWA:  Asanteni kwa maelezo yenu.

    Maswali
    1. Taja faida za wanyama wa porini.
    2. Taja njia mbili ambazo serikali hutumia kuhifadhia wanyama wa porini.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako. Jadilianeni kuhusu umuhimu wa wanyama wa porini nchini Rwanda.

    D . Matini ya Kiswahili kuhusu kilimo na ufugaji pamoja na vipengele vya kisarufi
    Nomino
    Je, unakumbuka maana na aina za nomino ulizosoma katika kidato cha kwanza?
    Zitaje.
    Nomino ni neno linalotaja mtu, kitu, hali au jambo. Zipo aina mbalimbali za nomino.
    Zifuatazo ni baadhi ya nomino hizo.

    a) Nomino za pekee
    Nomino za pekee hutaja vitu au watu wenye sifa za kipekee. Zinapoandikwa katika
    sentensi, lazima zianze kwa herufi kubwa hata zikiwa katikati au mwishoni mwa
    sentensi. Kumbuka hapa ya kuwa majina haya hayachukui hali ya wingi.
      Mifano ya nomino za pekee katika sentensi.
    i) Rwanda ni nchi yenye wanyama wengi wa porini.
    ii) Mukangango ananyoa sufu ya kondoo.
    iii) Mwenyezi Mungu atujalie mvua nyingi ili tulime.
    iv) Kigali ni jiji linalopendeza.


    Zoezi

    a) Andika sentensi sahihi ukitumia nomino hizi za pekee:
        i) Munyana        ii) Kamana          iii) Mola
      iv) Mei                 v) Mto Kivu          vi) Msitu wa Nyungwe
    b) Tambua makosa katika sentensi hizi na uyarekebishe.
        i) Mimi na kayitesi tunapenda somo la kilimo.
        ii) Nitavuna mihogo yangu mwezi wa februari.
        iii) Ng’ombe anaitwaje kwa kinyarwanda?

    b) Nomino za kawaida
    Nomino za kawaida hutaja vitu vya kawaida vinavyoweza kuchukua umoja na
    wingi kama jina lolote lile. Nomino hizo zinapoandikwa, huchukua herufi ndogo
    isipokuwa pale zinapojitokeza mwanzoni mwa sentensi.

    Mifano ya nomino za kawaida:
    i) Nomino za viumbe wenye uhai:
      
    ii) Nomino zinazomtambulisha mtu na kazi yake:
         

    iii) Nomino za vitu vya kawaida
       
    iv) Nomino za mahali: shambani, uwanjani, mbugani, zizini, porini
    Kumbuka hapa kuwa nomino hizi za mahali huundwa kwa kuongeza ‘ni’ mwishoni
    mwa nomino husika.

    Mifano ya matumizi ya nomino za kawaida katika sentensi.
    i) Mavuno ya mwaka huu ni mazuri.
    ii) Niletee jembe hilo.
    iii) Sufu za kondoo hutumiwa kutengenezea sweta.
    iv) Mkulima hodari hupata mazao mengi.
    v) Ndovu ni mnyama mkubwa wa porini.

    Zoezi

    Tunga sentensi kumi sahihi ukitumia nomino za kawaida.

    c) Nomino za jamii
    Nomino za jamii pia huitwa nomino za makundi. Hizi ni nomino ambazo hutaja
    jumla ya vitu vingi au vitu katika makundi.

    Mifano ya nomino za jamii:


    Mifano katika sentensi
    i) Makole ya ndizi yamevunwa.
    ii) Matuta yamepigwa shambani.
    iii) Matita ya kuni yatatumika kuchomea nyama.
    iv) Mitumba ya aina hii haifai wakulima.
    v) Bunge letu limetenga pesa nyingi kwa wizara ya kilimo.
    vi) Baraza la wafuga farasi limevunjwa.
    vii) Hili ni robota la pamba.

    Zoezi

    Fanya utafiti kupata nomino kumi zaidi za jamii. Tunga sentensi ukitumia kila
    nomino hizo katika umoja na wingi.

    d) Nomino za dhahania
    Katika kikundi hiki hupatikana nomino ambazo ni za kufikirika tu na wala
    haziwezi kuguswa. Chukua nomino kama urafiki. Urafiki ni neno la kufikirika au
    kudhaniwa tu na wala haliwezi kuonekana wala kushikika. Nomino hizi haziwezi
    pia kuhesabika.
    Mifano katika sentensi
    i) Upanzi hufanywa mvua inapoanza kunyesha.
    ii) Kilimo kinasaidia kumaliza umaskini nchini Rwanda.
    iii) Ushirikiano wao katika kupalilia unawafaidi.
    iv) Fikira za wafugaji hao ni za hekima.
    v) Tutafanya uvunaji mwezi ujao.

    Zoezi

    Tunga sentensi zozote kumi kuhusu kilimo na ufugaji ukitumia nomino za jamii.

    e) Nomino za wingi
    Hizi nazo ni nomino za vitu ambavyo daima hupatikana kwa wingi pekee au umoja
    pekee. Vitu vinavyotajwa na nomino hizi haviwezi kugawika.

    Mifano ya nomino za wingi:
    maziwa, sukari, chumvi, uji, chai, manukato, mvua na kadhalika.

    Mifano katika sentensi:
    i) Sukari ni zao la miwa.
    ii) Maua yale hutumiwa kutengenezea manukato.
    iii) Chai hii ni tamu.
    iv) Maji yanyunyiziwayo hapa ni ya mto huo.

    Zoezi

    Soma kifungu kilichopo hapa chini. Tambua na uanishe nomino mbalimbali kifunguni.
    Hapa nchini Rwanda, Mwenyezi Mungu ametujalia mazingira mazuri yenye
    kufanikisha ufugaji. Ufugaji ni kazi ya kutunza wanyama, ndege na hata wadudu.
    Mfugaji anaweza kufuga wanyama ama wadudu. Ikiwa ni wanyama, anaweza
    kutunza ng’ombe, mbuzi, kondoo, farasi, nguruwe, na kadhalika. Ikiwa nia yake ni
    kufuga ndege, anaweza kuwatunza kuku, bata na kadhalika. Hata hivyo, akichagua
    wadudu huweza kuwafuga nyuki.
    Ufugaji una kazi nyingi sana. Kwa mfano, mfugaji wa ng’ombe anapotaka matokeo
    ya kuridhisha, itambidi atumie njia za kisasa katika ufugaji wake. Kwanza kabisa, ni
    lazima awatafute ng’ombe bora wa maziwa. Ng’ombe hawa huleta mapato ya juu.
    Mbali na hayo ni sharti ahakikishe kwamba wanyama wake wana lishe ya kutosha
    hasa kwa ng’ombe wanaokaa ndani kwa ndani. Ng’ombe hawa, hasa ng’ombe jike,
    wa kukaa ndani kwa ndani hulishiwa zizini na kulala humo humo zizini. Hata hivyo,
    ni lazima zizi hilo liwe safi na ng’ombe huyo alale pahali safi. Kukosa kufanya hivyo
    ni kukaribisha magonjwa ya namna kwa namna.
    Iwapo mfugaji atawalisha wanyama wake vizuri, atafaidika pakubwa. Ataweza
    kupata maziwa ya kutosha. Atauza maziwa hayo na kujinunulia bidhaa nyinginezo
    kama vile chumvi, sukari, chane za ndizi na kadhalika. Umaskini pia utaisha.

    Vivumishi
    Je, unakumbuka vivumishi mbalimbali mlivyosoma katika kidato cha kwanza?
    Kwa kawaida, kivumishi ni neno linaloongezea nomino maana. Zipo aina mbalimbali za
    vivumishi. Baadhi ya vivumishi hivyo ni:

    a) Vivumishi vya sifa
    Haya ni maneno yatajayo tabia au sifa za kitu, mtu ama jambo.
    Zipo aina mbili za vivumishi vya sifa: vivumishi vya sifa vinavyochukua viambishi na
    vivumishi vya sifa visivyochukua viambishi.

    Mifano ya vivumishi vya sifa vinavyochukua viambishi:
    -aminifu         -zuri
    -pana             -kubwa
    -pya               -dogo
    -bovu             -fupi

    Kumbuka kuwa kiambishi au viambishi vinavyochukuliwa na vivumishi hivi hutegemea ngeli.
    Mifano katika sentensi:

    ii) Vivumishi vya sifa visivyochukua viambishi
    Hivi ni vivumishi ambavyo havibadiliki katika umoja na wingi au kutoka ngeli moja
    hadi nyingine; hubakia jinsi vilivyo.
    Mifano: bora, safi, hodari, bandia, haba, duni, laini na kadhalika.

    Mfano katika sentensi.
     


    Zoezi

    a) Tunga sentensi sahihi kuhusu kilimo na ufugaji katika umoja na wingi ukitumia vivumishi hivi vya sifa.
        i) -baya          ii) -fupi           iii) -dogo
       iv) -ingi           v) -chache
    b) Tunga sentensi sahihi ukitumia vivumishi hivi katika umoja na wingi.
       i) bora           ii) dhalimu       iii) duni
      iv) tele            v) laini
    c) Andika sentensi hizi katika umoja au wingi.
       i) Nipe ndizi chache.
      ii) Mhindi mrefu unafaa.
     iii) Farasi wakubwa watatubeba.
     iv) Zizi safi halileti magonjwa.
      v) Upanzi bora ni huu.
     vi) Mkulima nadhifu anapita.
    d) Tunga sentensi zozote kumi kuhusu wanyama wa porini na kilimo zenye
         vivumishi vya sifa katika umoja na wingi.

    b) Vivumishi vya pekee
    Vivumishi vya pekee hutoa habari kuhusu nomino au kiwakilishi chake kwa njia ya
    kipekee. Vivumishi vya peke ni sita katika Kiswahili kama ifuatavyo:

    i) -enye
    Huonyesha hali ya ‘kuwa na’ au ‘kumiliki’. Ni sharti kivumishi hiki kifuatwe na nomino wala si kitenzi.

    ii) -enyewe
    a) Hutumika mwanzoni mwa sentensi kuonyesha jambo au kitu kinachotarajiwa.

    b) Hutumika mwishoni mwa sentensi kuonyesha kuwa jambo limetokea bila
        kusababishwa na yeyote au chochote.
      
    iii) -ote
    Huleta maana mbili:
    a) Kuonyesha kila sehemu ya kitu hasa katika umoja.
     
    b) Kuonyesha kila kitu; bila kubakisha lolote hasa katika wingi.

    Zoezi

    Eleza maana ya sentensi ikiwa ni ‘kila sehemu’ au ‘kila kitu’.
    i) Zizi lote limefagiliwa.
    ii) Mazao yote yamevunwa.
    iii) Paka amekunywa maziwa yote.
    iv) Ndizi yote imeiva.
    v) Simba wote wamepita.

    iv) -o-ote
    Huonyesha mojawapo ya vitu au baadhi ya vitu bila kubagua.

    Zoezi

    Tumia ‘-ote’ au ‘-o-ote’ pamoja na viambishi sahihi vya ngeli kujazia pengo katika sentensi zifuatazo.
    1. Nitatumia jembe _____ nitakalopewa.
    2. Miharagwe _________ imemea.
    3. Kuku ______ wamepewa chakula.
    4. Sitachukua nanasi ____________.
    5. Fyeka nyasi____________.

    v) -ingine
    Kivumishi hiki cha pekee huweza kuwa na maana tatu:
    a) Kuonyesha kitu tofauti na kile kilichotajwa au kilichopo.
     

    b) Kuonyesha kitu zaidi/nyongeza


    c) Kuonyesha ‘baadhi ya’


    vi) -ingineo
    Kivumishi hiki hutumika kuleta maana mbili:
    a) 'zaidi ya'

    b) Kuonyesha hitimisho ya orodha ambayo haikukamilika.
      

    Zoezi

    a) Tumia ‘-ingine’ au ‘-ingineo’ pamoja na viambishi sahihi vya ngeli kujazia mapengo.
        i. Amevuna mananasi ____________.
        ii. Sitaki panga hili, nipe panga _____________.
       iii. Mama amepanda mbegu za maharagwe, mtama, mahindi na _____________.
       iv. Usiwakame ng’ombe __________. Maziwa haya yametosha.
       v. Mpe migomba hiyo na ______________.
    b) Tunga sentensi tano sahihi kuhusu kilimo na ufugaji katika umoja na wingi
         ukitumia nomino zozote na kivumishi cha ‘-ingine’.
    c) Tunga sentensi tano sahihi kuhusu wanyama wa porini na mifugo katika
         umoja na wingi ukitumia nomino zozote na kivumishi cha ‘-ingineo’.

    c) Vivumishi vionyeshi
    Vivumishi vionyeshi au viashiria ni maneno ya kuonyesha alipo mtu au kitu, yaani
    ujirani. Kuonyesha huko kunaweza kuwa kwa ujirani wa karibu – hapa, ujirani wa
    mbali kidogo – hapo, na ujirani wa mbali – pale.

    Mifano ya vivumishi hivi ni hii ifuatayo:

    Mfano katika sentensi:
    i) Kijijini humu mna mfugaji hodari.
    ii) Hizi juhudi zenu za kulima zitamaliza umaskini.
    iii) Ng’ombe wale wanakunywa maji.
    iv) Fyekeo hilo halikati majani.
    v) Shambani pale pamepaliliwa.

    i) Vivumishi vionyeshi radidi
    Vivumishi hivi hutokana na kurudia vivumishi vionyeshi. Huleta maana ya kutilia mkazo.

    ii) Vivumishi vionyeshi visisitizi
    Hutumiwa kusisitiza jambo.

    Zoezi

    a) Jaza kila pengo kwa vivumishi sahihi vilivyowekwa katika mabano.
        i. Mazao __________ yatajaza guni. (vionyeshi visisitizi vya karibu)
        ii. Mkulima _________ analima. (vionyeshi vya mbali)
       iii. Twiga __________ ni wengi. (vionyeshi viradidi vya mbali kidogo)
       iv. Nyama __________ ni tamu. (vionyeshi vya karibu)
       v. Wafugaji _________ wana bidii. (vionyeshi vya mbali kidogo)
    b) Tunga sentensi tano tano kuhusu kilimo na ufugaji katika umoja na wingi
         ukitumia vivumishi vionyeshi, vivumishi vionyeshi rejeshi na vivumishi
         vionyeshi visisitizi.

    d) Vivumishi vya idadi
    Vivumishi vya idadi ni maneno yanayoonyesha idadi ya watu ama vitu.
    Vipo vivumishi vya idadi kamili, vivumishi vya idadi ya jumla na vivumishi
    vya idadi ya matokeo.

    i) Vivumishi vya idadi kamili
    Pia huitwa vivumishi vya idadi halisi au bainifu. Huonyesha hesabu halisi ya nomino
    husika.Baadhi ya vivumishi hivi huchukua viambishi vya ngeli kutegemea nomino
    inayohesabiwa.
    Mfano: -moja, -wili, -tatu, -nne, -tano na -nane.

    Baadhi ya vivumishi vya idadi kamili havichukui viambishi vyovyote vya ngeli.
    Yaani hutumika jinsi vilivyo bila kubadilika.
    Mfano: sita, saba, tisa na kumi, makumi, mia na kadhalika

    ii) Vivumishi vya idadi ya jumla/isiyo kamili
    Huonyesha idadi ambayo ujumla wake haujulikani. Baadhi ya vivumishi hivi
    huchukua viambishi vya ngeli ya nomino.

    Mfano: -chache na –ingi

    Mfano katika sentensi:
    1. Kuku hawa wametaga mayai machache.
    2. Mwaka huu tumepanda mbegu nyingi.
    3. Wakulima wengi wamevuna.
    4. Wao huuza maziwa mengi sana.
    Baadhi ya vivumishi vya idadi ya jumla havichukui viambishi vya ngeli.
    Yaani hubakia vivyo hivyo.
    Mfano: kadhaa, tele, kiasi, kidogo na haba.


    iii) Vivumishi vya idadi ya matokeo
    Pia huitwa vivumishi vya nafasi katika orodha. Vivumishi hivi huonyesha nafasi ya
    nomino katika orodha.

    Zoezi

    a) Jaza kila pengo kwa kivumishi sahihi katika mabano.
       i. Sungura ________ wanakimbia. (chache)
      ii. Masokwe __________ wanacheza. (sita)
     iii. Mkulima __________ atapewa mbolea. (moja)
     iv. Amenunua maembe_________. (ingi)
      v. Tumelima mashamba___________. (nane)
    b) Tunga sentensi kumi sahihi kuhusu kilimo na ufugaji ukitumia vivumishi vya
         idadi jumla na isiyo jumla.

    e) Vivumishi viulizi
    Hili ni kundi la vivumishi ambalo lina maneno yatumiwayo kuulizia maswali.
    Baadhi ya mifano ya vivumishi viulizi ni:

    i) Kiulizi -pi?

    ii) Kiulizi -ngapi?

    iii) Kiulizi gani?
    Kiulizi hiki hakichukui kiambishi chochote cha ngeli.

    Tanbihi
    Kivumishi kiulizi kinastahili kuandamana na nomino au kiwakilishi cha nomino.
    Viulizi ambavyo havitumiwi pamoja na nomino au viwakilishi vya nomino haviwezi
    kuitwa vivumishi bali ni viulizi.
    Mfano: lini, nani, nini, vipi. Hivi si vivumishi viulizi kwa sababu havitumiwi pamoja
    na nomino au kiwakilishi cha nomino.

    Zoezi

    a) Tumia kiulizi ‘-pi’ kwa usahihi kujazia kila pengo.
       i. Mashirika _________ yanasaidia wakulima?
      ii. Mkahawa __________ unakatwa?
     iii. Dawa _________ zinanyunyiziwa mimea?
     iv. Niwaite wafugaji ________?
     v. Kufyeka _______ kunafaa?
    b) Tumia kivumishi kiulizi ‘-ngapi’ kwa usahihi kujazia kila pengo.
     i. Tukupe magunia __________?
    ii. Pembe _________ zimekatwa?
    iii. Mbwa _________ wamechanjwa?
    iv. Mipera ___________ inapandwa?
    v. Vibuyu _________ vina maziwa?

    f) Vivumishi vimilikishi
    Maneno katika kundi hili la vivumishi hujibu swali mtu, kitu au jambo ni la nani au
    lina nini? Vivumishi hivi huwa sita pekee katika Kiswahili.
    -angu            -etu
    -ako              -enu
    -ake              -ao

    Kutokana na haya, unapata maneno kama vile:
    wangu               wetu
    chako                chenu
    kwake                kwao

    Unaweza kutunga sentensi hizi ukitumia vivumishi vimilikishi:
    1. Jibini hii ni yangu.
    2. Mawele yako yameliwa na fukusi.
    3. Mbatata zenu zinauzwa Zambia.
    4. Njugu za kwao ni tamu mno.
    5. Huwezi kusema kuwa huu ni mchicha wako!

    Zoezi

    Jaza kila pengo kwa kivumishi kiwakilishi sahihi.
    1. Nyinyi mna mihogo. Mihogo ni ___________.
    2. Sisi tuna maembe. Maembe ni _____________.
    3. Wao wana sufu. Sufu ni _____________.
    4. Mimi nina sukari. Sukari ni ____________.
    5. Yeye ana kole la ndizi. Kole ni __________.
    6. Wewe una muhogo. Muhogo ni _____________.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Someni kifungu kifuatacho huku mkitambua jinsi
    vivumishi vilivyotumiwa.
    Mimi ni mwanafunzi mwenye bidii. Nia yangu kuu maishani mwangu ni kuridhika
    na shughuli za kilimo cha kisasa kama mojawapo ya njia nzuri za kupigana dhidi
    ya umaskini. Lengo langu kuu la kwenda shuleni hasa ni kupata maarifa mema ya
    kuniwezesha kuishi maisha ya kitajiri. Maarifa hayo yataniwezesha kuwa mkulima
    bora.
    Nitaendelea na masomo hadi chuo kikuu. Nitafanya somo la Kilimo katika chuo
    kikuu. Hata hivyo, hilo pekee halitatosha. Nitafanya kazi ndogo ndogo kwa muda
    ili kutafuta pesa za kuanzisha kilimo. Kufikia hapo, nitakuwa nimepiga hatua lakini
    bado sitakuwa nimefikia lengo langu.
    Kuanzisha kilimo cha kisasa kutakuwa ni hatua kubwa lakini bado kutakuwa
    na kazi kubwa ya kufanywa. Ni sharti niupige vita vikali umaskini kupitia kilimo
    hicho. Umaskini ni adui mbaya ambaye lazima niangamize. Njia moja ya kumaliza
    umaskini ni kuweka uvivu kando.
    Mbali na kulima, nitafuga mifugo wengi. Nitahakikisha ya kuwa nina vifaa vyote
    vinavyohitajika kwa kufanyia kazi hizo mbili. Kutakuwa na trekta kubwa kubwa
    na mashine za kukamua. Nitanunua magari mazuri ya kusafirisha mazao mengi
    nitakayovuna. Nitawapa vijana wenzangu kazi ili nao wawe na kipato kizuri. Kwa
    jumla, nitahakikisha kuwa vitu vyote anavyohitaji mkulima wa kisasa vipo.
    Mwisho, nitatafuta masoko mazuri na ya kuaminika. Nia yangu hapa ni kuuza
    bidhaa zangu katika masoko yaya haya ya hapa kwetu. Baadaye nitaziuza katika
    masoko, nje ya nchi yetu. Hizi zote zitakuwa ni juhudi za kuendeleza vita vikali dhidi
    ya umaskini au uchochole.

    Zoezi

    1. Orodhesheni vivumishi vyote vilivyomo kifunguni humu kwa kuzingatia aina
        ya kila kivumishi husika.
    2. Tunga sentensi fupi fupi na sahihi ukitumia vivumishi mlivyoorodhesha hapo juu.

    Viwakilishi
    Viwakilishi ama vibadala ni maneno ama viambata (sehemu za maneno)
    vinavyosimama badala ya majina. Kundi hili la maneno huweza kugawika katika
    sehemu mbalimbali ifuatavyo.

    a) Viwakilishi nafsi
    Husimamia nafsi za nomino inayozungumziwa katika umoja au wingi. Kuna aina
    mbili kuu za viwakilishi vya nafsi:

    i) Viwakilishi nafsi huru
    Huwakilisha nafsi iliyo huru, yaani isiyounganishwa na kitenzi katika umoja na
    wingi kwenye sentensi.
    Mfano: nafsi ya kwanza (mimi, sisi), nafsi ya pili (wewe, nyinyi), nafsi ya tatu (yeye, wao).

    Zoezi

    Umoja                                                    Wingi
    1. Mimi ninalima.                                   Sisi tunalima.
    2. Wewe unavuna.                               Nyinyi mnavuna.
    3. Yeye anafyeka.                                Wao wanafyeka.

    ii) Viwakilishi nafsi viambata
    Viwakilishi hivi huambatanishwa na vitenzi.
    Mfano: nafsi ya kwanza (ni-, tu-), nafsi ya pili (u-, m-) nafsi ya tatu (a-, wa-)
    ii) Pia, vipo viwakilishi ambata vya ngeli. Navyo ni:
    b) Viwakilishi vitokanavyo na vivumishi
    Je, unakumbuka vivumishi ulivyosoma hapo juu? Endapo kivumishi husika
    kimetumika badala ya nomino, kivumishi hicho kinakuwa kiwakilishi. Nacho
    kiwakilishi hicho huchukua jina la kivumishi hicho. Mfano:
    i) Viwakilishi vionyeshi
    Hutokana na vivumishi vionyeshi. Tazama vivumishi vionyeshi. Unapoondoa
    nomino katika vivumishi hivyo, unapata viwakilisihi vionyeshi.
    Kumbuka kwamba hufai kutumia nomino na kiwakilishi katika sentensi moja.

    ii) Viwakilishi viulizi
    Viwakilishi hivi vinatokana na vivumishi viulizi.
    iii) Viwakilishi vimilikishi
    Viwakilishi hivi hutokana na vivumishi vimilikishi. Tazama mifano hapa chini.

    Zoezi A

    Tunga sentensi ukitumia viwakilishi mbalimbali.

    Zoezi A

    Soma kifungu kifungu kifuatacho huku ukitambua jinsi viwakilishi vilivyotumiwa.
    Zama hizo, fisi alikuwa jirani ya binadamu aliyependa kulima. Binadamu alimiliki
    shamba kubwa la mihogo. Naye Fisi alikuwa mvivu aliyependa kumtembelea
    binadamu kwake. Alidhani kuwa huyo binadamu naye alimpendana sana. Hata
    hivyo, binadamu hakumpenda sana fisi. Fisi hakupenda kulima bali alipenda sana
    kula.    
                                       
    Siku moja jioni, fisi alimuaga binadamu na kusema,    “Kesho nitaamkia huku kwako ili uniandalie kiamshakinywa! ”Kwa roho ya ndani, mwanadamu alijisemea, ‘Huyu hapendi kufanya kazi, anapenda tu kula. Kwa nini haoni kuwa simpendi?’Akamwambia fisi, “Labda utanipata, labda utanikosa.”
    Fisi kuona kuwa anaweza kukosa mlo alisema, “Basi nitajaribu nije hata mapema zaidi. Kwa namna hiyo tunaweza kula halafu wewe uende shambani. Napenda sana namna unavyopika nyama.” Bila kungoja jawabu, alitoka na kujiendea zake.
    Keshoye, mwendo wa saa kumi na moja asubuhi, fisi alibisha hodi kwa mwanadamu. Naye mwanadamu hakusita kumfungulia mlango. Mwanadamu aliazimia kumfunza fisi adabu.
    “Karibu, karibu kwangu rafiki yangu,” mwanadamu alijibu.
    Naye fisi kwa kusukumwa na njaa yake ya asubuhi pamoja na ulafi wake, alimpita
    tu na kuingia ndani. Harufu ya nyama mle ndani ilimfanya fisi ameze mafunda ya mate.
    “Karibu, karibu kaa,” mwanadamu alimlaki fisi. “Nipe dakika chache tu na chakula
    kitamu na kingi kitakuwa mezani hapa.”
    “Basi fanya haraka. Ninakufa kwa njaa,” fisi alisema.
    Baada ya muda usiokuwa mrefu vile, mwanadamu alikuwa ameandika meza
    kwa kila namna ya nyama ya mifupa. Ohoo! Fisi kuona hivyo, nusura kuirukia
    lakini mwanadamu akamzuia kwa kusema, “Bwana fisi, ili leo ushibe vya kutosha,
    tumbukiza kila sahani mdomoni mwako na umeze tu bila kutafuna.
    ”Hata kabla ya mwanadamu kumaliza usemi wake, fisi alikuwa ametumbukiza
    sahani mbili kinywani mwake!
    “Mbona hiki cha leo ni kikali jinsi hii? Lo! Kinawasha sana! Loooooooooo!”
     Fisi alilalamika.
    Kumbe mwanadamu alijaza pilipili kwenye nyama. Tangu siku hiyo, fisi hakurudi
    tena kwa mwanadamu.

    Maswali
    1. Je, fisi alikuwa mnyama wa aina gani?
    2. Ni kwa nini mwanadamu hakumpenda fisi?
    3. Mwanadamu aliikomeshaje tabia mbaya ya fisi?
    4. Unadhani ni yapi yaliyompata fisi?
    5. Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Bainisheni viwakilishi vyote vilivyomo
        katika kifungu mlichosoma hapo juu. Tungeni sentensi sahihi mkitumia
        vivumishi hivyo.

    Vielezi
    Vielezi pia huitwa viarifa. Ni maneno yafafanuayo vitenzi, vivumishi au vielezi
    vingine. Mathalan, ukisema Anatembea haraka, neno 'haraka' linaeleza jinsi
    anavyotembea mhusika. Kwa hivyo, neno hilo linalokuarifu mengi kuhusu
    kutembea ni kielezi.
    Maneno haya hujigawa katika vikundi mbalimbali kama ifuatavyo:

    a) Vielezi vya namna au jinsi
    Haya ni maneno ambayo huarifu jinsi ya kutendeka mambo.
    Mfano: sana, bure, kitoto, vizuri, upesi, kwa miguu, kwa bidii, bwe!
    b) Vielezi vya wakati
    Nayo haya ni maneno yanayofafanua ama kueleza wakati wa kutokea tendo.
    Mathalan, ukisema Mgeni alifika jioni neno jioni ni kielezi cha wakati.
    Vipo vielezi vya wakati vya aina mbili:

    i) Vielezi vya wakati maalumu.
    Mfano: Januari, Disemba, Jumamosi, saa tatu, kesho, leo, mtondo na kadhalika.
    ii) Vielezi vinavyotaja wakati kwa jumla
    Mfano: baadaye, zamani, daima, milele, awali, punde, karibuni, zama hizo.

    c) Vielezi vya kiasi/idadi
    Vielezi vya kiasi ni namna ya maneno ambayo hufafanua vitenzi kwa kujulisha
    limetokea mara ngapi tendo linalotajwa.

    d) Vielezi vya mahali
    Haya nayo ni maneno ama mafungu ya maneno yanayofafanua panapotokea kitendo.
    Mara nyingi, maneno haya huwa ni majina ya mahali.

    Zoezi

    Jiunge na wenzako watatu na mworodheshe vielezi vyote vilivyomo kifunguni humu
    huku mkivitungia sentensi fupi na sahihi.
    Gakwerere alikuwa mfugaji mwenye bidii nyingi sana tangu zamani. Mwanzoni,
    Gakwerere alikuwa akifuga ng’ombe wa kienyeji. Aliwalisha ng’ombe hao uwanjani
    na pembeni mwa mashamba. Hata hivyo, ng’ombe hao hawakuwa wakimpa kiasi
    cha maziwa alichotarajia. Angewakamua mara moja tu kwa siku. Alikata shauri
    kuanzisha ufugaji wa ng’ombe bora wa maziwa.
    Mfugaji huyu aliwapeleka ng’ombe wake wa kienyeji sokoni na kuwauza mnamo
    Novemba. Baada ya kuwauza, aliamka alfajiri na kufunga safari ya kuzuru shamba
    la kisasa la Nyinawumuntu. Bi. Nyinawumuntu alikuwa mfugaji na mkulima
    mashuhuri sana katika eneo hilo alilokaa Gakwerere. Alipofika huko, alimpata
    bibiye yupo na wakaanza kupiga bei. Baada ya kukubaliana bei, alinunua mitamba
    wawili kwa bei nafuu. Alilipa papo hapo kwa sababu hakutaka kuwa na deni.
    Kumaliza hivi tu, yule bibi alimpa Gakwerere gari lake ili alitumie kuwasafirisha
    ng’ombe wake. Gakwere alimshukuru kwa wema wake na akawasafirisha hao
    mitamba wake hadi kwake.
    Alipofika nyumbani kwake, mfugaji huyo alianza kuwalisha ng’ombe wake kwa njia
    za kisasa. Kwa kuwa walikuwa wakilishwa kwa lishe bora ya ng’ombe, haukuchukua
    muda mrefu kuwapandisha. Muda ulipowadia, walizaa ndama wawili wenye afya
    nzuri.
    Baada ya muda usio mrefu, Gakwerere alianza kuvuna matokeo ya jasho lake la kila
    siku. Hakuamini kiasi cha maziwa alichokuwa akikama kila asubuhi na jioni.
    Aliweka akiba kwa muda. Hatimaye, mfugaji huyu alinunua gari. Alitumia gari hilo
    kuwatafutia na kuwabebea chakula ng’ombe hao wake wa gredi.

    E . Matumizi ya wakati uliopo na uliopita na vitenzi vya silabi moja
    i) Matumizi ya wakati uliopo (-na-) na vitenzi vya silabi moja
    Wakati uliopo -na-unaweza kuwa katika hali mbili: Hali hizo ni hali yakinishi na hali
    kanushi. Hali yakinishi ni ya ukubali na hali kanushi ni ya ukatavu.
    Soma sentensi hizi.

    Hali yakinishi
    Hali yakinishi ni hali ya kukubali. Tazama tena mifano iliyopo hapo juu. Vitenzi
    unakufa, anakula, anakunywa, anakuja, anampa na inanyesha vimo katika hali
    yakinishi, yaani hali ya kukubali.
    Hali kanushi
    Nayo hali kanushi ni hali ya kukataa. Itazame tena mifano hapo juu. Vitenzi haufi,
    hali, hanywi, haji, hampi na hainyeshi vipo katika hali kanushi, yaani hali ya kukataa.

    Unaweza kutunga sentensi zaidi za namna hii kama ifuatavyo:

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwenzako. Tafuteni vitenzi zaidi vyenye silabi moja katika kamusi huku
    mkijadiliana mabadilko ambayo hutokea vitenzi hivyo vinapotumiwa katika hali
    kanushi na yakinishi.

    ii) Matumizi ya wakati uliopita -li- na vitenzi vya silabi moja
    Wakati uliopita huonyesha kuwa kitendo kilifanyika muda mrefu uliopita. Wakati
    huu huwakilishwa na -li-. Vitendo husika vinaweza kuwa katika hali yakinishi au
    kanushi. Kama ujuavyo, hali yakinishi ni ya kukubali na hali kanushi ni kukataa.

    Tazama mifano ifuatayo:

    Vitenzi hivyo vipo katika wakati uliopo. Tunaweza kuvigeuza viwe katika wakati
    uliopita kwa kuweka ‘-li-‘ mahali pa ‘-na-‘. Tunapofanya hivyo, tunamaanisha kuwa
    vitendo hivyo vilifanyika muda au wakati uliopita. Tazama jedwali hili.

    Tazama mifano ifuatayo:


    Katika jedwali lililopo hapo juu, vitenzi ulikufa, alikula, alikunywa, alikuja, alimpa,
    na ilimnyeshea vimo katika hali yakinishi au kukubali kwa wakati uliopita. Navyo
    vitenzi haukufa, hakula, hakunywa, hakumpa, haikumnyeshea vimo katika hali ya
    kukataa yaani hali kanushi.

    Mazoezi ya ziada

    Zoezi A

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako na mworodheshe vitenzi vinane vya silabi moja
    huku mkivitungia sentensi sahihi katika wakati uliopita. Sentensi zenu zihusiane na
    kilimo na ufugaji. Someaneni vitenzi na sentensi huku mkisahihishiana.

    Zoezi B

    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Msomeane tungo au hadithi
    mbalimbali zilizopo katika kitabu hiki na vitabu vingine. Mbainishe na kuainisha aina
    za maneno katika tungo hizo (vivumishi, viwakilishi na vielezi) kama vinavyotokea
    katika umoja na wingi pamoja na matumizi ya wakati uliopo na wakati uliopita.
     
                              Maswali ya marudio
    li kujikumbusha mengi ya yale uliyojifunza katika sehemu hii, yajibu vilivyo maswali
    haya yafuatayo yote.
    1. Bila ya kuangalia popote, taja maneno kumi yanayohusu mazao na kumi
        yanayohusu ufugaji huku ukiyaeleza.
    2. Ipo misimu mingapi hapa Rwanda? Ieleze huku ukirejelea upanzi na uvunaji
        wa mimea.
    3. Tazama picha zifuatazo. Eleza misimu kulingana na kila mchoro.

    4. Tunga sentensi sahihi ukitumia msamiati ufuatao:
        a) mahindi
        b) ndizi
        c) kahawa
        d) viazi mviringo
        e) maharagwe
        f ) njugu
    5. a) Jaza kila pengo kwa jina sahihi la kifaa cha kilimo.
         i) Ndoli anafyeka shamba kwa ______________.
        ii) Mkulima yule anatumia _________ la mkono kulimia shamba lake.
       iii) Shamba kubwa hulimwa kwa _______________.
       iv) __________ hutumiwa kukata matawi ya miti shambani.
    6. Tunga sentensi tano fupi ukitumia vifaa mbalimbali vya kilimo ambavyo vinatumiwa katika eneo utokako.
    7. Eleza jinsi unavyopanga kupiga vita uchochole kwa kilimo cha kisasa.
    8. Taja majina kumi ya mifugo nchini Rwanda na uyatungie sentensi sahihi.
    9. Taja chuo cha kilimo hapa nchini ambacho ungependa kukiingia baada ya
         masomo yako huku ukieleza ni kwa nini unakistahi chuo hicho.
    10. Eleza umuhimu wa ufugaji katika jamii unapotoka.
    11. Zipo tamaduni zozote za kikwenu zihusuzo kilimo na ufugaji? Zitaje
         huku ukieleza huo uhusiano.
    12. Taja wanyama kumi wa porini wanaopatikana nchini Rwanda.
    13. Andika majina na sifa za wanyama wafuatao wa porini:

    14. Eleza faida za wanyama wanaoishi porini.
    15. Pendekeza njia zinazoweza kutumiwa kuwavutia watalii wanaozuru mbuga
          zetu za wanyama wa porini.
    16. Eleza maana ya:
         a) nomino
         b) vivumishi
         c) vielezi
         d) viwakilishi
    17. Huku ukitoa mifano, eleza aina nne nne za:
        a) nomino
        b) vivumishi
        c) vielezi
    18. a) Je, vitenzi vya silabi moja ni maneno ya aina gani?
          b) Andika mifano minne ya maneno yenye silabi moja na uyatungie sentensi sahihi.
    19. a) Huku ukitoa mifano, eleza tofauti zilizopo kati ya:
           i) wakati uliopo na wakati uliopita
          ii) hali kanushi na yakinishi
    b) Andika sentensi zifuatazo katika hali yakinishi au kanushi.
        i) Baba anakula mahindi.
       ii) Mahindi hayafi wakati wa kiangazi.
      iii) Ng’ombe hakunywa maji jana.
      iv) Mkulima alimpa ndizi nyingi.
    c) Andika sentensi zifuatazo katika wakati uliopo au uliopita.
       i) Ndoli anakula mihogo.
      ii) Mimi sinywi maziwa.
     iii) Mama alinipa jembe.
     iv) Kuku hao hawakufa.
    20. Kwa ufupi, elezea mambo muhimu uliyojifunza katika sura hii na useme jinsi
          yatakavyokufaidi na jamii.
    Files: 3
  • Sura 2: Utungaji

     

    Mada ndogo: Barua kuhusu matembezi, Barua za kirafiki,

                          Barua za mwaliko, Simu,Tangazo/Ilani.


    A Barua
    Barua ama waraka ni maandishi yaliyopangwa kwa utaratibu na mtiririko maalumu
    kwa minajili ya kuwasilisha ujumbe fulani. Zipo aina mbili kuu za barua: Ipo barua
    ya kirafiki ambayo pia huitwa barua ya kindugu na ipo barua rasmi.
    a) Barua za kirafiki
    Barua ya kirafiki ni barua ambayo huandikiwa mtu ama watu mbalimbali walio na
    uhusiano wa karibu na anayeandika; kama vile rafiki, mzazi, dada na kadhalika.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwenzako na mjadili barua zenu mlizoandika. Je, waandikiwa walikuwa
    kina nani? Ujumbe ulikuwa upi na ni lugha gani uliyotumia?

    Mifano ya barua za kirafiki
    i) Barua ya mwana kwa mzazi

                                                     

    Ukimwandikia mama barua, barua hiyo ni ya kirafiki

    Zoezi

    Mwandikie ndugu yako barua ukimweleza maendeleo yako katika masomo.
    ii) Barua ya mapenzi

                                      

                  

    Barua ya kindugu inaweza kuwa ya mapenzi pia.

    Zoezi

    Jifanye kuwa una zaidi ya miaka kumi na minane. Mwandikie mchumba wako barua
    ukimweleza sababu ya kumpenda na kutaka kumwoa.

    ii) Barua ya kutoa ushauri
    Isitoshe, barua ya kirafiki inaweza kuwa ni ya mzazi anayetoa ushauri kwa mwanawe.


    Zoezi

    Wewe ni mzazi ambaye mwanao amepotoka. Mwandikie barua ya
    kumwelekeza kuepukana na upotovu huo na arudie wema wake wa awali.
    Someni barua zenu mbele ya darasa.

    Sehemu kuu za barua za kirafiki

    Barua za kirafiki huwa na sehemu au muundo fulani maalumu.

    Kazi ya kikundi

    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Tazameni mifano ya barua za kirafiki iliyotolewa na mingineyo. Jadilianeni kuhusu sifa zinazofanana katika barua zote. 

    Tazama mfano wa muundo wa barua ya kirafiki. Kuna uhusiano gani kati ya yaliyomo na barua za kirafiki ulizosoma? 

             Anwani

            Tarehe 

            Kutaja mwandikiwa

            Utangulizi/salamu 

            Mwili wa barua           

            Hitimisho  

            Jina la mwandishi.

    Barua ya kirafiki huwa na sehemu kuu zifuatazo:
    i) Anwani moja ya mwandishi: Huandikwa juu, pembeni.
    ii) Tarehe: Huandikwa chini ya anwani kwa kuacha nafasi ya mstari mmoja.
    iii) Kutaja mwandikiwa: Huja chini ya tarehe kwa kuacha nafasi ya mstari mmoja.
    iv) Utangulizi: Hujitokeza katika aya ya kwanza. Mwandishi humjulia hali mtu
         anayeandikiwa na wenzake. Pia, husema hali yake.
    v) Mwili wa barua: Mwandishi hupitisha ujumbe wa barua/kuelezea kiini cha
        kuandikwa kwa barua husika.
    vi) Hitimisho/Kufunga barua: Mwandishi huhitimisha barua yake kwa kumtakia
         heri aliyeandikiwa. Jina la mwandishi wa barua huja chini ya hitimisho.

    Zoezi

    Tazama barua iliyopo hapa chini. Je, barua hii ina makosa gani? Andika upya barua
     hii kwa kusahihisha makosa yaliyopo na kuongezea sehemu zinazokosekana.

    Kwa Shangazi Mpendwa,
    S.L.P, 45
    Kigali
    Rwanda

    Wako Mpendwa,

    Ninajua wewe unapenda sana kilimo cha ndizi. Juzi tulisoma kuhusu kilimo bora
    cha ndizi. Mwalimu wetu alitufunza mbinu mpya za kupanda ndizi. Tukifunga,
    nitakutembelea ili nikufunze mbinu hii mpya itakayokupa mavuno mengi zaidi.

    Unisalimie wote waliopo nyumbani. Waambie nitawatembelea wakati wa likizo.

    Kwanza, ningependa kukueleza kuwa ninazidi kutia bidii katika masomo. Juzi
    tulifanya majaribio na niliibuka nafasi ya tatu katika darasa letu. Ninatia bidii zaidi.
    U hali gani? Mimi nipo salama. Nia yangu kuu ya kukuandikia barua hii ni kukujulisha
    kuhusu mambo mawili makuu.

    Kanuni za kuzingatiwa katika uandishi wa barua za kirafiki
    Zipo kanuni mbalimbali za kuzingatiwa wakati wa kuandika barua ya kirafiki.
    Soma kifungu kifuatacho ili kubainisha baadhi ya kanuni hizo.

                  

    USANASE: Hujambo, Gabiro?
    GABIRO:     Sijambo Usanase.
    USANASE: Unaonekana mwingi wa huzuni. Pana jambo linalokutatiza?
    GABIRO:    Ni kweli. Ninataka kuandika barua kwa mjomba. Sijui endapo pana
                        kanuni zozote ninazofaa kuzingatia.
    USANASE: Ahaa! Zipo kanuni za kufuatwa wakati wa kuandika barua ya kirafiki.
    GABIRO:    Kanuni hizo ni gani?
    USANASE: Kwanza, hufai kuandika kichwa.
    GABIRO:    Niandike tu moja kwa moja?
    USANASE: Naam. Kabla ya kuandika kiini au mwili wa barua, hakikisha kuwa
                        umeandika anwani yako kama mwandishi.
    GABIRO:    Anwani moja inatosha?
    USANASE: Naam. Chini ya anwani, andika tarehe kisha umtambulishe unayemwandikia.
    GABIRO:    Ninaweza kumtambulisha vipi?
    USANASE: Mtambulishe kwa kudhihirisha uhusiano uliopo baina yenu. Kwa
                        mfano, Kwa Mjomba Mpendwa.
    GABIRO:    Ahaa! Ninakupata vizuri sana. Je, ninafaa kujikita katika ujumbe
                        mmoja mkuu?
    USANASE: Hapana. Una uhuru wa kuzungumzia maudhui mengi. Unaweza
                        kutaja mambo mengi yasiyohusiana. Mfano, unaweza kumwambia
                        kuhusu hali ya anga na masomo shuleni. Baadaye, unaweza
                        kumwuliza kuhusu mazao yake yalivyo shambani na mambo mengi.
                        Uhakikishe kuwa kila maudhui au ujumbe upo katika aya yake.
    GABIRO:    Ninafaa nitumie kiwango gani cha lugha?
    USANASE: Hujafungwa katika kiwango fulani cha lugha. Lugha utakayotumia
                        inategemea uhusiano uliopo kati yako na mjomba au yeyote
                        unayemwandikia.
    GABIRO:    Kwa hivyo si lazima lugha yangu iwe rasmi?
    USANASE: Naam. Si lazima uzingatie kiwango cha juu cha adabu kama ilivyo
                        katika barua rasmi. Hilo halimaanishi kuwa unaruhusiwa kutumia lugha chafu au
                        lugha isiyokuwa na tasfida.
    GABIRO:    Kwa hivyo ninaweza kutumia lugha yenye utani, vichekesho na yenye
                        kuibua hisia ya huzuni, furaha au huruma.
    USANASE: Naam.
    GABIRO:    Je, ninafaa kuzingatia urefu kiasi gani?
    USANASE: Kama nilivyosema hapo mbeleni, una uhuru wa kuzungumzia
                        mambo mengi utakavyo katika barua ya kirafiki. Urefu utategemea
                        jumla ya mambo hayo. Una uhuru wa kuandika barua ndefu au fupi
                       utakavyo. Hakuna urefu maalumu.
    GABIRO:    Nikimaliza, ninafaa kutia sahihi?
    USANASE: La hasha! Barua ya kirafiki si lazima itiwe sahihi.
    GABIRO:     Asante sana rafiki yangu kwa maelezo hayo. Sasa ninaweza kuandika
                        barua yangu.
    USANASE: Karibu. Ukiwa na swali lingine, utaniuliza.

    Zoezi

    Jiunge na mwenzako na muigize mazungumzo yaliyopo hapo juu. Andikeni kanuni za kuzingatiwa katika uandishi wa barua za kirafiki zilizopo kwenye ufahamu.

    Kazi ya kikundi

    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Andikianeni barua za kirafiki kuhusu mada yoyote mpendayo. Someni barua zenu huku mkisahihishiana.

    b) Barua rasmi

    Tazama michoro hii. Je, mwalimu na wanafunzi hawa wanajadiliana kuhusu nini?
    Je, unajua jinsi ya kuandika barua rasmi?

                            

    Barua rasmi ni barua zinazoandikiwa mtu au watu wenye nyadhifa kwa lengo
    maalumu la kuwasilisha ujumbe rasmi.Mifano ya barua rasmi.

    i) Barua ya kuomba kazi

    Hii ni aina ya barua ambayo mtu huandika wakati anapotaka kuajiriwa mahali. Kuna aina mbalimbali za barua za kuomba kazi.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili

    Jiunge na mwenzako. Jadilianeni kuhusu jinsi ya kuandika barua ya kuomba kazi. Andikeni barua hiyo kwa msingi wa majadiliano hayo.


    Zoezi

    Andika barua ya kuomba kazi yoyote upendayo. Angazia mambo yafuatayo katika barua yako:

    i) jinsi ulivyopata kuwepo kwa nafasi ya kazi hiyo,
    ii) tajiriba yako, wasifu wako mfupi,
    iii) sababu ya kutaka kazi hiyo,
    iv) mambo mapya ambayo utafanya ukipewa nafasi hiyo na kadhalika.                                                                                                                                                                                                                                                                                      

    ii) Barua ya kuomba ruhusa

    Hii ni aina ya barua ambayo mwandishi huomba kupewa fursa ya kutoshiriki katika shughuli fulani muhimu. Unaweza kusema kwa nini hutakuwepo au usiseme. 



    Zoezi

    Mwandikie mwalimu wako barua ukiomba ruhusa yoyote. Mweleze sababu za kuomba ruhusa hiyo.                                              

    iii) Barua ya huduma

    Barua ya huduma ni aina ya barua ambayo humhitaji mtu, kundi la watu, shirika lisilo la kiserikali au idara ya serikali au kampuni kutoa huduma fulani katika jamii. Wakati mwingine huandikwa kutoa maoni kuhusu hatua ambazo jamii ingependa kuchukuliwa, kwa mfano, idara ya polisi ama hospitali kuweka visanduku vya kupokea maoni kutoka kwa wananchi kuhusu namna wangependa kuhudumiwa kwa ubora zaidi.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Nyinyi ni vijana wanaojihusisha katika
    kufanya utafiti wa mbinu bora za kilimo katika wilaya yenu. Kipeni kikundi chenu
    jina na mchague katibu mkuu. Andikeni barua kwa shirika lolote linalojihusisha
    na kilimo katika eneo lenu. Elezeni shirika hilo kuhusu utafiti mliofanya wa kukuza
    kilimo katika wilaya yenu na msaada mnaohitaji kutoka kwao.

    Aina zaidi za barua rasmi
    Mbali na mifano iliyotolewa, zipo aina zaidi ya barua rasmi. Barua hizo ni kama vile:
    i) Barua ya kuomba nafasi katika shule fulani
    ii) Barua ya kuomba msamaha
    iii) Barua ya shukrani
    iv) Barua ya malalamiko
    v) Barua kwa mhariri
    vi) Barua ya mapendekezo
    vii) Barua ya uteuzi
    viii)Barua ya kusimamishwa au kufutwa kazi.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Fanyeni utafiti kuhusu jinsi barua zilizotajwa
    hapo juu huandikwa. Kila mwanafunzi aandike mojawapo ya barua hizo kuhusu
    mada yoyote kisha amsomee mwenzake. Sahihishianeni.

    Sehemu kuu na kanuni za barua rasmi
    Barua rasmi huwa na sehemu au muundo fulani maalumu kama ufuatao:
    Anwani ya mwandishi
    Tarehe
    Anwani ya mwandikiwa
    Mtajo/Kutaja mwandikiwa kwa heshima
    Kichwa
    Utangulizi/Kutajwa kwa kiini
    Mwili wa barua
    Hitimisho
    Wako mwaminifu/mtiifu
    Sahihi
    Jina la mwandishi
    Cheo cha mwandishi (ikiwa mwandishi anaandika
    kwa niaba ya shirika fulani, kikundi au kampuni)

    Soma mazungumzo haya na ujibu maswali chini yake.
                                          

    UMUHIRE: Mwenzangu, nieleze kuhusu jinsi ya kuandika barua rasmi.
    NDOLI:       Lazima uandike anwani yako na ile ya mwandikiwa. Anwani yako
                       kama mwandishi huja juu. Unapoandika anwani ya mwandikiwa, ni
                       sharti uandike cheo chake kwanza kabla ya kuandika jina na anwani
                       ya kampuni chini ya cheo chake kama vile,  'MKURUGENZI MKUU,
                       MWENYEKITI, MWALIMU MKUU’ na kadhalika.
    UMUHIRE: Baada ya anwani, ninaandika nini?
    NDOLI:      Unaandika ufunguzi wa barua kama vile Kwa Mbunge Mheshimiwa,
                       Kwa Mheshimiwa, Kwa Meneja Mkuu, Kwa Meneja, Kwa Mgeni wa
                       Heshima na kadhalika. Unaweza kuandika jina lake la pili baada ya
                       Bw au Bi.
    UMUHIRE: Naam! Kwa hivyo, baada ya kutambulisha mwandikiwa, ninaandika
                       kichwa au vipi?
    NDOLI:       Naam, rafiki yangu. Kichwa hudokeza kiini cha kuandika barua yako.
                       Unapoandika kichwa, unaanza kwa kutumia kifupisho MINT: au KUH:
    UMUHIRE: MINT na KUH vinasimamia nini?
    NDOLI:       MINT husimamia Mintaarafu au kwa mintaarafu ya, KUH husimamia
                       kuhusu. Kichwa au mada yako haifai kuzidi maneno sita isipokuwa
                       pale ambapo pana lazima.
    UMUHIRE: Ninapoanza kuandika mwili, ninafaa kusema nini?
    NDOLI:      Ikiwa ni barua ya kuomba kazi, ni vizuri uanze kwa kurejelea tangazo
                      la kazi hiyo au jinsi ulivyopokea kuwepo kwa nafasi hiyo. Baadaye,
                      andika moja kwa moja kiini cha barua hiyo.
    UMUHIRE: Hakuna salamu?
    NDOLI:       Naam. Barua rasmi haina salamu. Unaeleza moja kwa moja kiini
                       cha kuandika barua. Unafaa kujikita katika ujumbe mmoja mkuu,
                       yaani jambo linalokufanya uiandike barua hiyo. Ikiwa unaomba kazi,
                       toa maelezo muhimu kukuhusu. Maelezo hayo yawe na uhusiano na
                       kazi unayolenga kupata. Epuka maelezo mengi yasiyokuwa na manufaa.
    UMUHIRE: Lugha yangu inafaa kuwa ya namna gani?
    NDOLI:       Lugha yako sharti izingatie adabu ya hali ya juu na kiwango cha juu cha urasmi.
                       Lugha yako iwe sahihi. Ikiwa unaandika kwa kalamu, tumia hati nadhifu. Usitaje
                       chochote cha kuonyesha mambo au hisia za kibinafsi au uhusiano wa kibinafsi
                       na unayemwandikia.
    UMUHIRE: Nini huandikwa katika hitimisho la barua hii rasmi?
    NDOLI:       Unaandika tumaini lako la majibu mazuri. Chini yake, unaandika:
                       Wako Mwaminifu au Wako Mtiifu kisha unaweka sahihi. Chini ya sahihi yako,
                       andika jina lako kamili. Ikiwa unaandika kwa niaba ya shirika au kampuni au kikundi,
                       andika cheo chako chini ya jina lako.
    UMUHIRE: Asante kwa maelezo haya.

    Maswali
    i) Je, barua rasmi ina kanuni zipi za kuzingatiwa?
    ii) Linganisheni sehemu na kanuni za kuandika barua za kirafiki na zile za
        kuandika barua rasmi. Jadilianeni kuhusu tofauti zilizopo kati ya barua za
        kirafiki na barua rasmi.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako. Tazameni mifano ya barua rasmi iliyotolewa na
    mingineyo. Jadilianeni kuhusu miundo ya barua hizo. Andikianeni barua rasmi
    kuhusu mada yoyote.
        
      B. Matangazo mbalimbali                             
    Tangazo ni mpangilio wa maandishi
    kwa mtindo maalumu kwa lengo la
    kupasha ama kupokeza ujumbe fulani
    wa kidharura au muhimu.
    Zipo aina mbalimbali za matangazo:

    i) Matangazo ya biashara
    Matangazo ya biashara ni maandishi
    ambayo yanalenga kutoa maelezo fulani
    kuhusu kitu, bidhaa, mahali au jambo
    kwa ajili ya kuwashawishi wasomaji
    kununuana kutumia bidhaa husika au

    kuzuru mahali husika. Matangazo haya yanaweza pia kuwajulisha watu kuhusu bidhaa mpya zilizoingia sokoni au kuimarishwa kwa bidhaa zilizopo kwa sasa.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Tajeni matangazo mbalimbali
    yaliyomo katika redio, televisheni, magazeti na vibango mbalimbali karibu na
    maeneo mnapoishi. Jadilianeni kuhusu jinsi istilahi au msamiati ulivyotumika
    katika matangazo hayo na malengo ya matangazo hayo. Je, istilahi hizo zimefaulu
    katika kuafikia malengo husika?



    Jinsi ya kufika huko
    Unaweza kusafiri angani kwa ndege hadi uwanja wa ndege wa Gisenyi. Hapo,
    waajiri wetu watakupokea kwa tabasamu na unyenyekevu.
    Ikiwa una gari, pitia barabara kuu ya Kaskazini Magharibi kutoka jijini Kigali.
    Itakuchukua saa tatu pekee.
    Tembelea hoteli ya Sabyinyo leo upate uhondo wa burudani.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Someni tena matangazo yaliyopo hapo juu kwa
    makini huku mkitambua sifa na miundo ya matangazo hayo.

    Sifa na miundo ya matangazo ya biashara
    Soma kifungu hiki na ujibu maswali chini yake.
    Matangazo ya biashara huwa na utangulizi wenye mvuto na hitimisho lenye
    ushawishi. Kumbuka kuwa lengo kuu la tangazo lolote la biashara ni kuwavutia
    wasomaji.
    Yapo matumizi ya takriri. Takriri ni kurudiarudia neno au maneno fulani. Kwa kuwa
    matangazo ya biashara hulenga kutambulisha bidhaa fulani au mahali fulani, bidhaa
    au mahali husika hurudiwarudiwa katika mwili wa tangazo ili wasomaji au wateja
    lengwa wazikumbuke. Pia, jina la bidhaa na kampuni hutajwa na kurudiwarudiwa.
    Watu hupenda sana kusoma maneno mafupi na ni rahisi kuyakumbuka. Maneno
    marefu kwa upande mwingine huchosha na huchukua nafasi kubwa. Matangazo
    ya biashara huandikwa kwa maneno mafupi mafupi yenye mnato na ujumbe mzito.
    Maneno mafupi hupunguza gharama ya matangazo hayo.
    Katika matangazo ya biashara kwenye redio na televisheni, matangazo hayo
    huambatana na sauti ya kimuziki. Sauti hiyo hulenga kuwavutia wanaosikiza
    matangazo hayo. Pia, huchangia katika kupitisha ujumbe uliokusudiwa.
    Wakati mwingine, matangazo hufuata mtindo wa dayalojia. Hapa, watu
    wanaohusika katika kutangaza bidhaa fulani huulizana maswali na kupashana
    ujumbe. Kwa mfano
    MTU I: Je, umejaribu sabuni hii?
    MTU II: Bado
    MTU I: Ijaribu leo. Hii ndiyo suluhisho ya kudumu kwa madoa sugu.
    Matangazo ya biashara pia hutumia lugha ya kushawishi. Lugha hiyo huwa sahihi
    au hukosa usahihi. Lugha inayotumika hutegemea umri, jinsia ya wanunuzi
    wanaolengwa.
    Matangazo ya biashara hueleza ubora wa bidhaa pekee na manufaa yake. Hutilia
    mkazo mambo haya kwa undani na wakati mwingine hutilia chumvi ubora na
    manufaa ya bidhaa husika.
    Matangazo mengi ya biashara hayataji bei ya bidhaa. Pia, hueleza zinakopatikana
    bidhaa zenyewe au jinsi ya kuzipokea mahali unapoishi. Wakati mwingine, hutoa
    mwito wa kutembelewa kampuni husika.

    Zoezi

    1. Taja sehemu kuu za matangazo ya biashara kwa mujibu wa kifungu na
         matangazo ya biashara uliyosoma au kusikia.
    2. Taja kanuni au sifa kuu za kuzingatiwa katika uandishi wa matangazo ya
         biashara.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Fanyeni mradi wa kuandika
    matangazo mbalimbali ya biashara kuhusu bidhaa mtakazojichagulia.

    ii) Matangazo ya mkutano
    Katika matangazo haya, mwandishi hutaja kiini au ajenda za mkutano, mahali pa
    mkutano, tarehe na wakati ambapo mkutano utaandaliwa na maelezo mengine
    muhimu.


    iii) Matangazo kuhusu ziara ya rais
    Ziara ni tendo la kwenda mahali kwa sababu fulani kama vile kuzindua ujenzi wa
    barabara, kuwahutubia wananchi na kadhalika. Nalo tangazo lake linaweza kuwa
    kama hili lifuatalo:


    Zoezi

    Liandike tangazo kwa watu wote waliomo shuleni mwenu kuhusu ziara ya
    waziri wa elimu shuleni humo. Liandike tangazo hilo kwa niaba ya mwalimu mkuu.

    iv) Matangazo ya kuwachagua watu kujiunga na kikosi cha polisi
    Huweza kutokea kwamba serikali inataka kuchagua watu kujiunga na kikosi cha
    polisi. Basi, huweza kulitangaza jambo kwa wananchi.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Someni tangazo lililopo hapo juu na matangazo
    mengineyo ya mikutano. Jadilianeni kuhusu sehemu muhimu za matangazo ya
    mikutano na kanuni za kuzingatiwa katika uandishi wa matangazo maalumu.

    v) Matangazo kuhusu nafasi za kazi
    Hutolewa kwa lengo la kufahamisha watu kuhusu kuwepo kwa nafasi fulani ya/za
    kazi katika kampuni, shirika ama idara fulani.

    Mfano

    HALMASHAURI YA WILAYA YA NYAGATARE
    Tarehe 3/07/2016.
    NAFASI ZA KAZI
    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyagatare anatangaza kuwepo
    kwa nafasi zifuatazo za kazi:
    1. MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA (Nafasi 1)
    Sifa za Mwombaji kazi
    Ni sharti awe:
    i) mkazi wa muda mrefu wa Wilayani Nyagatare,
    ii) na shahada ya uzamifu katika usimamizi,
    iii) mwenye umri wa miaka 35 au zaidi,
    iv) na tajiriba ya miaka 5 katika kusimamia watu katika shirika kubwa tajika,
    v) na rekodi nzuri ya utendakazi,
    vi) mwenye uwezo wa kuwatia motisha wafanyakazi ili kuinua hadhi ya bodi hii,
    vii) mtu mwenye kutoshawishika katika misimamo sahihi yake na ile ya
          halmashauri.
    Wajibu na majukumu
    i) Kutangaza nafasi za ajira,
    ii) Kupendekeza kupandishwa vyeo kwa wafanyakazi,
    iii) Kutoa mafunzo au maelekezo kwa waajiriwa wapya,
    iv) Kupendekeza nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi,
    v) Kutekeleza majukumu mengineyo kama itakavyopendekezwa mara kwa mara.

    Kiwango cha mshahara
    Kitajadiliwa wakati wa mahojiano.
    2. MAAFISA WA UCHUKUZI DARAJA LA II ( Nafasi 5)

    Sifa za mwombaji kazi
    Ili kufuzu katika nafasi hii, unahitajika kuwa na:
    i) shahada katika masuala ya usimamizi wa kibiashara,
    ii) tajiriba ya miaka 3 katika kitengo hiki,
    iii) uelewa wa masuala ya uchukuzi katika forodha na kanuni za barabara,
    iv) rekodi nzuri ya utendakazi,
    v) ufahamu wa matumizi ya kompyuta na mtandao.

    Majukumu
     i) Kutayarisha bajeti na kuendesha uchukuzi,
    ii) Kuhakikisha kuwa takwimu, stakabadhi na kumbukumbu zinazohusu vyombo
        vya usafiri pamoja na mitandao yake zinatunzwa vyema,
    ii) Kukusanya na kuandaa takwimu kuhusu maendeleo ya sekta ya uchukuzi na
        kuziwasilisha kwa wadau ndani na nje ya wilaya,
    iv) Kuweka faili za uchukuzi nchini,
    v) Kukadiria na kushauri juu ya utendaji wa miradi mbalimbali ya sekta ya
        uchukuzi.

    Kiwango cha mshahara
    Kitajadiliwa wakati wa mahojiano.

    Ikiwa una sifa hizi na ungependa kujiunga nasi, tuma barua ukionyesha kazi
    unayoomba na uambatanishe wasifukazi wako wa hivi karibuni, nambari ya/za
    simu na warejelewa watatu kwa mawasiliano wakati wa mchana. Tuma kwa anwani
    hii kabla ya usiku wa manane ya tarehe 23/08/2016.
    J.M. Gatete,
    Halmashauri ya Wilaya ya Nyagatare,
    S.L.P. 3013,
    NYAG ATA R E .    
    Tanbihi
    Halmashauri hii ni huru katika utoaji wa nafasi sawa za kazi bila kubagua yeyote.
    Ombi litakataliwa moja kwa moja endapo anayeomba kazi atahonga afisa yeyote
    kwa ajili ya kupendelewa.

    Zoezi

    Tafuta matangazo mbalimbali kuhusu nafasi za kazi katika magazeti, mabango na
    kadhalika. Soma matangazo hayo na ubainishe sifa zayo na kanuni zilizozingatiwa
    katika uandishi huo.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Huku mkirejelea matangazo
    mbalimbali, jadilianeni kuhusu tofauti zilizopo katika matangazo hayo mkizingatia:
    i) sifa
    ii) sehemu kuu
    iii) kanuni
    iv) msamiati
    v) malengo

    C . Ilani
    Ilani ni tangazo ambalo hutahadharisha au kuarifu kuhusu aina ya jambo ama tukio
    ambalo linastahili kuepukwa, lau sivyo madhara hutokea.
    Ilani huwa na wazo moja tu maalumu. Hutolewa mahali penye shughuli nyingi ama
    palipo na watu wengi kama vile shuleni, chuoni, kanisani msikitini na kadhalika.
                      
    Ilani mara nyingi huwa na mtindo rasmi. Ilani nyingi huwekwa katika mabango
    makubwa, magazetini, kwenye majarida na kadhalika.

    Mifano

    i) Ilani kuhusu mkurupuko wa ugonjwa
    ILANI
    WIZARA YA AFYA, KUPITIA HOSPITALI KUU YA MKOA,
    INAWATANGAZIA KUZUKA KWA UGONJWA HATARI WA
    KIPINDUPINDU.
    WATU WOTE WANASHAURIWA KUZINGATIA USAFI WA MWILI NA MAZINGIRA.
    ILI KUJIKINGA KUTOKANA NA MAAMBUKIZI YA UGONJWA HUU
    HATARI, MAMBO YAFUATAYO NI SHARTI YAZINGATIWE:
    i) KILA MTU AHAKIKISHE ANATUMIA CHOO.
    ii) KILA MTU ANAWE MIKONO KWA MAJI SAFI NA SABUNI BAADA YA KUTOKA CHOONI.
    iii) HAKIKISHA UNAKULA KATIKA MAHALI SAFI
    iv) WATU WASILE KWENYE MIKAHAWA.
    v) ALIYE NA DALILI ZA KUENDESHA NA KUTAPIKA AKIMBIZWE MARA
        MOJA HOSPITALINI KWA UCHUNGUZI NA MATIBABU.
    vi) ALIYEAMBUKIZWA APEWE MAJI MENGI YA KUNYWA WAKATI
         ANAPOPELEKWA HOSPITALINI.
    vii) KILA MTU ACHEMSHE MAJI YA KUNYWA.
    viii)MTU YEYOTE ALIYEAMBUKIZWA ATENGWE NA WATU WENGINE.
          ONYO:
    MTU YEYOTE ATAKAYEPATIKANA AKIUZA CHAKULA KATIKA
    MAENEO WAZI ATASHTAKIWA.

    ii) Ilani kuhusu unywaji wa pombe

    Mfano

    POMBE HATARI
    Serikali, kupitia wizara ya afya, inawatahadharisha wananchi kuhusu kuzuka kwa
    pombe hatari ya SUMEDA inayonywewa sana katika sehemu mbalimbali nchini.
    SUMEDA ni pombe hatari kwa afya yako kwa kuwa inatengenezwa kwa kutumia
    dawa ya kuhifadhi maiti na kemikali nyingine hatari.
    Pombe hii hatari imesababisha vifo vya watu zaidi ya 50, kuwapofusha
    wengine wengi pamoja na kutoa mimba.
    Atakayepatikana akiuza ama kunywa aina hii ya pombe atakamatwa.
    Ofisi ya mkuu wa wilaya.

    iii) Ilani ya kutokanyaga nyasi

    Mfano

                                                  ILANI
                          HAPANA RUHUSA KUKANYAGA NYASI
                                             NA MENEJIMENTI

    Zoezi

    i) Tazama mifano ya ilani zilizotolewa hapo juu. Je, ilani hizo zina sifa gani?
    ii) Andika ilani kuhusu mada yoyote upendayo.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Andikeni ilani kuhusu mada hizi na mziweke
    kwenye maeneo husika shuleni.
    i) Kutokanyagwa kwa sehemu fulani zenye nyasi.
    ii) Kuwepo kwa mjadala kuhusu: mbinu za kisasa za kilimo ni bora kuliko mbinu
        za jadi za kilimo.
    iii) Kuwafahamisha wanafunzi kunawa mikono watokapo msalani.
    iv) Kuzingatia usafi jikoni

    D. Mialiko
    Mwaliko ni mwito wa kumtaka mtu au watu kuhudhuria shughuli au hafla fulani.
    Wito wa namna hii huweza kufanywa kwa njia ya barua ya kirafiki au barua rasmi
    na hata kwa matangazo.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako na mchunguze mchoro huo uliopo hapo chini.
    Jadilianeni kuhusu mambo yaliyomo ubaoni.
                                         
    Mifano ya mialiko
    i) Mwaliko wa harusi
    Je, umewahi kualikwa katika harusi au kuona kadi ya mwaliko wa harusi? Je,
    mwaliko huo ulikuwa na mambo gani?
    Mwaliko wa harusi huwaomba jamaa na marafiki kuhudhuria sherehe ya harusi.
    Kadi za mialiko ya harusi huchukua miundo na sura tofautitofauti. Miundo ya
    kadi hizo hutegemea ubunifu wa anayeziunda au mapendekezo ya maarusi au
    waandalizi wa harusi.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako. Tazameni mialiko ya harusi iliyotolewa hapa chini.
    Jadilianeni kuhusu mambo yaliyomo katika mialiko hiyo.

    Mfano
                

      
                A .     



                 B. 


    Kanuni za kuzingatiwa katika uandishi wa mwaliko wa harusi
    Unapoandika mwaliko wa harusi, ni sharti utaje majina ya watu wanaofunga ndoa,
    tarehe ya harusi, mahali pa harusi na wakati sherehe itakapoanza.
    Watu mbalimbali huandika mialiko ya harusi kwa njia tofauti tofauti. Mara
    nyingi, kadi hutumika. Wao hurembesha kadi za harusi ili kuwavutia wasomaji
    na kuonyesha mapenzi yaliyopo kati ya maharusi. Wengine hunukuu maandiko
    takatifu yanayotaja mapenzi na ndoa. Almuradi, kila mwaliko wa harusi huwa na
    umbo lake maalumu.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako na mchukulie kuwa nyinyi ni wanachama wa kamati
    inayoandaa harusi. Mna nia ya kutengeneza kadi nzuri ya mwaliko wa harusi. Kila
    mmoja achore kadi ya mwaliko na aweke ujumbe wake. Linganisheni mialiko yenu
    na mchague mwaliko bora zaidi kisha muufanye urembeke zaidi. Onyesheni na
    mlisomee darasa zima kadi yenu.

    ii) Mwaliko wa kutembelea mbuga ya wanyama
    Mwaliko kama huu huchukua umbo la barua rasmi.

    ii) Mwaliko wa maonyesho ya vitabu

                        

      Zoezi

    i) Soma tena barua za mialiko hapo juu. Taja mambo muhimu yaliyozingatiwa
       katika uandikaji wazo.
    ii) Mwandikie aliyekuwa mwalimu wako barua ya kumwalika kwenu kwa
        sherehe ya kukuaga kwa safari ya kwenda ng’ambo kusoma.

    Zoezi la ziada
    Andika barua za mialiko kuhusu mada yoyote.

    E . Aina za alama za uandishi na matumizi yake
    Wenzetu wanapozungumza, tunaweza kutambua wanapomaliza usemi wao kwa
    kusikia sauti zao. Lakini katika uandishi, hakuna sauti. Badala ya sauti, zipo alama
    za uandishi ambazo hutumiwa kuwakilisha sauti katika uandishi. Kutokana na
    alama hizo, tunatambua kama usemi umekwisha, kuulizwa swali, kushangaa na
    kadhalika. Pia, tunaposoma, tunajua wapi tunafaa kupumua kidogo, kushusha au
    kupandisha sauti na kadhalika.
    Alama hizi huitwa viakifishi. Hivyo basi, viakifishi ni alama zinazotumiwa katika
    maandishi ili kuleta maana ikusudiwayo katika matini mbalimbali kama vile
    sentensi, aya, mtungo, barua, mialiko, matangazo, ilani na kadhalika.

    Aina za viakifishi
    Nukta (.)
    a) Huwekwa mwishoni mwa sentensi. Kwa mfano:
       i) Nimechoka.
       ii) Waziri mkuu wa Uchina amewasili mjini Kigali.
    b) Hutumiwa kuonyesha ufupisho wa maneno. Kwa mfano:
       i) S.L.P. – Sanduku la Posta
       ii) Bi. – Bibi
    c) Hutumika kubainisha saa na dakika au tarehe. Kwa mfano:
       i) 3.20 – saa tisa na dakika ishirini
       ii) 14.5.2016- tarehe kumi na nne, mwezi wa tano, mwaka wa elfu mbili na kumi na sita
    d) Hutumiwa kuonyesha vipashio vya pesa. Kwa mfano:
        Sh. 10.50 – shilingi kumi na thumuni hamsini
    e) Zikitumiwa mara tatu mfululizo (...), huonyesha kutokamilika kwa sehemu
        husika. Kwa mfano:
                        Nitakupa lakini ni sharti...
    Mkato/koma ( , )
    a) Hutumiwa kuonyesha pa kutua kwa muda mfupi katika sentensi. Kwa mfano:
        i) Nilipowasili nyumbani, nilienda kuteka maji kisimani.
       ii) Kwa kuwa tulijiandaa vilivyo kwa mtihani wa kitaifa, tulipita.
    b) Hutumiwa kutenga maneno yaliyo katika orodha:
        i) Kwenda sokoni ununue mboga, nyama, mafuta, na unga.
        ii) Mwanafunzi huyu ni mtiifu, mwerevu, mtanashati, na mwenye bidii.
    c) Hutumiwa kubainisha sehemu mbili za sentensi zilizo kinyume:
        i) Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.
        ii) Aliniambia atakuja, hakuja.
    d) Hutumiwa kabla ya alama za mtajo. Kwa mfano:
        Mama akasema, “Niletee chumvi.”
    e) Hutumiwa wakati sentensi inapoanza kwa kiunganishi. Kwa mfano:
        Kweli, alikuwa mtu mwovu.
    f ) Hutumiwa unapoita mtu ili kupata usikivu wake kabla hujamwambia
        chochote. Kwa mfano:
        Nkusi, niletee kalamu.
    g) Hutumiwa unapokubali au unapokataa kitu. Mfano:
       i) Ndio, nitakuja.
       ii) Hapana, sitakulipa.

    Nukta mbili/koloni (smile
    a) Hutumiwa kutanguliza maneno yaliyo katika orodha.

    Kwa mfano:
        i) Nenda kaniletee: kalamu, karatasi na kifutio.
        ii) Amenunua: machungwa, sukari, na ndizi.
    b) Hutumiwa kuashiria maneno ya msemaji badala ya alama za mtajo hasa katika
         uandishi wa mazungumzo au tamthilia.
        i) Mama: Lazima uniambie ulikokuwa tangu jana.
       ii) Mwalimu alisema: Ingieni darasani.
    c) Hutenganisha numerali za saa.

    Kwa mfano:
           4:10 – saa kumi na dakika kumi
    Nukta na kituo (;)
    a) Hutumiwa kuunganisha vishazi vikuu bila kutumia kiunganishi. Kwa mfano:
        Sikwenda Kayonza; nilienda Kirehe.
    b) Hutumiwa kumpumzisha msomaji katika sentensi iliyo ndefu ili apumzike
        zaidi kuliko pale inapotumiwa koma. Kwa mfano:
        Alipofikiri sana, alitanabahi kuwa hakikuwepo cha kutorokwa; yeye angeweza
        kuondoka nyumbani au kumwacha mumewe, aende popote kufanya lolote.
    Kistari kifupi (-)
    a) Hutumiwa kuonyesha kuwa neno linakatwa kwa vile limefika ukingoni mwa
         mstari husika na bado linaendelea katika mstari unaofuatia.
         Tanbihi: Neno la silabi moja halikatwi.
    b) Hutumiwa kuunga maneno yanayojenga neno moja. Mtindo
         huu aghalabu hujitokeza katika maneno yenye asili ya kigeni. Kwa mfano:
        i) Idd-el-Fitri
        ii) Dar-es-Salaam
    c) Huweza kutumiwa badala ya koma. Kwa mfano:
        Nyimbo za asili-hasa rumba-zinapendwa na wengi.

    Alama ya mshangao (!)
    Hutumiwa kuashiria mahangaiko ya moyo kama vile hasira, hofu, mshangao na
    kadhalika.
           i) Lo! Mwanafunzi ameangusha kitabu cha mwalimu matopeni.
           ii) Wamefungwa mabao kumi kwa nunge!
    Alama ya kuulizia/kiulizi (?)
    a) Hutumiwa mwishoni mwa sentensi kuonyesha kuwa sentensi hiyo ni swali.

    Mwa mfano:
    Unaitwa nani?
    b) Hutumiwa kuonyesha ukosefu wa uhakika kuhusu jambo kama vile mwaka.
        Kwa mfano:
        Shule hii ya Tumaini ilianzishwa 1992 (?)

    Mabano/parandesi egg
    a) Hutumiwa kufunga maneno ya ziada katika sentensi. Kwa mfano:
        Nyamata (makao makuu ya Bugesera) inakua kwa kasi.
    b) Hutumiwa mwandishi anapotaka kutoa ufafanuzi kwa lugha nyingine tofauti
         na ile anayoitumia.
    Kwa mfano: Walowezi (settlers) walifukuzwa
    c) Hutumiwa kufungia herufi za kuorodhesha. Kwa mfano:
         (a) huelimisha,                  (b) huburudisha,                (c) huonya

    Mkato (/)
    Hutumiwa kuonyesha kuwa mojawapo ya vitu vilivyotajwa chaweza kutumiwa
    badala ya hivyo vingine.
    Tazama: Abera alishangaa/aliduwaa
    Mtajo: (“ ” au ‘ ’)
    Hutumiwa kuonyesha maneno halisi ya mzungumzaji. Kwa mfano:
    “Nitafika kesho jioni,” alisema mdogo wake.
    Herufi kubwa (H)
    Hizi ndizo alama za uandishi zinazotumiwa sana kuliko nyingine zote. Hutumiwa
    kila baadaya herufi kubwa.
    Mama anapika.

    Zoezi

    Kiakifishe kifungu kifuatacho
    Ilikuwa asubuhi na mapema bw butera alipotoka kwake kwenda kazini fikirani
    mwake alijikumbusha pindi nikifika ofisini nitaomba ruhusa niende nimlipie binti
    yangu karo
    aliabiri gari linaloelekea ruhango baada ya mwendo mfupi tu lo gari hilo lilipata
    ajali liligongana na lori japo ng'ombe waliokuwemo njiani walikufa takriban wote
    abiria walipata majeraha madogo madogo lakini ililazimu wapelekwe hospitalini
    hivyo butera hakutimiza azma yake

    Mazoezi ya ziada

    Zoezi A

    Andika kifungu cha habari kuhusu mada yoyote ukitumia alama za uandishi kwa
    usahihi.


    Zoezi B

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako na msome vifungu mbalimbali vya habari
    vilivyomo katika kitabu hiki, magazeti, na vitabu vinginevyo. Bainisheni na kuainisha
    alama mbalimbali za kuakifisha zilizotumika na jinsi zilivyotumiwa.

                                                Maswali ya marudio
    1. Eleza maana ya barua ya kirafiki.
    2. a) Taja watu watano wanaoweza kuandikiwa barua ya kirafiki.
        b) Mwandikie mmoja wa hao uliowatajia barua ya kirafiki.
    3. Zitaje sehemu zote kuu za barua ya kirafiki huku ukizieleza.
    4. Eleza maana ya barua rasmi.
    5. Taja aina tano za barua rasmi.
    6. Mwandikie Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi ulikosomea ukiomba nafasi ya
         kufunza katika shule hiyo.
    7. Zitaje sehemu kuu za barua rasmi.
    8. Eleza kanuni za kuzingatiwa wakati wa kuandika barua rasmi.
    9. Eleza tofauti zilizopo kati ya barua rasmi na barua ya kirafiki.
    10. Kwa maneno yako mwenyewe, eleza tangazo ni nini.
    11. Ipo tofauti gani kati ya matangazo na barua rasmi?
    12. Eleza tofauti kati ya tangazo la tanzia na tangazo la mkutano.
    13. a) Ilani ni nini?
          b) Andika ilani utakayoweka msalani ili kuwatahadharisha wanafunzi
               wenzako kuhusu madhara ya kutonawa mikono baada ya kutoka msalani.
    14. a) Eleza sifa za matangazo ya biashara.
          b) Andika tangazo la biashara kuhusu bidhaa upendayo.
    15. Eleza umuhimu wa mwaliko.
    16. Je, kuakifisha ni kufanya nini?
    17. Eleza umuhimu wa uakifishaji.
    18. Yataje kwa mifano matumizi matano ya nukta.
    19. a) Eleza maana ya mtajo.
          b) Andika mifano miwili ya matumizi ya mtajo.
    20. Eleza kwa ufupi mambo muhimu uliyojifunza katika sura hii. Taja jinsi mambo
          hayo yatakavyokusaidia na kuisaidia jamii yako.



  • Sura 3: Matumizi ya lugha katika mazingira mbalimbali

    Mada ndogo: Rejesta za mpira na burudani

    A   Rejesta mbalimbali nchini Rwanda 
    Rejesta au sajili ni lugha inayotumiwa mahali ama katika hali fulani na wala haiwezi
    kuhamishwa kutoka mazingira yale na kutumiwa katika mahali pengine. Lugha hizi
    hutofautiana kwa misingi ya msamiati, muundo wa sentensi na kadhalika. Kutokana
    na tofauti hizi, tunapata rejesta za aina mbalimbali. Baadhi ya rejesta hizo ni kama
    hizi zifuatazo.

    i) Rejesta ya mpira wa miguu
    Mpira wa miguu pia huitwa kandanda, soka au kambumbu. Huu ni mchezo
    maarufu sana hapa nchini Rwanda na duniani kote. Kwa mfano, mashindano ya
    kombe la dunia hutazamwa na watu wengi sana kote duniani. Mashindano hayo
    huandaliwa kila baada ya miaka minne. Pia, yapo mashindano ya Bara la Afrika,
    Kombe la Kagame, ligi mbalimbali na kadhalika.
    Baadhi ya watu hufuatilia mechi mbalimbali kupitia redio au televisheni. Wapo
    wanahabari ambao hutangaza mpira kupitia vyombo hivyo. Rejesta ya mchezo
    hujitokeza kupitia matangazo hayo.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tazameni mchoro huu. Jadilianeni kuhusu
    yaliyomo michoroni na myahusishe na mazingira yenu.

                                    

                    

    Soma kifungu hiki na ujibu maswali chini yake. 

    Matangazo ya kandanda sehemu I

    Hujambo msikilizaji. Karibu katika matangazo haya ya moja kwa moja ya kabumbu.
    Ni mimi mtangazaji wako, Teta. Huu ni mchuano wa fainali ya kuwania kombe la
    Fahari ya Rwanda kati ya shule ya wasichana ya Elimu Bora na Tusonge Mbele.
    Timu hizi mbili ni wapinzani sugu tangu jadi. Elimu Bora inajivunia historia nzuri
    kwa kushinda kombe hili mara kumi. Wao ndio bingwa tetezi. Tusonge Mbele
    imeshinda kombe hili mara tatu. Mwaka jana walitimuliwa katika nusu fainali.
    Katika awamu hii, wana rekodi ya kutoshindwa katika mechi zote hadi kufikia
    fainali. Je, rekodi hiyo itavunjwa na Elimu Bora?
    Naona timu zote mbili zikiingia uwanjani tayari kwa pambano. Kwa sababu ya muda
    sitataja majina ya wachezaji wote. Nitayataja kadri wanavyozidi kucheza. Kwa ufupi,
    kila timu ina golikipa mmoja. Elimu Bora wameweka wachezaji watatu katika safu
    ya ulinzi nao Tusonge wanawachezesha wachezaji wanne katika safu hiyo hiyo.
    Timu ya Elimu Bora wametia wachezaji watano katika kiungo cha kati nao Tusonge
    wanawachezesha wachezaji watatu. Elimu Bora wana washambulizi wawili nao
    Tusonge wana washambulizi watatu katika safu ya mashambulizi. Timu zote mbili
    zina wachezaji wa akiba watano. Refa mkuu anapuliza kipenga nao wasaidizi wake
    wawili wanakimbia pembeni mwa uwanja kuinua kijibendera. Mmoja anakimbia
    kushoto naye mwingine anakimbia kulia.
    Manahodha wa timu zote mbili wapo pale katikati ya uwanja kurusha sarafu ili
    kuamua timu inayoanzisha mpira. Mashabiki wa timu zote mbili wanaimba nyimbo
    za kushangilia timu zao. Nao makocha wao wamekaa pembeni mwa uwanja
    kushuhudia wasichana wao wakimenyana.
    Naam, refa anapuliza kipenga. Mpira unaanzishwa pale na Ikirezi na Uwamwiza
    wa timu ya Elimu Bora. Ikirezi anapiga pasi kwake Gwiza. Gwiza anapiga chenga.
    Anaangalia aupige wapi. Anapiga pasi safi kwake Umuliza. Umuliza na mpira.
    Umuliza anakwenda. Anapiga shoti ndefu kuelekea lango la Tusonge. Munyana
    anajibu kombora kwa kichwa. Mpira unakuwa mwingi na kutoka nje.
    Hee! Hee! Elimu Bora wameanza mchuano huu kwa kasi mno. Wanatafuta bao
    la mapema. Kamaliza anarusha ngoma ile kwake Muteteri. Muteteri anateleza
    na kuanguka. Refa anasema twendelee. Mutoni anachukua mpira. Tusonge
    wanafanya shambulizi la kujibu. Kamiza kwake Umuhire. Umuhire...Umuhire na
    mpira. Umuhire anakwenda. Umuhire anavuka mstari wa katikati. Anatoa pasi safi..
    go..go..ah! Kijibendera kipo juu. Tona amejenga kibanda katika ardhi ya wenyewe
    pasi ruhusa. Lo! Leo kuna kazi hapa.
    Msamiati
    kabumbu – mchezo wa mpira wa mguu/kandanda
    mchuano – mashindano baina ya timu mbili
    fainali – shindano la mwisho kabisa la kutafuta mshindi
    kuwania kombe – kushindania kombe/tuzo katika mchezo
    wapinzani – kikundi cha watu wanaoshindana na wengine
    bingwa tetezi – timu ambayo iliibuka mshindi/kuchukua kombe katika awamu
                             iliyopita ya shindano fulani.
    nusu fainali – mchezo unaotangulia fainali ambapo washindi hucheza katika fainali
    safu ya ulinzi – wachezaji ambao huzuia wapinzani kufunga bao
    kiungo cha kati – wacheza ambao hucheza sana katikati ya uwanja
    washambulizi – wachezaji ambao hucheza karibu na lango la wapinzani ili wafunge bao
    wachezaji wa akiba – wachezaji ambao hukaa nje ya uwanja na ambao huingizwandani kuchukua nafasi
                                        za wenzao waliopata jeraha au kuchoka
    kuinua kijibendera – kuonyesha kuwa mchezaji amekiuka kanuni za mchezo
    kurusha sarufi – kuamua timu gani inaanzisha mchezo kwa kurusha sarafu juu.
    anapiga pasi – mchezaji mmoja kumpigia mwenzake mpira
    anapiga chenga – kumhepa au kumpita mpinzani kwa mpira
    anapiga shoti – kupiga mpira kuelekea lango la mpinzani
    anajibu kombora – kuzuia mpira kwa kuupiga kuelekea upande wa pili
    mpira unakuwa mwingi – mpira kukosa kuthibitiwa na wachezaji
    mpira umetoka nje – mpira kuenda nje ya mstari wa nje uwanjani
    bao – mpira kuingia ndani ya lango
    shambulizi la kujibu – wachezaji kuelekeza mpira kwa kasi kuelekea lango la
                                        wapinzani punde tu baada ya mpira kuelekezwa
                                        langoni mwao
    kujenga kibanda/kuotea – kuvunja kanuni za ushambulizi kwa kushambulia
                                              ghafla nyuma ya mchezaji wa mwisho wa timu pinzani

    Zoezi

    1. Tunga sentensi sahihi ukitumia msamiati uliotolewa maelezo hapo juu.
    2. a) Orodhesha na utoe maana ya maneno yote katika rejesta ya kandanda
            kifunguni humu lakini ambayo hayakuelezwa hapo juu.
        b) Tunga sentensi ukitumia msamiati uliotaja hapo juu.

    Kazi ya kikundi
    Wewe ni mtangazaji wa mpira wa miguu. Andika matangazo ya mchezo kati ya
    timu zozote mbili upendazo. Baada ya kuandika, jiunge na mwanafunzi mwenzako.
    Kila mmoja amsomee mwenzake matangazo yake.

    Sifa za rejesta ya mpira wa miguu
    Tazama matangazo ya mpira katika kifungu ulichosoma. Je, pana sifa gani katika
    rejesta hiyo?
    Zifuatazo ni orodha ya sifa za rejesta ya mpira wa miguu.
    i) Hujaa jadhba hasa baada ya mchezo kuanza,
    ii) Hujaa mazungumzo ya kuhamisha ndimi ambapo baadhi ya maneno ya
        Kiingereza na hata kienyeji hutumiwa,
    iii) Huwa na lugha ya kuchekesha na kuburudisha wanaoisikiliza,
    iv) Hujaa maoni mbalimbali kuhusu nani atashinda, nani mchezaji bora zaidi,
         na kadhalika,
    v) Huwepo kurudiarudia maneno kama vile majina ya wachezaji, dakika zilizopita,
        mabao yaliyofungwa na kadhalika,
    vi) Huwa na lugha ya kuibua hisia na kumfanya mtu kuingiwa na mahangaiko ya moyo,
    vii) Sentensi fupi fupi huweza kutumika pamoja na taswira ya kuchora picha kamili ya
         yanayotendeka.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwenzako mmoja. Someni kifungu hiki ili mbainishe rejesta ya mpira wa
    miguu na sifa zao.
    Matangazo ya kandanda sehemu II
    Mlinda lango wa Elimu Bora anaenda kupiga mpira wa madhambi. Anapiga kombora
    ndeeeefu na kutoka nje. Munyana anarusha ngozi iliyowambwa na kutengenezwa mpira.
    Kamiza anapiga chenga. Anatoa pasi kwake Usanase. Usanase anakwenda.
    Anaingia ndani ya kijisanduku. Hatari katika lango la Tusonge. Hatariiiii! Lo! Kayitesi
    ananawa mpira. Refa anasemaje. Naam, kipenga kinapulizwa. Refa anawapa Elimu
    Bora penalti. Shangwe na vifijo kutoka kwa mashabiki wa Elimu Bora. Kayitesi
    anaonyeshwa kadi ya manjano. Kayitesi amecheza rafu. Achunge asionyeshwe kadi
    nyingine ya manjano kwani atatolewa uwanjani.

    Haya! Tuone jinsi mambo yatakavyokuwa hapa. Refa anahesabu miguu kumi na
    miwili kutoka lango la Tusonge. Anaweka mpira chini. Ikirezi amesimama nyuma
    ya mpira ule tayari kupiga mkwaju wa penalti. Mlinda lango wa Tusonge, Kabatesi,
    amesimama mbele ya wavu. Refa anapuliza kipenga. Ikirezi anapiga hatua mbili
    tatu nyuma. Anapiga...go...goo... Nje! Heeee! Heee! Ikirezi ameshindwa kutikisa
    wavu. Alipiga kombora zito. Kabatesi akaruka na kuupiga mpira ule ukapitia juu ya
    mtambaa panya wa goli hadi nje. Kona! Kona ile inapigwa kutoka kushoto wa goli
    la Tusonge.
    Dakika zilizokatika hapa ni dakika kumi na tano. Bado dakika thelathini kipindi
    cha kwanza kikamilike. Tutakupa nafasi ya kuwasiliana nasi wakati wa mapumziko
    ambao utachukua dakika kumi na tano. Baadaye tutarudi hapa kwa kipindi cha
    pili ambacho kitachukua dakika nyingine arubaini na tano pamoja na dakika za
    nyongeza kutoka kwa refa mkuu. Ikiwa timu hizi zitatoka sare baada ya kipindi
    cha lala salama, dakika thelathini za ziada zitaongezwa. Ikiwa bado mshindi
    hatapatikana, watapiga penalti ya kuamua mshindi. Mshindi na mshinde sharti
    wapatikane leo kwa sababu hii ni fainali.
    Umuliza anapiga kona safi pale. Uwamwiza anakimbilia mpira ule. Anapiga kichwa..
    go..goo...goooooool! Mpenzi msikilizaji, hayawi hayawi huwa! Hatimaye Elimu
    Bora wamepata goli la kwanza. Uwamiza amecheka na wavu. Yeye ndiye mfungaji
    bora kufikia sasa. Mashabiki wote wa Elimu Bora na makochi wao wameacha viti
    vyao. Mashabiki wa Tusonge wameinamisha vichwa vyao. Wachezaji wa Tusonge
    wamepandwa na mori. Wamemzingira refa mkuu. Wanadai kuwa Uwamwiza
    alikuwa ameotea. Nahodha wao, Mutoni, ambaye ni beki wa kupanda na kushuka
    anammiminia refa maneno makali. Refa anatia mkono katika mfuko wa nyuma
    ya kaptura na kuchomoa kadi nyekundu. Salaale! Mutoni ameonyeshwa kadi
    nyekundu kwa kukosa adabu. Anasindikizwa nje ya uwanja. Timu ya Tusonge
    wamebaki na wachezaji kumi pekee. Je, itakuaje?

    i) Rejesta ya burudani
    Kama ujuavyo, burudani ni shughuli ifanywayo kwa ajili ya kuchangamsha na
    kufurahisha watu. Nayo mazingira ya namna hii yana msamiati wake ambao ndio
    lengo la sehemu hii.
    Tazama mchoro huu na ueleze mambo yanayojiri katika mchoro wenyewe.
                                                         
    Soma kifungu hiki cha habari na ujibu maswali chini yake.
    MFAWIDHI:Leo ni leo! Asemaye kesho....?
    WATU:        Ni mwongo!
    MFAWIDHI:Hapana! Asemaye kesho hayuko hapa. (Watu wanacheka) Leo showhii itakuwa ya kukata na shoka.
                       Kama huna shoka sijui utakata na nini.
    MTU I:        Tutakata na wembe.
    MFAWIDHI: Wembe utavunjika. (Watu wanacheka) Tuna wasanii wanaotajika ambao wamefika hapa kututumbuiza.
                        Mko tayari kuvunjika mbavu?
    WATU:        Ndiyooooo!
    MFAWIDHI: Shauri yenu. Mimi sitagharamia matibabu ya mbavu zitakazovunjika.
                        (Watu wanacheka) Mabibi na mabwana, sote tumkaribishe mwimbaji
                         katika jukwaa kwa makofi na vigelegeleeeeee!
                        (Watu wanapiga makofi. Mwimbaji anaingia.)
    MFAWIDHI: Kwenu mnanunua sindano kweli?
    MWIMBAJI: Hapana.
    MFAWIDHI: Ningeshangaa. Wewe ni sindano tayari. (Watu wanacheka)
    MWIMBAJI: Kwetu tuko wengi sana.
    MFAWIDHI: Mko wengi hadi mnapika chapati moja kisha mnapiga chapa.
                        (Kicheko). Kabla hatujaanza, ebu tupe historia fupi kuhusu safari
                        yako katika muziki.
    MWIMBAJI: Nilianza kwa kucheza kayamba kanisani.Hapo ndipo bendi ya
                        Umoja Jazz wakatambua kipawa changu. Wakanichukua kuwachezea
                         tarumbeta. Baada ya muda mfupi, nikaanza kujisimamia. Nikatunga
                        na kurekodi nyimbo zangu kama na kujichezea gitaa.
                        Hivi karibuni nitaunda bendi yangu.
    MFAWIDHI: Usikose kunijumuisha katika kwaya yako. Nitakuimbia soprano.
                        (Watu wanacheka) Leo umetuandalia nini?
    MWIMBAJI: Leo nitawatumbuiza kwa taarabu.
    MFAWIDHI: Haya haya! Wakati wa burudani umewadia. Kila mtu atafute nafasi
                        na mwandani wake. Muwe wawili wawili. Kama huna wako, eleka
                        jiwe. Kuna mawe mengi hapa. (Kicheko) Hakuna kukanyagana mguu.
                        (Watu wanacheka). Kama hujui kucheza miondoko ya taarabu,
                        kuja hapa mbele nikufunze. (Watu wanacheka). Haya twende kazi.
                        (Mwimbaji anaimba. Watu wanacheza.)

    Maelezo ya msamiati

    kukata na shoka – kufana
    kuvunjika mbavu – kucheka
    kayamba – ala ya muziki yenye umbo la kisanduku ambayo
                       hutengenezwa kwa matete na kutiwa punje kavu au
                       changarawe na hutikiswatikiswa wakati wa kuimba
    bendi – kikundi cha waimbaji wanaoimba pamoja
    tarumbeta – ala ya muziki ya kupuliza ambayo hutengenezwa kwa shaba na
                          hutoa sauti mbalimbali
    gitaa – ala ya muziki ambayo kwa kawaida huwa na nyuzi sita
    kwaya – uimbaji wa pamoja katika kikundi maalamu cha kuimba
    taarabu – muziki wenye mahadhi ya mwambao wa Afrika Mashariki
                    unaotumia mchanganyiko wa ala za Kiarabu, Kihindi na Kizungu

    Zoezi

    1. Tunga sentensi sahihi ukitumia msamiati uliotolewa maelezo hapo juu.
    2. Toa mifano zaidi ya rejesta ya burudani. Andika msamiati wa kimsingi
         unaotumika katika rejesta hizo.
    3. Eleza sifa ya lugha iliyotumika kifunguni.

    Sifa za rejesta ya burudani

    Rejesta ya burudani huwa na sifa mbalimbali. Tazama baadhi ya sifa hizo katika orodha ifuatayo:
    i) Kuwa na maneno ya raha,
    ii) Huibua hali za kutuliza na kupumbaza mshiriki,
    iii) Kuwepo na uwezekano wa washirika wake kukesha hadi che huku
         wakijifurahisha kwa namna wapendavyo,
    iv) Kuwepo bendi ya muziki na wanasarakasi,
    v) Hali ya kusahau shida na mahangaiko aliyonayo mshiriki angalau kwa wakati mfupi tu.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Fanyeni mazoezi haya:
    1. Toeni mifano zaidi ya rejesta za burudani.
    2. Jadilianeni sifa za lugha inayotumika katika rejesta mlizotaja.
    3. Linganisheni na mtofautishe msamiati uliotumika katika rejesta hizo mbalimbali za burudani.

    Umuhimu wa michezo na burudani
    a) Umuhimu wa michezo
    Michezo ni shughuli za kushindana kati ya timu au watu tofauti tofauti ili kutafuta ushindi.
    Je,wewe unapenda kucheza mchezo gani?

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tazameni michoro iliyopo hapo chini na mtaje yanayotendeka.
      

    Soma kifungu na ujibu maswali yaliyoulizwa chini yake.
    Michezo ina umuhimu mkubwa kwetu kutokana na sababu mbalimbali. Kwanza,
    mchezo huimarisha afya yetu. Wachezaji hufanya mazoezi ya viungo. Mazoezi
    hayo ya viungo husaidia miili yetu kuyeyusha mafuta ya ziada, kunyosha misuli,
    kuimarisha mapigo ya moyo na kadhalika.
    Pili, michezo huleta umoja miongoni mwa jamii. Watu wanapoenda kutazama
    mchezo kama vile kandanda, hujumuika pamoja kushabikia timu fulani. Pale,
    wao hujenga urafiki. Mathalan, timu yetu ya taifa inapocheza, Wanyarwanda
    wote huja pamoja kuishabikia. Tunapofanya hivyo, tunajenga umoja wetu kama
    Wanyarwanda. Baadhi ya mashabiki pia husafiri pamoja na timu yetu ya taifa
    wanapocheza nje ya Rwanda. Safari kama hizo huchangia kujenga umoja na
    urafiki miongoni mwa mashabiki hao.
    Tatu, michezo huleta fahari. Mchezaji mashuhuri, timu bora na taifa bingwa katika
    michezo fulani hujulikana kwingi na kusifiwa. Sifa hizi huinua hadhi ya mtu binafsi,
    timu na taifa kwa jumla. Nchi inayosifika kwa mchezo au michezo fulani huwa
    katika hali nzuri ya kuvutia watalii.
    Michezo huleta pato la kuridhisha. Pato hili huwa kwa mchezaji binafsi, kwa
    kilabu na hata kwa taifa. Wachezaji wa vilabu mbalimbali na timu ya taifa hulipwa
    mshahara na marupurupu mengi. Baadhi ya wachezaji hawa hasa wanaochezea
    vilabu vya kimataifa ni matajiri wa kutajika kutokana na michezo.
    Vilabu mbalimbali pia hunufaika pakubwa. Wao hukusanya pesa nyingi kutokana na
    mauzo ya tikiti, matangazo ya biashara katika viwanja vyao, kuuzwa kwa wachezaji
    wao kwa vilabu vinginevyo na kadhalika. Taifa zima pia hunufaika kutokana na
    ushuru mbalimbali unaolipwa na wachezaji pamoja na vilabu husika.
    Michezo huburudisha na kutuliza roho. Baada ya shughuli nyingi za siku au wiki,
    mashabiki hujipumzisha akili kwa kutazama michezo wanayopenda. Pia, kushabikia
    timu na kusherehekea ushindi huleta uchangamfu.

    Maswali
    1. Taja umuhimu wa michezo kulingana na kifungu hiki.
    2. Michezo ni njia bora kuu ya kuimarisha afya yetu. Tetea kauli hii.
    3. Eleza jinsi michezo huleta ushirikiano kati yetu.
    4. Jadilianeni kuhusu jinsi mnavyoweza kutumia michezo kukuza ushirikiano,
         kuboresha afya na kutatua matatizo yanayokumba jamii yenu.

    b) Umuhimu wa burudani
    Tazama michoro iliyopo hapa chini. Je, mambo gani yanafanyika?

    Soma kifungu kifuatacho na ujibu maswali chini yake.
    Kama ilivyo michezo, burudani ina umuhimu mkubwa kwa jamii. Kwanza, burudani
    hukuza umoja na utangamano miongoni mwa wanajamii. Watu wanapokuja pamoja
    kucheza densi, kutazama sarakasi, sinema na kadhalika, wao hujenga urafiki na
    uhusiano mwema miongoni mwao.
    Vilevile, burudani hukuza ushirikiano. Watu wanaoshiriki katika kuwaburudisha
    wanajamii huja pamoja ili kuafikia malengo hayo. Mfano, bendi au kwaya
    hushirikisha watu mbalimbali. Ushirikiano huu hukuza umoja miongoni mwa wahusika wote.
    Burudani pia hukuza afya yetu. Tunaposhiriki katika densi, viungo vya miili
    yetu hupata mazoezi muhimu ambayo huboresha afya yetu. Vilevile, akili zetu
    huchangamka kupitia burudani hasa baada ya kazi nyingi za siku au msiba.
    Uchangamfu huu huleta utulivu na liwazo katika akili zetu. Pia, hutuepushia
    huzuni ambayo ni hatari kwa afya yetu.
    Burudani hudumisha utamaduni. Hapa, chukua mfano wa ngoma zetu maarufu.
    Unapata kuwa ngoma hizo zilichezwa enzi za kale. Kupitia nyimbo hizo, tunafahamu
    hali ya maisha katika enzi hizo za kale. Kwa hivyo, hii ni njia moja ya
    kuhakikisha kuwa utamaduni wetu haupotelei mbali.
    Burudani pia ni chanzo cha ajira na pato. Watu wengi wameajiriwa kupitia burudani
    kama vile bendi, sarakasi, mchezo wa kuigiza na kadhalika. Burudani pia huweza
    kumletea mtu sifa nzuri. Kwa mfano, wapo waimbaji, waigizaji, wanasarakasi
    na kadhalika ambao wanajulikana kote ulimwenguni na kupendwa na wengi.

    Maswali
    1. Kwa maneno yako mwenyewe, eleza maana ya burudani.
    2. Je, ni jambo lipi unaloliona kuwa ni la muhimu zaidi kuhusu burudani? Kwa nini?
    3. Andika sifa ambazo zinafanya michezo na burudani kuwa sawa
    .4. Taja umuhimu wa burudani ambao haukutajwa kifunguni humu.


    Kazi ya wanafunzi wawili wawili

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Jadilianeni kuhusu umuhimu wa burudani kiafya na kiushirikiano

    iii) Rejesta ya hotelini

    Hoteli ni nyumba ambamo vyakula na vinywaji huuzwa. Vyumba vya kulalia pia
    hupatikana hotelini. Rejesta ya hoteli hutumika katika mazingira haya.

    Jiunge na mwenzako na msome kifungu kifuatacho.



    NDOLI:   Karibuni katika hoteli yetu! Jina langu ni Ndoli na mimi ndiye mhudumu.
    ITUZE:    Asante sana kwa makaribisho yenu.
    GANZA: Tunashukuru. Mna nini leo?
    NDOLI:  Tuna vyakula vingi kwenye ankra. Tuna tilapia, matoke, ugali, kisamvu na mizuzu.
                   Pia tuna vinywaji vingi. Tuna uji, chai na kahawa.
    GANZA: Niletee matoke sahani moja.
    ITUZE: Mimi juisi ya baridi. Nitaitisha vingine baadaye.
                 (Ndoli anaondoka na kurudi na vyakula vilivyoagizwa)
    NDOLI: Karibuni. Mjihisi nyumbani.
    GANZA: Asante. Nina swali kabla hujaenda. Sisi ni wageni hapa Kigali. Jioni tutahitaji mahali pa kulala.
                  Je, tunaweza kupata vyumba vya kukaa?
    NDOLI: Bila shaka vyumba mtapata. Vyumba vyetu vyote ni vya hali ya juu kwa wageni kama nyinyi.
                 Vyumba hivyo vina maji moto, televisheni nahuduma za bure za mtandao.
                 Pia, tunawapa wageni wetu kiamsha kinywa, chamcha na chajio.
    GANZA: Mna huduma gani zaidi?
    NDOLI: Tuna mabwawa ambapo wageni wetu huogelea. Pia, tuna ukumbi wa mazoezi ya viungo.
                  Mtakaa kwa muda gani?GANZA: Tutakaa kwa siku tatu. Tunahudhuria kongamano kuhusu
                 mbinu mpya za kilimo. Baadaye tutazuru mbuga ya wanyama ya Akagera.
    NDOLI: Karibuni tena.GANZA na ITUZE: Asante sana.

    Maswali

    1. Eleza maana ya msamiati mbalimbali wa hoteli jinsi ulivyotumika kifunguni.
    2. Tunga sentensi sahihi ukitumia msamiati uliotaja hapo juu.
    3. Je, pana umuhimu gani kwa mhudumu kuonyesha adabu na heshima
        anapozungumza na wateja katika hoteli?

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Fanyeni utafiti kuhusu lugha gani inayotumika
    katika mazingira ya hoteli nchini Rwanda. Wasilisheni matokeo yenu mbele ya darasa.

    Sifa za rejesta ya hotelini
    Rejesta ya hotelini huwa na sifa zifuatazo:
    i) Kuwepo kwa lugha ya vyakula mbalimbali,
    ii) Kupatikana kwa msamiati wa vinywaji vingi,
    iii) Wahudumu kuzungumza na wateja kwa unyenyekevu,
    iv) Kupatikana maneno ya huduma mbalimbali,
    v) Lugha ya mkato hutumika.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Fanyeni maigizo ya mazungumzo ya
    hotelini kati ya mhudumu na wateja. Zingatieni sifa mbalimbali za rejesta ya hoteli.

    iv) Rejesta ya mahakamani
    Mahakamani au kortini ni mahali pa kusikilizwa na kuamuliwa mashtaka na kesi mbalimbali.
    Yeyote anayefanyiwa mabaya ana ruhusa ya kumshtaki mahakamani aliyemfanyia ubaya huo.
    Je, umewahi kuhudhuria vikao vya mahakama?

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tazameni mchoro uliopo hapa chini.
    Jadilianeni kuhusu watu waliopo kwenye mchoro na shughuli zinazoendelea.
    Linganisheni yaliyomo humo na yale mnayofahamu kuhusu mahakama.

    Soma kifungu kifuatacho na ujibu maswali chini yake.

    Mahakamani sehemu I
    KARANI: Shughuli za korti hii zimeanza. Hakimu Ganza ndiye mwamuzi
                    katika kesi hii. Ketini tafadhali. (watu wanakaa)
    HAKIMU: Ninatangaza rasmi kusikilizwa kwa kesi ya Thierry Ngabo dhidi ya
                    Jane Usanase. Je, pande zote mko tayari?
    KIONGOZI WA MASHTAKA: Tayari kwa niaba ya upande wa mashtaka,Mheshimiwa.
    WAKILI: Tayari kwa niaba ya mshtakiwa, Mheshimiwa.
    HAKIMU: Thierry Ngabo?
    MSHTAKIWA: Naam, mheshimiwa. HAKIMU: Natumai unajua haki zako.
                            Una haki ya kuwakilishwa na wakili mbele ya mahakama hii.
                            Una haki ya kunyamaza kimya au kujibu mashtaka. Pia,
                            una haki ya kukata rufaa ikiwa hutaridhika na uamuzi wa mahakama.
                            Je, ni kweli kuwa unajua haki hizi?
    MSHTAKIWA: Naam.
    HAKIMU: Unashtakiwa kwa mashtaka mawili. Katika shtaka la kwanza,
                    unashtakiwa kuwa mnamo usiku wa tarehe ishirini na tisa, mwezi
                    wa kumi na moja mwaka wa elfu mbili kumi na sita ulipatikana
                    ukiendesha gari la kibinafsi lenye nambari ya usajili ASA000R
                     katika barabara kuu ya kutoka Ngoma kuelekea Kirehe bila idhini
                     ya mmiliki wa gari hilo. Gari hilo liliripotiwa kupotea mnamo
                     tarehe ishirini na nane, mwezi wa kumi na moja mwaka wa elfu
                      mbili kumi na sita. Katika shtaka la pili, unashtakiwa kwa kukwepa
                      vizuizi vya polisi na kutumia njia mbadala polisi walipojaribu
                        kukusimamisha. Unakubali au unakataa shtaka la kwanza?
    MSHTAKIWA: Ninakataa.
    HAKIMU: Unakubali au unakataa shtaka la pili?
    MSHTAKIWA: Ninakataa.
    HAKIMU: Upande wa mashtaka.
    KIONGOZI WA MASHTAKA: Asante Mheshimiwa. Nina ushahidi wa kutosha kuthibitisha
                                                    kuwa mshukiwa ana hatia kwa mashtaka mawili yaliyopo mbele
                                                    ya mahakama. Mheshimiwa, ushahidi utaonyesha kuwa gari
                                                    ASA 000 R liliibwa mnano tarehe ishirini na nane, mwezi
                                                    wa kumi na moja mwaka wa elfu mbili kumi na sita, usiku. Siku
                                                    moja baadaye, mshukiwa alipatikana akiendesha gari hilo.
                                                    Mheshimiwa, mshukiwa alishindwa kutoa idhini ya mwenyegari na stakabadhi za kumiliki
                                                    gari hili. Alama za vidole vya mshukiwa pia vilipatikana katika funguo bandia zilizotu
                                                    mikakatika wizi wa gari husika. Mheshimiwa, kwa mshukiwa kujaribukukwepa
                                                    vizuizi vya polisi ni ithibati tosha kuwa aliiba gari hili.
                                                    (Wakili anaomba nafasi ya kuchangia. Hakimu anampa nafasi.)
    WAKILI: Mheshimiwa, ni haki kwa Kiongozi wa mashtaka kudai kuwamshukiwa ana hatia bila kuthibitisha?
                   Mheshimiwa, kwa mujibu wa sheria kuhusu haki za mshtakiwa, mteja wangu hana hati
                   hadi mahakama hii itakapoamua kesi yake hii. Wakati wa kesi hii, utajua ukweli wa mambo.
                   Ngabo alikuwa akiendesha gari ambalo liliibwa na mtu mwingine. Ngabo alipogundua kuwa
                   gari limeibwa, alikuwa mbioni kurejesha gari hilo. Alikuwa amempigia polisi simu katika kituo
                   cha polisi mjini Kerehe kuwa gari analoendesha limeibwa. Hakuwa na nia ya kukwepa vizuizi vya polisi.
                  Alikuwa na nia ya kukwepa mlolongo mrefu wa magari ili afike mjini Kerehe mapema iwezekanavyo.
                  Mheshimiwa, mteja wangu ni mtu asiyekuwa na rekodi yoyoteya wizi.
                  Ndio maana alipewa dhamana bila kuhitajika mdhamini.
                  Kwa hivyo mteja wangu hana hatia.

    Msamiati
    korti – mahali ambapo kesi na mashtaka mbalimbali husikilizwa na kuamuliwa.
               Pia huitwa mahakama.
    hakimu – mtaalamu wa sheria anayeajiriwa kusikiliza mashtaka kortini na kutoa maamuzi
    kesi – mashtaka yanayosikilizwa mahakamani
    mshtakiwa – mtu anayefikishwa kortini kwa kudaiwa kufanya kosa
    mheshimiwa – jina la heshima ambalo watu hutumia kortini kumrejelea hakimu
    kukata rufaa – mshtakiwa kukataa hukumu aliyopewa kwa kuomba mahakama
                            ya juu isikilize tena kesi yake au ipunguze adhabu aliyopewa
    unashtakiwa kwa mashtaka mawili – makosa mawili yameletwa mbele ya mahakama dhidi yako.
    ushahidi – thibitisho kuwa jambo fulani lilifanyika au halikufanyika

    Maswali
    1. Bainisha msamiati zaidi wa kimsingi katika rejesta ya mahakama katika kifungu ulichosoma.
    2. Eleza maana ya kila msamiati na utungie sentensi sahihi.

    Sifa za sajili ya mahakamani
    Baadhi ya sifa zinazoweza kubainisha rejesta ya mahakamani ni:
    i) Matumizi ya lugha ya adabu,
    ii) Kuwepo tafsiri na fasiri ya yanayosemwa hasa ambapo mshtaki ama
        mshtakiwa haijui lugha rasmi ya mahakamani,
    iii) Mawakili hutumia lugha iliyojaa msamiati wa sheria,
    iv) Kunukuliwa kwa vifungu mbalimbali vya katiba au sheria,
    v) Kukosekana kupinga uamuzi wa korti papo kwa papo bali kupinga huja baadaye,
    vi) Kuwepo msamiati wa Kilatini.

    Soma mazungumzo haya ya mahakamani na ujibu maswali.
    Mahakamani sehemu II

    HAKIMU: Upande wa mashtaka, mna mashahidi?
    KIONGOZI WA MASHTAKA: Naam, Mheshimiwa.
    HAKIMU: Walete kizimbani.
                    (Askari analeta shahidi wa kwanzaAnasimama kwenye kizimba.
                    Karani wa korti anaelekea alipo shahidi akiwa na Biblia na Kurani.)
    KARANI: Unaitwa nani?
    SHAHIDI I: Jane Usanase.
    KARANI: Uko mbele ya mahakama. Mahakama inataka kujua ukweli.
                    Usimwogope mshukiwa wala mtu yeyote. Ujikaze ili korti ijue
                    ukweli wa mambo. Utakula kiapo kwa Biblia au Kurani?
    SHAHIDI I: Biblia. (Jane anainua Biblia kwa mkono kwa kulia)
    KARANI: Uyarudie maneno haya kwa sauti. Mimi Jane Usanase.
    SHAHIDI I: Mimi Jane Usanase.
    KARANI: Ninaapa kwamba yale ambayo nitasema mbele ya korti hii ni ukweli.
    SHAHIDI I: Ninaapa kwamba yale ambayo nitasema mbele ya korti hii ni ukweli.
    KARANI: Ewe Mungu nisaidie.
    SHAHIDI I: Ewe Mungu nisaidie. (Karani anakaa. Kiongozi wa Mashtaka anaamka
                       na kuelekea alipo shahidi.)
    KIONGOZI WA MASHTAKA: Unafanya kazi wapi?
    SHAHIDI I: Katika Halmashauri ya Wilaya ya Kerehe.
    KIONGOZI WA MASHTAKA: Unatumia mbinu gani za usafiri ukienda kazini?
    SHAHIDI I: Gari langu la kibinafsi.
    KIONGOZI WA MASHTAKA: Gari hilo lilikuwa wapi mnamo usiku wa tarehe 29/11/2016?

    SHAHIDI: Nilikuwa nimeliegesha mbele ya hoteli ya Starehe mjini Kirehe.
    KIONGOZI WA MASHTAKA: Nambari ya usajili wa gari hilo ni A...
    WAKILI: (Baada ya kumwomba Hakimu nafasi ya kuongea) Mheshimiwa,
                   nihaki kwa kiongozi wa mashtaka kumwelekeza shahidi katika kutoa
                   ushahidi wake? Gari likiwa lake, mbona asiseme nambari yake
                   ya usajili bila kuambiwa?
    HAKIMU: Kiongozi wa mashtaka, shahidi anajua nambari ya usajili wa gari lake.
                    Mwache aitaje.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako na mfanye mazoezi haya:
    i) Jadilianeni kuhusu sifa za rejesta ya mahakamani.
       Rejeleeni vifungu mlivyopewa na ikiwezekana msikilize rekodi
       za matukio mahakamani au kuhudhuria vikao vya mahakama.
    ii) Kamilisheni kesi iliyopo mahakamani kuanzia ilipofikia katika kifungu cha pili kwa kuigiza.

    v) Rejesta ya bungeni
    Bunge ni baraza la taifa linalotunga sheria na lenye wajumbe waliochaguliwa na
    wananchi kwa kupigiwa kura ama kwa kuteuliwa na rais.
    Soma kifungu kifuatacho na ujibu maswali chini yake.
       



    KARERA: Jina langu ni Karera.
    RUSARO: Na mimi ninaitwa Rusaro.
    RURANGIRWA: Nami ninaitwa Rurangirwa.
    KARERA: Tupo hapa mbele yenu, wanadarasa wenzetu, kukuelezeni
                      mengi kuhusu bunge letu ama baraza letu la taifa. Mambo haya
                      tumeyapata kupitia kwa utafiti wa kina ambao tumekuwa tukiufanya.
    RUSARO: Wabunge wetu huwawakilisha watu waliowachagua amavikundi fulani
                      fulani vya raia wa jamhuri yetu.
    RURANGIRWA: Namo bungeni, yamo mambo mengi unayostahili kuyajua.
                              Mathalan, mwenye mamlaka ya kuongoza, kuamuru au kuzuia
                             shughuli bungeni ni spika ambaye husaidiwa na naibu wa spika.
    RUSARO: Spika ana mamlaka ya kuamua ni mbunge gani atazungumza,
                     atazungumzaje na kwa muda gani na kadhalika. Hapana lolote
                     linaloweza kuendelea bungeni bila yeye kuliruhusu.
    KARERA: Hali kadhalika, yamo mambo mengi mengineyo yanayopatikana bungeni.
                     Mambo hayo ni kama vile rais, makamuwa rais, sheria, kutunga sheria,
                     hoja, upinzani, kura, uchaguzi, wakala, eneo la ubunge, piga kura,
                     mjumbe mteule,  mjumbe wakilishi na kadhalika
    RUSARO: Tukianza na rais tunapata kuwa hakuna bunge bila kuwepo rais.
                      Yeye huhitaji kutawala serikali na nchi nzima kwa mujibu wa sheria.
    RURANGIRWA: Nazo sheria hizo ni lazima zitungwe na bunge. Kwa hivyo,
                               kila nchi huhitajika kutawaliwa na rais kwa sheria zilizotungwa
                               na bunge.Naye makamu wa rais ni yule anayemsaidia rais kutawala nchi.
                               Lakini, je, sheria nazo ni nini?
    RUSARO: Sheria ni kanuni za kutawalia nchi na ambazo, kama ilivyotajwa awali,
                       hutungwa na bunge. Wabunge huwasilisha hoja bungeni na zikajadiliwa.
                       Baadhi yazo hupitishwa kuwa sheria baada ya kuidhinishwa na rais.
                       Lakini zile hoja zinazopingwa na upinzani na kukataliwa haziwi sheria.
                       Nazo zile anazozikataa rais hurudishwa bungeni ama kurekebishwa
                       ama kutupiliwa mbali.
    KARERA: Nao takriban wabunge wote hupigiwa kura ili kuingia bungeni.
                      Wafikapo huko huwa ni mawakala wa wale waliowachagua kutoka
                      maeneo yao ya bunge na huhitajika kufanya juu chini ili kuwainulia
                      hali yao ya kimaisha.
    RURANGIRWA: Hata hivyo, huwepo wajumbe wateule ambao huteuliwa na rais
                                ili kuwakilisha sehemu fulani fulani. Kwa mfano, panaweza kuwepo
                                mbuge mteule anayewawakilisha masilahi ya wanawake ama vijana.
    KARERA: Isitoshe, ipo kura ya kutokuwa na imani na mtu ama tume fulani.
                      Inaweza kutokea kwamba kiongozi fulani anatuhumiwa kukosea.
                      Basi, bunge linaweza kupitisha kura ya kutokuwa na imani naye na akafutwa kazi.
                      Katika hali kama hii, mara nyingine huteuliwa tume ya kuchunguza ukweli wa tuhuma
                      kabla ya uamuzi kama huu kutolewa.

    Zoezi

    Bainisha msamiati maalumu wa bungeni kutoka katika kifungu huku ukiutungia sentensi sahihi.

    Sifa za rejesta ya bungeni
    Rejesta ya bungeni kama rejesta yoyote ile huwa na sifa zake. Ifuatayo ni orodha ya
    baadhi ya sifa hizo:
    i) Kumrejelea spika kila wakati kwa heshima,
    ii) Matumizi ya maneno yenye adabu,
    iii) Kutokuwepo ruhusa ya kumshtaki mzungumzaji kwa maneno aliyotamka,
    iv) Kuwepo kwa lugha ya kupiga kura kwa hoja fulani,
    v) Kuwepo kwa mtindo fulani wa kuandika ama kuwasilisha hoja,
    vi) Kuwepo kwa utaratibu wa kuzungumza,
    vii) Kurejelewa kwa vifungu vya sheria mbalimbali za bunge na katiba kila wakati,
    viii)Kutumika kwa lugha ya utafiti.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Sokoni ni mahali penye mkusanyiko wa watu wanaouza na kununua bidhaa mbalimbali.
    Wauzaji wengi huuza bidhaa zao kwa rejareja, kwenye kibanda au katika maduka.
    Baadhi ya masoko hutenga siku moja au mbili kama siku maalumu za soko kila wiki.
    Siku kama hiyo ya soko huitwa chete. Masoko mengine huendesha shughuli zake kila
    siku. Bidhaa nyingi huuzwa sokoni.

    Soma kifungu hiki ili kujifunza mengi kuhusu rejesta ya sokoni.
    (Umuhire anaingia sokoni. Sauti za wauzaji mbalimbali zinasikika.)

    SAUTI: Mia bei! Mia bei...Karibu mteja..Ni za leo...ni za leo...bei rahisi...bei ya
                 jioni...bei ya hasara...karibu, chagua...chagua...beba nguo na hamsini...
    MWUZAJI: (Umuhire anaingia katika kioski kimoja.) Karibu mteja wangu! Bei
                        rahisi kwa bidhaa nzuri! Karibu katika kibanda changu! Karibu
                        uchague bidhaa utakazo. Leo nina mboga safi safi, matunda
                        matamu matamu na nyanya kubwa kubwa.
    UMUHIRE: Ahaa! Leo sina pesa ya matunda. Nitanunua siku nyingine.
                      Una kitunguu?                              
    MWUZAJI: Siwezi kukosa                              
                       vitunguu, bi mdogo.                     
                        Ndivyo hivi hapa.
    UMUHIRE: Je, kifungu kimoja ni
                       pesa ngapi?
    MWUZAJI: Hicho ni bei rahisi sana.
                       Kila kifungu ni faranga kumi tu.
                       Nikufungie ngapi?
    UMUHIRE: Aa! Hiyo ni bei ghali mno.
                       Tafadhali, niuzie vifungu
                        vitano kwa faranga arubaini.
    MWUZAJI: Hapo umenizamisha, bi mdogo.
                       Sitapata faida yoyote. Bei ni hiyo tu.
    UMUHIRE: Wewe nawe!
                       Faida utapata  kwa       
                       bidhaa nyingine.
                       Hutaki nirudi tena?
    MWUZAJI: Ninataka urudi kila mara. Basi ongeza faranga tano nikufungie.
    UMUHIRE: Jamani! Unataka tule mboga bila chumvi?
                        Hiyo faranga tano ni ya chumvi.
    MWUZAJI: (Anacheka) Nami hutaki nile chamcha?
                        Hiyo faranga tano ni ya kujinunulia chakula.
                        Unataka babu yako afe kwa njaa?
    UMUHIRE: Haya! Chukua faranga zako arubaini na tano.
    MWUZAJI: Asante bi mdogo. Chukua bidhaa zako.
    UMUHIRE: Asante.
    MWUZAJI: Karibu tena. Mbona hununui mboga pia?
    UMUHIRE: Mboga ninazo katika shamba langu nyumbani.
    MWUZAJI: Pongezi sana. Una aina gani ya mboga?
    UMUHIRE: Nina sukumawiki.
    MWUZAJI: Unaweza kuniuzia gunia moja la sukumawiki?
    UMUHIRE: Sawa. Nitakuletea siku ya Jumamosi. Nyama inauzwa wapi?
    MWUZAJI: Nyama inauzwa kwenye buchari. Buchari ipo nyuma ya kibanda hiki.
    UMUHIRE: Nimeshukuru.: Jamani! Unataka tule mboga bila chumvi? Hiyo
                       faranga tano ni ya chumvi.
    MWUZAJI: (Anacheka) Nami hutaki nile chamcha? Hiyo faranga tano ni ya
                       kujinunulia chakula. Unataka babu yako afe kwa njaa?
    UMUHIRE: Haya! Chukua faranga zako arubaini na tano.
    MWUZAJI: Asante bi mdogo. Chukua bidhaa zako.
    UMUHIRE: Asante.
    MWUZAJI: Karibu tena. Mbona hununui mboga pia?
    UMUHIRE: Mboga ninazo katika shamba langu nyumbani.
    MWUZAJI: Pongezi sana. Una aina gani ya mboga?
    UMUHIRE: Nina sukumawiki.
    MWUZAJI: Unaweza kuniuzia gunia moja la sukumawiki?
    UMUHIRE: Sawa. Nitakuletea siku ya Jumamosi. Nyama inauzwa wapi?
    MWUZAJI: Nyama inauzwa kwenye buchari. Buchari ipo nyuma ya kibanda hiki.
    UMUHIRE: Nimeshukuru.

    Zoezi

    1. Eleza maana ya maneno yaliyokolezewa wino katika kifungu.
    2. Tunga sentensi ukitumia msamiati ulioorodhesha hapo juu.

    Sifa za rejesta ya sokoni
    Sifa zinazobainisha rejesta ya sokoni ni:
    i) Lugha ya kurudiarudia maneno hutumika huku bidhaa zikinadiwa,
    ii) Lugha ya kuwavutia wateja huweza kutumiwa,
    iii) Hutumika lugha isiyo rasmi na sarufi hukosa kufuatwa,
    iv) Kiimbo cha wauza bidhaa hutumika kama vile kuzungumza kwa upole kwa
         wazee na kutumia lugha ya kusifu kwa wateja wanaonekana tajiri,
    v) Lugha ya kununua na kuuza hutumiwa kama vile: panda bei, shuka bei

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Igizeni mazungumzo kati ya mwuzaji na mnunuzi.
    Zingatieni sifa za rejesta ya sokoni.

    vii) Rejesta ya kanisani
    Kanisa ni jengo ama mahali panapotumiwa na Wakristo kufanyia ibada.
    Ama pia neno hili lina maana ya Jumuiya ya Wakristo.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wenzako watano na mjadili mambo mnayoyaona katika mchoro ufuatao.


    Sasa someni kifungu kifuatacho na halafu mjibu maswali yaliyoulizwa.

    Mambo yote yanayohusu kanisa na imani ya mtu ni mambo magumu sana maishani mwetu.
    Amri Kumi za Mungu pamoja na amri nyingine zozote zinazohusu dini ya kweli,
    huhitaji mwanadamu kukaa katika mema na haki mbele ya Mwenyezi Mungu.
    Hayo ndiyo masharti ya Neno ama Biblia. Mitume na malaika wa Mungu
    waliwajia mara kwa mara waumini walioamini katika dini kuwakumbusha haya.
    Nayo misahafu dini mbalimbali za haki huyasisitiza yaya haya.
    Sasa ugumu huja katika kuyatekeleza.
    Hata hivyo, kupo kutubu. Huku kutubu ni njia ya pekee ya kuondoa ugumu huo.
    Kila atendaye dhambi mbele ya Mola ana ruhusa ya kutubu. Makasisi, mapadri,
    wachungaji, maaskofu, maaskofu wakuu pamoja na viongozi wengine makanisani
    wana jukumu la kuhakikisha kuwa waumini wao hutubu na kumrudia Manani.
    Nako kutubu huko kunaweza kufanywa wakati wa ibada wanapokuwa wanamwabudu
    Muumba ama wakati mwingine wowote. Kunaweza pia kufanywa kupitia kwa sala.
    katika haya yote, ni sharti ikumbukwe kwamba mwovu shetani hapumziki mpaka
    aone kuwa binadamu wengi ama wote wamo katika dhambi. Binadamu huyo akitubu,
    malaika mbinguni wanafurahi sana. Lakini shetani anatafuta njia nzuri
    nzuri za kumfanya mwanadamu yuyo huyo arudi dhambini tena.
    Mbinu zake nyingi huwa za msingi wa raha. Anajua kuwa binadamu ni mpenda raha.
    Hata hivyo, lipo Neno linalovunjavunja juhudi kama hizo.
    Kanisa huhubiri habari za jahanamu, kuangamia motoni, kuingia mbinguni, njia
    pana, njia nyembambana, msalaba wa Yesu, Mwokozi Yesu, Utatu wa Uungu, na
    hata siku ya kiama. Jahanamu ama ahera ni pahali ambapo inaaminika roho za wale
    waliokufa huenda kungoja siku ya kiama ambayo itakuwa siku ya kutolewa
    hukumu na Mungu Muumba. Swali kuu siku hiyo litakuwa, Umefanya nini na Neno langu?
    Wale ambao hawatajibu vilivyo watatupwa motoni na wale ambao watajibu vilivyo wataingia mbinguni.
    Jambo jingine kanisani ni msalaba. Yesu Kristo alisulubishwa kwenye msalaba
    ili amfie mwanadamu apate kuokolewa na damu yake. Kwa hiyo, msalaba ni
    ukumbusho kwamba tayari mwanadamu ameokolewa na analohitaji kufanya ni kuungama dhambi zake.
    Jambo jingine ni kwamba maeneo mbalimbali ya kuabudia huwa na maneno
    wanayochukulia kuwa yanawawezesha kuwasiliana vilivyo na Mungu.
    Maeneo hayo ni kama vile kanisani, msikitini, hekaluni na kwingineko kukiwa pamoja na barabarani.

    Zoezi
    Jiunge na mwenzako. Jadilianeni maana ya maneno yaliyokolezewa wino na
    msamiati zaidi unaotumiwa kanisani na msikitini.

    Sifa za rejesta ya kanisani
    Baadhi ya sifa za rejesta ya kanisani ni kama vile:
    i) Huwepo na pahali pa kumwabudia Mungu,
    ii) Katika baadhi ya dini, hutumika msamiati wa wale walioileta dini k.v. Kiingereza,
    iii) Huwezekana kuwepo mkalimani wa kutafsiri na kufasiri,
    iv) Baadhi ya wahubiri huanza kuzungumza kwa kasi wanapopandwa na jadhba,
    v) Sadaka hupewa majina mbalimbali na huwa ni sharti zitolewe,
    vi) Waumini hawana ruhusa ya kuulizia wasilolielewa wakati mhubiri anapokuwa anahubiri,
    vii) Ni sharti msamiati wa kidini utumiwe badala ya ule wa lugha ya kawaida,
    viii)Huwepo kwaya ama mwimbaji, ix) Vifungu mbalimbali vya Biblia hunukuliwa.

    viii) Rejesta ya sarufi ya Kiswahili
    Sarufi ni kanuni za lugha zitumiwazo ili kupata ufasaha katika lugha. Kila lugha
    huwa na sarufi yake. Hivyo basi, ipo sarufi ya Kiswahili ambayo ina rejesta yake.





    Someni kifungu kifuatacho ili kujifunza maneno zaidi ya sajili hii ya lugha.

    Fikiria ingekuwaje kama hatungekuwa na lugha? Hata ishara mbalimbali zina msingi wa lugha.
    Ama kwa kweli, mambo mengi yangalikwama kama hapangekuwa na lugha.
    Rejesta ya lugha ni muhimu kama lugha ilivyo kwa kuwa mambo hayo mawili
    ni jambo moja tu. Katika rejesta ya sarufi mna maneno kama vile sajili, sarufi,
    Kiswahili, sentensi, lafudhi, alfabeti, vitenzi, mnyambuliko, maandishi, majina,
    namna za majina, vivumishi, vielezi, viwakilishi, viunganishi, vihusishi, vihisishi,
    aya, kuakifisha na kadhalika.
    Ukija kuangalia maana ya maneno haya, unapata kuwa sajili ni rejesta kama
    ilivyoelezwa hapo awali lakini sarufi ni sheria ziongozazo lugha fulani. Nacho
    Kiswahili ni lugha izungumzwayo na Waswahili lakini sentensi ni tungo
    ijitoshelezayo na ambayo huhusisha mtendaji na kitendo. Nayo lafudhi au lafidhi
    ni namna maneno yanavyotamkwa ilhali alfabeti ni herufi za lugha ambazo
    zimepangwa kwa utaratibu maalumu.
    Navyo vitenzi ni maneno yakuambiayo cha kufanya na mnyambuliko ni namna
    vitenzi hivyo hujigeuzageuza ili kuleta maana ihitajikanayo. Maandishi nayo ni
    kuwakilisha sauti kwenye karatasi kwa kutumia kalamu ilhali majina ni neno la
    kumtaja mtu, kitu au jambo.
    Namna za majina ni vikundi vya majina yanayochukua sifa fulani inayoyasawazisha.
    Vivumishi ni maneno yaongezeayo majina maana na pia kujiongezea maana.
    Vielezi navyoni maneno yaongezeayo vitenzi maana ilhali viwakilishi ni maneno a
    ma viungo vya maneno vinavyosimamia majina.
    itoshe, kuna viunganishi, vihusishi, vihisishi, aya, na kuakifisha. Viunganishi ni
    maneno yanayounganisha maneno mengine lakini vihusishi huhusisha watu ama
    vitu na mahali. Navyo vihisishi ni maneno yanayoonyesha mahangaiko ya moyo
    ilhali aya ni fungu la sentensi lililo na maana kamilifu, yaani paragrafu. Nako
    kuakifisha ni kuwakilisha sauti kimaandishi. Ufahamu ni pale ambapo mtu husoma
    kifungu na halafu akapima ama akapimwa ufahamu wake kuhusu hayo aliyoyasoma.
    Imla nayo ni pale ambapo unasomewa maneno ama kifungu huku ukiandika.

    Zoezi

    Jiunge na wenzako watatu na mjadili maana na matumizi ya maneno haya yafuatayo:
    1. mtungo au insha                       2. msamiati                                  3. rejesta
    4. vitendawili                                 5. methali                                      6. misemo
    7. nahau                                        8. mafumbo                                  9. barua
    10. masimulizi                               11. dhahania                                12. istilahi
    13. kiimbo

    Sifa za rejesta ya sarufi ya Kiswahil
    Nazo sifa za rejesta ya sarufi ya Kiswahili zinaweza kuwa hivi:
    i) Imejaa maneno ya kitaalamu,
    ii) Hufundisha jinsi ya kutunga tungo sahihi,
    iii) Huwa na semi za kutia hekima,
    iv) Huwa ndio msingi wa maongezi yote katika lugha husika,
    viii)Huwezesha kuhifadhi mila za kabila husika,
    ix) Huwa na tamathali za usemi za kuungia usemi

    Zoezi la ziada
    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako na mjibu maswali yaliyopo hapa chini.

    Jazeni jedwali hili. Sehemu ya kwanza imejazwa kama mfano










    B . Matumizi ya majina ya ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi

    Ngeli ya KI-VI hujumuisha majina mbalimbali. Majina yote katika ngeli hii huchukua
    upatanisho wa sarufi, ki- katika umoja na vi- katika wingi. Hii ndiyo sababu ya ngeli
    hii kuitwa ngeli ya KI-VI. Maumbo ya majina katika ngeli ya KI-VI hubadilika kutoka umoja hadi wingi.

    Je, unakumbuka majina yanayopatikana katika ngeli hii? Yataje matano katika
    umoja pamoja na wingi wayo.
    Tazama jedwali hili. Je, ni mabadiliko gani yanayotokea katika majina yanapotoka umoja hadi wingi?






    Yapo makundi mbalimbali ya majina yanayopatikana katika ngeli ya KI-VI.

    i)    Majina yanayoanza kwa ki- katika umoja na kuchukua vi- katika wingi
    Kundi hili la majina ndilo huwa na majina mengi ya ngeli hii ya KI-VI.


    Kumbuka
    Majina ya viumbe wenye uhai ambayo huanza kwa kiambishi ki- katika umoja na vi- katika
    wingi hayawekwi hapa bali huchukua viambishi ngeli vya ngeli ya A-WA

    Zoezi

    Andika majina kumi zaidi ya ngeli ya Ki-Vi pamoja na wingi wayo.

    ii) Majina yanayoanza kwa ch- katika umoja na kuchukua vy- katika wingi

    Kumbuka
    Majina ya viumbe wenye uhai ambayo huanza kwa kiambishi ch- katika umoja na
    vy- katika wingi hayawekwi hapa bali huchukua viambishi ngeli vya ngeli ya A-WA.

    Zoezi

    Andika majina kumi zaidi yanayopatikana chini ya orodha hii ya majina katika ngeli ya KI-VI.

    iii) Majina kutokana na vitenzi

    Yapo baadhi ya majina ambayo huundwa kutokana na vitenzi. Majina hayo pia hupatikana katika ngeli ya KI-VI.
    Mfano

    Zoezi

    Andika majina kumi zaidi yaliyomo katika kundi hili.

    iv) Majina yanayoanza kwa ki- lakini hayachukui wingi
    Yapo majina katika Kiswahili ambayo huanza kwa kiambishi ki- lakini hayana wingi.
    Majina haya huwa ya viumbe wasiokuwa na uhai.

    Zoezi

    Andika majina matano zaidi yanayopatikana katika kikundi hiki.

    v) Majina ya vitu katika hali ya udogo
    Katika Kiswahili, majina yanaweza kuwa katika hali ya wastani, udogo au ukubwa.

    Majina yote yanapoandikwa katika hali ya udogo, huwekwa katika ngeli ya KI-VI
    iwe majina ya viumbe wenye uhai au vitu visivyokuwa na uhai.
    Katika mfano uliotolewa hapo juu, mtu na mtoto ni viumbe wenye uhai.
    Majina haya hupatikana katika ngeli ya A-WA. Unaposema kijitu au kitoto,
    unarejelea mtu mdogo zaidi ya kawaida. Kwa hivyo, majina kitoto na kijitu yanawekwa katika
    ngeli ya KI-VI. Katika wingi huwa tunasema vitoto au vijitu. Vilevile, nyumba ipo katika ngeli ya I-ZI.
    Hata hivyo, kijumba (nyumba ndogo kupita kiasi) hupatikana katika ngeli ya KI-VI.
    Tazama mifano zaidi katika jedwali hapa chini.

    Zoezi

    Andika majina matano zaidi yanayopatikana katika orodha hii ya majina katika ngeli ya KI-VI.

    Matumizi ya majina ya ngeli ya KI-VI
    Kama ilivyoelezwa hapo mwanzoni, vitenzi vinavyoambatana na majina katika
    ngeli hii ya KI-VI huchukua kiambishi ki- katika umoja na vi- katika wingi.
    Tazama mifano iliyotolewa katika jedwali lifuatalo:

    Zoezi

    1. Eleza maana ya ngeli ya KI-VI.
    2. Eleza mabadiliko yanayotokea katika wingi ukirejelea majina haya ya ngeli ya KI-VI.
        i) chombo    ii) kioo    iii) kiti     iii) cheo
    3. Kamilisha sentensi zifuatazo:
       i) ___akula ___livyonunuliwa ___meliwa.
      ii) ___dege ___mekamatwa.
     iii) ___beti ___mejaa faranga.
     iv) ___sima vya maji ___nachimbwa hivi sasa.
      v) Niliwaambia waniletee ___uma ___livyokunjwa.
     vi) Nitasoma kwa bidii ili niingie katika __uo _kuu.
    4. Bainisha sentensi sahihi kutoka kwa zile zisizokuwa sahihi na uzisahihishe.
        Nambari za kwanza mbili zimetolewa kama mfano.
      i) Kiti hiki kinapendeza. SAHIHI
     ii) Choo vimebomolewa. SI SAHIHI. Vyoo vimebomolewa. SAHIHI
    iii) Viswahili kinazungumzwa Afrika Mashariki.
    iv) Kioo kinanipendeza.
     v) Kitoto anaruka.
    vi) Kijiti limevunjika.
    vii) Vyuo vikuu vinatoa elimu ya juu.
    viii)Vyuma kinachomwa.
    ix) Kigelegele kinasikika.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tungeni sentensi sahihi katika umoja na wingi
    mkitumia majina ya ngeli hii ya KI-VI.

    Matumizi ya majina ya ngeli ya KI-VI pamoja na vivumishi
    Je, unakumbuka vivumishi ulivyosoma katika sura ya kwanza? Rejelea vivumishi hivyo.

    a) Majina ya ngeli ya KI-VI pamoja na vivumishi vya sifa
     Vivumishi vya sifa ni maneno yatajayo tabia au sifa za mtu, kitu au jambo.
    Mifano katika sentensi:


    Zoezi

    Tunga sentensi zozote kumi ukitumia majina ya ngeli ya KI-VI na vivumishi mbalimbali vya sifa.

    b) Majina ya ngeli ya KI-VI pamoja na vivumishi vya pekee
    Vivumishi vya pekee hutoa habari kuhusu nomino au kiwakilishi chake kwa njia ya kipekee.
    Huwa vitano.

    i) -enye           ii) -enyewe          iii) -ote          iv) -o-ote          v) -ingine
    Majina katika ngeli ya KI-VI huchukua kiambishi ch- katika umoja na vy- katika wingi yanapotumika pamoja na
    vivumishi vya pekee vyote isipokuwa -ingine au -ingineo.

    Hata hivyo, kivumishi cha pekee -ingine na -ingineo huchukua viambishi ki- katika umoja na vi- katika wingi kinapotumika na majina ya ngeli ya KI-VI.

    Zoezi

    Tunga sentensi zozote kumi ukitumia majina ya ngeli ya Ki-Vi pamoja na vivumishi mbalimbali vya pekee.

    c) Majina ya ngeli ya KI-VI pamoja na vivumishi vionyeshi
    Vivumishi vionyeshi au viashiria ni maneno ya kuonyesha alipo mtu au kitu, yaani ujirani.
    Kuonyesha huko kunaweza kuwa kwa ujirani wa karibu – hapa,
    ujirani wa mbali kidogo – hapo, na ujirani wa mbali – pale.

    Katika ngeli ya KI-VI, kivumishi kionyeshi cha karibu huwa: hiki (umoja) na hivi (wingi),
    kionyeshi cha mbali kidogo huwa hicho (umoja) na hivyo (wingi) na kionyeshi cha mbali huwa
    kile (umoja) na vile (wingi).

    Mfano katika sentensi:

    Zoezi

    Tunga sentensi zozote sita ukitumia majina ya Ki-Vi pamoja na vivumishi vionyeshi mbalimbali.

    d) Majina ya ngeli ya KI-VI pamoja na vivumishi vya idadi
    Vivumishi vya idadi ni maneno yanayoonyesha idadi ya watu ama vitu. Vipo vivumishi vya idadi kamili,
    vivumishi vya idadi ya jumla na vivumishi vya idadi ya matokeo.

    Majina ya ngeli ya KI-VI huchukua viambishi ki- katika umoja na vi- katika wingi
    yanapotumika pamoja na vivumishi vya idadi vinavyochukua viambishi.
    Kumbuka
    Idadi sita, saba, tisa na kumi hazichukui kiambishi chochote cha ngeli.

    Zoezi

    Tunga sentensi zozote kumi ukitumia majina katika ngeli ya KI-VI na vivumishi mbalimbali vya idadi.

    e) Majina ya ngeli ya KI-VI pamoja na vivumishi viulizi
    Hili ni kundi la vivumishi ambalo lina maneno yatumiwayo kuulizia maswali.
    Baadhi ya mifano ya vivumishi viulizi ni: -pi?, na -ngapi?

    Majina katika ngeli ya KI-VI huchukua kiambishi ki- katika umoja na vi- katika wingi yanapotumiwa pamoja na viulizi.
    Kumbuka
    Kiulizi -ngapi hutumika katika wingi pekee.
    Kiulizi gani? hakichukui kiambishi.
    Tunasema: Kijiko gani? au vijiko gani?

    Zoezi

    Tunga sentensi zozote tano ukitumia majina ya ngeli ya KI-VI na vivumishi viulizi mbalimbali.

    f) Majina ya ngeli ya KI-VI pamoja na vivumishi vimilikishi
    Maneno katika kundi hili la vivumishi hujibu swali mtu, kitu au jambo ni la nani?
    Maneno haya huwa sita pekee katika Kiswahili.
    -angu           -etu
    -ako             -enu
    -ake             -ao

    Katika ngeli ya KI-VI, kiambishi ch- hutumika katika umoja na vy- katika wingi.

    Zoezi

    Tunga sentensi zozote sita ukitumia majina katika ngeli ya KI-VI na vivumishi mbalimbali vya kumiliki.

                                  Maswali ya marudio
    1. Kwa maneno yako mwenyewe, eleza maana ya rejesta za lugha.
    2. Jaza jedwali hii kwa kuandika mifano kumi ya msamiati unaotumika katika kila rejesta iliyotajwa.
       
    3. Eleza sifa za rejesta zifuatazo:
        a) Michezo
        b) Burudani
        c) Hotelini
        d) Sokoni
    4. Pana tofauti gani kati ya rejesta ya burudani na ile ya michezo?
    5. Rejesta ya hotelini ni sawa kabisa na ile ya sokoni. Je, haya ni kweli? Kwa nini?
    6. a) Bainisha aina mbalimbali za michezo katika jamii.
        b) Eleza umuhimu wa michezo katika afya ya binadamu.
    7. a) Taja namna mbalimbali za burudani katika jamii.
        b) Eleza umuhimu wa burudani kiafya na kiushirikiano.
    8. Eleza umuhimu wa kuonyesha adabu na heshima kwa watu katika mazingira mbalimbali.
    9. Bainisha rejesta zifuatazo na utaje sifa zao za kimsingi:
       a) Mheshimiwa spika, sheria hii imekiuka katiba ya nchi yetu. Mheshimiwa spika,
           ikiwa sheria hii itapitishwa jinsi ilivyo, patatokea migogoro.
       b) Bei rahisi...bei imeshuka...njoo mteja..karibu..usitembee kwa miguu
           mitupu....nunua viatu kabla bei kupanda...
       c) Maandiko yanasema kuwa wenye dhambi watachomwa motoni.
    10. Linganisha na utofautishe rejesta ya bungeni na mahakamani.
    11. Rejesta ya hospitalini inaweza kufaa sana katika mazingira ya jikoni.
          Hili ni sawa? Kwa nini?
    12. Taja maneno sita ya rejesta ya utamaduni.
    13. Huku ukitoa mifano, eleza rejesta ya sarufi.
    14. Tunga sentensi sahihi ukitumia msamiati ufuatao:
        a) mwana mpotevu
        b) baraka
        c) mpira umekuwa mwingi
        d) densi
        e) bei ghali
        f ) ankra
        g) kukata rufaa
    15. Andika maneno haya katika wingi:
       a) chombo
       b) kiti
       c) kioo
       d) choo
    16. Eleza muundo wa nomino za ngeli ya Ki-Vi katika umoja na wingi.
    17. Tunga sentensi tano tano ukitumia majina ya ngeli ya Ki-Vi na vivumishi
           vilivyotolewa hapa chini katika umoja na wingi.
        a) vivumishi vya sifa
        b) vivumishi vionyeshi
        c) vivumishi viulizi
        d) vivumishi vimilikishi
    18. Sahihisha makosa katika sentensi hizi:
         a) Kijiko vyangu kimenunuliwa.
         b) Vioo vikumi vitaletwa kesho.
         c) Niletee kitabu hivyo.
         d) Vyumba chote vimefagiliwa.
    19. Tunga sentensi sahihi ukitumia vivumishi vilivyotolewa.
         a) vyetu
         b) vinane
         c) kile
         d) kipi
         e) vyenyewe
    20. Eleza jinsi utakavyotumia ujuzi uliopata katika sura hii.

  • Sura 4: Mazungumzo na mawasiliano katika shughuli mbalimbali za kijamii

    Mada ndogo: Msamiati katika kazi za jumuiya

    A . Shughuli mbalimbali za jumuiya

    i) Mkutano wa kijiji chetu
    Kijiji ni mgao wa chini zaidi katika migao ya utawala. Kijiji aghalabu hujumuisha
    watu wanaotoka koo mbalimbali na ambao wanajuana. Watu hawa huja pamoja
    kufanya shughuli mbalimbali. Mikutano mbalimbali ya vijijini huweza kutumiwa
    kuinua hali ya maisha ya jamii ya vijiji hivyo.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Je, kijiji chenu kinaitwaje? Je, umewahi kuhudhuria mkutano wa kijiji chenu? Jiunge
    na mwanafunzi mwenzako na mjadilianeni shughuli mbalimbali ambazo hufanyika
    katika mikutano vijijini mwenu.

    Sasa tazameni michoro iliyopo hapa chini na msome kifungu cha habari.
    Mimi ni Munyana. Leo ni siku ya mkutano wa kijiji hiki chetu. Mwenyekiti wa
    kijiji chetu anamwomba Nziza kufungua                
    mkutano kwa maombi. Wanakijiji wote
    wanasimama na kuomba kisha wanakaa.

    “Asanteni sana kwa kuitikia mwaliko wa
     mkutano wetu. Shughuli yetu kuu siku
    ya leo ni kujadiliana kuhusu ugonjwa
    wa UKIMWI. Patakuwepo upimaji
    wa UKIMWI ndani ya hema. Upimaji
    utakuwa kwa hiari yako. Kwa sasa,
    ninamwalika mgeni wa heshima katika
    mkutano wetu huu wa leo atuhutubie.
    Mgeni huyo ni afisa wa afya kutoka
    Wizara ya Afya, Bi. Abigael Uwera.
    Tumkaribishe kwa makofi na vigelegele.”
    Watu wote wanasimama na kupiga
    makofi.

    “Mabibi na mabwana, UKIMWI ni ugonjwa usiojua umri, utajiri wala umaskini. Uwe
    tajiri au maskini unaweza kuupata. Unamshika yeyote anayeshiriki ngono hasa
    bila kutumia kinga. Pia, unaweza kuambukizwa ikiwa damu yenye maradhi haya
    imechanganyika na damu yako. Damu hizi zinaweza kuchanganyika kwa kutumia
    sindano au wembe mmoja au kugusa damu ya mtu aliyeambukizwa. Tukumbuke
    kuwa huwezi kupata UKIMWI kwa kumsalimia au kumkumbatia au kula pamoja na
    mtu aliyeambukizwa.”
    Watu wanatazamana na kunong’onezana. Ninainua mkono na kumwuliza mgeni
    wa heshima ikiwa ugonjwa huu una tiba.
    “La hasha! Ugonjwa huu hauna tiba. Hata hivyo, zipo dawa nzuri za kupunguza
    makali yake. Unapougua UKIMWI, ni sharti utumie dawa hizi tena kwa wakati
    uliopendekezwa bila kukosa. Ni vizuri sote tujue kuwa miili yetu ina chembechembe
    katika damu zetu ambazo hutukinga dhidi ya magonjwa. UKIMWI hudhoofisha
    chembechembe hizi. Miili yetu hukosa uwezo wa kupiga vita dhidi ya magonjwa.
    Hivyo, waathiriwa huweza kuuliwa na magonjwa kama vile malaria, kifua kikuu na
    magonjwa mengineyo.”
    Bi. Mutesi anainua mkono. Anapewa nafasi ya kuongea.
    “Mimi ni mwathiriwa wa ugonjwa huu wa UKIMWI. Bwanangu aliaga dunia kutokana
    na ugonjwa huu. Wanangu wawili pia wanaugua ugonjwa huu. Sote tumekubali
    hali zetu. Tunatumia dawa za kupunguzia makali. Tunakula vizuri na kuendelea na
    shughuli zetu za kila siku. Ningependa kuwaambia wenzangu ambao wanaugua
    ugonjwa huu wasiogope. Ninawashukuru sana wanakijiji hiki kwa kunionyesha
    mapenzi na kunisaidia kukubali hali yangu. Kwa wale ambao hawana UKIMWI,
    nawasihi mwepuke ngono nje ya ndoa. Wasichana kwa wavulana, jiepusheni na
    ngono hadi mfunge ndoa. Asanteni.”
    Tunampigia Bi. Mutesi makofi. Wengine wanasimama na kumkumbatia. Anaonekana
    mwenye afya nzuri. Kumbe mtu anayeugua UKIMWI huwa na afya nzuri! Huwezi
    kujua anayeugua ugonjwa huu kwa kumtazama. Njia ya kipekee ni kupitia upimaji.
    Ninasimama na kuwahutubia wanakijiji.
    “Mimi nipo tayari kupimwa. Baada ya kupimwa, nitakubali hali yangu. Ikiwa
    sina, nitajilinda. Baada ya kumaliza masomo na kuanza kufanya kazi, nitakubali
    kuchumbiwa. Nitamwambia mpenzi wangu tujipime ili tuwe na uhakika wa hali
    zetu. Nitakuwa mwaminifu kwake. Nipo tayari kushirikiana na wanakijiji wenzangu
    ili tuwapende na kuwasaidia waathiriwa wa UKIMWI. Pia, nipo tayari kujiunga na
    wanakiji kufanya kampeni ya kuwahamasisha wenzetu wajue kuhusu UKIMWI na
    waepuke kuambukizwa ugonjwa huu. Asanteni.”
    Wanakijiji wote wanasimama. Wanasema kwa pamoja kuwa wako tayari kujua na
    kukubali hali zao za UKIMWI.
    “Haya, twende tukajipime wenzangu,” anasema Kiongozi wa kijiji. Watu wote
    wanapiga foleni nyuma yake.

    Maswali
    1. Bainisha msamiati wa kimsingi kifunguni kuhusu shughuli katika mkutano na
        uutolee maana.
        Mfano: kufungua mkutano: kutangaza rasmi kuwa mkutano umeanza.
    2. Ni nini kilichokuwa kiini cha mkutano uliopo kifunguni?
    3. Nani alikuwa mgeni rasmi katika mkutano wa kijiji?
    4. Eleza mambo muhimu yanayojitokeza katika kifungu hiki.
    5. Toa muhtasari wa kifungu cha habari ulichosoma hapo juu katika aya moja.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wenzako katika kikundi. Nyinyi ni wanachama wa kijiji kimoja. Mmeandaa
    mkutano. Jadilianeni kuhusu mambo mbalimbali mtakayofanya ili kuangamiza
    umaskini katika kijiji chenu.

    ii) Sherehe ya harusi ya rafiki yangu
    Kazi ya wanafunzi wawili wawili

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Jadilianeni kuhusu mambo muhimu ambayo

    hufanyika katika sherehe ya harusi. Kwa mfano:

    1. Watu huja pamoja kutengeneza hema la wageni.

    2. Maarusi huimbiwa na kuchezewa.

    Baada ya kujadiliana mambo muhimu katika harusi, simulianeni kuhusu sherehe ya harusi mliyohudhuria.

    Tazama michoro hii. Je, mambo gani yanafanyika?
     

      

    Someni mazungumzo haya na mjibu maswali chini yake.

    SHEMA: Hujambo mwenzangu?

    TONA: Sijambo, ulikuwa wapi wiki nzima?

    SHEMA: Nilihudhuria harusi ya rafiki yangu.

    TONA: Kumbe! Ndiyo sababu una furaha tele.

    SHEMA: Mbona nisiwe na furaha? Ndoa ni jambo linalowafurahisha watu wengi. Kutajwa tu kwa neno hili hufanya roho za kila mtu kusisimka kwa furaha.

    TONA: Haya! Hata mimi ipo siku nilikuwa mpambe nilipokuwa mdogo. Bibi. harusi alivaa mavazi yake maalumu ya kupendeza kweli. Sisi wapambepia tulinunuliwa viatu na nguo za kupendeza. Sisi na bibi harusitulipambwa tukapambika. Nieleze kuhusu harusi hiyo uliyohudhuria.

    SHEMA: Sikujua kuwa Ganza angeweza kumchumbia msichana mrembo kamayule. Aliponiambia eti posa yake imekubalika nilidhani ananitania.Aliniandikia barua kunieleza eti amepeleka mahari. Bado sikuamini hadi aliponitumia kadi ya kunialika harusini.

    TONA: Ehe...

    SHEMA: Mimi nilifika mapema na wenzangu kumsaidia rafiki yangu.Tulitengeneza mahema na kupanga viti hemani. Wengine walirembeshamahema kwa maua, baluni, na mapambo yenye rangi mbalimbali. Mahema yale yalivutia kwelikweli. Wengine walikuwa jikoni wakiandaa vyakula nao wengine walipokea wageni ambao walianza kuwasilimapema. Tukakodisha magari ambayo yangemsafirisha bwana na bibiharusi. Tukahakikisha kuwa vyombo vya burudani vipo katika hali sawatayari kuwatumbuiza wageni.

    TONA: Ahaa! Bibi harusi alikuwa wapi wakati huu wote?

    SHEMA: Ah! Kwani hujui? Bibi harusi alikuwa mahali kusikojulikana. Huko alikuwa na wapambe ambao walikuwa wakimrembesha.

    TONA: Ehe...

    SHEMA: Baada ya maandalizi, nikajiunga na wanaume ambao huandamana nabwana harusi. Pale, tulipewa mafunzo ya jinsi ya kutembea nakumsindikiza bwana harusi. Tukapima suti zetu nyeusi na kujaribu kutembea kwa viatu vyetu vipya. Bwana harusi naye akajaribu kuvaa pete ili ahakikishe kuwa inamtosha. Kila kitu kikawa shwari.

    TONA: Nieleze mambo yaliyojiri siku ya harusi.

    SHEMA: Harusi hiyo ilianza kwa watu kukaa kanisani kwa matarajio makubwahuku wakinong’onezana. Mara mfawidhi akatangaza kuwa tusimamekwa kuwa bibi harusi sasa anaingizwa kanisani. Bibi harusi akasindikizwa kanisani na babake na kupelekwa pale mbele alipokuwa akisubiriwa na mchumba wake pamoja na mchungaji. Hapo, waliapishwa na halafu kuvishana pete na mwishowe kutangazwa bibi na bwana. Wacha sasasherehe kamili zianze. Waliokula walikula na waliokunywa walikunywa.Nao waliocheza walicheza na waliofanya urafiki kwa matarajio yakufanya ndoa kama hiyo walifanya.

    TONA: Ama kwa kweli harusi hiyo ilifana kweli! Asante.

    SHEMA: Karibu.

    Maswali

         1. Kwa nini ndoa ni jambo la kufurahisha?

         2. Eleza maana ya msamiati uliowekewa wino nzito.

         3. Tunga sentensi sahihi ukitumia msamiati ulioeleza hapo juu.

         4. Eleza mambo muhimu yanayofanyika harusini kwa mujibu wa kifungu hiki.

         5. Eleza umuhimu wa ushirikiano katika jamii kwa kurejelea matukio kifunguni.

         6. Toa muhtasari wa kifungu hiki cha habari katika aya moja.

    iii) Mazishi

    Mazishi ama maziko ni shughuli za kuzika mfu au wafu. Mfu ni mtu aliyeaga dunia. Shughuli hizi huendeshwa kutegemea utamaduni na imani za kidini za wahusika au waathiriwa.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tazameni mchoro ulio kwenye ukurasa ufuatao. Je, ni shughuli gani inayofanywa? Jadilianeni kuhusu shughuli ambazo hufanywa wakati wa mazishi katika jamii yenu.

    Soma kifungu kilichopo hapa chini na ujibu maswali chini yake.

    Sikujua kuwa sigara huua hadi nilipompoteza mjomba wangu mwaka jana. Mjomba aliaga dunia kutokana na ugonjwa wa saratani ya mapafu. Alipenda sana kuvuta sigara. Aliaga dunia katika hospitali moja jijini Kigali. Punde tu alipofariki, mwili wa mjomba ulipelekwa katika mochari. Huko, mwili wake ulisafishwa na wahudumu wa mochari na kuwekwa katika jokofu.

    Jamaa na marafiki walikuja pamoja kumpa mjomba heshima zake za mwisho. Wanakijiji na watu kutoka mbali walishiriki katika shughuli mbalimbali kufanikisha mazishi ya mjomba.

              

    Wanakijiji walichanga pesa za kulipia gharama za mochari na shughuli nyinginezo. Wengine walijitolea kutengeneza jeneza zuri la kumzikia mjomba. Wengine walinunua sanda. Wengine walichimba kaburi. Kila mtu alishiriki katika shughuli hizi kadiri ya uwezo wake.

    Mwili wa mjomba uliondolewa kwenye mochari baada ya wiki moja. Mwili huo ulisafirishwa hadi kanisani. Alifanyiwa ibada ya wafu. Jamaa na marafiki walifika kanisani kushiriki katika ibada hiyo.

    Baada ya maombi, watu walipewa ruhusa ya kutazama mwili wa mjomba. Hali ya huzuni ilitanda kanisani.Baada ya ibada, mwili huo ulisafirishwa nyumbani kwake. Mimi na jamaa za mjomba tulihuzunika. Wanakijiji na marafiki zetu walitufariji.

    Siku ya mazishi ilipofika, ibada ya wafu iliandaliwa. Mchungaji aliendesha shughuli akishirikiana na familia ya marehemu mjomba. Mchango wa kusaidia familia ya marehemu mjomba pia ulifanywa. Wanakijiji na wageni walitoa michango yao. Hatimaye wakati wa kuteremshwa kwa jeneza kaburini ulifika. Baada ya maombi mafupi kando ya kaburi, jeneza lilitiwa ndani ya kaburi. Mchungaji alituhutubia.

    “Tunasikitika kuwa marehemu aliaga dunia kutokana na uvutaji wa sigara. Nawasihi vijana kwa wazee mwepuke uraibu wa sigara na dawa za kulevya. Tumempoteza mwenzetu aliyekuwa na bidii ya mchwa. Tuige tabia zake nzuri na kuepuka zile mbaya. Ikiwa pana mtu ambaye mfu huyu alikuwa na deni lake, aseme sasa.”

    Hakuna aliyeinua mkono. Mhubiri alifanya ombi la mwisho kisha shughuli za kufunika kaburi zikaanza. Familia ya mjomba ilikuwa ya kwanza kuweka mchanga kwenye kaburi. Baadaye, wanakijiji walisaidia katika kufunika kaburi.

    “Asanteni kwa kushiriki katika mazishi haya. Tunamwomba Mungu amlaze mahali pema peponi,” mhubiri alisema kisha watu wakaondoka.

    Wageni kutoka mbali walipewa vyakula na vinywaji. Baadaye waliondoka kwenda zao.

    Maswali

    1. Kwa maneno yako mwenyewe, eleza maana ya mazishi.

    2. Bainisha na utoe maana ya msamiati mbalimbali kuhusu mazishi kifunguni.

    3. Tunga sentensi ukitumia msamiati uliotajwa hapo juu.

    4. Eleza shughuli muhimu za mazishi zilizotajwa kifunguni.

    5. Kwa maneno yako mwenyewe, eleza mambo muhimu kifunguni katika aya moja.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako. Jadilianeni kuhusu utaratibu wa mazishi ya kienyeji katika sehemu mtokako.

    iv) Kazi ya umuganda
    Umuganda ni mkusanyiko wa watu kutoka vijiji mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa taifa. Mnamo siku ya Jumamosi ya mwisho kila mwezi, Wanyarwanda wote walio na miaka kati ya kumi na minane na sitini na mitano hukusanyika katika makundi mbalimbali kushiriki katika kazi za umuganda.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na wanafunzi wenzako. Jadilianeni kuhusu shughuli mbalimbali ambazo hufanywa siku ya kazi ya umuganda.

    Tazama michoro hii kuhusu shughuli mbalimbali za umuganda na usome kifungu cha habari.

      
       
    Wanyarwanda hushiriki katika shughuli mbalimbali siku ya kazi ya umuganda. Umuganda huandaliwa kila Jumamosi ya mwisho ya mwezi. Kila kijiji huamua shughuli muhimu wanazostahili kufanya. Wao huchagua shughuli ambayo ina umuhimu kwao.

    Baadhi ya wanakijiji huweka vizuizi vya mmomonyoko wa udongo kwa kuchimba mitaro. Wengine wanajaza mitaro hiyo kwa magunia yaliyojaa mchanga. Wengine wanafunika magunia hayo kwa mchanga. Mvua inaponyesha, maji tu ndiyo hupita lakini udongo hubakia kwenye mitaro na magunia yaliyowekwa. Hivyo, rutuba hubakia kwenye udongo nayo ardhi huweza kutumiwa tena katika shughuli za kilimo.

               
    Wanyarwanda pia huja pamoja kusafisha maeneo wanamoishi. Watu hupewa majukumu mbalimbali wakati wa usafishaji. Baadhi ya watu huondoa taka kwenye mitaro ya maji machafu. Wengine hupewa jukumu la kuokota taka zilizotapakaa. Wengine huchoma taka hizo. Nao baadhi ya watu kufyeka nyasi zilizomea kando ya mitaro na maeneo mengineyo. Shughuli hizi hulenga kudumisha usafi katika miji na vijiji vyetu.



           
    Wanyarwanda pia hupanda miti siku ya kazi ya umuganda. Wao hupanda miti hasa kwenye ardhi tambarare. Wengine hunyunyizia miche maji. Miti mingi hupandwa na wanakijiji mbalimbali kwa kuwa miti ni muhimu katika mazingira yetu.

              
    Mbali na hayo, baadhi ya Wanyarwanda hulima na kupalilia mashamba yao. Wao huja pamoja kwa ajili ya kuwasaidia wenzao hasa wazee katika mashamba yao.

    Maswali
    1. Eleza umuhimu wa kazi ya umuganda katika jamii zetu.
    2. Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Kila mwanafunzi asimulie mambo muhimu yanayojitokeza katika shughuli ya kijamii aliyoshiriki zaidi.

    Kazi ya kikundi

    Jiunge na wanafunzi wenzako. Jadilianeni kuhusu shughuli za kijamii mlizoshiriki kisha mziwasilishe mbele ya darasa.

    B. Namna sahihi ya kuuliza maswali

    Kufikia sasa, umejifunza mengi kuhusu shughuli mbalimbali za kijamii. Unaposhiriki katika mazungumzo kuhusu shughuli hizi za kijamii au mambo mengineyo, unaweza kuuliza maswali mbalimbali.

    Katika Kiswahili, zipo namna mbalimbali za kuuliza swali. Maneno ambayo hutumiwa kuulizia maswali huitwa viulizi. Zipo aina mbalimbali za viulizi. Je, unakumbuka viulizi hivyo?

    Viulizi huuliza maswali kuhusu jinsi kitendo kilivyotendeka (vipi), wakati kitendo kilipofanyika (lini), mahali kitendo kilipofanyika (wapi), aliyetenda kitendo (nani), kitendo chenyewe (nini), idadi (-ngapi) na namna ya kitendo au kifaa (gani).Hapa, maneno yaliyowekwa kwenye mabano ndiyo viulizi vinavyotumiwa kuulizia maswali.

    Soma kifungu hiki ili ujifunze mengi kuhusu namna sahihi ya kuuliza maswali.

        

    INEZA: Wenzangu, kwa nini hamkuhudhuria mkutano wa kijiji uliokuwepoJumamosi iliyopita?

    TONA: Shoga yangu, wewe unafahamu kuwa mamangu mzazi hajisikii vizuri.Sasa, siku hiyo ilibidi niondoke niende kumtazama.

    NDOLI: Nami wenzangu sina sababu ya kutohudhuria bali nilisahau tu na kutanabahi mkutano umekwisha. Mambo gani yalijiri mkutanoni humo?

    INEZA: Lo! Tulifanya shughuli mbalimbali...

    TONA: Samahani kwa kukutatiza usemi. Shughuli hizo mlizifanya wapi?

    INEZA: Tulikusanyika katika uwanja wa mkutano wa kijiji kisha tukajigawa katikavikundi mbalimbali. Kila kikundi kilishiriki kufanya kazi katika maeneo mbalimbali.

    NDOLI: Kwa jumla, vikundi vilikuwa vingapi?

    INEZA: Vikundi vyote vilikuwa tisa.

    TONA: Nani aliongoza kikundi chenu?

    INEZA: Kikundi chetu kiliongozwa na Bi. Kabatesi.

    NDOLI: Nini alichowapa kabla ya kazi?

    INEZA: Alitupa vifaa mbalimbali.

    TONA: Mlipewa vifaa gani?

    INEZA: Tulipewa mapanga na majembe.

    NDOLI: Mlifanya kazi ipi katika kikundi chenu?

    INEZA: Tulifyeka na kulima shamba la nyanyake Teta.

    TONA: Mkutano ujao utakuwa lini?

    INEZA: Mkutano ujao utakuwepo Jumamosi ya mwisho, mwezi ujao. Msikosekuhudhuria kikao.

    NDOLI: Ni vifaa gani vitahitajika katika kazi hiyo ya umuganda?

    INEZA: Vifaa vitakavyohitajika vitakuwa fagio, ndoo, majembe, mapanga namafyekeo. Msikose kushiriki.

    TONA na NDOLI: Tukijaaliwa tutakuwepo. Asante.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tungeni maswali sahihi kuhusu shughuli mbalimbali za kijamii mkitumia viulizi vifuatavyo. Sahihishianeni majibu yenu.

          a) vipi

          b) lini

          c) wapi

          d) nani

          e) nini

          f ) -ngapi

          g) gani

    Kazi ya kikundi

    Jiunge na wanafunzi wenzako katika kikundi. Rejeleeni vifungu vya habari mlivyosoma kuhusu shughuli mbalimbali za kijamii katika vipindi vilivyopita. Tumieni viulizi mbalimbali kuulizana maswali kwa zamu kutokana na yaliyomo kwenye vifungu hivyo. Anayeulizwa ajibu kila swali kwa usahihi. Anapopata jibu, naye amwulize mwenzake swali.

    Mifano

    1. Afisa wa afya kutoka wizara ya kilimo alisema nini kuhusu UKIMWI?
    2. Nani alifanya harusi?

    C. Aina saba za maneno

    Lugha ya Kiswahili huwa na aina saba kuu za maneno. Maneno haya hutambuliwa kulingana na muundo na matumizi yake katika sentensi. Maneno hayo saba huwa nomino, vitenzi, vielezi, vivumishi, viwakilishi, viunganishi na vihisishi.

    Nomino

    Kufikia sasa, umejifunza mengi kuhusu aina mbalimbali za nomino. Je, unazikumbuka?Tunaweza kutumia nomino mbalimbali kutaja mtu au watu walioshiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii. Pia, tunaweza kutumia nomino kutaja vifaa mbalimbali vilivyotumika kutendea shughuli fulani za kijamii, mahali shughuli hizo zilipofanyika na kadhalika. Tazama aina mbalimbali za nomino katika jedwali na usome mifano kando yake.

    Zoezi A

    Soma kifungu kifuatacho cha habari. Bainisha na uainishe nomino mbalimbali katika kifungu.

         

    Ama kwa kweli, ndoa ni jambo linalowafurahisha watu wengi. Kutajwa tu kwa neno hili hufanya roho za watu wengi kusisimka. Takriban watu wote husikia neno hili kwa upendo. Kwa nini upendo? Unapotajiwa neno hili, fikira ya kwanza kukujia ni raha. Watu husikia raha kwa sababu huwepo maakuli na vyakula vingi vya bwerere. Pia, harusi huleta heshima na umaarufu.

    Kabla ya kufanya harusi, yapo mambo mengi ambayo hufanyika. Kwanza kabisa, ni sharti mchumba apatikane. Halafu ni sharti ujumbe wa posa upelekwe na mshenga kwa kina mchumba. Ukikubalika, mahari huzungumziwa na kulipwa. Ni baada ya haya yote tu ambapo siku ya harusi huwekwa.

    Nayo matayarisho ya harusi huwa mengi. Bi harusi pamoja na wapambe wake sharti wanunuliwe mavazi mbalimbali ya harusi. Mavazi haya huwa pamoja na nguo maalumu za Bi harusi na wapambe wake. Pia ni sharti pawepo jozi mpya za viatu, pete ya harusi, mashada ya maua na kadhalika. Matayarisho mengine ni usafiri, waendesha harusi, kwaya, na matayarisho mengine mbalimbali.

    Hatimaye huja siku yenyewe ya harusi. Mfano mzuri wa siku hii ni harusi ya rafiki yangu Iliza iliyofanyika Ijumaa jijini Kigali. Umati wa watu ulihudhuria harusi hiyo. Baada ya ibada, tulienda katika Hoteli ya Serena ambapo sherehe kamili iliandaliwa.

    Zoezi B

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tungeni sentensi zinazohusu shughuli mbalimbali za kijamii kwa kutumia nomino mbalimbali mlizobainisha kifunguni.

    Vitenzi

    Kitenzi ni neno lielezalo jambo la kutendwa au kufanywa.

    Je, unakumbuka mifano mbalimbali ya vitenzi ulivyosoma?

    Tunaposhiriki katika mazungumzo kuhusu shughuli mbalimbali za kijamii, ni sharti tutumie vitenzi mbalimbali.

    Tazama aina mbalimbali za vitenzi katika jedwali na usome matumizi yake.

    Zoezi A

    Soma kifungu kifuatacho cha habari. Bainisha na uainishe vitenzi mbalimbali vilivyomo kifunguni.

      
    “Tuharakishe. Ujenzi wa choo umeanza,” Ikirezi aliniambia. Alikuwa akihema. “Mimi ni mgonjwa. Ningali ninaumwa na tumbo lakini nitajikaza,” nilimjibu. Hatimaye tuliwasili penye mkutano. Watu walikuwa wamejigawa katika vikundi tayari kwa kazi mbalimbali.

    “Tazama. Kila mtu ameanza kujenga choo isipokuwa sisi,” nilimwambia Ikirezi. Kiongozi wa kijiji alinisikia.“Msiwe na shaka. Nyinyi mtaokota taka zote zilizopo pale uwanjani. Baada ya hapo, mtafagia kando ya barabara. Kazi hiyo si ngumu,” kiongozi wa kijiji alisema.

    Mimi na Abatoni tulitafuta fagio. Tuliongezewa vijana watatu ili watusaidie kufanya kazi hiyo. Tulifurahia sana kushirikiana na wanakijiji.

    Zoezi B

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tungeni sentensi zinazohusu shughuli mbalimbali za kijamii kwa kutumia vitenzi mbalimbali mlivyobainisha kifunguni.

    Vielezi

    Vielezi pia huitwa viarifa nayo ni maneno yafafanuayo vitenzi, vivumishi au vielezi. Tunaweza kutumia vielezi kueleza jinsi shughuli mbalimbali za kijamii zilivyofanywa. Mathalan, ukisema: Anafanya kazi haraka neno haraka linaeleza jinsi kazi inavyofanywa.

    Je, unakumbuka vielezi ulivyosoma?

    Tazama aina mbalimbali za vielezi katika jedwali na matumizi yavyo.

    Zoezi A

    Soma kifungu kifuatacho cha habari. Bainisha na uainishe vielezi mbalimbali kifunguni.



    Ilikuwa siku ya Jumamosi. Ilikuwa siku ya kuwasaidia wazee kuandaa mashamba yao na kupanda mbegu. Wanakiji wote waliamka alfajiri. Mimi pia nilijiunga nao kwa hiari. Wa kwanza kusaidiwa aliitwa Abera. Tulitembea upesi kuelekea shambani mwake ili tufike mapema. Tulipofika ndani ya shamba, kila mtu alipewa jukumu. Wengine walifyeka majani marefu yaliyomea pembeni mwa shamba.

    Waliyafyeka majani kwa panga. Wengine walilima kwa jembe la mkono. Wengine waliondoa magugu hatari kutoka shambani na kuyachoma kwa moto. Sisi tulipanda mbegu. Kila mtu alipewa kazi ya kufanya mara kwa mara. Hakuna aliyekaa bure. Sote tulifanya kazi kijeshi.

    Zoezi B

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tungeni sentensi zinazohusu shughuli mbalimbali za kijamii kwa kutumia vielezi mbalimbali mlivyobainisha kifunguni.

    Vivumishi

    Kwa kawaida, kivumishi ni neno linaloongezea nomino maana. Vivumishi vinaweza kutumiwa kuelezea sifa za mtu au watu walioshiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii. Pia, tunaweza kutumia vivumishi kueleza sifa za vifaa vilivyotumika katika shughuli za kijamii na kadhalika.Kumbuka kuwa vivumishi ni sharti vitumiwe pamoja na nomino. Je, unakumbuka vivumishi gani ulivyosoma?

    Tazama aina mbalimbali zifuatazo za vivumishi huku ukisoma matumizi yaliyotolewa.

    Zoezi A

    Soma kifungu kifuatacho cha habari. Bainisha na uainishe vivumishi mbalimbali katika kifungu.

    Ni taifa gani ambalo halipendi maendeleo? Ama ni watu wepi ambao hawapendi kuendelea? Sisi Wanyarwanda tunapenda maendeleo ili taifa letu likue hata zaidi. Nchi yenye watu wanaopenda maendeleo hukua haraka. Ili jambo hili liwezekane, ni sharti tufanye mambo kadhaa.

    Kwanza kabisa, nchi yetu haiwezi kukua bila masomo. Lazima watoto wote waliofika umri wa kuenda shule waende shuleni. Nasi wanafunzi wenyewe tulenge kufikia elimu ya chuo kikuu. Ili kufaulu masomoni, ni sharti tushirikiane na jamii. Ujuzi huu tunaopata shuleni ni sharti tuutumie kusaidia jamii. Tusingoje hadi tumalize chuo kikuu ndipo tuanze kujenga taifa hili letu.

    Pili, usafi ni jambo muhimu sana. Jamii haiwezi kujenga taifa lake kama haina afya nzuri. Je, kina nani wanafaa kudumisha usafi huu? Watu hao si watu wengine bali ni mimi na wewe. Kila mmoja wetu ahakikishe kuwa anaishi katika mazingira safi kila siku.

                          

    Tatu, kuna shughuli ya mikutano tofauti tofauti ya kutangaza na kuhimiza maendeleo. Jamii inapokutana na kuelezwa maendeleo yaliyopatikana, hupata motisha ya kufanya mengi zaidi. Hali hii basi huwa ni msukumo muhimu katika kazi zao. Vilevile, vijiji hushindana katika maendeleo. Mashindano ya dhati kati ya vijiji huwa ni motisha nzuri ya ujenzi wa taifa. Kumbuka kuwa vijiji vikipiga hatua mbele nalo taifa hufanya vivyo hivyo.

    Jambo jingine linalohitajika katika huu ujenzi wa taifa ni kuwa na mikakati kabambe ya kushughulikia mikasa. Mathalan, tumejitayarisha vipi kukabiliana na mkurupuko wa magonjwa hatari na njaa? Ni sharti tushirikiane ili kuibuka na mikakati kabambe ya kukabiliana na mikasa kama hii.

    Ili haya yote na mengine mengi yafaulu, umoja na ushirikiano wetu lazima uwepo. Kumbuka kuwa kidole kimoja hakivunji chawa nalo jiwe moja haliinjiki chungu.

    Zoezi B

    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Tungeni sentensi zinazohusu shughuli mbalimbali za kijamii kwa kutumia vivumishi mbalimbali mlivyobainisha kifunguni.

    Viwakilishi

    Viwakilishi ama vibadala ni maneno kamili ama viambata (sehemu za maneno) vinavyosimama badala ya majina. Je, unakumbuka viwakilishi ulivyosoma?Tazama aina mbalimbali hizi za viwakilishi katika jedwali lifuatalo huku ukisoma matumizi yake.

    Zoezi

    Soma kifungu kifuatacho cha habari. Bainisha na uainishe viwakilishi mbalimbali katika kifungu.

          
    Waliosema kuwa umoja ni nguvu hawakukosea bali waligonga ndipo. Mimi ninaamini sana katika msemo huu. Ninaamini kwa sababu ya mambo niliyoshuhudia nilipompoteza mama mzazi. Mama alikuwa mtu wa watu. Aliwapenda wanakijiji nao wanakijiji wa mbali na wa karibu wakampenda. Kifo chake kiliwashtua wengi. Kilifanya kijiji kizima kiomboleze. Watu walifurika nyumbani kwetu kutupa pole. Kuwepo kwao kulituliwaza. Licha ya machungu, tulihisi kuwa hatupo peke yetu. Nani angekosa kupata nguvu katika hali kama hii? Msiba huleta unyonge. Wetu ulileta nguvu kutokana na ushirikiano huo.

    Mbali na kutupa moyo, wanakijiji waligharamia mazishi. Wao walisimamia kila kitu. Sisi tulishuhudia tu mambo yakitendeka. Hawakutaka tushiriki katika shughuli zozote kutokana na huzuni. Waliopika walipika. Waliotengeneza jeneza walifanya hivyo tena kwa ustadi. Waliochimba kaburi hawakusita kumaliza mapema. Kila kitu kilifanywa kwa haraka na ustadi. Mama akalazwa na kupewa heshima zake za mwisho kwa ushirikiano wa wanakijiji. Wao hao wakatuchangia pesa za matumizi ya baadaye. Tulikosa maneno ya kuelezea furaha na shukrani zetu kwao. Kweli, umoja ni nguvu.

    Viunganishi

    Haya ni maneno yanayotumika kuunganisha maneno, vikundi vya maneno au sentensi ili kupitisha ujumbe fulani.

    Tazama mifano hii ya viunganishi.

       1. Tulikuja pamoja ili kuwafariji waliofiwa.

       2. Mkutano uliahirishwa kwa sababu mvua kubwa ilinyesha.

       3. Mbali na kufagia, wanakijiji hupanda miti na kujenga vizuizi vya kukinga mmomonyoko wa udongo.

       4. Tulisameheana maadamu tulishiriki kazi pamoja.

    Zoezi

    Soma kifungu kifuatacho. Bainisha aina mbalimbali ya viunganishi vilivyotumika.

       

    Kila jamii huwa na ngoma yao waipendayo. Aghalabu wao huipenda kwa sababu wameirithi kutoka kwa mababu zao. Mathalan, Waswahili hupenda sana msondo. Je, nyinyi mnapenda ngoma gani katika jamii yenu?Kwa kawaida, ngoma kama hiyo huchezwa na wale waliopo sasa. Baadaye hupitishwa kwa vizazi vijavyo. Kwa namna hiyo, ngoma husika huja ikawa sehemu kuu ya utamaduni wao japo baadhi ya mambo ya kisasa huongezwa. Mambo hayo ya kisasa huongezwa pasipo kubadilisha asilia ya ngoma hizo.

    Sisi Wanyarwanda pia tunapenda ngoma zetu za kiasili. Itokeapo shughuli muhimu, sisi hushiriki katika kuimba na kucheza ngoma zetu za kitamaduni. Hivyo basi, ngoma huchezwa kama njia mojawapo ya kujiburudisha. Shughuli hii huambatana sana sana na sherehe fulani kama vile siku za kitaifa, harusi, kusherehekea mavuno, siku ya kutoka jandoni au kuvunja ungo na kadhalika. Mbali na hayo, ngoma ni njia moja kuu ya kutuleta pamoja ili kufanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

    Aidha, tunapocheza ngoma fulani siku ya taifa, tunapata kumbukumbu muhimu katika historia yetu. Kwa mfano, tunakumbuka jinsi tulivyokuja pamoja kujikomboa kutoka kwa minyororo ya wakoloni. Ikiwa umoja wetu ulifukuza wakoloni sembuse umaskini?

    Ngoma vilevile hutukumbusha umuhimu wa kuwepo kwa amani. Pia, ngoma hutuonya dhidi ya kuchukiana. Hutukumbusha kuwa amani, upendo na umoja ni mambo muhimu katika ujenzi wa nchi yetu.

    Iwapo tutapenda ngoma zetu za kienyeji na kutunga nyimbo za kisasa zenye kukuza ushirikiano, basi tutapiga hatua kubwa katika maendeleo yetu.

    Kazi ya kikundi

    Jiunge na wanafunzi wenzako. Jadilianeni kuhusu aina na mifano mbalimbali ya viunganishi katika Kiswahili. Tungeni sentensi sahihi mkitumia viunganishi hivyo.

    Vihisishi

    Vihisishi ni maneno ambayo huonyesha hisia mbalimbali za mzungumzaji. Unaweza kuelezea hisia zako kuhusu shughuli mbalimbali za kijamii kwa kutumia vihisishi. Vihisishi hutumika pamoja na alama ya hisi (!).

    Tazama mifano iliyotolewa hapa chini.

      a) Huree! Tumemaliza kujenga nyumba.

      b) Alaa! Mbona harusi haijaanza?

      c) Ole wangu! Kumbe nilikosa mengi katika mkutano wenu!

      d) Inshallah! Tukutane kesho twendelee na kazi yetu.

    Zoezi

    Soma kifungu kifuatacho. Bainisha aina mbalimbali za vihisishi vilivyotumika.

      
    Sote tulifunga safari ya kumtembelea Gatete kijijini mwao. Lo! Hatukuamini macho yetu tulipofika huko. Kumbe kijiji hicho kilikuwa safi na tulivu mno!Gatete alipokuja kutulaki, tulimpa pongezi. “Hongera! Mnafanya kazi nzuri kweli,” Ndoli alisema.Gatete alimtazama Ndoli kwa mshangao. Hakuelewa sababu za hongera zake.

    “Jamani! Mbona kijiji hiki chenu ni safi namna hii?” nilimwuliza Gatete.“Ahaa! Sisi hutupa taka zote katika majaa. Pia, tunachimba mitaro ili tusiwe na vidimbwi vya maji. Yeyote, awe mdogo au mkubwa, huokota majani makavu au taka zozote popote,” Gatete alisema akitabasamu.“Maskini sisi! Hatufanyi hivyo hata!” Ndoli alisema.

    “Alaa! Mnafaa mwanze kufanya hivyo moja kwa moja. Usafi ni jambo muhimu sana katika maisha yetu.”“Naam! Kuanzia leo, nitahimiza wanakijiji wenzangu ili kwa pamoja tudumishe usafi.”

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi wenzako. Fanyeni utafiti kuhusu aina mbalimbali za vihisishi katika Kiswahili. Tungeni sentensi sahihi mkitumia vihisishi hivyo.

    Zoezi la ziada

    Soma kifungu hiki. Bainisha na uanishe aina saba za maneno ya Kiswahili (nomino, vitenzi, vivumishi, vielezi, viwakilishi, viunganishi na vihisishi)

                                            Kukoga mwaka


    Hapo zamani, watu tofauti walikuwa na itikadi mbalimbali kuhusu kuanza kwa mwaka. Baadhi yao walisherehekea siku hiyo kwa kuchinja na kuandaa karamu murua! Nao wengine waliwatambikia wazee wao waliofuata njia ya marahaba. Zaidi ya haya, baadhi ya watu waliamini kuwa ni lazima mwaka mpya uanze kwa usafi. Hii ndiyo ilikuwa sababu ya kukoga mwaka.

    Kukoga mwaka kulikuwa na utaratibu wake. Kazi hizo zote zilitegemea mwanzo wa mwaka wa kiasili bali si ule wa kizungu. Mwaka huo wa kiasili ulikuwa ukianza saa thenashara hivi za asubuhi. Hivyo basi, kabla ya wakati huo, wenyeji walirauka saa kumi. Madhumuni ya kuamka wakati huo yalikuwa kusafisha kila kitu kabla ya mapambazuko. Basi wanawake waliamka na kukusanya vitu vyote ambavyo viliweza kuoshwa na kuvipeleka mtoni. Wengine walibaki nyumbani kusafisha vile vitu ambavyo havikuweza kuchukuliwa mtoni lakini ambavyo vilihitaji kuoshwa au kusafishwa.

    Baadhi ya vitu vilivyooshwa mtoni vilikuwa nguo zilizomea koga, vyungu, sahani, sufuria na vyombo vinginevyo. Baadhi ya watu walisafisha vyombo hivyo kwa sabuni lakini wengine walivisafisha kwa majani maalum. Jambo lililokuwa la mwisho kufanywa huko mtoni ni kuwaosha watoto. Baadaye watu wazima wangeoga wao wenyewe. Wakati mwingine, watu wangeosheana miguu kama ishara ya upendo.

    Nao wanawake wale waliobaki nyumbani walikuwa na kazi kubwa ya kusafisha nyumba mbalimbali za msonge. Baadhi yao walipaka sakafu kwa samadi mbichi iliyochanganywa na udongo na maji. Nao wanawake wengine waliondoa masizi yaliyokuwa yakining’inia kwenye mapaa.

    Vijana nao walisomba maji kutoka mtoni. Maji hayo yangetumiwa na wanaume kuogea. Wao pia wangeoga baadaye.

    Wanaume nao hawakukaa bure. Ilikuwa kazi yao kufyeka na kusafisha uani, mbele na pande zote za nyumba. Pia ilikuwa kazi yao kufyeka nyasi zo zote zilizokuwepo pale kiamboni pamoja na kukata matagaa yasiyohitajika ili kwamba jua la mwaka mpya lichomozapo liangaze boma zima.

    Je, ni kwa nini kazi hizo zote zilifanyika? Hata wakati huo, wenyeji waliamini kuwa Mungu hakupenda uchafu. Isitoshe, waliamini kuwa mtu akianza jambo fulani kwa nuksi basi hatafanikiwa katika mambo mengi. Hivyo basi, imani yao ilikuwa kwamba mwaka ukianza kwa uchafu basi shughuli zao zote mnamo mwaka huo zingekumbwa na nuksi. Hapana hata mmoja aliyetaka kutofanikiwa. Naam! Mwaka mpya ungeanza kwa usafi kweli.

    Kazi ya kikundi
    Jiunge na wanafunzi mwenzako. Someni vifungu mbalimbali vya habari vilivyopo katika sura hii ya nne. Bainisheni na kuainisha aina saba za maneno ya Kiswahili katika vifungu hivyo.

    D. Matumizi ya wakati uliopita -li- hali yakinishi na hali kanushi


    Tunaweza kuzungumzia shughuli mbalimbali za kijamii tulizoshiriki muda au wakati uliopita. Wakati huu huwasilishwa na -li-. Vitendo katika wakati uliopita vinaweza kuwa katika hali yakinishi au katika hali kanushi. Hali yakinishi ni ya kukubali na hali kanushi ni kukataa.

    Tazama mifano ya matumizi ya wakati huu iliyotolewa kwenye jedwali lifuatalo.

    Je, unaona mabadiliko gani katika hali kanushi ya vitenzi hivyo? Katika jedwali lililopo hapo juu, vitenzi walihudhuria, nilienda na ilianza vipo katika hali yakinishi au kukubali kwa wakati uliopita.

    Vitenzi hawakuhudhuria, sikuenda na haikuanza vimo katika hali ya kukataa yaani hali kanushi kwa wakati uliopita. Kiambishi ‘li-‘ hakitumiki katika hali kanushi. Huondolewa.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili

    Jiunge na mwenzako. Tungeni sentensi sahihi kuhusu shughuli za kijamii mkitumia wakati uliopita katika hali yakinishi na kanushi.

    E. Matumizi ya wakati ujao -ta- katika hali yakinishi na hali kanushi

    Wakati ujao hutumiwa kuelezea mawazo au vitendo vitakavyofanyika baadaye. Kiambishi -ta- hutumika pamoja na kitenzi husika kuonyesha kuwa kitendo kitafanyika baadaye.

    Tunaweza kuzungumzia shughuli mbalimbali za kijamii ambazo zitafanyika baadaye. Mfano: unapoandika ratiba ya shughuli au kutoa maelekezo ya mambo yanayofaa au ambayo hayafai kufanywa, unatumia wakati ujao.

    Vitendo katika wakati ujao vinaweza kuwa katika hali yakinishi au kanushi. Hali yakinishi ni ya kukubali na hali kanushi ni kukataa.

    Tazama mifano iliyotolewa kwenye jedwali lifuatalo.

    Vitenzi vilivyopo katika jedwali viko katika wakati ujao.
    Je, unaona mabadiliko gani katika hali kanushi ya vitenzi hivyo?
    Katika jedwali lililopo hapo juu, vitenzi utaandaliwa, litatufaa na mtafyeka vipo katika hali yakinishi au kukubali kwa wakati ujao.
    Vitenzi hautaandaliwa, halitatufaa na hamtafyeka vimo katika hali ya kukataa yaani hali kanushi kwa wakati ujao.

    Kazi ya wanafunzi wawili wawili
    Jiunge na mwenzako. Tungeni sentensi sahihi kuhusu shughuli za kijamii mkitumia wakati ujao. Mzingatie hali yakinishi na kanushi.

    Mifano

    ABATONI: Vijana watafyeka barabara.
    NDOLI: Vijana hawatafyeka barabara. Watasomba maji ya kujengea nyumba.
    ABATONI: Wazee hawatasomba maji ya kujengea nyumba. Watatoa maelekezo.

        Maswali ya marudio


    1. Eleza mambo muhimu ambayo hutendeka katika shughuli za ubudehe.

    2. Linganisha na utofautishe shughuli za mazishi na harusi katika jamii.

    3.  a) Bainisha wahusika wakuu katika shughuli hizi za kijamii:

              i) Mazishi

              ii) Harusi

              iii) Ibada msikitini au kanisani

         b) Eleza tofauti za kimawasiliano katika shughuli zilizotajwa hapo juu.

    4. Tunga sentensi ukitumia msamiati ufuatao:

              a) kuchimba mitaro

              b) kusomba maji

              c) kula kiapo

              d) peleka mahari

    5. Taja sherehe nne muhimu za jamii katika eneo utokako huku ukiielezea kila moja umuhimu wayo.

    6. Wewe ni kiongozi wa kikundi kinachoshiriki katika shughuli fulani ya kijamii. Chagua shughuli upendayo kisha utoe maelekezo kwa wanachama wa kikundi chako.

    7. Eleza manufaa ya kazi ya umuganda kwa jamii ya Wanyarwanda.

    8. Taja mambo mawili yanayoweza kukuonyesha kuwa tungo ni swali.

    9. Tunga maswali matano ukitumia viulizi mwafaka.

    10. Zipo aina ngapi za maneno ya Kiswahili? Zitaje.

    11. Yataje maneno kumi ya Kinyarwanda ambayo ni sawa na yale ya vihisishi vya Kiswahili.

    12. a) Nomino ni nini na huweza kuitwaje pia?

          b) Tunga sentensi tano sahihi ukitumia aina mbalimbali za nomino.

    13. Tambulisha vitenzi katika maneno yafuatayo:msamaha samehe hisi kihisishi rehema kurehemu rehemu fikira fikiri kilio lia

    14. Zieleze aina zote za vivumishi ambazo umejifunza hadi sasa. Tunga sentensi ukitumia kila mojawapo.

    15. Eleza tofauti iliyopo kati ya viunganishi na vihisishi.

    16. Andika aya moja kuhusu shughuli fulani ya kijamii. Tumia maneno yote saba ya Kiswahili katika aya hiyo kwa usahihi.

    17. Pigia kistari sentensi zilizopo katika wakati ujao na useme ikiwa ni hali yakinishi au kanushi.

              i) Siendi Kigali.

              ii) Wanaenda harusini.

              iii) Nitashiriki katika kazi zote kijijini.

              iv) Aliniita sikusikia.v) Hawatachelewa leo.

    18. Eleza umuhimu wa ushirikiano katika jamii.

    19. Taja mambo yote muhimu uliyojifunza katika sura hii.

  • Faharasa

    adimika           – kosa kupatikana kwa urahisi
    ambukiza        – enezea ugonjwa
    andaa          - tayarisha
    ankra           – orodha ya vitu vilivyouzwa pamoja na bei ya kila bidhaa
    anuani         – maelezo ya mahali mtu anapoishi ambayo huandikwa katika barua
    asali            – namna ya kitu kioevu na kitamu sana kitengenezwacho na nyuki
    azma          – lengo au shabaha
    bainisha     – tambua jambo
    bao            – mpira kuingia katika lango katika mchezo wa kandanda (goli)
    baridi kali  – hali isiyokuwa na joto na isisimuayo sana mwili
    bei            – kiasi cha pesa kinachotumiwa kununulia ama kuuzia bidhaa fulani
    burudani  - starehe
    burudisha – sababishia raha
    chai          – zao la mchai
    dumisha   – endeleza
    faranga    – pesa, fedha, dirhamu, senti, fulusi
    filisika      – ishiwa na mali
    fyeka       – kata nyasi
    gharamia – lipia gharama
    harage/haragwe– nafaka ya jamii ya kunde
    haramu     – -siyoruhusiwa, -siyokuwa halali
    Hisabati    – sayansi ya tarakimu ijumuishayo aljebra
    hitaji         – kuwa na haja ya kitu
    huzuni     – hisia za majonzi
    ibuka       – tokeza
    idadi        – hesabu au jumla ya vitu
    ilani         – tangazo la kuonya watu wasifanye jambo fulani hasa lenye
                       kuleta madhara
    ingawa    – hata ikiwa
    jadhba/jazba – hisia isababishayo kujisahau
    jamii       – watu wanaoishi pamoja
    jangili    – mwindaji haramu
    jedwali  – orodha ya maelezo kuhusu mambo fulani kwa namna
                      yatakavyofuatana
    jibini      – chakula kinachotengezwa kwa kuyagandisha maziwa na kuyatoa
                      maji
    jukumu  – wajibujumuiya– mkusanyiko wa watu
    kabuti    – koti zito la kuzuia baridi
    kagua    – chunguza kwa makini
    kahawa  – zao la mkahawa ama mbuni
    kandanda – mchezo wa miguu
    kauli         – usemi
    kiasili       – kienyeji
    kifaa        – chombo
    kikao       – mkutano
    kipindi     – muda
    kipusa    – pembe ndogo ya kifalu
    kivuna nafaka – mashine kama trekta ambayo huvuna ngano huku
                                ikiitoa wishwa
    kiwanda – mahali panapotengenezwa bidhaa
    kodi ya mapato – fedha zinazolipwa serikali kama ushuru wa mapato ya mtu
    kupanda– tia mbegu mchangani ili ziote
    limbikiza – weka vitu kidogo kidogo ili viwe vingi
    lishe bora – chakula kinachohitajika kwa afya nzuri ya mwili
    maabara – mahali mnamofanyiwa majaribio ya kisayansi
    maalumu – -enye sifa ya kipekee
    mada– kiini cha jambo linalozungumziwa
    majira– wakati au kipindi
    majira ya kiangazi – kipindi cha kiangazi
    majira ya kipupwe – kipindi cha baridi
    majira ya mvua– kipindi cha mvua
    majira ya vuli– kipindi cha mvua chache
    majivuno – hali ya kujiona
    manufaa  – faida
    mapato    – kitu kinachopatikana kama vile baada ya kufanya kilimo ama
                        kufanya biashara.
    masuala mtambuka – mambo muhimu yanayoiathiri jamii katika kipindi cha
                                         sasa
    matini          – kifungu cha habari iliyoandikwa
    mazingira    – mambo yanayotuzunguka mahali tunapoishi
    maziwa        – kitu kioevu kitokacho ndani ya titi la mnyama
    mbatata       – namna ya viazi vilivyo mviringo na visivyo na ladha
    mbinu          – njia au namna ya kufanyia jambo
    mbuga        – eneo lililotengewa wanyama wa porini
    mchele       – mpunga uliokobolewa,yaani kuondolewa mashuke
    mfawidhi    – mtu aliyepewa wajibu wa kuendesha shughuli fulani, kama vile
                           mkutano au sherehe fulani
    mfugaji tajiri – mfugaji ambaye ana mali nyingi
    mifugo          – wanyama wanaotunzwa nyumbani
    mikahawa     – mimea izaayo kahawa
    mkulima tajiri – mkulima ambaye ana mali nyingi
    mmomonyoko – kuchukuliwa kwa udongo wenye rutuba
    mori          – hasira kali
    mshinde   – aliyeshindwa
    mshindi    – aliyeshinda
    msimu      – majira
    mtama      – zao la mtama
    muhogo   – mzizi wa muhogo unapokuwa umekomaa tayari kwa kuliwa
    ndama     – mtoto wa ng’ombe
    ndizi        – tunda la mgomba linalomea kwenye mkungu.
    ngeli       – kikundi cha majina au nomino zinazofuata kanuni sawa za kisarufi
    njugu      – mbegu zitengenezewazo mafuta ya karanga
    nyama    – sehemu laini ya mwili ambayo ikikatwa hutoka damu
    pandwa  – ingiwa na
    pekee     – pweke; bila ya -ingine
    pesa       – noti na sarafu zinazotolewa na kuidhinishwa na serikali kuwa ni
                      fedha rasmi za kubadilishana na bidhaa.
    pori        – mahali palipo na miti mingi, nyasi na vichaka
    ratiba     – mpango wa mfululizo wa shughuli fulani
    refa        – mwamuzi katika mchezo wa mpira
    rejesta   – lugha inayotumiwa katika mahali maalum, kama vile hospitalini, hotelini, msikitini na kwingineko
    rutuba   – mbolea ya kukuzia mimea ardhini
    sajili      – rejesta
    shabiki  – apendaye sana timu
    sheria    – kanuni za kuongoza watu
    shime   – neno la kuhimizia mtu
    shiriki  – husika au kuungana na watu katika kufanya shughuli fulani
    soseji   – namna ya chakula kinachotengenezwa kutoka kwa nyama ya
                     nguruwe au ya ng’ombe
    suala       – jambo au hoja
    sufu        – manyoya ya kondoo
    takwimu – nambari zinazoeleza ukweli kuhusu matukio ya mambo, kwa
                       mfano idadi ya watu katika eneo fulani
    tambua   – fahamu au maizi
    tanbihi    – maelezo yanayotoa habari muhimu
    tathmini – pima
    tegemea– weka matumaini kupata kitu
    tia mdomoni– kumsema ama kumsengenya mtu
    ulinzi          – ulindaji, hali ya kulinda
    upanzi        – upandaji (uwekaji mbegu ardhini)
    utafiti          – uchunguzi wa kisayansi
    vanila          – kiungo kiyafanyayo maziwa yaliyoganda kuwa na ladha ya
                            kupendeza
    viazi vitamu– namna ya viazi vikubwa na vilivyo vitamu
    wadau          – mtu mwenye maslahi katika shughuli fulani
    wadhifa        – madaraka au cheo fulani
    waligonga ndipo – walisema ukweli
    wasifukazi     – maandishi yanayoeleza kuhitimu kwa mtu katika
                             kutekeleza kazi fulani, aghalabu, kimasomo, tajiriba ya kazi
                             na ujuzi wake
    wishwa        – takataka za nafaka kama vile mtama au ngano
    yakinishi     – hali ya kukubali
    zao               – kile kinachozaliwa na mmea
    zaraa           – kilimo
  • Vitabu vya rejea

    Kagwa, F.M. na Waihiga, G. (2007) Kamusi Changanuzi ya Methali. Nairobi:
    Moran (E.A.) Publishers.

    Kipande, M. (2013) Sarufi. Nairobi: Moran (E.A.) Publishers.

    Massamba D.P.B. (2004) Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha. Dar es Salaam.
    TUKI.

    Mogambi Hezron (2007) Premier Golden Tips; Kiswahili kwa Shule za Upili.
    Nairobi: Moran (E.A.) Publishers.

    Mutali Chesebe (2010) Premier Golden Tips; Stadi za Uandishi wa Insha. Nairobi:
    Moran (E.A.) Publishers.


    Oxford University Press (2013). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Toleo la tatu.
    Oxford University Press.

    Rwanda Education Board. (2015) Kiswahili Sylabus for Ordinary Level. S1-S3.
    Kigali: Rwanda Education Board.

    TUKI (1990) Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha. Dar es Salaam. TUKI.