• MADA YA 5 KISWAHILI KATIKA SHUGHULI ZA KIBIASHARA

    Uwezo mahususi wa mada: Kuzungumza na kuandika kwa ufasaha matini 
    fupifupi kwa kutumia msamiati unaofaa katika shughuli za kibiashara.
    Malengo ya ujifunzaji:
    • Kufanya mazungumzo kati ya mfanyabiashara na mteja, 
    • Kutumia kwa ufasaha mizani au vipimo katika hesabu,
    • Kuainisha pesa zitumiwazo katika shughuli za kibiashara, 
    • Kuainisha bidhaa mbalimbali zipatikazo sokoni,
    • Kutumia kwa ufasaha ngeli ya I-ZI katika sentensi sahihi,
    Kidokezo

    Taja baadhi ya msamiati maalumu unaotumiwa katika mazingira ya 

    biashara

    SOMO LA 19: MAWASILIANO SOKONI

    cc

    Kazi ya 1:
    Tazama mchoro hapa juu na kueleza kinachofanyika hapo.
    19.1. Kusoma na ufahamu: Safari ya Niwemwiza na Kayigi sokoni
    dd


    Siku moja nilitembea sokoni na kaka yangu Kayigi ili kununua vifaa vya 
    shule. Soko hilo linaloitwa Gatare lilikuwa katika kilomita kumi na tano kutoka 
    kwetu. Mama alitupatia pesa za nauli na nyingine za kununua vifaa tofauti 
    vya shule na bidhaa nyingine za kutumia nyumbani.
    Tulitoka nyumbani saa tatu za asubuhi na kufika sokoni saa nne. Tulipokuwa 
    garini, Kayigi aliniuliza kama ninakumbuka vifaa ambavyo mama alituambia 
    kununua. Nilimkumbusha kwamba alituambia kununua vifaa vifuatavyo: 
    shati, jaketi, jozi ya viatu, sidiria, madaftari kumi, kalamu nane, soksi mbili 
    na sabuni vilevile.

    Kayigi aliniuliza kama hakuna vitu vingine amabavyo nimesahau ili 
    anikumbushe tusije tukasahau na vile vilivyokuwa vinahusu matumizi ya 
    nyumbani. Kwa kusema hayo nilianza kuangalia kulia na kushoto, mbele 
    na nyuma kwa ajili ya kuchunguza aina mbalimbali za bidhaa tofauti ili nisije 
    nikasahau chochote nilichoambiwa na mama.
    Nilikumbuka kuwa, mama alikuwa ameniambia kununua nyama, viazi vitamu, maharagwe na sukari. Tulipofika sokoni, tulishangaa kuona watu wengi wa marika tofauti wakijaa sehemu zote. Kelele nyingi za watu sokoni zilikuwa zimehanikiza si huku si kule.

     Kayigi alinishika mkono na kunielekeza pahali panapouzwa bidhaa tofauti. Sauti hizo zilikuwa za wauzaji wakisema: Mia bei! Mia bei! ….karibu mteja… bei rahisi…..chagua….chagua…..kaptula hii ni mia tatu, jaketi hii ni mia tano. Karibu mteja wangu. Karibu katika kibanda changu. Bidhaa ni nyingi utachagua zile utakazo. Tulianzia sehemu panapouzwa nguo.

     Kayigi nami tulifika mbele ya kibanda cha nguo tukaanza kuuliza bei ya vile tulivyokuwa tunataka. Kwanza niliuliza bei ya jaketi niliyokuwa nimechagua. Muuzaji alinijibu kuwa jaketi ilikuwa elfu moja. Nilimwambia apunguze kidogo kwa kuwa bei ilikuwa ghali. Tulijadiliana bei mpaka akakubali mia tisa.
     Baada ya kununua nguo, tuliendelea kutembea sokoni tukanunua vifaa vya shule. Kwenye kibanda cha vifaa vya shule, tulinunua madaftari na kalamu. Bei za kila bidhaa zilikuwa ni bei nafuu. Daftari moja tulilinunua kwa mia moja na hamsini na kalamu kwa mia tu.

    Kabla ya kurudi nyumbani, tulikumbuka kuwa mama alitutuma kununua nyama kwenye bucha. Nilichunguza mfukoni mwangu pesa nilizokuwa nabaki nazo nikaona mnabaki dola mia tano za Marekani tu. Niliuliza dada yangu jambo la kufanya akanishauri kwenda kwenye duka la kubadilisha pesa za kigeni. Tulikwenda mbio na kufika kwenye nyumba ya ghorofa kubwa ambapo pamekuwa maduka mengi ya kubadilisha pesa.

     Tuliingia duka moja ambamo tulikaribishwa na kijana mmoja aliyetubadilishia pesa zetu katika pesa za Rwanda tukarudi sokoni.
    Kwenye bucha, bei ilikuwa ghali pia kwani kilo moja ya nyama ilikuwa mbili elfu mia tano. Kayigi alijaribu kupunguzisha bei. Muuza nyama alikataa kuipunguza akisema kuwa hawezi kupata faida akipunguza. Je, mnataka nipate hasara? Muuza nyama aliuliza. Nilimwomba kupunguza bei kidogo kufika mbili elfu mia tatu.

     Aidha, tulinunua kifungu kimoja cha mboga za sukumawiki, vifungu viwili vya nyanya na kilo moja ya chumvi.
    Ilipofika saa saba za mchana tulichukua basi tukarudi nyumbani. Tulipofika nyumbani mama alitushukuru kwa kuwa hatukukawia kurudi na kuwa
    tulitumia pesa vizuri. Kila mmoja alimwahidi kumpa tuzo ya peremende mbili.

    Kazi ya 2:
    Maswali ya ufahamu
    a. Taja aina mbili za bidhaa ambazo mama aliwatuma wanawe sokoni.
    b. Ni kwenye sehemu gani ya soko ambapo Kayigi na Niwemwiza walinunua madaftari na kalamu?
    c. Nini kilichosababisha Kayigi na Niwemwiza kushangaa walipofika sokoni?
    d. Kwa sababu gani mchinjaji alikataa kupunguza bei ya kilo moja ya nyama?
    e. Ni kwa sababu gani mama aliwapongeza wanawe walipotoka sokoni?
    19.2. Matumizi ya msamiati
    Kazi ya 3: Toa maana ya msamiati ufuatao:
    a. Faida
    b. Bei ghali
    c. Kununua
    d. Kuuza
     e. Bucha
     f. Hasara

    19.3. Sarufi: Matumizi ya ngeli ya I-ZI
    Kazi ya 4:
    Tazama sentensi zifuatazo na kujadili mabadiliko ya kisarufi yanayojitokeza.
    a. Biashara imetajirisha watu wengi duniani na kuendeleza hali yao ya 
    maisha (Umoja).
    • Biashara zimetajirisha watu wengi duniani na kuendeleza hali yao 
    ya maisha (Wingi).
    b. Nguo ambayo imechafuka imemuambukiza magonjwa (Umoja).
    • Nguo ambazo zimechafuka zimewaambukiza magonjwa (Wingi).
    Maelezo muhimu
    Ngeli hii ya I-ZI inajumuisha nomino za vitu visivyo na uhai. Nomino hizi 
    umoja na wingi wake huwa ni sawa. Isitoshe, nomino hizi ni za vitu ambavyo 
    vinaweza kuhesabika k.m kalamu, meza, sahani, rafu, linga, saa, rula, soksi, 
    nyumba, karatasi, kamusi, wiki, siku, chaki, chupa, ndizi, kamba, bawaba, 
    pete, n.k.
    Majina ya ngeli hii hutumia kiambishi nafsi “I” katika umoja na kiambishi nafsi 
    “ZI” katika wingi kufuatana na upatanisho wa kisarufi.
    Matumizi ya majina ya ngeli ya I-ZI na vivumishi vya sifa
    • Vivumishi “-baya” na”-pya” huchukua kiambishi “m-“ badala ya “n-“.
    Mfano: 
    Umoja: Barabara mpya ilijengwa Kiramuruzi na kurahisisha 
    mawasiliano baina ya raia huko. 
    Wingi: Barabara mpya zilijengwa Kiramuruzi na kurahisisha 
    mawasiliano baina ya raia huko. 
    Umoja:Tabia mbaya inakemewa na wengi
    Wingi: Tabia mbaya zinakemewa na wengi
    Vivumishi vinavyoanza na “r” herufi hiyo hugeuka “nd” inapotanguliwa na 
    kiambishi “n”.
    Mfano:
    Umoja: Ndoo ndefu imewekwa bafuni ili kuogea mikono.
    Wingi: Ndoo ndefu zimewekwa bafuni ili kuogea mikono. 
    • Vivumishi vinavyoanza na “ch, f, p, k, t” havipachikwi viambishi katika 
    umoja wala wingi.
    Mfano:
    Umoja: Meza chafu imetupwa nje.
    Wingi: Meza chafu zimetupwa nje.
    Umoja: Nyumba kubwa na ya kisasa inahitajika mjini.
    Wingi: Nyumba kubwa na za kisasa zinahitajika mjini.
    Umoja: Sketi fupi inakatazwa shuleni.
    Wingi: Sketi fupi zinakatazwa shuleni.
    Umoja: Meza kubwa imewatosha watu wengi harusini.
    Wingi: Meza kubwa zimewatosha watu wengi harusini.
    Umoja: Ndizi tamu imenunuliwa sana sokoni.
    Wingi: Ndizi tamu zimenunuliwa sana sokoni.
    Umoja: Nyumba pana iliwatosha wageni wote wakati wa mkutano wa 
    kimataifa.
    Wingi: Nyumba pana ziliwatosha wageni wote wakati wa mkutano wa 
    kimataifa.

    Kazi ya 5:

    Chagua neno linalofaa na kuliandika katika nafasi iliyoachwa wazi.
    1. Barabara hii ni ……….lakini imepasuka kwa sababu haikujengwa 
    vizuri. (Zipya, kipya, mpya)
    2. Tafadhari nipe Kamusi ya Kiswahili ……… kuna msamiati mgumu 
    ninaotaka kuchunguza ( kisanifu, jisanifu, sanifu)
    3. Karatasi …………zimetupwa jalalani ( mchafu, wachafu, chafu).
    4. Meza …………imewekewa bidhaa nyingi sokoni (vipana, pana, 
    kipana)
    5. Pombe ………iliwalevya watoto na kusababisha kutohudhuria 
    masomo (mtamu, litamu, tamu)
    Kazi ya 6:
    Kwa kutumia vivumishi vya sifa, tunga sentensi sahihi kwa kutumia 
    maneno yafuatayo:

    a. Nyumba 
    b. Shule 
    c. Karatasi 
    d. Baiskeli 
    e. Nyumba
    19.4. Matumizi ya lugha: Msamiati maalumu katika uwanja 
    wa kibiashara

    Kazi ya 7:
    Taja istilahi tano zitumiwazo katika shughuli za kibiashara na kueleza 
    maana yake.

    Maelezo muhimu kuhusu msamiati unaotumiwa katika shughuli za 
    kibiashara. 

    • Biashara: ununuzi na uuzaji wa bidhaa na/au huduma.
    • Faida/tijara/kivuno/chumo/ziada - Pato libakialo baada ya kuondoa 
    gharama za kufanya biashara k.v. ununuzi na usafirishaji.
    • Hasara: Ukosefu wa faida; hali ya kupoteza pato au mali katika biashara. 
    • Bei: Kiwango cha pesa kununulia au kuuzia bidhaa au huduma fulani. 
    • Bei: Kiwango cha pesa kununulia au kuuzia bidhaa au huduma fulani. 
    • Uuzaji wa rejareja: Uuzaji wa kiasi kidogo kidogo. 
    • Uuzaji wa jumla: Uuzaji wa kwa pamoja 
    • Bei rafi: Bei ambayo haipunguzwi. 
    • Kipimo rafi: Kipimo ambacho hakipunguzwi. 
    • Bei ya kuruka: Bei isiyokubalika kisheria/haramu.
    • Rasilimali: Jumla ya mali inayomilikiwa na mtu au nchi.
    • Malighafi: Mali inayotumika kutengeneza vitu vingine k.m. pamba ni 
    malighafi ya kutengenezea nguo.
    • Maliasili: Utajiri kama vile madini, misitu, maziwa, mito, anga 
    vinavyopatikana katika mazingira. 
    • Uwekezaji: Kutumia pesa / mali ili kuzalisha fedha/mali zaidi (ilikupata 
    faida).
    • Kitegauchumi: Rasilimali k.v. kiwanda inayotumika kuzalisha mali. 
    • Ujasiriamali: Uwekezaji mtaji katika biashara.
    • Mtaji: Mali ya kuanzisha biashara au kuipanulia.
    • Ulanguzi: Ufichaji wa bidhaa ili bei yake iruke.
    • Magendo: Upigaji biashara kwa njia haramu/isiyo halali. 
    • Chenji: pesa inayobaki baada ya kununua kitu 
    • Maduhuli: Bidhaa ambazo hununuliwa kutoka nchi za nje.
    • Mahuruji: Bidhaa zinazouzwa nchi za nje.
    • Ushuru: Kodi ya kuingiza bidhaa nchini au kuziuza/Ada ya forodha. 
    • Ruzuku: Pesa inayotolewa na serikali kwa idara mbalimbali ili 
    kujiendeleza. 
    • Mshitiri: Mnunuzi. 
    • Mteja: Mtu aendaye kununua bidhaa au huduma.

    • Wakala: Ajenti

    • Utandawazi: Utaratibu wa mataifa kushirikiana katika nyanja mbalimbali 
    k.v. biashara.
    • Ubinafsishaji: Hali ya kusababisha mali ya umma imilikiwe na watu 
    binafsi. 
    • Ubia: Ushirikiano wa watu wawili au zaidi katika shughuli k.v. ya 
    biashara. 
    • Hawala: Hundi/ cheki yaani cheti maalumu cha benki kinachotumiwa 
    kuidhinisha aliyetajwa kwenye cheti hicho apewe fedha za mwenye 
    hesabu. 
    • Amana: Kitu unachomwekea mwenzako hadi atakapokihitaji.
    • Turuhani: Kiwango kinachotolewa kutoka katika bei iliyotangazwa. 
    • Iktisadi: Uangalifu katika kutumia fedha/mali. 
    • Ubepari: Mfumo wa uchumi ambao unawawezesha watu wachache 
    kumiliki rasilimali na vitegauchumi.
    • Ukiritimba: Hali ya kuzuia wengine kufanya biashara au kushindana 
    katika biashara.
    • Dukakuu: Duka kubwa ambapo wateja hujichukulia bidhaa watakazo 
    kutoka rafuni.

    • Hisa: Sehemu ya mtaji katika biashara.

    Kazi ya 8:
    Tunga sentensi sahihi kwa kutumia maneno yafuatayo
    a. Hundi
    b. Mteja
    c. Ruzuku
    d. Magendo
    e. Rasilimali

    19.5. Kusikiliza na kuzungumza
    Kazi ya 9:
    Tega sikio habari inayosimuliwa na mwanafunzi mwenzako kuhusu 
    safari yake sokoni na kusimulia hali ya safari hiyo mbele ya darasa.
    19. 6. Kuandika
    Kazi ya 10:
    Tunga kifungu cha habari chenye aya tatu kuhusu safari yako sokoni.
    SOMO LA 20: MAJADILIANO DUKANI
    Kazi ya 1:
    Taja mahali fulani panapofanyiwa biashara na huduma zinazotolewa hapo.

    20.1. Kusoma na ufahamu: Muuzaji na mteja

    vv

    Mazungumzo yafuatayo yanahusu Kalisa ambaye ni mteja na Uwera ambaye 

    ni muuzaji. Wanajadiliana bei dukani. 

    Kalisa : Habari za asubuhi bibi !
    Uwera : Nzuri. Nikusaidie nini ?
    Kalisa : Nataka kununua bidhaa tofauti tofauti katika duka lako. Naona duka 
    lako lina bidhaa mbali mbali zinazovutia macho. 
    Uwera : Ndiyo. Mimi ninaagiza bidhaa kufuatana na mahitaji ya wateja ili 
    waweze kufaidika na kile wanachokinunua.
    Kalisa : Mimi nahitaji sabuni, kilo moja ya chumvi, kilo mbili za sukari, nusu 
    ya vitunguu, lita ya mafuta ya kupikia na sufuria moja.
    Uwera : Vyote hapa Kalisa. 
    Kalisa :Kila bidhaa ambayo nimekutajia inauzwa kwa bei gani ?
    Uwera : Bidhaa hizi zote zinauzwa kwa bei nafuu. Sabuni moja ni faranga 
    mia moja, kilo moja ya chumvi ni faranga mia tatu, nusu ya vitunguu ni 
    faranga mia moja hamsini, lita ya mafuta ya kupikia ni mia tano na sufuria 
    hii ni moja elfu. 
    Kalisa : Mbona sufuria ni bei ghali ? Je, unaweza kupunguza kidogo ?
    Uwera : Hiyo ni bei rafi bwana. Ungenunua sufuria mbili ningekupunguzia.
    Kalisa : Nipunguzie faranga mia moja nitaendelea kununulia hapa.
    Uwera : Ninakupunguzia faranga hamsini tu kwa sababu sufuria hii ni kubwa.
    Kalisa : Asante. lakini chukua mizani unipimie kilo ya chumvi na nusu ya 
    vitunguu.
    Uwera : Ndiyo. Angalia hapa vipimo vinaenea. Kwa uhakika mizani yangu 
    ni mpya sikunyang’anyi.
    Kalisa : Hakuna nyongeza bibi ?
    Uwera : Nitakupatia nyongeza ya kutosha siku ijayo.
    Kalisa : Ni pesa ngapi ya kulipa kwa jumla?
    Uwera : Mbili elfu kwa jumla.
    Kalisa : Ahsante sana bibi.
    Uwera : Asante kwa kushukuru. Karibu tena.

    Kalisa :Kwaheri !

    Kazi ya 2:
    Maswali ya ufahamu
    1. Taja bidhaa zinazozungumziwa katika mazungumzo haya.
    2. Kalisa alinunua nini dukani ?
    3. Nini umuhimu wa mizani ?
    4. Ni kwa sababu gani Uwera huuza bidhaa zinazovutia macho ya watu ?

    5. Uwera alimwahidi Kalisa kumfanyia nini siku ijayo ?

    20.2. Matumizi ya msamiati
    Kazi ya 3:
     Toa maelezo ya bidhaa zifuatazo:
    a. Kekee
    b. Patasi 
    c. Chungu 
    d. Jiko la mkaa 
    e. Almasi 
    f. Dhahabu 
    g. Maziwa 
    h. Kuku
    i. Maparachichi 

    j. Tikitimaji

    20.3. Sarufi: Matumizi ya ngeli ya I-ZI na vivumishi vya a-unganifu
    Kazi ya 4:
    Tazama sentensi katika sehemu A na sentensi katika sehemu B na 

    kueleza mabadiliko ya kisarufi yanayojitokeza.

    cc

    Maelezo muhimu kuhusu matumizi ya vivumishi vya a-unganifu
    Majina ya ngeli ya I-ZI yakitumiwa pamoja na vivumishi vya a-Unganifu, 
    umoja wake huchukua ya na wingi huchukua za.
    Mfano: 
    Umoja: Runinga ya Gakire ilinipasha habari kuhusu nanma ya kuleta umoja na maridhiano kwetu
    Wingi: Runinga za Gakire zilinipasha habari kuhusu nanma ya kuleta umoja na maridhiano kwetu.
    Umoja: Rafu ya mama inajaa bidha nyingi.
    Wingi: Rafu za mama zinajaa bidha nyingi.

    Kazi ya 5:
    Tunga sentensi 5 kwa kutumia majina ya ngeli ya I-ZI na kiambishi 
    cha -a unganifu

    20.4. Matumizi ya lugha: Aina za bidhaa zinazopatikana 
    sokoni

    Kazi ya 6
    Bainisha aina kumi za bidhaa zinazopatikana sokoni.
    Maelezo muhimu
    Kuna aina mbalimbali za bidhaa zinazouzwa na kununuliwa sokoni. Baadhi 
    ya bidhaa hizo hutokana na kilimo, ufugaji, vifaa vya ufundi na vile ambavyo 
    hutengenezewa viwandani.
    Kazi ya 7:
    Toa mifano miwili miwili ya bidhaa zinazoweza kupatikana katika mazingira 
    ya sokoni (Bidhaa zitokanazo na viwanda, mazao, ufugaji, madini)
    20.5. Kusikiliza na kuzungumza
    Kazi ya 8:
    Buni mazungumzo kati yako na mwenzako kuhusu majadiliano 
    kati ya muuzaji na mnunuzi. Majadiliano haya yafanyike sokoni na 
    yaonyeshe kutokubaliana kwenye bei ya bidhaa zinazouzwa.
    20.6. Kuandika
    Kazi ya 9:
    Tunga mazungumzo yasiyopungua ukurasa mmoja kuhusu 

    majadiliano ya bei dukani.

    cc

    Kazi ya 1:
    Tazama mchoro hapo juu na kueleza kinachofanyika.

    21.1. Kusoma na ufahamu: Matumizi bora ya mizani

    vv

    Bwana Muhire ni mfanyabiashara katika soko linaloitwa Maridadi. Biashara 
    yake inahusu uuzaji wa matunda, bidha za kula, na mafuta ya kupikia. Mara 
    nyingi raia humlalamikia wakisema kuwa yeye hatumii vipimo sahihi.
     

    Siku moja, Amina alikwenda sokoni kununua bidhaa tofauti za matumizi 
    ya nyumbani. Soko hilo lilikuwa kwenye umbali wa kilomita mbili kutoka 
    kwake. Alipofika sokoni, alikaribishwa na muuzaji aitwae Muhire. Muhire 
    anajulikana sana katika soko hili la Maridadi. Muhire alimwomba kutaja vitu 
    vyote alivyokuwa anataka kununua. 

    Baadhi ya bidhaa alizokuwa anahitaji kulikuwa kilo kumi za maharage, 
    kilo moja na nusu ya chumvi, lita tano za mafuta ya kupikia, gramu mia 
    mbili hamsini ya nyama za kupikia ndugu yake mdogo, mafungu mawili ya 
    sukumawiki na fungu moja la nyanya.

    Baada ya kuorodhesha bidhaa hizo zote, aliomba Muhire kuchukua mizani 

    na kupima ili kuhakikisha kwamba hamnyang’anyi. Muhire alichukua 
    mizani na kuanza kupima maharagwe. Alipomaliza kupima, Amina aliona 
    kuwa maharagwe yaliyokuwa yamepimwa yalikuwa machache akaanza 
    kumlalamikia. Mbona unanipa maharagwe kidogo? “Mizani yako si sahihi,” 
    Amina alisema. Amina alienda nyuma ya kibanda akapigia simu mfanyakazi 
    katika Bodi ya Mapato Rwanda. 

    Katika dakika thelathini viongozi wanaohusika na ushuru nchini walitembelea 
    soko hilo na kuwakagua wafanyabiashara halamu. Walitembelea watu 
    ishirini na kukagua jumla ya mizani ishirini na miwili. Baadhi ya mizani hiyo, 
    iliyokutwa sahihi ni ishirini na jumla ya mizani miwili ilikutwa na kasoro. 
    Tokea hapo, mizani hii haikuruhusiwa katika biashara mpaka itengenezwe 
    na mafundi na kuhakikiwa upya na wakala wa Vipimo ili iweze kuruhusiwa 
    kutumiwa katika biashara.

    Wafanyabiashara waliotuhumiwa ni Muhire na Kazimoto ambao walikubali 
    kosa lao la kutaka faida nyingi mno kwa njia isiyo halali. Bila kusita , viongozi 
    waliwashawishi raia na wafanyabiashara kutumia mizani iliyopimwa tu yaani 
    iliyo sahihi.

    Katika hatua nyingine, kiongozi mkuu aliwaonya wafanyabiashara 
    wanaolalamikiwa kuweka mawe, kokoto pamoja na mchanga,vipande vya 
    vyuma na aina nyingine za vitu kwenye mizani kwa ajili ya kuongeza uzito 
    waache tabia mbaya hiyo mara moja kwani wakikamatwa watapata hasara. 
    Alieleza kwamba sheria ya vipimo ipo na inafanyakazi kwa pande zote mbili 
    yaani kwa muuzaji na mnunuzi. 

    Wote hawatakiwi kufanya udanganyifu wowote katika biashara. Alisisitiza 
    kuwa wale watakaobainika kuchezea mizani kwa ajili ya kuwaiba wananchi 
    adhabu ni kubwa sana kwawo kama vile kifungo au kutozwa faini au vyote 
    kwa pamoja ; shabaha ikiwa ni kumlinda mlaji ili apate faida na thamani ya 
    kile alichozalisha ama kukinunua na siyo tu kupunjwa na wafanyabiashara 
    wajanjawajanja.

    Baada ya mkutano, mbele ya watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo 
    sokoni, viongozi walitoa tuzo ya mizani nne kwa wafanyabiashara ambao 
    hawakuwa na makosa yoyote katika shughuli zao za kibiashara. Hii ilikuwa 
    ni kutoa mfano kwa watu wote ili kusipatikane tena kosa lile la kuiba watu. 

    Watu waliokuwepo walifurahi na kuwapigia makofi viongozi wao. Viongozi 
    nao waliwapongeza kwa kuwa waliwajulisha hali ya makosa yanayofanywa 
    na wafanyabiashara wakiwanyonya raia.

    Kazi ya 2:

    Maswali ya ufahamu
    1. Nani ambaye alilalamikiwa kuwa na matumizi ya mizani isiyo sahihi?
    2. Bainisha aina mbili za adhabu ambazo hupewa mtuhumiwa anayehusika na matumizi ya mizani isiyo sahihi.
    3. Ni onyo gani lililotolewa na kiongozi mkuu kwa wafanyabiashara wanaotumia mizani kinyume na sheria? 
    4. Eleza lengo la ziara ya viongozi wanaohusika na ushuru katika soko la Maridadi.
    5. Afanyaye vizuri hutuzwa. Eleza kauli hii kwa kutoa mfano kutoka katika kifungu hiki cha habari.
    21.2. Matumizi ya msamiati
    Kazi ya 3:

    Oanisha maneno katika sehemu A na maana yake katika sehemu B.

    ccc

    21.3. Sarufi: Matumizi ya ngeli ya I-ZI na vivumishi vya kurejesha
    Kazi ya 4
    Soma sentensi katika sehemu A na kujadili mabadiliko ya kisarufi 

    yanayojitokeza katika sehemu B:

    vv

    Maelezo muhimu
    Majina ya ngeli ya I-ZI, katika sentensi hutumia kirejeshi -yo katika umoja 
    na kirejeshi -zo katika wingi. Vivumishi hivi kuwa vinarejelea nomino.
    Mfano: 
    Umoja: Pikipiki ambayo amenunua imemtajirisha.
    Wingi: Pikipiki ambazo wamenunua zimewatajirisha.
    Kazi ya 5
    Kwa kutumia kirejeshi amba-, tunga sentensi katika umoja na wingi 
    kwa kutumia maneno yafuatayo:

    a. Klabu
    b. Chupa
    c. Redio
    d. kaptula
    e. suruali

    21.4. Matumizi ya lugha: Matumizi ya mizani katika hesabu na aina za pesa
    Kazi ya 6
    Taja aina za mizani au vipimo unavyovijua
    Maelezo muhimu
    A. Matumizi ya mizani au vipimo
    Kipimo ni kiasi au kadiri. Kuna vipimo vya aina tofauti.
    Jedwali lifuatalo linaonyesha aina mbalimbali za vipimo.
    vv
    B. Hesabu

    Mifano ya hesabu kwa tarakimu na kwa maneno kutoka 1-1,000,000

    vvv

    cc

    Kazi ya 7:
     Andika kwa tarakimu 
    a. Kumi na sita
    b. Thelathini na moja
    c. Sabini na saba
    d. Mia tatu hamsini
    e. Moja elfu mia mbili na saba
    f. Laki tano
    g. Moja elfu mia mbili ishirini na sita
    C. Alama za hesabu
    Alama ni mchoro wa kutambulisha kitu (Ishara)

    Jedwali lifuatalo linaonyesha alama za hesabu na maana zake.

    vv

    Kazi ya 8:
    Andika kwa tarakimu
    a. Sitini jumlisha kumi ni sawa na sabini.
    b. Mia moja arobaini toa ishirini na saba ni sawa na mia moja na kumi na tatu.
    c. Mia nane na themanini gawanya kwa nane ni sawa na mia moja na kumi.
    d. Sabini na moja ni kubwa kuliko kumi na nne.
    e. Mia moja ni ndogo kuliko laki moja.
    f. Tisini mara tatu ni sawa na mia mbili na sabini.
    D. Aina za pesa zitumiwazo katika shughuli za kibiashara
    Kazi ya 9:

    Tazama mchoro ufuatao na kueleza shughuli zinazofanyiwa hapo.

    ccc

    Maelezo muhimu
    Pesa ni nini?
    Pesa ni chombo cha kubadilishana bidhaa na huduma kati ya watu. Pesa 
    zenyewe hazina faida na hazitoshelezi mahitaji ya binadamu ila zimekubalika 
    katika jamii kama njia ya kujipatia mahitaji mengine. Kuna majina mengine 
    ya pesa katika Kiswahili, kama kwa mfano: hela, fedha, dirhamu, darahima, 
    fulusi au sarafu, n.k.

    Pesa hutolewa na serikali ya nchi au na taasisi kama vile benki kuu inayofanya 
    kazi hii kwa niaba ya serikali.

    Kuna aina nyingi za pesa zinazotumiwa duniani katika biashara. Jedwali 
    lifuatalo linatuonyesha baadi ya aina tofauti za pesa na nchi au bara 
    zinakotumiwa.
    cc
    Kazi ya 10:
    Kamilisha sentensi hizi kwa kutumia aina ya pesa zinazotumiwa 
    katika nchi au bara husika.
    a.       Wanyarwanda wengi hutumia …………………..katika shughuli 
                   nyingi za biashara ya ndani.
    b.          Mjomba wangu alikwenda kumtembelea rafiki yake anayeishi 
                Uganda. Kabla ya kuvuka mpaka alikwenda kwenye duka la 
                  kubadilisha pesa ili wampe ………..za Uganda.
    c.            Mama aliniahidi kwamba nikishika nafasi ya kwanza katika kidato 
                 cha kwanza atanitembeza Marekani. Katika safari yetu tutatumia 
                 ………………… mia nne za kimarekani.
    d.         Shughuli za biashara anazozifanya mama yangu huhusisha 
               uagizaji wa bidhaa kutoka Japani. Kila wiki hulipa ……..elfu tano.
    e.       Je, uliwahi kufika katika duka la kubadilisha pesa? Mimi nilifikapo 
               nikaona faranga za Rwanda, Shilingi za Kenya, Dola za Marekani 
               na Kanada na ………..za Uingereza.
    Kazi ya 11:
    Tafuta aina tofauti za pesa zinazotumiwa katika nchi nyingine ambazo 
    hazikushughulikiwa katika somo hili.
    21.5. Kusikiliza na kuzungumza
    Kazi ya 12:
    Katika jozi, simulia mwenzako sifa za soko fulani uliyoitembelea na 
    kueleza bidhaa ulizoziona.
    21.6. Kuandika
    Kazi ya 13:
    Tunga kifungu cha habari kifupi kuhusu umuhimu wa biashara
    Tathmini ya mada
    1. Taja angalau vifaa kumi vinavyouzwa sokoni.
    2. Chagua neno linalofaa katika mabano na kukamilisha sentensi 
    zifuatazo:
    a. Mwalimu wetu huvaa suti nzuri sana. Wanafunzi wote hufikiri 
    kwamba suti zake hununuliwa kwa bei ………. (ghali, rahisi, rafi).

    b. Dada yangu amekwenda sokoni …………………….sare ya shule ili arudi 
    shuleni kesho kuanza masomo ya muhula wa tatu( kununua, kuuza).
    c. Uwantege anauza matunda katika soko la Nyagasambu. Kwenye kibanda 
    chake kuna ,………….,………,……… na ………….( maembe, ndizi 
    mbivu, machungwa, viazi vitamu, tikitimaji, mchele, madaftari, mananasi).
    d. Mwenye duka la vitabu alitoa ………………………………. ya kitabu 
    kimoja cha hadithi za Kiswahili kwa wateja wote ambao hununua kwake 
    kila wiki (nyongeza, mtaji).
    e. Wakati wa uhaba wa …………… sokoni, bei hupanda sana (wateja, 
    wanunuzi, bidhaa).
    3. Kwa kuzingatia matumizi ya ngeli ya I-ZI, tunga sentensi sahihi kwa 
    kutumia maneno yafuatayo:
    a. Nchi
    b. Tarafa 
    c. Serikali 
    d. Barabara
    e. Shule
    4. Kamilisha kifungu cha habari hiki kwa kutumia maneno sahihi.
    Mama Mutoni ni mfanyabiashara katika soko la Nyarugenge. Mara nyingi 
    huagiza bidhaa kutoka nchi zinazopakana na Rwanda. Anapoagiza 
    bidhaa kutoka Uganda inambidi abadilishe …………za Rwanda katika 
    ……………..za Uganda. Ni sawa na kuagiza bidhaa kutoka Tanzania na 
    Kenya.
     

    Ikiwa Mama anahitaji bidhaa zinazotengenezewa katika nchi za Ulaya 
    kama Vile Uingereza, inambidi kutumia ………………Mwezi uliopita 
    rafiki yake ambaye anaishi Marekani alimwambia kuwa kuna bidhaa 
    nzuri zinazoweza kumletea faida nyingi anapoziuza kwa Wanyarwanda. 
    Mama aliamua kumtumia ………….elfu tatu za Marekani ili amnunulie 
    bidhaa hizo.

    Kazi ya biashara naipenda sana. Kuna wakati amabapo naenda pamoja 
    na mama yangu Zambia na Libya kufanya biashara huko nikaona namna 
    anavyobadilisha faranga zake katika …………….. Libya au ……….za 
    Zambia nikawa na motisha ya kufanya biashara ya kubadilisha pesa siku 
    moja. Mimi nafikiri kwamba aina hii ya biashara itachangia kuongeza 
    mapato yetu nyumbani.
    5. Buni mazungumzo yenye ukurasa mmoja kati ya muuzaji na 
    mnunuzi katika duka la vitabu.


    MADA YA 4 MSAMIATI KUHUSU MAENEO YA UTAWALAMADA YA 6 UIGIZAJI WA MAZUNGUMZO