• MADA YA 4 MSAMIATI KUHUSU MAENEO YA UTAWALA

    Uwezo mahususi : Kuzungumza na kuandika kwa ufasaha matini fupifupi 
    kwa kutumia msamiati unaofaa katika maeneo ya utawala.Malengo ya ujifunzaji:
    • Kutoa msamiati utumiwao katika maeneo ya utawala, ngazi za utawala na viongozi wakuu wa kiserikali,
    • kutaja aina za vitambulisho vinavvotumiwa na sikukuu za kitaifa,
    • Kuainisha makazi ya watu mbalimbali, 
    • Kutumia kwa usahihi vivumishi vya majina ya ngeli ya U-ZI,
    • Kuzungumza na kuandika kwa ufasaha Kiswahili kwa kutumia msamiati kuhusu utawala.Kidokezo
    • Katika mazingira unamoishi kuna viongozi wa aina gani?
    • Je, tarehe ya 1 Februari inakukumbusha nini kila mwaka? 

    • Taja aina tatu za vitambulisho unavyovijua.

    tt

    Kazi ya 1:
    Jengo hili linakuonyesha nini?
    15.1. Kusoma na ufahamu: Ofisi za kiutawala
    Soma mazungumzo yaliyo hapa chini baina ya Abayo, Baba, Gloriose 
    na Anezerwe.

    (Abayo alikubaliana na babake kwenda kuwashawishi rafiki zake ili 
    waambatane kumpokea rais wa jamhuri katika ziara yake wilayani kwao) 
    Abayo: Shikamoo baba!
    Baba: Marahaba mwanangu. U safi leo kabisa!
    Abayo: Ndiyo, leo tutampokea rais wetu wa jamhuri hapa kwetu.
    Baba: Hilo ni jambo muhimu sana. Kila mtu ataenda kumpokea.
    Abayo: Unajua atazuru miundombinu kadhaa wilayani humu kama vile: 
    kuanzisha mradi wa umwagiliaji, kuzindua mradi wa ukarabati wa 
    nyumba kwa familia zilizokumbwa na mvua kali na ukarabati wa 
    barabara ya lami.
    Baba: Nenda uwajulishe rafiki zako Gloriose na Anezerwe ili wasikose kuhudhuria. 
    Abayo: Kweli kabisa! Ebu niende. 
    Baba: Haya, safari njema.
    Abayo: Hamjambo rafiki zangu.
    Gloriose: Hatujambo sana! Karibu kwetu.
    Abayo: Ningetaka kuwakumbusha ziara ya rais wa jamhuri katika wilaya 
    yetu. Sherehe za kumpokea zinatarajiwa kufanyika kwenye uwanja 
    wa michezo Ituze.
    Gloriose: Uwanja huo unapatikana wapi?
    Abayo: Unapatikana katika kijiji cha Kinini, kata ya Gitabi, tarafa ya Bwiza, 
    wilaya Bikombe, mkoa wa Mashariki.
    Anezerwe: Haaa! Nyinyi mmeisha kuwa wanasiasa! Hayo yote mimi siyajui.
    Abayo: Ni kusema kwamba hujui hata wilaya yetu pamoja na mkoa?
    Gloriose: Tafadhali, acha Abayo aendelee na habari yake ya ziara ya rais.
    Abayo: Nimekuja kuwaalika ili msije mkakosa bahati ya kuwaangalia viongozi mbalimbali.
    Anezerwe: Kweli? Viongozi wepi? Jamaa, tupatie mfano.
    Abayo: Mawaziri mbalimbali akiwemo wa elimu, wabunge na maseneta, 
    gavana wa mkoa wetu, wakuu wa wilaya mbalimbali, viongozi wa tarafa, wakuu wa jeshi na polisi kwenye ngazi mbalimbali, n.k.
    Gloriose: Ehee! Viongozi wanapaswa kuweko ili wananchi wakiuliza swali lo lote watoe mchango wao katika kujibu au kumfafanulia rais.
    Anezerwe: Hii ndiyo fursa yangu kuuliza swali kiongozi wa tarafa 
    aliyetunyang’anya mabati yetu ya kutujengea nyumba baada ya dhoruba kali kuiangusha nyumba yetu.
    Gloriose: Rais wetu ni mzuri atawauliza viongozi walichokifanya ili tusiteswe namna hii.
    Abayo: Jamani! Naona saa za kuenda zimefika. Twende tufike mapema ili umati wa watu usitukataze kumwona rais.
    Anezerwe: Eeeh!Twende. Asante sana Abayo kutujulisha.
    Gloriose: Mienendo bora ya wananchi ni kujiendeleza, uzalendo na ushikamano, n.k.

    Abayo: vizuri, twende.

    Kazi ya 2:
    Maswali ya ufahamu
    A. Baada ya kusoma mazungumzo hapo juu, jibu maswali yafuatayo:
    1. Ni wahusika gani wanaozungumza?
    2. Kwa sababu gani Abayo aliamua kwenda nyumbani kwao Gloriose 
    na Anezerwe?
    3. Sherehe zinatarajiwa kufanyika wapi?
    4. Raia wamealikwa kuwapokea viongozi gani?
    5. Eleza miundombinu zilizotajwa katika kifungu cha habari.
    6. Andika baadhi ya mienendo bora uliyoisoma katika mazungumzo.
    B. Jaza sentensi zifuatazo kwa kutegemea mazungumzo hapo juu
    i. ……….. ndiye alikwenda kuwaarifu………………ziara 
    ya……………………..
    ii. Ziara hii inatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi kadhaa kama 
    vile………………..
    iii. Lengo kuu la ziara hii ni kuanzisha miradi ya kimaendeleo kama 
    vile……………..
    15.2. Matumizi ya msamiati 
    Kazi ya 3:
    Fafanua msamiati ufuatao:
    Rais 
    Mbunge
    Waziri 
    Umwagiliaji 
    Dhoruba 

    Miundombinu 

    Kazi ya 4:

    Oanisha msamiati wa sehemu A na viongozi katika sehemu B

    rr

    rr

    Kazi ya 6:
    Tazama sentensi zifuatazo zilizo katika sehemu A na sehemu B na 

    kueleza mabadiliko ya kisarufi yanayojitokeza.

    cc

    Maelezo ya kuzingatia
    Ngeli hii inajumuisha nomino za vitu visivyo na uhai ambazo zinajigawa 
    katika makundi matano yafuatayo:
    1. Nomino ambazo umoja huanza kwa u- na wingi Ø-.
    Kwa mfano: unywele, ukuta, ufagio, ufunguo, unyasi, utepe, utosi, ukoo, 
    upote, upenu, upondo, upongoo, upanga, upepeo, n.k.
    2. Nomino ambazo umoja huanza kwa u- na wingi wake huanza kwa ny-
     Kwa mfano: uta, ufa, uwanja, uso, uwayo, uzi, uwalio, ugwe.
    3. Nomino ambazo umoja huanza kwa w- na wingi huanza kwa ny-
    Kwa mfano
    : waraka, wakati, wembe, wimbo, wayo, waya, wavu, wanja, 
    wanda, wadhifa, waadhi.
    4. Nomino ambazo umoja huanza kwa u- na wingi huanza kwa nd-
    Kwa mfano: ulimi, uele.
    5. Nomino ambazo umoja huanza kwa u- na wingi huanza kwa mb-
    : ubao, ubavu, ubati, ubale.
    Mifano zaidi katika sentensi:
    Umoja: 

    1. Ukuta huu umebomolewa na Umutoni.
    2. Ufunguo wake utafungua vizuri.
    3. Ukurasa wenyewe si mrefu.
    4. Ukucha ule umechorwa na Nikuze.
    5. Uso wa Solange ni mzuri 
     Wingi:
    1. Kuta hizi zimebomolewa na Umutoni
    2. Funguo zao zitafungua vizuri
    3. Kurasa zenyewe si ndefu
    4. Kucha zile zimechorwa na Nikuze
    5. Nyuso za solange ni nzuri
    ff

    Vivumishi katika ngeli ya U-ZI
    1. Vivumishi vya kuonyesha
    Mfano:
     Umoja                                                     Wingi
    Wimbo huu unapendeza.                      Nyimbo hizi zinapendeza.
    Uzi huu umetoka wapi?                          Nyuzi hizi zimetoka wapi?
    Ukurasa huo umeandikwa vizuri.      Kurasa hizo zimeandikwa vizuri.
    Utepe ule umenunuliwa leo.                Tepe zile zimenunuliwa leo.
    Maelezo:
    Maneno ule,zile,hizo na huo ni vivumishi vya kuonyesha katika ngeli ya U-ZI, 
    kwa sababu vinaonyesha jina au nomino fulani. Katika umoja: huu,huo na

    ule hutumiwa na hizi,hizo,zile hutumiwa katika wingi.

    Kazi ya 8:
    Jaza sentensi hizi kwa kutumia jibu sahihi kutoka mabanoni.

    1. Ufito ……………utakatwa upya.(huyu,huu,hii).
    2. Fizi ……….zilijeruhiwa kutokana na ajali ya baiskeli (hio,huo,hizo).
    3. Ufunguo…………unaweza kufungua nyumba yangu (ule,ile,zile).
    4. Mwanafunzi ataandika ukurasa…………. vizuri(hio,huo,hizo).
    5. Nyufa ……………. zitazibwa na mwashi hodari (huu,hizi,hii).

    2. vivumishi vya pekee

    Kazi ya 9:
    Soma kifungu cha habari kifuatacho na kueleza matumizi ya maneno 
    yaliyopigiwa mstari 

    Bwana Kamali ni Mwalimu kwenye shule ya Mahoro. Siku moja akiwa 
    njiani kuelekea shuleni alipoteza funguo zake pamoja na ufunguo 
    wenyewe wa gari lake. 

    Kwa bahati nzuri funguo zile zote zilipatikana na kumwezesha kufika 
    shuleni. Alipofikapo aliwapa wanafunzi wake kazi ya kuandika kurasa 
    kumi za insha. Binti mmoja aitwaye Tamari aliandika ukurasa mmoja tu. 
    Kwenye ukurasa wenyewe alichora picha za wanyama wenye kucha 
    ndefu. Kucha zenyewe zilikuwa chafu mno. Mwalimu alimwonyesha 
    mfano mzuri wa kufuata. Kwa hiyo, binti alikubali mfano wa mwalimu.
    Uso wa mwalimu ulionekana kuwa na furaha vilevile na uso huo wa binti 
    Tamari ukaonyesha furaha tele.
    Maelezo
    Maneno wenyewe na zenyewe ni vivumishi vya pekee vyenye dhana 
    kurejesha katika ngeli ya U-ZI, kwa sababu vina uaminifu wa kulirejea lile jina 
    linalowakilishwa.Katika umoja wenyewe hutumiwa na zenyewe ikatumiwa katika  wingi.
    Mfano:                 Umoja                                               Wingi
                    Uzi wenyewe                                    Nyuzi zenyewe
                    Ukurasa wenyewe                           Kurasa zenyewe
                    Mifano katika sentensi
    Umoja                                                               Wingi
    Uso wenyewe umeharibika.              Nyuso zenyewe zimeharibika
    Ufagio wenyewe umepotea.              Fagio zenyewe zimepotea.

    15.4. Matumizi ya lugha: Ngazi za utawala
    Kazi ya 10:
     Jadili maswali yafuatayo:
    a. Maeneo ya utawala nchini Rwanda yanaonekana katika muundo gani?
    b. Panga viongozi wa utawala nchini Rwanda kulingana na ngazi zao
    Maelezo muhimu
    1. Muundo wa ngazi za utawala nchini Rwanda
    Kijiji
    kata 
    Tarafa
    Wilaya
    Mkoa
    Taifa/nchi
    2. Ngazi za viongozi
    Mkuu wa kijiji
    Katibu mtendaji wa kata
    Katibu mtendaji wa tarafa
    Meya/mkuu wa wilaya
    Gavana
    Viongozi wakuu wa taifa (Rais, waziri mkuu, mawaziri,wabunge, maseneta)
    Nchi ya Rwanda ina jumla ya Mikoa 5, Wilaya 30, Tarafa 416 na Kata 2 148 
    na Vijiji 14 837.

    Mji wa Kigali huongozwa na Meya wa mji. Viongozi wengine wanaopatikana 
    katika ngazi za utawala ni wale wanaosimamia ngazi za usalama kama 
    vile jeshi na polisi pamoja na viongozi wa vyeo mbalimbali vya kiserikali. 
    Maseneta, Wabunge, Makatibu katika wizara tofauti, wakuu wa jeshi, wakuu 
    wa polisi,…….Wote hushirikiana ili kuliendeleza taifa na kumsaidia rais wa 
    jamhuri kuyafikia majukumu yake.Hii inamaanisha kwamba viongozi wote 
    wakitimiza majukumu yao, nchi itaweza kuendelea haraka na kuukuza 
    uchumi wake.
    Kazi ya 11:
    Oanisha sehemu A na sehemu B
    cc

    Kazi ya 12:
    Kamilisha sentensi zifuatazo:
    1. Karongi ni mojawapo ya …………………...zinazounda …………….
    wa Magharibi.
    2. ………………………wa jamhuri ya Rwanda alihutubia raia wote.
    3. Nishati, umeme, ukarabati wa barabara ni baadhi ya …………………
    4. Gavana ni kiongozi mkuu wa ………………………………………….
    5. a.Idadi fulani ya kata inaunda …………………………………………
    b. Jamhuri ya Rwanda inaongozwa na ……………………………
    c. Rwanda imegawanyika katika mikoa ifuatayo:…………………
    15.5. Kusikiliza na Kuzungumza
    Kazi ya 13:
    Igiza na wenzako mazungumzo kuhusu kifungu cha habari 
    kilichosomwa awali “Ofisi za kiutawala.”
    Kazi ya 14:
    Iandae ziara kwenye kituo cha utawala kilichoko karibu yako na 

    kusimulia mbele ya darasa kuhusu ziara yako.

    Kazi ya 15:
    Jitambulishe kwa mwenzako kwa kuzingatia maeneo ya utawala 
    unamoishi pamoja na viongozi wake.
    15.6. Kuandika 
    Kazi ya 16:
    Tunga mazungumzo kati ya raia mmoja na kiongozi wilayani juu ya 
    huduma ya kuomba kitambulisho fulani. 
    Kazi ya 17:
    Tunga kifungu cha habari kifupi kwa kutumia msamiati ufuatao:
    a. Mkoa
    b. Jamhuri
    c. Kata

    d. Wilaya

    SOMO LA 16: MAKAZI YA WATU

    ccc

    Chunguza mchoro huu, kisha ueleze ikiwa unayoyaona yanahusiana 

    na makazi ya watu

    16.1. Kusoma na ufahamu: Makazi ya watu

    Makazi ni eneo au  mazingira ambayo ni makao ya mnyama au mmea fulani 
    au aina nyingine ya  viumbe hai. Ni mazingira ya asili ambapo kiumbe 
    huishi, au mazingira ambayo yanazunguka idadi ya jamii. Kuhusu makazi 
    ya bianadamu, haya ni mazingira ambayo binadamu huishi na kuingiliana. 
    Kwa mfano, nyumba ni makazi ya binadamu, ambapo binadamu hulala na 
    kula. Haya yanaweza kuwa mjini au vijijini. Makazi ya mjini ni aina ya makazi 
    ambayo watu wanajenga nyumba zao mijini, karibu na wenzao wengi. Mji 
    wenye wakaaji wengi ni mji mkuu wa Kigali na miji kama Musanze, Huye, 
    Rubavu, Rusizi, Muhanga na Nyagatare inayosaidia jiji la Kigali. Miji hii yote 
    ina miundombinu mbalimbali kama vile umeme, maji safi, viwanda kadhaa, 
    hospitali, barabara za lami, n.k.

    Makazi ya vijijini ni aina ya makazi ambayo watu hujenga nyumba zao 
    sehemu za vijijini. Asilimia kubwa ya Wanyarwanda huishi sehemu hii lakini 
    serikali inaendelea kuwapa miundombinu tofauti kama inavyofanyia miji. 

    Nchini kwetu, serikali imewakataza raia kujenga na kuishi katika maeneo 
    hatari kama vile vinamasini, mabondeni, milimani na sehemu nyingine zote 
    zinazoweza kuhatarisha maisha yao. Serikali imetoa mchango mkubwa 
    kulitatua tatizo hili kwa kuhamisha raia wote waliokuwa katika maeneo haya 
    ya hatari ikiwapatia maeneo mazuri pia salama na kuwajengea nyumba bora 
    vilevile. Hii inalenga wale wanaoishi katika mabonde chini ya milima mirefu 
    kuepuka mmomonyoko wa ardhi na watu waliokuwa wamejenga kando ya 

    mito na maziwa. 

    Kazi ya 2:
    Maswali ya ufahamu
    1. Taja aina za makazi bora kwa binadamu? 
    2. Eleza maeneo yasiyokubaliwa kuishi nchini Rwanda.
    3. Serikali ya Rwanda ilifanya nini kuwaokoa waliokuwa wanaishi katika maeneo ya hatari?
    4. Taja miundombinu ambayo serikali ilifikisha vijijini ili kusaidia raia kuishi vema.
    5. Je, mmomonyoko wa ardhi husababishwa na nini?

    6. Je, ungependa kuishi wapi kati ya mjini na kijijini? Kwa nini?

    7. Jibu “NDIYO au HAPANA” kwa sentensi zifuatazo:
    a. Binadamu hukaa katika nyumba.
    b. Mji wa Kigali ni mji wenye wakaaji wengi duniani.
    c. Sehemu za vijijini nchini Rwanda zina miundombinu mbalimbali.
    d. Nchini Rwanda raia wanaweza kujenga nyumba zao sehemu 
    yoyote.
    16.2. Msamiati kuhusu makazi
    Kazi ya 3:
    Fafanua maneno yafuatayo:
    a. Nyumba 
    b. Bondeni 
    c. Mmomonyoko wa ardhi: 
    d. Kinamasi 

    e. Mjini 

    Kazi ya 4:

    Oanisha maneno katika kundi A na maana yake katika kundi B

    bb

    16.3. Sarufi: Matumizi ya ngeli ya U-ZI
    Vivumishi vya idadi 
    Kazi ya 5:
    Tazama sentensi hizi na kujadili mabadiliko ya kisarufi yaliyojitokeza:
    Ufagio mmoja umetumiwa kwetu.
    Ukurasa mmoja umeandikwa vizuri.
    Kuta mbili zitajengwa lini?
    Fagio tatu zimeletwa na wavulana.
    Nyufa chache zimezibwa na Ishimwe.
    Maelezo 
    Maneno mmoja, mbili, tatu, nne, chache,…. ni vivumishi vya idadi katika 
    ngeli ya U-ZI, kwa sababu vinaonyesha idadi au hesabu ya vitu. Aina hii ya 
    vivumishi tunaweza kuigawa katika makundi mawili:
    • Vivumishi vya idadi vinavyoonyesha idadi kwa jumla.
    • Vivumishi vya idadi vinavyoonyesha idadi kwa hesabu.
    Vivumishi vya idadi vinavyoonyesha idadi kwa jumla. Mifano ya vivumishi 
    vya idadi vya kundi la kwanza ni kama:
    i. chache
    ii. ingi
    iii. maridhawa
    iv. pungufu
    v. haba
    vi. kidogo, n.k.
    • Vivumishi vya idadi vinavyoonyesha idadi dhahiri: ni vya idadi isiyo kikomo 
    kwani vinahusu hesabu ya nambari kuanzia moja na kuendelea.
    Mfano:
    i. moja
    ii. mbili 
    iii. tatu 
    iv. nne
    v. kumi
    vi. miavii. 
    vi.elfu

    viii. milioni, n.k.

    Kazi ya 6:

    Weka sentensi hizi katika umoja au wingi:

    cc

    Kazi ya 7:
    Jaza nafasi zilizoachwa wazi kwa kutumia kivumishi kinachofaa mabanoni.
    a. Upondo ……………….. umewekwa ndani ya mtumbwi (moja, mmoja, mbili).
    b. Petero aliandika kurasa…………………..(zitano,tano,moja).
    c. Umutoni na Abayo walipokea fagio………………. Siku ile (nyingi, moja, wengi).
    d. Mtoto aliwaandikia wazazi wake nyaraka……………katika muhula wa tatu. (nyingi, zingi, lingi).
    e. Wembe ……………ulimkata kidole (moja, mmoja, wumoja).
    16.4. Matumizi ya lugha: Makazi ya watu
    Kazi ya 8:
    Jadili maswali yafuatayo:
    a. Makazi ni muhimu sana kwa binadamu.
    b. Serikali ya Rwanda iliwakataza raia kujenga na kuishi katika maeneo hatarishi.

    Maelezo muhimu

    Kama ilivyoandikwa katika kifungu cha habari, makazi  ni eneo 
    au mazingira ambayo ni makao ya mnyama au mmea fulani au aina nyingine 
    ya viumbe hai. Ni mazingira ya asili ambapo kiumbe huishi, au mazingira 
    ambayo yanazunguka idadi ya  jamii. Binadamu anaweza kuishi katika 
    nyumba kubwa au ndogo kulingana na uwezo wake. Nyumba hizi lazima 
    ziwe safi ili kujiepusha na magonjwa yatokanayo na uchafu. Ghorofa ni aina 
    ya nyumba pia ambayo familia moja au nyingi huweza kuishi.
    16.5. Kusikiliza na kuzungumza: Majadiliano kuhusu makazi
    Kazi ya 9:
    Zungumzia wenzako umuhimu wa kuishi katika maeneo yasiyo hatari.
    Kazi ya 10:
    Simulia wenzako kuhusu picha au video ulizoziona zinazohusu 
    makazi nchini Rwanda hasa hasa mji wa Kigali. 
    16.6. Kuandika: Utungaji wa insha kuhusu makazi
    Kazi ya 11:
    Tunga insha yenye aya 3 (Maneno yasiyopungua mia moja) ukielezea 
    umuhimu wa kuishi katika maeneo yasiyo hatari.

    SOMO LA 17: SIKUKUU ZA KITAIFA
    ccc

    17.1. Kusoma na ufahamu: Sikukuu za kitaifa

    Mwaka jana Yusufu alikuja kututembelea kwenye sikukuu ya Krismasi. 
    Alipofika nyumbani kwetu tulimpokea vizuri kwa chakula pamoja na vinywaji 
    mbalimbali. Tulipomaliza sherehe zetu, mwalimu wetu aliingia ndani na 
    kutuuliza sababu tulikuwa tunafurahi sana. Bila kukawia nilimwambia kuwa 
    nchini Rwanda kuna sikukuu za kitaifa nyingi zinazosherehekewa na kwamba 
    siku hiyo tulikuwa tukisherehekea Krismasi. Mwalimu alituomba kumfafanulia 
    sikukuu nyingine za kitaifa zinazosherehekewa nchini Rwanda. Tulianza 
    kukodoleana macho tukingoja mmoja kati yetu ajibu swali hilo. Mwalimu 
    alipoona kuwa kimya kimetutawala alianza kutufafanulia sikukuu hizo ili mara 
    nyingine tusije tukatatizika. Yusufu alimwambia kwamba hakukumbuka na 
    habari. Mwalimu alianza kumfafanulia sikukuu hizo ili mara nyingine asije 
    akaziuliza tena. “Tarehe ya 1 Januari kila mwaka ni sikukuu ya mwaka 
    mpya, tarehe 1 Februari sikukuuu ya mashujaa, tarehe 7 Aprili kila mwaka ni 
    kumbukumbu ya mauaji ya kimbari dhidi ya watutsi, siku ya kuwakumbuka 
    jamii ya Wanyarwanda iliyoangamia mwaka 1994,” alisema mwalimu. Nami 
    niliongeza kuwa tarehe 1 Mei ni sikukuu ya kazi ulimwenguni, sikukuuu ya 
    uhuru wa Rwanda ikasherehekewa kwenye tarehe 1 Julai na tarehe 4 Julai 
    kila mwaka ikawa sikukuuu ya ukombozi wa Rwanda. 

    Yusufu alituomba kutosahau sikukuu za kidini kama vile Idi kwa waumini wa 
    kiislamu, sikukuu ya Bikira Maria kwa wakatoliki, sikukuu ya pasaka katika 
    mwezi Machi au Aprili, n.k. 

    Kitu kingine alichotuambia mwalimu ni kwamba sikukuu hizi huwapa viongozi 
    fursa ya kukutana na wananchi, kuwajulisha mipango ya serikali, pia hupata 
    fursa ya kupumzika na kuwatembelea jamii na marafiki.

    Kazi ya 1:

    Maswali ya ufahamu
    1. Yusufu alikuja kututembelea kwenye sikukuu ipi?
    2. Nani aliingia baada ya chakula na kinywaji? Alisema nini?
    3. Ni kwenye tarehe gani ulimwengu mzima husherehekea sikukuu ya kazi?
    4. Andika majina matatu ya sikukuu za kidini zinazosherehekewa 
    nchini Rwanda.

    5. Ni kitu gani kinachowanufaisha viongozi kwenye sikukuu hizi?
    17.2. Msamiati kuhusu sikukuu za kitaifa
    Kazi ya 2:
    Eleza maneno yafuatayo ukiyahusisha na kifungu hicho.Tumia 
    kamusi ya Kiswahili Sanifu pale panapohitajika.

    1. Krismasi
    2. Mashujaa 
    3. Kukomboa
    4.Kimbari
    5. Fursa 
    Kazi ya 3:
    Jaza sentensi kwa kutumia msamiati huu: Uhuru, mashujaa, kimbari, 
    makazi, kuikomboa, Krismasi, Idi.

    1. Katika mwezi wa Februari sisi husherehekea sikukuu ya ……………
    lakini ile ya ………….. wa taifa ni mwezi wa Julai.
    2. Mauaji ya …………nchini Rwanda yaliacha watu wengi 
    bila………………
    3. Majeshi ya RPF Inkotanyi yaliwahi…………………..nchi ya 
    Rwanda.
    4. …………………….huanza kulingana na kalenda ya waislamu.
    5. Kwenye sikukuu ya ………..wao walikula chakula kizuri sana.

    17.3. Sarufi: Matumizi ya ngeli ya U-ZI na vivumishi vya sifa

    Kazi ya 4:
    Tazama sentensi hizi na kueleza maneno yaliyopigiwa kistari:
    • Ufunguo mpya unafungua mlango vizuri.
    • Funguo nzuri zinafungua milango vizuri.
    • Ukurasa mbaya umeandikwa na Irakiza. 
    • Kurasa nyekundu zimeandikwa na Irakiza 
    • Mugabekazi ametuagizia ufagio mzito.
    • Mugabekazi ametuagizia fagio nzito.
    Maelezo muhimu
    Vivumishi vya sifa ni vivumishi vinavyotaja tabia au namna vitu vilivyo au 
    vinavyoonekana. Vivumishi vinavyoonyesha tabia hii ni kama hivi vifuatavyo:
    i. -ema                        v. -nyenyekevu
    ii. -pevu                      vi. -danganyifu
    iii. -nyamavu            vii. -changamfu   
    iv. -pumbavu            viii. -ovu, n.k
    Katika mfano hapo juu tunaona kuwa kuna vivumishi vya sifa vinavyoonyesha 
    tabia hasa ya viumbe hai. Ifuatayo ni mifano ya vivumishi vya sifa 
    vinavyoonyesha jinsi vitu vilivyo hai au vinavyoonekana:
    i. -zuri                       v. -nene      
    ii. -baya                    vi. -eusi
    iii. -gumu                 vii. -pya 
    iv. -zito                     viii. -kongwe, n.k

    Kazi ya 5:

    Jaza nafasi zilizoachwa wazi kwa kutumia kivumishi kinachofaa kutoka mabanoni.
    a. Ukucha wake ……………….. umekatwa na Ahirwe (mbaya, baya, mabaya).
    b. Mbwa huyu ana nyayo……………… (msafi, safi, usafi).
    c. Kalisa aliandika kurasa…………………..(refu, ndefu, urefu).
    d. Ufunguo ………………. umepotea njiani (ndogo, mdogo, wadogo).
    Kazi ya 6:
    Andika sentensi mbili zenye vivumishi vya sifa vinavyoonyesha 
    tabia na nyingine mbili za vivumishi vya sifa vinavyoonyesha jinsi 

    vitu vilivyo au vinavyoonekana katika jedwali hili:

    vv

    17.4. Matumizi ya lugha: Sikukuu za kitaifa
    Kazi ya 7:
    Chagua maneno haya na kuyapanga katika kundi A au B
    Pasaka
    Sikukuu ya mashujaa 
    Sikukuu ya ukombozi
    Sikukuu ya kazi ulimwenguni
    Krismasi
    Sikukuu ya uhuru wa taifa
    Sikukuu ya watakatifu wote

    Idi

    Maelezo muhimu
    Sikukuu ni siku yenye shamrashamra ya kuadhimisha tukio fulani. Hii ni siku 
    maalumu ya kukumbuka, kusheherekea au kufurahia jambo fulani. Kati ya 

    sikukuu za umma kuna sikukuu za kidini na sikukuu za kiserikali.

    dd

    17.5. Kusikiliza na kuzungumza: Sikukuu za kitaifa
    Kazi ya 8:
    Jadili kuhusu sikukuu za kitaifa na kutoa matokeo yako hadharani.
    Kazi ya 9:
    Ukitumia sikukuu uliyoisherehekea siku moja au zaidi, zungumzia 
    wenzako jinsi ilivyokuwa.
    17.6. Kuandika 
    Kazi ya 10:
    Tunga kifungu cha habari kuhusu sikukuu fulani uliyoisherehekea 

    siku moja au zaidi kisha uonyeshe vile ulivyoona pale. 

    cc

    vvv

    Kitambulisho cha shule

    18.1. Kusoma na ufahamu: Ombi la vitambulisho
    Uwera, Aline na Rwema walienda kwenye ofisi ya tarafa ili kutafta vitambulisho mbalimbali
    Uwera: Shikamoo Katibu Mtendaji!
    Katibu Mtendaji: Marahaba bibi. Nikusaidie nini?
    Uwera: Nimekuja hapa ili nipate cheti cha kuzaliwa.
    Katibu Mtendaji: Karibu ofisini. Nipe kibali cha Katibu Mtendaji wa Kata.
    Uwera : Hiki hapa Katibu.
    Katibu Mtendaji: Naona wewe namaliza kukupa huduma yako. Mwambie mwingine aingie.
    Uwera: Kwaheri. (Mwingine anayehitaji huduma aingie).
    Rwema: Mimi nataka kadi ya uraia nimetimiza miaka kumi na sita.
    Katibu Mtendaji: Ndiyo. Na wewe?
    Aline: Nimekuja mniandikie kibali niende kwenye wilaya kutafuta pasipoti kwani nitaenda Marekani mwezi ujao.
    Katibu Mtendaji: Barabara kabisa. Rwema, nenda ukamkute mtumishi 
    wa mtandao Irembo atakusaidia haraka. Na wewe Aline mwambatane kwa sababu mna shida sawa.
    Aline& Rwema: Asante sana katibu. Nchi yetu imepiga hatua kiteknolojia.
    Katibu Mtendaji: Asante kushukuru.
    Kazi ya 1:
    Maswali ya ufahamu
    1. Mazungumzo haya yametokea wapi? 
    2. Kwa nini raia walitembelea ofisi ya katibu mtendaji wa tarafa?
    3. Kiongozi yule aliwapokeaje raia?
    4. Rwema aliambiwa kupata alichokitaka wapi?
    5. Ni kwa nyanja gani Rwanda ina maendeleo?
    18.2. Msamiati kuhusu aina ya vitambulisho
    Kazi ya 2:
    Toa maana ya msamiati huu na uutumie katika sentensi
    i. Cheti
    ii. Ofisi
    iii. Huduma
    iv. Kibali
    v. Kuambatana
    Kazi ya 3:
    Jaza sentensi kwa kutumia msamiati ufuatao: pasipoti, huduma, ofisi, cheti
    i. Nilipoingia kazini ilinibidi nitafute………………cha kuzaliwa.
    ii. Mujawase ataulizwa………………..kabla ya kuenda nchini 
    Ujerumani.
    iii. Katibu mtendaji wa tarafa anawapa raia …………….nzuri sana.
    iv. ……………ya wilaya yetu inapatikana mbali na nyumba yangu.

    18.3. Sarufi: Matumizi ya ngeli ya U-ZI na vivumishi vya kumiliki
    Kazi ya 4:
    Tazama sentensi hizi na kujadili mabadiliko ya kisarufi yanayojitokeza.
    1. Wimbo wake unapendeza mno (umoja).
    2. Nyimbo zoo zinapendeza mno (wingi).
    3. Upinde wangu umevunjika (umoja).
    4. Pinde zetu zimevunjika (wingi)
    Maelezo muhimu
    Majina ya ngeli ya U-ZI yametumiwa pamoja na vivumishi vya kumiliki.
    Vivumishi vya kumiliki ni maneno yanayoonyesha kitu ni cha nani, mtu fulani 
    ni wa nani au kitu kina nini . Navyo ni sita: –angu, -etu -ako,-enu -ake,-ao
    Mifano zaidi
     Umoja                                                                                Wingi
    Uso wangu ni mzuri sana.                                   Nyuso zetu ni nzuri sana
    Ufunguo wako ni mchafu kabisa                     Funguo zenu ni chafu kabisa
    Ukuta wake utajengwa upya                            Kuta zao zitajengwa upya
    Kazi ya 5:
    Jaza sentensi hizi kwa kutumia vivumishi vya kumiliki vinavyofaa 
    kulingana na kiambishi cha nafsi ambacho kimeandikwa katika mabano:
    1. Ukucha …………………umerefuka sana (yeye).
    2. Uzi …………………..ni mweusi sana (Kagorora na mimi).
    3. Kazeneza na Mwami waliibiwa funguo ………….zote (wao).
    4. Usikose kupaka rangi ukuta ………..ule kwani umechafuka sana 
    (wewe).

    Kazi ya 6:

    Soma kifungu hiki cha habari na kueleza matumizi ya maneno 
    yaliyopigiwa kistari

    Habari gani Dusabe? Mbona umenunua kufuli lenye ufunguo mmoja? 
    Bila shaka utalirudisha sokoni. “Funguo zipi baba?” Dusabe aliniuliza. 
    “Funguo nyingine nimeziweka kabatini,” Dusabe aliendelea kueleza. 
    Baada ya maelezo yake nilifungua kabati na kuziona zote ndani. Nilikosa 
    cha kusema na kumwambia maneno haya: Samahani binti yangu 
    sitakusumbua tena nimeziona. Uwineza ndiye alikuwa amezichukua. 
    Niliendelea kumwuliza, “umeleta wembe upi?” Tuliongea mengi na 
    kumruhusu aende kula chakula cha mchana. Tokea siku hiyo, Dusabe na 
    Uwineza ni wasichana wapole wenye ukweli.

    Maelezo muhimu: 

    Vivumishi vya kuuliza hutumika kwa kuuliza swali. Badhi ya vivumishi viulizi 
    huchukua viambishi vya ngeli wakati ambapo vingine havichukui viambishi 
    hivyo vikitumiwa pamoja na nomino za ngeli ya U-ZI.
    Kivumishi kinachochukua kiambishi ngeli nitongueouti? Wakati ambapo viulizi –
    ngapi? na gani? Havichukui viambishi vya ngeli.
    Mfano:
     Umoja                                                                                                  Wingi
    Ukuta upi umejengwa ?                                                Kuta zipi zimejengwa ?
    -                                                                                               Kuta ngapi zimejengwa?
    Ukuta gani umejengwa?                                               Kuta gani zimejengwa?
    Kazi ya 7:
    Uliza maswali matatu ukitumia vivumishi –pi au gani katika ngeliya U-ZI
    Kazi ya 8:
    Jaza sentensi hizi ukitumia kivumishi cha kuuliza kinachofaa.
    i. Uwineza alichukua funguo…………….?
    ii. Mchana huo Dusabe aliambiwa habari…………..?
    iii. Ni wembe…………….ambao binti yangu atauleta?
    iv. Tumbili wanapenda kuparamia ukuta………….?
    v. Karatasi …………..zilitengenezwa katika miti ya kwetu?

    18.4. Matumizi ya lugha
    Kazi ya 9:
    Jibu maswali yafuatayo:
    1. Je, raia anaweza kupata vitambulisho vifuatavyo katika ngazi zipi 
    za kiutawala?
     Pasipoti, cheti cha kuzaliwa, Cheti cha ndoa na leseni ya udereva.
    2. Ikiwa kitambulisho fulani kimepotea au kimeibiwa, raia aliyekipoteza 
    atafanya nini?
    3. Je, kuna kosa lolote la utumiaji mbaya wa vitambulisho vya kitaifa? 
    Eleza.
    Maelezo muhimu: Vitambulisho.
    Kitambulisho ni cheti au kadi, aghalabu yenye picha inayotumiwa kwa ajili ya 
    kumtambulisha mtu na mahali pa kazi au mahali pengine ambapo kitu kama 
    hicho kinahitajika. Baadhi ya vitambulisho hivyo ni kama:
    1. Kitambulisho cha utaifa
    2. Cheti cha kuzaliwa
    3. Cheti cha elimu ya msingi,
    4. Pasi ya kusafiria (Pasipoti)
    5. Cheti cha elimu ya sekondari (kidato cha vi)
    6. Leseni ya udereva
    7. Kadi ya bima ya afya
    8. Kadi ya mpigakura
    9. Nambari ya mlipa kodi (Tin. No)
    10. Cheti cha ndoa 
    11. Cheti cha kufariki
    • Nchini Rwanda, idadi kubwa ya vitambulisho hupatikana kupitia 
    mtandao rasmi wa kiteknolojia -IREMBO na kumwangalia kiongozi 
    husika baadaye.

    UMUHIMU WA KITAMBULISHO
    Vitambulisho vya Taifa ni msingi wa maendeleo ya kiuchumi, kijamii 
    na kisiasa.
    1. Vitasaidia kuongeza wigo wa mapato ya Serikali
    2. Vitasaidia kumtambua mhusika kwa urahisi anapohitaji huduma 
    katika taasisi mbalimbali kama vile benki, taasisi za mikopo na huduma za afya.
    3. Vitarahisisha kuwatambua wakwepaji wa kurejesha mikopo kutoka 
    kwenye benki na asasi mbalimbali za fedha nchini.
    4. Vitasaidia kuweka kumbukumbu za matukio ya uhalifu katika daftari la kumbukumbu la kielektroniki.
    5. Vitawezesha kumtambua mtu anapofanya biashara au shughuli nyingine kwa kutumia majina tofauti.
    6. Vitafanikisha kuhakikisha kuwa mtu anapata stahili zake za jamii. 
    Kwa mfano, kupata malipo ya pensheni, haki za matibabu, haki za 
    kujiunga na masomo ikiwa ni pamoja na stahili zozote ambazo raia 
    wa Rwanda anastahili kupata kwa urahisi kwani kupitia kitambulisho 
    mtu atatambulika kwa urahisi (fulani ni nani?, yuko wapi?, na anafanya nini? katika taifa hili.
    7. Vitasaidia  kuondoa watumishi hewa kwenye mfumo wa malipo ya mishahara ya Serikali.
    8. Vitaimarisha utendajikazi Serikalini kwa kuwa na kumbukumbu sahihi 
    za watumishi na malipo ya stahili zao, hasa pale wanapostaafu.
    9. Vitarahisisha zoezi la kuhesabu watu (sensa).
    10. Vitarahisisha zoezi la kusajili wapigakura
    18.5. Kusikiliza na Kuzungumza
    Kazi ya 10:
    Zungumzia umuhimu wa kuwa na kitambulisho cha taifa na hasara za 
    kutokuwa nacho.
    18.6. Kuandika
    Kazi ya 11:
    Andika umuhimu wa vitambulisho vya kitaifa. Kwa kutumia maneno 
    yasiyopungua 100

    Tathmini ya mada

    Jibu maswali yafuatayo:
    1. Jamhuri ya Rwanda inaongozwa na nani?
    2. Jaza nafasi zilizoachwa wazi kwa kutumia vivumishi vilivyotolewa mabanoni:
    a. Ukuta ………………..ulioanguka ulikuwa haukujengwa vizuri 
    (moja,mmoja,mbili).
    b. Habimana hakuvunja ufunguo……………….(ndogo, mdogo, wadogo).
    c. Nyuzi…………………..ni nyeusi na nyekundu, pia (zao, wangu, yake).
    3. Taja majina ya kiutawala yanayotumiwa kwa viongozi wa ngazi zifuatazo:
    a. Wilaya b. Kijiji c. Tarafa
    4. Andika aina tano za vitambulisho vya kitaifa.
    5. Ni nini kinachowanufaisha viongozi wakati wa kusherehekea sikukuu za kitaifa?
    6. Taja mifano minne ya umuhimu wa vitambulisho kwa jamii ya Wanyarwanda.















    MADA YA 3 MSAMIATI KATIKA MAZINGIRA YA HOSPITALIMADA YA 5 KISWAHILI KATIKA SHUGHULI ZA KIBIASHARA