• MADA YA 2 MSAMIATI KUHUSU MAZINGIRA YA NYUMBANI

    Uwezo mahususi wa mada: Kuzungumza Kiswahili kwa ufasaha na 
    kuandika matini fupifupi kwa kutumia msamiati unaofaa katika mazingira ya 
    nyumbani.
    Malengo ya ujifunzaji:
    • Kutumia msamiati uhusuo mazingira ya nyumbani, mifugo na vifaa vya nyumbani,
    • Kuainisha watu wa nyumbani na uhusiano wa familia,
    • Kutumia majina ya ngeli ya LI- YA na vivumishi kwa ufasaha.
    Kidokezo
    1. Taja watu wote wanawopatikana nyumbani kwenu.
    2. Taja sehemu kuu za nyumba.
    3. Orodhesha vifaa na mifugo wanawopatikana nyumbani.
    SOMO LA 5: MAZINGIRA YA NYUMBANI
    ttt
    Kazi ya 1:
    Tazama mchoro hapo juu kisha jibu maswali yanayofuata: 
    a. Unaona nini kwenye picha hii? Eleza. 
    b. Kuna uhusiano gani kati ya mchoro huo na kichwa cha habari cha 
    hapa chini? 
    5.1. Kusoma na ufahamu: Makao ya Gakuba
    ccc
    Mimi na rafiki yangu Rurangwa tunazoea kutembea baada ya masomo ya 
    jioni. Siku moja tulipata gari na kuelekea kijijini.Tulipofika kijiji ambapo mzee 
    Gakuba anaishi tuliona nyumba yake na familia yake. Mzee Gakuba, mke 
    wake na watoto wao wawili walikuwa wanasimama mbele ya nyumba yao 
    katika bustani.Walikuwa wakizungumza.

     Tulipigwa na bumbuazi kwa sababu kabla ya kuenda likizoni hapo palikuwa 
    na nyumba ya msonge. Mapendekezo ya serikali ya Rwanda ni kuishi katika 
    nyumba za kisasa. Nyumba hii ina sehemu kuu zifuatazo: sebule,vyumba 
    vya kulala, chumba cha wageni, chumba cha vyombo, na jikoni. Nyumba hii 
    inajengwa kwa mchanga, saruji, vyuma, nondo, milango, madirisha, mawe, 
    matofali na mabati. Vifaa vyote hivi vinapatikana nchini Rwanda. Kwa kujenga 
    nyumba hii kuna: msingi, kuta, zege, paa, madirisha, milango, sakafu, dari, 
    bomba na kadhalika. Nyumba hii ina bustani na miti ya aina tofauti kama vile 
    mti wa machungwa na mti wa maembe. Tulitazama nyumba hiyo kwa makini 

    na kujiuliza mengi kuhusu mabadiliko ya muda mfupi.

    Tulichunguza gharama za ujenzi wa nyumba yake! Na kujiuliza Je, gharama 
    hizi zimetoka wapi? Gakuba na bibi yake, kwa ushirikiano wao walitumia 
    fedha za mkopo kutoka benki. Gharama za nyumba ni thamani ambayo 
    unapaswa kuilipa ili uweze kuipata nyumba hiyo unayoitaka! Sasa thamani 
    unaweza kuilipa kwa njia ya pesa, nguvu ya kazi yako, nguvu ya akili na 
    pesa. Ina maana kwamba bila kulipa gharama stahiki huwezi kupata thamani 
    ya nyumba ile unayoitaka. Gharama hizi unaweza kuwalipa watu wengine 
    wanaokufanyia kazi au wanaokuuzia bidhaa, lakini pia unaweza kuzilipa 
    wewe mwenyewe kama muda na nguvu zako. Bila kulipa gharama stahiki 
    huwezi kupata nyumba hiyo.

    Mara moja, Rurangwa alianza kuniuliza: “ je, unaona tofauti kati ya nyumba 
    za jadi na nyumba za kisasa?” Jibu langu lilikuwa hivi: “ kwanza ni vibaya 
    kwa maisha ya mtu anayeishi katika nyumba za msonge kwa sababu usafi 
    wa nyumba hizi si kazi rahisi. Nyingi zinajengwa kwa majani. Tena ni hatari 
    sana kuishi katika nyumba ya msonge: Nyumba hii inaweza kuangukia watu, 
    inaweza kuungua kwa sababu kunatumiwa majani kwa ujenzi wa nyumba 
    hii, na kadhalika. Tunahifadhi mazingira wakati tunapojenga nyumba 
    za kisasa kuliko ujenzi wa nyumba za jadi. Je, Rurangwa, unafahamu 
    umuhimu wa kuhifadhi mazingira wakati tunapojenga nyumba?” Rurangwa 
    anatoa jibu: “Hatuwezi kuorodhesha umuhimu wa mazingira kwa sababu 
    bila mazingira viumbe vyote haviwezi kuishi. Kuna mashirika mengi nchini 
    Rwanda yanayotetea uhifadhi wa mazingira. Bila mazingira hakuna maisha. 
    Binadamu na wanyama hupumua hewa nzuri kutoka kwenye mazingira. 
    Tunapata mvua kwa sababu mazingira yanahifadhiwa na kadhalika.” 

    Tulipomaliza matembezi yetu, tuliamua kuelezea wazazi wetu umuhimu wa 
    kuishi katika nyumba nzuri kwa kutumia vifaa ambavyo vinapatikana nchini 
    mwetu na kutumia fedha kutoka benki kwa njia ya mkopo. Na sisi kama 
    wanafunzi tutaunda klabu zitakazofundisha watu umuhimu wa kuishi mahali 

    pazuri na kuhifadhi mazingira.

    Kazi ya 2 :
    Maswali ya ufahamu 

    1. Taja majina ya watu wote wanaotajwa katika kifungu hiki.
    2. Familia ya Gakuba ina watu wangapi? Orodhesha watu hao.
    3. Kwa kujenga nyumba yao, walitumia vifaa gani? Kutoka wapi?
    4. Nyumba hii ilijengwa na nani? Toa maelezo.
    5. Je, Mtu mwenye uwezo mdogo wa kiuchumi anaweza kuishi katika 
    nyumba ya kisasa? Eleza.
    6. Kwa sababu gani tunatakiwa kuheshimu mazingira wakati 
    tunapojenga nyumba?
    7. Kama mwanafunzi wa mwaka wa kwanza, msaada wako ni upi 
    kwa kuhifadhi mazingira unamoishi?

    5.2. Matumizi ya msamiati 

    Kazi ya 3:
    Tumia maneno yafuatayo katika sentensi zako ukizingatia namna 
    yalivyotumiwa katika kifungu cha habari ulichosoma 

    1. Busitani
    2. Bumbuazi
    3. Mkopo 
    4. Kuhifadhi 
    5. Shirika
    6. Kupumua
    7. Kutetea
    8. Klabu

    Kazi ya 4:

    Oanisha maneno yaliyomo katika sehemu A na yale yaliyomo katika 

    sehemu B.

    ff

    5.3. Sarufi: Matumizi ya ngeli ya LI-YA.

    Kazi ya 5:

    Chunguza sentensi zifuatazo na kuandika viambishi nafsi 
    vinavyopatikana katika vitenzi

    1. Kundi la wanamuziki liliwatumbuiza watu jana. 
    2. Mashirika haya yaliundwa na vijana mbalimbali. 
    3. Koti hilo limeshonwa na mshonaji hodari. 
    4. Makabati yalitengenezwa na maseremala.

    5. Gari zuri lile lilitengenezwa nchini Rwanda

    Maelezo muhimu 

    • Vitenzi vilivyomo katika sentensi hapo juu, vinatumia viambishi nafsi LI-YA 
    • Matumizi ya viambishi hivi LI-YA yanategemea nomino zilizotumiwa katika sentensi hizo. 
    • Nomino hizo zikiwa katika umoja kitenzi huchukua LI; zikiwa katika wingi kitenzi huchukua YA. 
    • Nomino zilizopendekezwa katika umoja huchukua wingi wake kwa kuongeza ma- kwa jina hilo: 
    Mfano: 
    1. Kundi                   makundi 
    2. Shirika                mashirika 
    3. Jani                      majani 
    4. Gari                      magari 
    5. Darasa                 madarasa
    Tanbihi: Kuna majina ya ngeli hii yasiyokuwa na umoja. 
    Maji, mate, maziwa (ya kunywewa), mateso, mavi, manukato, mazishi, 
    matumizi, manufaa, masafa. Katika sentensi, majina ya ngeli hii hufuatwa 

    na kitenzi chenye kiambishi awali li- katika umoja na ya- katika wingi

    Mfano: 
    Umoja Wingi 
    1. Shirika liliundwa.                          Mashirika yaliundwa. 
    2. Koti lingesafishwa.                      Makoti yangesafishwa. 
    3. Chungwa liliangushwa.             Machungwa yaliangushwa.
    5.4. Matumizi ya lugha

    Kazi ya 6:
    Tunga sentensi sahihi kwa kutumia nomino hizi katika umuja na 
    wingi kisha ueleze kile ulichokigundua

     Umoja                                                                         Wingi 
    1. Kabati .......................................................... 
    2. Koti .............................................................. 
    3. Bega ............................................................ 
    4. Goti ............................................................. 
    5. Panga ......................................................... 
    6. Janga .......................................................... 
    7. Jangwa ....................................................... 
    8. Jina ............................................................. 
    9. Jibu ............................................................. 

    10. Jembe…………………………………………

    Kazi ya 7:
    Andika sentensi zifuatazo katika umoja au wingi. 
    1. Mimi nina lengo la kupambana na jangwa. 
    2. Wewe utaondoa jani kavu hilo. 
    3. Majani yalikauka. 
    4. Shavu linaniuma. 
    5. Kijana mrefu alibeba kasha kwenye bega. 
    6. Debe hilo linavuja kwa sababu limetoboka. 
    7. Watoto watano walilazwa hospitalini kwa sababu ya matatizo ya mapafu. 
    8. Madaftari yanapaswa kuhifadhiwa vizuri. 
    9. Tarumbeta lilitumiwa wakati wa burudani.

    10. Shirika la reli liliagiza garimoshi kubwa.

    5.5. Kusikiliza na kuzungumza
    Kazi ya 8:
    Simulia mbele ya darasa muhtasari wa kifungu “ Makao ya Gakuba.”
    5.6. Kuandika

    Kazi ya 9:
    Tunga kifungu cha mistari 12 kuhusu ujenzi wa nyumba ya wazazi 
    wako.

    SOMO LA 6: MSAMIATI KUHUSU WATU WANAOPATIKANA 
    NYUMBANI

    Kazi ya 1:

    Chunguza michoro hii kisha ujadili unachoona kwenye michoro hii.
    cc
    6.1. Kusoma na ufahamu: Watu wa nyumbani
    cc
    Familia ni jamaa ya watu wanaoishi pamoja yenye baba , mama na watoto. 
    Katika utamaduni wetu kama Wanyarwanda, watu hawa wana majukumu 
    tofauti katika familia.

    Baba pamoja na mama wana majukumu ya kutafuta maendeleo ya familia 
    yao. Baba kwa ushirikiano na mama wana wajibu wa kufanya juu chini ili 
    familia yao iweze kupiga hatua kimaendeleo na kujitegemea kikamilifu. 
    Kulinda usalama wa nyumbani ni mojawapo wa wajibu huo. Hapa mama na 
    baba ndio walinzi wa kwanza wa utaratibu nyumbani ili familia yao iwe na 
    amani kila wakati.

    Kuwalea watoto wao, wazazi wana majukumu makubwa sana kwa watoto 
    wao kama vile: kuwapenda, kuheshimu haki zote za mtoto na kukidhi mahitaji 
    yao yote kama vile kuwalisha, kuwasomesha, kuwalipia karo za shule na 
    kuwapeleka hospitalini wakati wanapoumwa, n.k. 

    Wazazi huwapa mawaidha mema na kuwafundisha mila na desturi za 
    Wanyarwanda kama vile: uzalendo, ushirikiano, kuheshimiana, n.k. Wazazi 
    pia huwasihi kuepukana na tabia za: ukatili, uongo, uovu, ulevi, uzembe, 
    kupiga marufuku itikadi ya mauaji ya kimbari, na mienendo yote isiyofaa. 
    Kwa upande wa watoto, nao wana majukumu ya kuwaheshimu wazazi wao, 
    kutimiza mipango ya wazazi kama ilivyopendekezwa na kutoa mchango 
    mwafaka wa maendeleo ya familia yao.

    Nyumbani, wageni wa aina yote hukaribishwa. Miongoni mwa wageni hao 
    ni kama babu, bibi, mjomba, shangazi, mpwa na shemeji. Wageni hawa 
    wanalakiwa vizuri.

    Kazi ya 2:

    Maswali ya ufahamu
    1. Kwa maoni yako, eleza maana ya familia.
    2. Kwa kawaida familia hujengwa namna gani?
    3. Katika utamaduni wetu kama Wanyarwanda, baba na mama 
    wanashirikiana vipi?
    4. Je, mchango wa watoto ni upi katika familia? 

    5. Eleza mila na desturi ambazo wazazi wanafundisha watoto wao.

    6.2. Msamiati kuhusu watu wa nyumbani
    Kazi ya 3:
    Baada ya kusoma kifungu cha habari, toa maana ya msamiati 
    unaofuata, kisha utunge sentensi zenye maana kamili kwa kutumia 
    msamiati huo.

    1. Majukumu
    2. Ushirikiano
    3. Usalama
    4. Uzalendo 

    5. Mienendo 

    Kazi ya 4:

    Oanisha maneno kutoka sehemu A na maana yake katika B

    xxx

    6.3. Sarufi: Matumizi ya vivumishi vya idadi katika ngeli ya 
    LI-YA

    Kazi ya 5:

    Chunguza sentensi zifuatazo, kisha ueleze muundo wa vivumishi 
    vilivyotumiwa

    1. Jibu moja limepatikana.
    2. Mawe sita yameanguka chini.
    3. Matunda saba yameiva.
    4. Madarasa tisa yanasafishwa.
    5. Makoti kumi yatashonwa.

    Maelezo muhimu 

    Katika matumizi ya ngeli ya li-ya na vivumishi vya idadi, idadi mbili ambayo 
    hugeuka -wili, tatu, nne, tano pamoja na nane huchukua kiambishi makatika wingi. Vivumishi hivyo huwa mawili, matatu, manne, matano na
    manane. 
    Kinyume na matumizi ya ngeli ya li-ya na vivumishi vya idadi tulivyoona 
    hapo juu, idadi, sita, saba, tisa na kumi havichukui kiambishi ma- katika 
    wingi. Vivumishi hivyo hubaki vile vilivyo yaani, sita, saba, tisa, na kumi. 
    Nomino za ngeli ya “li-ya” huweza kutumiwa na vivumishi vya idadi ya jumla 
    /isiyo kamili / isiyo dhahiri: 
    Kwa mfano
    Matendo mengi mazuri yamefanywa na watu hawa.

    Kazi ya 6:

    Andika sentensi zifuatazo kwa kutumia vivumishi vilivyomo ndani 
    ya mabano. 

    1. Mawe .................... yamewekwa kando ya barabara (tatu). 
    2. Madirisha ........................... yamefunguliwa (tano). 
    3. Meno ...................... yameng’oka (mbili). 
    4. Matunda ....................... yameiva (nane).
    5. Makundi ................................. ya wanafunzi yameshiriki vilivyo (nne). 
    6. Madarasa .............................. yamejengwa (tatu). 
    7. Taja mambo .............. yanayozingatiwa katika kazi ya fasihi (tatu). 

    8. Makoti ...................... yameuzwa na mfanyabiashara huyu (tano).

    Kazi ya 7:

    Chunguza vivumishi vya idadi isiyo dhahiri vya ngeli ya “li-ya” 
    vifuatavyo kisha utunge sentensi zenye vivumshi hivyo. 

    1. Machache 
    2. Mengi 
    3. Kadhaa 
    4. Tele 

    5. Kidogo

    6.4. Matumizi ya lugha

    Kazi ya 8:
    Kamilisha tungo zifuatazo kwa kutumia vivumishi vya idadi: toka 
    moja hadi arubaini (Andika kwa maneno) 

    1. Kanuni za Mungu ni ........................ 
    2. Mwaka una miezi ............................. 
    3. Ni rahisi kujua kwamba wiki moja ina siku ..................... 
    4. Watu wa zamani walipika kwa kuweka chungu juu ya mafiga 
    ........................... 
    5. Wanyarwanda huwapa majina watoto wao kwenye siku ya ..........
    ......................... 
    6. Nchi ya Rwanda ina majimbo/ mikoa................. na mji wa Kigali.
    7. Nchi yetu inapakana na nchi........................ 
    8. Dunia ina mabara............................ 
    9. Rwanda ina milima ya volkano.................. 
    10. Katika mchezo wa soka, timu moja huwa na wachezaji...................
    uwanjani. 
    11. Siku moja ina saa........................... 

    6.5. Kusikiliza na kuzungumza

    Kazi ya 9:
    Soma kifungu cha habari hapo juu “watu wa nyumbani” baadaye 
    utoe muhtasari kimazungumzo.
    Kazi ya 10:
    Kwa njia ya mazungumzo, zungumzia wanafunzi wenzako ushirikiano 
    uliopo baina ya watu wa familia yenu.
    6.6. Kuandika 
    Kazi ya 11:
    Buni, kwa kuandika, mazungumzo ya watu nyumbani wakishirikiana 
    katika kazi fulani unayoitaka.
    SOMO LA 7: UHUSIANO WA KIFAMILIA
    Kazi ya 1:
    Tazama mchoro huu. Unaona nini kwenye mchoro huu? 
    vvv


    gggfff
    Bi. Nyiranzage aliolewa na Bw. Rutebuka. Sasa, Bi Nyiranzage 
    anaitwa bibi Rutebuka. Wengine humwita Bi. Nyiranzage. Bwana 
    Rutebuka ni mume wa bibi Nyiranzage. Bibi Nyiranzage na 
    bwana Rutebuka, ni mke na mume. Bwana na bibi Rutebuka 
    walizaa watoto wawili tu. Kifunguamimba wao ni mwanamume. 
    Jina lake ni Matabaro. Mtoto wa pili ni mwanamke. Yeye anaitwa 
    Nyiratabaro. Kwa upande mwingine Rutabagisha ambaye ni jirani 
    yao amemuoa Nyiramavugo; hivyo wote huitana mume na mke. 
    Bw. Rutabagisha na Nyiramavugo nao walizaa watoto wawili 
    tu, mmoja wa kike anayeitwa Mukabutera ndiye aliyetangulia 
    kuzaliwa na mwingine wa kiume Butera alifuata baadaye. Wototo 
    wa familia hizi mbili husomea kwenye Chuo cha Ualimu cha 
    Gacuba II.
    Watoto wote ni wanafunzi wa shule za sekondari. Vifunguamimba 
    husoma katika mwaka wa tatu katika chuo cha Ualimu cha Gacuba II.

    Ilhali vifungamimba husoma katika mwaka wa pili. 

    Baada ya muda mfupi, majirani hawa walikata shauri ya 
    kushirikiana kimasomo. Vifunguamimba walitangulia kushirikiana 
    na kusaidiana kati yao na hata kuwasaidia wadogo wao kimasomo 
    na kuwahimiza kuwaiga. Walikuwa wakishika nafasi ya kwanza 
    kwa kila muhula wa masomo. Baada ya kuona matunda ya 
    kushirikiana kimasomo, wote waliamua kuwasaidia wanafunzi 
    wenzao waliokuwa wakishindwa shuleni wakifanya marudio nao. 
    Jambo hili lilishamiri sana na kujulikana shuleni kote. Ilitokea 
    Mkurugenzi wa shule akapata habari hii na kuwakabidhi zawadi 
    ya kusoma mwaka mzima bila kulipa ada ya shule. 

    Jambo hili liliwafurahisha wazazi na kuwapongeza watoto wao 
    kwa zawadi nono. Shuleni, walimu wote walikuwa wanatumia 
    mfano wao ili kuwahimiza wanafunzi wengine kuwaiga.

    Mwishowe, wanafunzi hawa walimaliza masomo yao na kuachia 
    shule yao makumbusho ya milele. Walianza maisha mapya 
    wakawa walimu mashuhuri. Baada ya miaka miwili, Matabaro na 
    Mukabutera walifunga ndoa na kuzaa mtoto anayeitwa Rubangura. 
    Punde si punde, Butera na Nyiratabaro walioana wakazaa mtoto 
    anayeitwa Rubaduka. Familia hizi ziliendelea kuishi pamoja na 
    kushirikiana katika shughuli zote za nyumbani.

    Kazi ya 2:
    Maswali ya ufahamu:
    1. Taja uhusiano uliopo baina ya Butera na Mukabutera.
    2. Bi. Nyiramavugo atamwitaje Mukabutera?
    3. Bw. Rutebuka atamwitaje Matabaro?
    4. Jaza mapengo kwa neno faafu:
    a. Bw. Rutebuka ni …………… wa Bi. Nyiranzage.
    b. Mukagatera ni ………….. yake Butera.
    c. Rutebuka ni ………….. yao Matabaro na Nyiratabaro.

    5. Nyiramavugo atamwitaje mke wa Butera?

    Kazi ya 3:
    Kamilisha sentensi zifuatazo kwa kutumia msamiati wa uhusiano wa 
    kifamilia unaofaa.

    1. Mama ya mama yangu anaitwa………………………. 
    2. Ndugu wa kike wa baba yangu anaitwa ……………….
    3. Baba ya mume wangu anaitwa …………………………
    4. Mtoto wa mtoto wangu anaitwa…………………………
    5. Baba ya baba yangu anaitwa ……………………………..
    6. Mtoto wa mjukuu wako anaitwa …………………………. 
    7. Mama ya mke wako anaitwa ……………………………..
    8. Mwanamke aliyeolewa na babako, na ambaye si mama yako wa 
    damu anaitwa …………………………………………………….
    9. Mtoto wa kwanza kuzaliwa anaitwa …………………………….
    10. Mtoto wa mwisho kuzaliwa anaitwa………………………… 
    Maelezo muhimu kuhusu uhusiano wa kifamilia
    • Mjomba: Mvulana aliyezaliwa na dada yako au kaka ya mama yako.
    • Shangazi: Msichana aliyezaliwa pamoja na baba yako au ndugu wa kike wa baba yako. 

    • Mpwa: Mtoto wa dada yako.

    • Binamu: Mtoto wa mjomba wako au wa shangazi yako. 
    • Shemeji: Ni ndugu zote wa mkeo au ndugu za kiume wa mumeo.
    • Wifi: Jina wanaloitana dada zako na mkeo. 
    • Mkaza mjomba: Mke wa mjomba wako. 
    • Mkaza mwana: Mke wa mtoto wako. 
    Mavyaa: Jina linalotumiwa katika kuitana baina ya mke na mama mkwe wake. 
    Kifunguamimba: Mtoto wa kwanza kuzaliwa. 
    • Kitindamimba:Mtoto wa mwisho kuzaliwa. 
    • Mapacha: Watoto wawili waliozaliwa siku moja kutokana na mimba moja. 
    • Baba wa kambo: Mwanaume aliyeoa mamako na ambaye si baba yako wa damu. 
    • Mama wa kambo: Mwanamke aliyeolewa na babako, na ambaye si mama yako wa damu. 
    • Kitukuu: Mtoto wa mjukuu. 
    • Kilembwe: Mtoto wa kitukuu. 
    Kilembwekeza/Kinying’inya: Mtoto wa kilembwe. 
    Kitojo: Mtoto wa kilembwekeza.
    7.2. Msamiati kuhusu uhusiano wa kifamilia
    Kazi ya 4:
    Eleza maneno yalopigiwa mistari katika sentensi hizi:
    1. Watoto wanaheshimu wazazi wao.
    2. Tunampokea nyanya yetu nyumbani.
    3. Kifunguamimba kutoka familia ya mjomba wetu anahifadhi mazingira.
    4. Baba wa kambo wa Juma anamsadia mtoto mwenzake mwenye matatizo ya kutembea.
    5. Binamu yenu anaunda shirika la kutetea watoto wenye matatizo.

    7.3. Sarufi: Matumizi ya vivumishi vya kuuliza katika ngeli ya LI-YA 

    Kazi ya 5:
    Chunguza sentensi zifuatazo kisha ueleze muundo wa vivumishi 
    vilivyotumiwa.

    1. Jengo lipi ni kubwa? 
    2. Mapapai yapi yameiva? 
    3. Tukupe magunia mangapi? 
    4. Mashirika gani yanasaidia wakulima? 
    5. Wewe unataka nikupe jembe lipi?
    Maelezo muhimu kuhusu vivumishi viulizi
    Vivumishi viulizi hutumika kuuliza swali kuhusu nomino. Vivumishi hivi 
    vinapotumiwa katika sentensi ni sharti sentensi hiyo ikamilishwe kwa alama 
    ya kiulizi. Vivumishi viulizi ni vitatutongueouti?, -ngapi? na -gani? Vivumishi viulizi 
    -ngapi? na -pi? huchukua viambishi vya ngeli lakini kiulizi “gani” hakichukui 
    kiambishi chochote cha ngeli.
    Kwa mfano: 
    1. Gari lipi linatembea? 
    2. Magari yapi yanatembea? 
    3. Je, nyumba yako ina madirisha mangapi? 
    4. Unapenda shirika gani? – 
    5. Unapenda mashirika gani?
    Kazi ya 6:
    Tumia vivumishi viulizi vilivyomo mabanoni ili kujaza sentensi 
    zifuatazo: 

    1. Jibu .............. limeishapatikana? (-pi) 
    2. Mawe ................. yamewekwa kando ya barabara? (-ngapi) 
    3. Madirisha .............. yamefunguliwa? (gani) 
    4. Meno ................ yameng’oka? (-pi) 
    5. Tunda ................ limeiva? (gani)

    Kazi ya 7:

    Andika sentensi zifuatazo katika umoja ama wingi. 
    1. Jengo lipi ni kubwa? 
    2. Mapapai yapi yameiva? 
    3. Tukupe magunia yapi? 
    4. Mashirika gani yanasaidia wakulima? 
    5. Wewe unataka nikupe jembe lipi?
    7.4. Matumizi ya lugha
    Kazi ya 8:
    Soma maelezo hapo juu kuhusu uhusiano wa kifamilia kisha umwambie 
    mwenzako hali halisi ya kila mtu katika familia yako binafsi.
    7.5. Kusikiliza na Kuzungumza
    Kazi ya 9:
    Baada ya kusoma maelezo kuhusu uhusiano wa kifamilia, zungumzia 
    darasa ukoo wako.
    7.6. Kuandika 
    Kazi ya 10:
    Tunga mazungumzo kuhusu 
     “ uhusiano wa kifamilia” ( angalau misitari 15)

    SOMO LA 8: VIFAA VYA NYUMBANI NA USAFI WAKE

    Kazi ya 1:

    Orodhesha vifaa mnavyotumia nyumbani kwenu mnapofanya usafi.

    8.1. Kusoma na ufahamu: Vifaa vya nyumbani na usafi wake 

    bb

    Usafi wa nyumbani na vifaa vyake ni njia ya kuendeleza afya kwa kuzuia 
    maradhi yanayotokana na athari za taka kwa binadamu. Athari hizo zinaweza 
    kuhusu miili yetu. 

    Usafi wa nyumbani ni jambo ambalo linafaa kutiliwa maanani na kila mtu, 
    kwani uchafu unachangia pakubwa kuharibu maisha ya binadamu. Jambo 
    la kushangaza ni kwamba watu wengi wanafikiri kuwa usafi unahusu miili na 
    mavazi tu, wakisahau kuwa usafi huhusu kila kitu kinachopatikana katika 
    mazingira wanamoishi.

    Tunapozungumzia usafi wa nyumbani, watu wengi huelewa shughuli 
    muhimu zinazostahili kufanywa katika kusafisha vyumba vya nyumbani na 
    kutengeneza bustani zinazozunguka nyumba hiyo. Lakini, ni lazima kujua 
    kwamba usafi huchunguzwa kupitia vifaa vya nyumbani vinavyotumiwa 
    kama vile: sahani, vikombe, vijiko, sufuria,vijiko, nguo, meza, kabati, 
    runinga, redio,na kadhalika. Tena inafaa kusafisha sehemu zote za nyumba 
    kama vile vyumba vya kula, sebule, jikoni, chooni, bila ya kusahau bustani.

    Kabla ya kufanya usafi wa vifaa na sehemu za nyumba, sisi wenyewe 
    tunaombwa kuwa na usafi ipasavyo. Kama vile: Kunawa mikono kwa maji 
    na sabuni hupunguza kwa kiasi kikubwa maambukizo ya ugonjwa wa 
    kuhara. Wazazi na walezi wengine wanapaswa kunawa mikono kwa sabuni 
    kila baada ya kumhudumia mtoto mchanga au mtoto mdogo aliyejisaidia, 
    kumpeleka mtoto msalani, kutoka msalani wao wenyewe, kabla ya kuandaa 
    chakula, kabla ya kulisha watoto wadogo na baada ya kuondoa takataka.
    Wazazi na walezi wengine wanapaswa kuwajengea watoto tabia ya kunawa 
    mikono kwa maji safi na sabuni kabla ya chakula na baada ya kutoka 
    msalani. Kinyesi cha wanyama na binadamu kisiruhusiwe kukaa ndani ya 
    nyumba, njiani, kwenye vyanzo vya maji na katika maeneo ya kuchezea 
    watoto. Matumizi ya vyoo pamoja na tabia ya usafi, hasa unawaji wa mikono 
    kwa sabuni ni mambo muhimu kwa afya ya jamii. Hutoa kinga kwa watoto 
    na kwa kaya kwa gharama nafuu pamoja na kuwapatia watoto haki yao ya 
    kuwa na afya njema na lishe bora.

    Tunaposafisha nyumba tunatumia maji, sabuni za kawaida, na sabuni za 
    majimaji au dawa za kuulia wadudu wenye kuambukiza watu magonjwa 
    mbalimbali.Tunawaonya watu wasitupe uchafu ovyoovyo. Taka ambazo 
    zinaweza kusababisha matatizo ya afya ni kinyesi cha binadamu na cha 
    wanyama, taka ngumu, maji machafu, taka za viwandani, na za kilimo, n.k. 
    Taka zote zinazotokana na vitu vyote vilivyotumiwa zinafaa kutupwa mahali 
    panapofaa kama vile jalalani au zikachomwa kupitia njia zinazokubaliwa. 
    Nyasi nazo zinazozunguka nyumba zetu zinafaa kufyekwa ili kuwafukuza 
    mbu wanaosambaza ugonjwa wa malaria.

    Maji yote ya kunywa na ya matumizi mengine yatoke kwenye vyanzo salama 
    na yachemshwe baadaye au yanyunyiziwe dawa ya kuulia vijidudu. Vyombo 
    vya kuwekea na kuhifadhia maji vitunzwe vizuri ndani na nje na kufunikwa ili 
    kuepukana na uchafu wa maji. Ni lazima iwepo mikakati rahisi ya kusafisha 
    maji yawe safi nyumbani kama vile kuyachemsha, kunyunyizia dawa ya maji 
    (klorini) ili kuua vijidudu. Vyakula vibichi au mabaki ya vyakula vilivyopikwa 
    yanaweza kuwa hatari. Vyakula vibichi visafishwe kwa maji safi kabla ya 
    kupikwa. Chakula kilichopikwa kiliwe kikiwa moto na kiporo kipashwe moto 
    vizuri kabla ya kuliwa. Chakula, vyombo na eneo la kutayarishia chakula 
    halina budi kuwa safi na mbali na wanyama.

    Chakula kihifadhiwe kwenye vyombo vilivyofunikwa. 

    Upungufu wa usafi wa mazingira ni sababu kuu ya maradhi kote duniani. 
    Uboreshaji wa mazingira una manufaa makubwa kwa afya ya watu katika 
    kaya na katika jamii.

    Kazi ya 2:
     Maswali ya ufahamu 
    1. Ni sehemu zipi za nyumba ambazo huhitaji usafi?
    2. Taja vifaa vya nyumbani vilivyotajwa katika kifungu hiki.
    3. Kwa sababu gani watoto wanapaswa kuepukana na uchafu?
    4. Tunatumia nini katika kufanya usafi wa nyumbani?
    5. Wazazi au walezi wengine wanafundisha watoto wao nini kuhusu 
    usafi?
    6. Ni umuhimu gani wa kuwa na maji safi?
    7. Ni dosari zipi za upungufu wa usafi kwa binadamu?
    8.2. Msamiati
    Kazi ya 3:
     Tunga sentensi sahihi kwa kutumia maneno yafuatayo:
    1. Athari
    2. Maanani
    3. Kuhara 
    4. Kinga
    5. Takataka
    6. Kaya
    Kazi ya 4:
    Baada ya kusoma kifungu cha habari hapo juu, kamilisha sentensi 
    zifuatazo kwa kutumia maneno yafuatayo: runinga, redio, kijiko, 
    sufuria, meza, malaria, usafi, tabia, sabuni, linafaa, vifaa.
    1. Mama anapika chakula ndani ya……………….
    2. Tunaposoma kiswahili nyumbani tunaandikia kwenye………..
    3. Nyanya yangu anatumia………….. wakati mimi ninatumia uma.
    4. Tunasikiliza habari za mpira kwenye………………
    5. Wanafunzi hupenda kutazama filamu kwenye…………
    6. Usafi nyumbani ni jambo ambalo ………..kutiliwa maanani.
    7. Watu wengi wanafikiri kuwa ……..unahusu miili na mavazi tu. 
    8. Usafi nyumbani huonekana kupitia ………. vinavyotumiwa nyumbani.
    9. Kunawa mikono kwa maji na …………hupunguza kwa kiasi kikubwa 
    magonjwa.
    10. Wazazi na walezi wengine wanapaswa kuwazoeza watoto ……….
    ya kunawa mikono kwa maji safi.
    11. Nyasi nazo zinazozunguka nyumba zetu zinafaa kukatwa ili 

    kuwafukuza mbu wanaosababisha ugonjwa wa…………..

    8.3. Sarufi: Nomino za ngeli ya LI-YA na vivumishi vya 

    kumiliki 
    Kazi ya 5:
    Chunguza mifano ya sentensi hapa chini, kisha ueleze aina za 
    maneno yaliyopigiwa mstari. 

    1. Koti langu limechafuka.
    2. Shirika lako linajulikana sana.
    3. Gari lake ni la kifahari. 
    4. Jumba letu linapendeza
    Maelezo muhimu kuhusu matumizi ya nomino za ngeli ya LI-Ya na 
    vivumishi vya kumiliki
    Vivumishi vya kumiliki ni -angu, -ako, -ake, -etu, -enu na -ao. Vivumishi 
    hivi katika ngeli ya Li-Ya huchukua kiambishi konsonanti l- katika umoja na 
    y- katika wingi. 
    Kazi ya 6:
    Andika wingi wa sentensi za hapa chini.
    Umoja                                                                                Wingi 
    1. Jembe langu limepotea. ------------------------------------------- 
    2. Janga kubwa limesababisha maafa. ----------------------------------
    3. Jaribio la leo limesahihishwa. ------------------------------------------- 
    4. Jeshi lao lina askari wengi. ------------------------------------------- 
    5. Jeraha lake lina uchafu sana. ------------------------------------------- 
    6. Jambo hili liliwafurahisha wengi. ----------------------------------------
    7. Jicho lake linaona mbali sana. ------------------------------------------
    8. Jiwe langu lina thamani kubwa. -----------------------------------------
    9. Jino lako limeng’oka? ------------------------------------------- 
    10. Jiko langu limeharibika. -------------------------------------------
    8.4. Matumizi ya lugha
    Kazi ya 7:
    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili jadilini kuhusu “Umuhimu 
    wa usafi na madhara ya kutokuwa na usafi.”
    Kazi ya 8:
    Eleza umuhimu wa vifaa hivi vya usafi:
    1. Bafu 
    2. Sabuni
    3. Deki 
    4. Ufagio 
    5. Taulo 
    8.5. Kusikiliza na Kuzungumza
    Kazi ya 9:
    Mwambie mwenzako namna mnavyofanya usafi nyumbani kwenu 
    na usafi wa vifaa vya nyumbani.
    8.6. Kuandika
    Kazi ya 10:
    Tunga kifungu cha habari kwa kutumia kichwa kifuatacho (maneno 
    yasiyopungua mia moja): “Uchafu ni asili ya maradhi mengi.”

    SOMO LA 9: MSAMIATI KUHUSU MIFUGO

    gg

    Kazi ya 1:
    Jiunge na mwanafunzi mwenzako. Kumbushaneni majina ya mifugo 

    mbalimbali mnayoyajua.

    9.1. Kusoma na ufahamu: Kazi nzuri ya ufugaji.

    cc

    Huyu ni Ikirezi. Ikirezi ni mfugaji wa nyuki. Ikirezi anarina asali. Baada ya 
    kurina, yeye husafisha asali yake na kuiuza. Asali hiyo hutumiwa kama 

    chakula au hutengenezewa dawa.vv

    vvvv

    Huyu ni Ituze. Ituze anakama ng’ombe. Kabla ya kukama, aliosha chuchu 
    kwa maji vuguvugu na kuzikausha kwa kitambaa safi. Anatumia mkebe safi 

    kuwekea maziwa. Ituze huwapandisha madume kwa mitamba au mpira.

    cc

    Hili ni josho. Ng’ombe hawa wanaogeshwa kwa dawa ndani ya josho. 
    Wafugaji huosha mifugo katika josho ili kuwakinga dhidi ya kupe. Dawa 

    huua viroboto wanaoishi kwenye ngozi za mifugo.

    cc

    Hawa ni Mudenge na Gatera. Mudenge anawalisha kuku kwa mahindi. Pia, 
    huwapa kuku mtama, ugali, wadudu na vyakula vinavyopatikana kwa urahisi. 
    Wakati mwingine, yeye huwapa kuku chakula maalumu kilichotengenezewa 
    katika viwanda. Mudenge anawafuga kuku wa mayai na wa nyama. Yeye 
    huuza baadhi ya mayai ili kujipatia riziki. Mudenge, pia, huwaatamisha 
    baadhi ya kuku wake ili apate vifaranga wa kuuza na kufuga. 

    Gatera, naye, anawalisha ng’ombe kwa nyasi. Gatera anawafuga ng’ombe 
    wake ndani kwa ndani. Anawapa lishe, maji na dawa humo humo zizini. 
    Gatera hukata pembe za ng’ombe wake. Ng’ombe hukatwa pembe ili 

    kumzuia kumdhuru mtu au kuharibu vitu.

    bb

    Huyu ni Kaliza. Kaliza anapenda kuchunga farasi. Anawachunga farasi 
    penye maji safi na nyasi nyingi. Kulisha mifugo ni shughuli muhimu ya 
    ufugaji. Mifugo wanapolishwa vizuri hukua kwa haraka, huwa na afya nzuri 

    na hutupatia mapato mazuri.

    vvv

    Kaliza anafagia zizi la ng’ombe. Mfugaji bora husafisha makao ya mifugo na 
    vyombo vyao vya kulia, kunywea na kulalia. Mifugo wanaolala katika mahali 

    safi na kulia katika vyombo safi huwa na afya njema.

    fff

    Daktari wa mifugo anamtibu kuku kwa kumdunga sindano. Kutibu mifugo 
    ni muhimu kwa mfugaji. Ni vizuri kutambua dalili ya ugonjwa ili watibiwe 
    mapema.
    Kazi ya 2:
    Maswali ya ufahamu
    1. Andika majina yote ya mifugo yaliyotajwa hapo juu.
    2. Asali ina umuhimu gani kwa maisha ya binadamu?
    3. Kwa sababu gani tunakata sufu ya kondoo?
    4. Kabla ya kukama ng’ombe, tunaombwa kufanya nini kwanza?
    5. Chagua mifugo watano katika vifungu vya habari hapo juu kisha 
    utaje umuhimu wao kwa binadamu.
    6. Kwa maoni yako, ufugaji unaleta matunda gani kwa maendeleo 
    ya nchi?
    9.2. Msamiati kuhusu mifugo 
    Kazi ya 3:
    Baada ya kusoma kifungu cha habari hiki, toa maana ya msamiati 
    unaofuata:

    • kurina 
    • kukata sufu 
    • kukama 
    • kupandisha madume kwa mtamba 
    • kufuga ng’ombe ndani kwa ndani 
    • kuwapeleka ng’ombe katika josho 
    • kuatamisha kuku 
    • kuchunga 

    • kukata pembe

    bbb

    9.3. Sarufi: Ngeli ya LI –YA na Vivumishi vya kuonyesha. 
    Kazi ya 5:

    Tazama sentensi zifuatazo na kujadili mabadiliko ya kisarufi yanayojitokeza.

    vvv

    Maelezo muhimu 
    Vivumshi vya kuonyesha hili, hilo, lile hufuata nomino katika umoja. 

    Vivumishi vya kuonyesha haya, hayo, yale hufuata nomino katika wingi. 

    Kazi ya 6:
    Chagua neno sahihi katika mabano na kujaza pengo.
    1. Debe ………….. lilitoboka (hii, haya, hili, hiyi). 
    2. Jambazi ……….liliadhibiwa (yule, hii, lile, hiyo). 
    3. Tafadhali kunja majamvi………..(ayo, hizo, hayo, halo). 
    4. Anakuomba umnunulie machungwa ………….(hizo, hayo, yayo). 
    5. Jahazi …….ni kubwa (lili, hile, jile, lile). 

    Kazi ya 7:
    Sahihisha sentensi zifuatazo: 
    1. Kabati kale kalivunjwa na wezi. 
    2. Maji haya alimwagwa ovyo sakafuni. 
    3. Alipotaka kujenga nyumba alitafuta majiwe makubwa. 
    4. Mafuta haya haamwagwi ziwani kwa sababu anaweza kuua samaki. 

    5. Maboga haya yana manufaa nyingi kwa mwili wako. 

    9.4. Matumizi ya lugha 
    Kazi ya 8:

    Husisha majina haya na mifugo wanaopatikana hapo chini: mbuzi, 

    mbwa, kuku, paka, na sungura.

    dd

    9.5. Kusikiliza na Kuzungumza: Majadiliano
    Kazi ya 9:
    Zungumzia wanafunzi jinsi mnavyofanya ufugaji wengine namna 
    gani nyumbani kwenu au kwa babu yako mnavyofanya ufugaji.
    9.6. Kuandika 
    Kazi ya 10:

    Tunga kifungu kifupi cha maneno yasiyozidi 100 kuhusu “Umuhimu 
    wa ufugaji nchini Rwanda.”

    Tathmini ya mada
    1. Tumia maneno yafuatayo ya ngeli ya LI-YA na vivumishi vya 
    kumiliki au vya kuonyesha katika sentensi sahihi katika 

    umoja. 
    a. Azimio
    b. Ini
    c. Jiko
    d. Ua
    e. Shamba
    2. Tumia sentensi za hapo juu katika wingi.
    3. Jaza sentensi zifuatazo kwa kutumia maneno: baba, wifi, 
    mama, shangazi, mjomba, mjukuu, binamu, mpwa, mapacha, 
    baba wa kambo. 
    a. Mke wa baba yako ni ……………………………….. yako.
    b. Mume wa mama yako utamuita……………………… yako.
    c. Mtoto wa mjomba au shangazi yako ni……………..
    d. Mtoto wa mtoto wako utamuita…………..
    e. Bwana ya mama yako ambaye si baba yako utamuita……..
    f. Dada ya baba yako utamuita……………………………….
    g. Kaka ya mama yako utamuita………………………………..
    h. Mke wa ndugu yako utamuita…………………………….
    i. Watoto wawili waliozaliwa siku moja na mama mmoja 
    tutawaita……..
    j. Mtoto wa dada yako utamuita……….

    4. Andika umuhimu wa vifaa vya nyumbani vifuatavyo:

    vv

    5. Tunga insha ndogo ya maneno yasiyozidi 100 kuhusu “Umuhimu 

    wa kuishi katika nyumba ya kisiasa kwa maisha ya binadamu”



    MADA YA 1 MATUMIZI YA KISWAHILI SHULENIMADA YA 3 MSAMIATI KATIKA MAZINGIRA YA HOSPITALI