• MADA YA 3 UTUNGAJI WA INSHA

    • Malengo ya Ujifunzaji
    -- Kueleza maana ya insha na aina zake,
    -- Kubainisha mbinu au taratibu za kutunga insha,
    -- Kutaja aina za insha,
    -- Kubainisha sifa za insha ya masimulizi na ya kubuni,
    -- Kuchunguza sifa za sehemu kuu za insha,
    -- Kupanga mawazo kwa mfuatano mzuri,
    -- Kutumia kwa ufasaha alama za vituo kulingana na kanuni za matumizi kwa
    kila alama,
    -- Kutunga aina mbalimbali za insha,
    -- Kutoa maana ya mnyambuliko na mnyumbuliko,
    -- Kueleza tofauti iliyopo kati ya mnyambuliko na mnyumbuliko wa maneno,

    -- Kunyambua na kunyumbua maneno ya Kiswahili.

    SOMO LA 5: MAANA YA INSHA
    5.1. Kusoma na Ufahamu: Asiyesikia la Mkuu Huvunjika
    Guu

    Soma kifungu kifuatacho, kisha ujibu maswali yaliyotolewa hapo chini
    Kanuma ni kijana ambaye alikuwa na tabia ya uvivu hasahasa darasani. Kila wakati
    mwalimu alikuwa akimuadhibu kwa vuruguvurugu na kuwa na tabia ya kusinzia
    darasani. Isitoshe, Kanuma hakuandika maandishi darasani na kila mwalimu
    alipokuwa akiacha kazi za nyumbani za kufanya alikuta Kanuma hajaanza wala
    kuandika maswali. Wakati wa mitihani na majaribio, Kanuma alikuwa na tabia
    ya kunakili na kumuuliza aliyekuwa akikaa karibu naye. Mara nyingine alikuwa
    akileta vikaratasi alivyotumia kwa kuandika majibu na alikuwa akivificha dawatini
    ili vimsaidie kunakili.

    Wazazi wake walijaribu kumfunza tabia ya kuwa na bidii kwani siku zote bidii
    huzaa matunda. Walipenda kumuonya ili aweze kuweka njia za kuepukana na
    tabia hizo mbaya za kotopenda kufanya kazi lakini yeye hakusikia. Wazazi wake
    walijaribu kushirikiana na walimu wake kumfanya awe mtu mwenye kujitegemea
    katika siku za baadaye kwa kumpa mfano wa ndugu yake mdogo aliyempita na
    ambaye alikuwa chuoni wakati huo. Kilichokuwa kinaaibisha ni kuwa Kanuma
    alikuwa angali katika kidato cha pili shule za sekondari kwa miaka yake kumi na

    sita.

    Kanuma aliendelea na tabia zake mbaya na kutia pamba masikioni kwa kukataa
    mashauri ya wazazi wake. Wakati wa kufanya mtihani wa taifa alitaka kunakili.
    Alipokamatwa na walimu, polisi waliitwa na hivyo akakamatwa na kupelekwa
    katika kituo cha kurekebisha maadili. Walimu na wanafunzi wenzake walipomuona
    na kukumbuka maonyo aliyopewa kutoka kwa wazazi wake na hata kwa walimu;
    walisema kuwa, “asiyesikia la mkuu huvunjika guu.”

    Kanuma alipofika katika kituo cha kurekebishia maadili alikutana na vijana wengine
    waliofanya makosa mengi kama ubakaji, uvutaji wa bangi, utumiaji wa dawa za
    kulevya, wizi, mauaji na kadhalika. Hapo alipolinganisha kosa lake na makosa ya
    wenzake, alianza kujutia matendo aliyoyafanya. Kituoni alikutana na rafiki mmoja
    aliyeitwa Kimasa. Kila siku Kimasa alikuwa akimsimulia namna ambavyo alitiwa
    nguvuni kwa kosa la ubakaji. Wakati wote, Kimasa alikuwa akimwambia kuwa
    alionewa. Siku moja Kimasa alitaka kumlawiti Kanuma lakini Kanuma akakataa
    kwa sababu alikumbuka kuwa tendo hilo ni tendo la aibu. Alipowazia makosa ya
    Kimasa, alikumbuka kwamba mwalimu wake alimfundisha kwamba ulawiti ni njia
    nyofu ya kuambukizana magonjwa ya zinaa hasa UKIMWI. Hapo aliona kwamba
    ilikuwa lazima atengane na Kimasa.

    Mbali na kurekebishwa kimaadili, Kanuma alifundishwa mambo mengi sana
    kituoni. Kwanza alifundishwa kucharaza gitaa akageuka mwimbaji hodari. Na
    wakati wa usiku yeye pamoja na vijana wenzake walikuwa wakiwaliwaza wenzao
    kwa nyimbo.

    Alipotoka kituoni aliwakuta wanafunzi wenzake wakiwa na kazi nzuri; wengine
    walikuwa katika vyuo vikuu, akajuta. Wakati huu, mdogo wake alikuwa daktari.
    Mtegemea cha nduguye hufa maskini. Kanuma aliona kuwa ilikuwa lazima
    ajitegemee ili asije akawa mzigo kwa mdogo wake. Ndipo alianza kazi ya kuimba
    vilabuni, hotelini, harusini na katika hafla nyingine. Kuanzia wakati huo pesa
    zilianza kumiminika, akaajiri waimbaji wengine wakaunda bendi kubwa iliyovuma
    nchini mwao na kuvuka mipaka. Nyimbo nyingi za bendi hii zilikuwa zikiwahimiza
    vijana kuwa na mienendo mizuri. Bendi hii inasifika sana kwa kuwa imeundwa na

    vijana chipukizi waliokuwa na mienendo mibaya hapo kabla.

    • Alama zilizopigiwa mstari chini huitwa alama za vituo au alama za
    uakifishaji.

    Maelezo muhimu kuhusu matumizi ya alama za vituo/ uakifishaji
    Binadamu wanapozungumza, tunaweza kutambua jinsi wanavyopandisha
    sauti au kuishusha kwa ajili ya kutoa ujumbe fulani (kuuliza, kushangaa,
    kushtuka, n.k). Vilevile, wanapomaliza usemi wao mtu huweza kutambua
    kuwa usemi umefikia kikomo kwa kusikia sauti zao tu. Lakini katika
    uandishi, hakuna sauti. Badala ya sauti, zipo alama za vituo ambazo hutumiwa
    kuwakilisha sauti katika uandishi. Kutokana na alama hizo, tunatambua kama
    usemi umekwisha, kuulizwa swali, kushangaa na kadhalika. Pia, tunaposoma,
    tunajua wapi tunafaa kupumua kidogo, kushusha au kupandisha sauti na
    kadhalika.

    Alama hizi huitwa p i a viakifishi. Hivyo basi, viakifishi ni alama zinazotumiwa
    katika maandishi ili kuleta maana ikusudiwayo katika matini mbalimbali
    kama vile sentensi, aya, mtungo, barua, mialiko, matangazo, ilani na kadhalika.

    Mifano zaidi ya alama za vituo au viakifishi
    1. Nukta (.)
    i) Huwekwa mwishoni mwa sentensi.
    Mifano:
    -- Amechoka.
    -- Rais wetu hapendi wachokozi.
    ii) Hutumiwa kuonyesha ufupisho wa maneno.
    Mfano:

    -- S.L.P. ( Sanduku la Posta )
    iii) Hutumika kubainisha saa na dakika au tarehe.
    Mifano:
    -- 9.20: saa tisa na dakika ishirini
    -- 14.11.2019: tarehe kumi na nne, Novemba, mwaka wa elfu mbili na kumi

    na tisa.
    2. Kistari kifupi (-)
    i) Hutumiwa kuonyesha kuwa neno linakatwa kwa vile limefika ukingoni mwa
    mstari husika na bado linaendelea katika mstari unaofuatia.

    ii) Hutumiwa kuunga maneno yanayojenga neno moja. Mtindo huu aghalabu
    hujitokeza katika maneno yenye asili ya kigeni.
    Mfano:
    -- Idd-el-Fitri
    -- Dar-es-Salaam
    iv) Huweza kutumiwa badala ya koma.
    Mfano: Nyimbo za asili-hasa Rumba-zinapendwa na wengi.
    v) Hutumiwa kutenga silabi au mofimu zinazojenga neno.
    Mifano:
    u-ku-li-ma
    ha-zi-na
    ku-end-a
    ku-li-a
    Hutumiwa pamoja na nukta mbili kabla ya orodha.
    Mfano:Jumuiya ya Afrika Mashariki inaundwa na nchi hizi:
    -- Rwanda
    -- Tanzania
    -- Uganda
    -- Kenya

    -- Burundi

    3. Kistari kirefu(—)
    i) Hutumiwa wakati panapotokea badiliko la ghafla katika sentensi. Hapo
    kinachukua nafasi ya mkato au mabano.
    Mfano: Wewe—nina hakika—hutaki kutusaidia.
    i) Hutumiwa baada ya orodha tangulizi / kauli tangulizi, labda kuifafanua zaidi.
    Mfano: Kiingereza, Historia, Kinyarwanda—haya ndiyo masomo yanayowavutia
    wengi—hayamo katika ratiba.

    ii) Hutumiwa kabla ya maneno ambayo ni msisitizo wa dhana iliyotajwa.
    Mfano: Uharibifu wa mazingira—mnaona jinsi ulivyozidi—unatia wasiwasi.
    iii) Hutumiwa kuonyesha kauli isiyomalizika au kukatizwa kwa kauli.
    Mfano: Kalisa alisema, “nita —”
    iv) Hutumiwa badala ya neno mpaka au hadi.
    Mifano: Hesabu kutoka 20—50.
    Alianzia hapa—pale.

    4. Alama ya mshangao (!)
    i) Hutumiwa kuashiria mahangaiko ya moyo kama vile hasira, hofu,
    mshangao na kadhalika.
    Mifano:
    -- Lo! Mwanafunzi ameangusha kitabu cha mwalimu matopeni!
    -- Wamefungwa mabao kumi kwa nunge!

    5. Alama ya kuulizia/kiulizi (?)
    i) Hutumiwa mwishoni mwa sentensi kuonyesha kuwa sentensi hiyo ni swali.
    Mfano: Unaitwa nani?
    ii) Hutumiwa kuonyesha ukosefu wa uhakika kuhusu jambo kama vile mwaka.
    Mfano: Shule hii ya Kigali ilianzishwa 1992?

    6. Mabano/parandesi egg
    i) Hutumiwa kufunga maneno ya ziada katika sentensi.
    Mfano: Nyamata (makao makuu ya Bugesera) inakua kwa kasi.

    ii) Hutumiwa na mwandishi anapotaka kutoa ufafanuzi kwa lugha nyingine

    tofauti na ile anayoitumia.

    3. Kistari kirefu(—)

    i) Hutumiwa wakati panapotokea badiliko la ghafla katika sentensi. Hapo

    kinachukua nafasi ya mkato au mabano.

    Mfano: Wewe—nina hakika—hutaki kutusaidia.

    i) Hutumiwa baada ya orodha tangulizi / kauli tangulizi, labda kuifafanua zaidi.

    Mfano: Kiingereza, Historia, Kinyarwanda—haya ndiyo masomo yanayowavutia

    wengi—hayamo katika ratiba.

    ii) Hutumiwa kabla ya maneno ambayo ni msisitizo wa dhana iliyotajwa.

    Mfano: Uharibifu wa mazingira—mnaona jinsi ulivyozidi—unatia wasiwasi.

    iii) Hutumiwa kuonyesha kauli isiyomalizika au kukatizwa kwa kauli.

    Mfano: Kalisa alisema, “nita —”

    iv) Hutumiwa badala ya neno mpaka au hadi.

    Mifano: Hesabu kutoka 20—50.

    Alianzia hapa—pale.

    4. Alama ya mshangao (!)

    i) Hutumiwa kuashiria mahangaiko ya moyo kama vile hasira, hofu,

    mshangao na kadhalika.

    Mifano:

    -- Lo! Mwanafunzi ameangusha kitabu cha mwalimu matopeni!

    -- Wamefungwa mabao kumi kwa nunge!

    5. Alama ya kuulizia/kiulizi (?)

    i) Hutumiwa mwishoni mwa sentensi kuonyesha kuwa sentensi hiyo ni swali.

    Mfano: Unaitwa nani?

    ii) Hutumiwa kuonyesha ukosefu wa uhakika kuhusu jambo kama vile mwaka.

    Mfano: Shule hii ya Kigali ilianzishwa 1992?

    6. Mabano/parandesi egg

    i) Hutumiwa kufunga maneno ya ziada katika sentensi.

    Mfano: Nyamata (makao makuu ya Bugesera) inakua kwa kasi.

    ii) Hutumiwa na mwandishi anapotaka kutoa ufafanuzi kwa lugha nyingine

    tofauti na ile anayoitumia.

    Mfano: Wandishi (editors) waalikwa.

    iii) Hutumiwa kufungia herufi za kuorodhesha.

    Mifano:

    (a) huelimisha, (b) huburudisha, (c) huonya.

    7. Mkwaju (/)

    i) Hutumiwa kwa kuandika kumbukumbu namba za barua.

    Mifano: Kumb. Na 002/001/0012/KGL/002

    Kumb. Na 112/012/0099/NY/012

    Hutumiwa kwa kuandika tarehe.

    Mfano: Leo ni terehe 12/07/2019

    Hutumiwa badala ya neno « au », « ama ».

    Mifano: Mbweha/mbwamwitu ni mkali sana.

    Beberu / mbuzi dume yule ni mkongwe.

    Hutumiwa kwa kuandika akisami.

    Mifano:

    2/3

    3/4

    4/9

    8. Mtajo: (“ ” au ‘ ’)

    i) Hutumiwa kuonyesha maneno halisi ya mzungumzaji.

    Kwa mfano: “Nitafika kesho jioni,” alisema mdogo wake.

    ii) Hutumiwa kwa kuonyesha maneno yaliyonukuliwa katika kitabu au

    maandishi mengine.

    Mfano: Kama Kamusi ya Kiswahili Sanifu inasema, “boi ni mwanamume

    aliyeajiriwa kufanya kazi za nyumbani” (Uk30).

    i) Hutumiwa kwa kurejerea anwani za makala mbalimbali katika maelezo.

    Mfano: Kitabu cha “Darubini ya Sarufi” ni kizuri sana.

    ii) Hutumia kuonyesha neno geni katika lugha au lenye maana au kazi maalum.

    Mifano: Mimi sipendi “matoke”.

    Tulikwenda mjini tukaona ma “lorries”mengi.

    iii) Hutumiwa kuandika jina la gazeti.

    Mfano: Mnapaswa kusoma « Imvaho Nshya » ili mjue habari za ulimwengu.

    9. Mkato

    i) Hutumika kwa kutenganisha sehemu mbili za tungo

    Mfano: Mtoto anasoma Kiswahili, wazazi wanamtafutia karo.

    ii) Hutumika kwa kutenganisha maneno yanayofuatana.

    Mfano: Wao hufuga kuku, mbuzi, kondoo na ng’ombe.

    10. Ritifaa (’)

    i) Hutumiwa kwa kuonyesha sauti/ herufi fulani imeachwa.

    Mifano:

    ’likukanya (nilikukanya)

    ’kawa (ukawa)

    ’siniudhi (usiniudhi)

    ’19 (2019)

    ii) Hutumiwa kwa kuonyesha sauti za ving’ong’o.

    Mifano:

    Ng’ombe

    kung’aa

    Kung’oa

    11. Nukta za dukuduku (…)

    Hutumiwa:

    i) Badala ya neno na kadhalika.

    Mifano: Alinunua viazi vitamu, nyama, nyanya, …

    ii) Kuonyesha mambo yasiyotajika katika sentensi.

    Mfano: Niliamshwa alfajiri na mapema…

    iii) Kuonyesha kukatizwa kwa kauli/ usemi.

    Mfano: La …ki …kini una …unani … ni …penda.

    • Maana ya utungaji wa insha
    Utungaji ni neno linalotokana na kitenzi “kutunga”. Kitenzi hiki kinamaanisha
    “kutoa mawazo kutoka ubongoni na kuyakusanya, kisha kuyadhihirisha kwa
    maandishi, kwa kusimulia, kwa kuyaimba au kwa muziki. Kwa hiyo tunaweza
    kusema kuwa, utungaji ni utoaji wa mawazo binafsi kutoka akilini mwa mtu
    kuhusiana na mambo mbalimbali katika jamii, kisha kuyaweka wazi kwa njia ya
    mdomo au maandishi. Insha ni mtungo wa maneno kwa mtindo wa nathari juu

    ya jambo fulani.

    • Sehemu za insha

    Insha huwa na sehemu kuu tatu ambazo ni:

    • Utangulizi (Mwanzo)

    Katika sehemu hii inampasa mwandishi atoe maelezo mafupi na maana ya habari

    aliyopewa.

    • Kiini cha insha (Kati/insha yenyewe)

    Sehemu hii ni insha yenyewe. Katika sehemu hii inamlazimu mwandishi afafanue

    kwa mapana mada anayoishughulikia huku akitoa mifano hai inayoendana na

    hali halisi. Kwa kawaida, sehemu hii hueleza kwa ukamilifu kila hoja iliyodokezwa

    katika utangulizi.

    • Hitimisho (Mwisho)

    Hii ni sehemu ya mwisho. Katika sehemu hii inampasa mwandishi kutoa

    mapendekezo (maoni) ya msingi au kusisitiza kwa ufupi yale aliyoyaelezea katika

    habari yenyewe. Mwisho wa insha huonyesha uhusiano uliopo kati ya utangulizi

    na maelezo yaliyomo katika mwili.

    • Taratibu za kutunga insha

    Kwa kuweza kutunga insha vilivyo, huna budi kufuata taratibu zifuatazo:

    -- Kusoma kwa makini mada/kichwa/anwani uliyopewa zaidi ya mara moja, ili

    uielewe vizuri.

    -- Kufikiria mada/kichwa/anwani kwa muda.

    -- Kuandika mambo muhimu yatakayokuongoza katika kuiandika insha.

    -- Maelezo yote yatolewe kwa undani na kwa njia ya kuvutia.

    -- Kupanga mawazo katika mtiririko wenye mantiki.

    -- Kutumia msamiati mwafaka wa kutosha kwa kutegemea mada

    (kutorudiarudia maneno).

    -- Kutumia sentensi fupi.

    -- Kutumia vizuri alama za uakifishaji.

    -- Kutumia lugha safi na yenye adabu.

    -- Kuandika methali, misemo na nahau ambazo unadhania zinaweza kukufaa

    katika utungaji.

    • Aina za insha

    Insha ni za aina nyingi kulingana na namna zilivyoandikwa au kulingana na kusudi

    lake. Katika utungaji wa insha kuna insha za wasifu, insha za picha, insha za

    mdokezo, insha za maelezo, insha za masimulizi, insha za methali, insha za hoja

    na insha za kubuni.

    Jibu maswali haya

    1. Kwa maoni yako nini maana ya insha ?

    2. Kwa sababu gani katika utungaji wa insha ni lazima kuheshimu sehemu

    za insha ?

    3. Andika sifa kuu tano za insha.

    6.1. Kusoma na Ufahamu: Mafanikio ya Kudumu
    Soma kifungu hiki kisha ujibu maswali uliyopewa hapo chini

    Masengesho ni, kijana aliyezaliwa mwanapekee katika familia yake. Hakubahatika
    kulelewa na wazazi wake kwani walifariki angali mdogo kutokana na ugonjwa wa
    UKIMWI. Baada ya wazazi wake kufariki, alichukuliwa na kulelewa na shangazi
    yake. Wakati huo, alikuwa katika shule za sekondari. Alipomaliza masomo yake
    katika shule za sekondari, alipata cheti cha kuhitimu masomo hayo akiwa na
    alama nzuri. Jambo hili liliwafurahisha watu wengi wakiwemo walimu na majirani
    zake. Ndiyo maana ilikuwa tafrija ya kijiji kizima. Hii ni siku tuliposherehekea
    kupata tuzo kwa kijana hodari ambaye aliyamudu maisha yake kiasi cha kuigwa
    na vijana wengine.

    Wengi waliompongeza siku hiyo walimletea zawadi nyingi. Alikuwa mwanafunzi
    mwenye bidii tangu shule ya chekechea hadi kiwango alichofikia. Muda mfupi
    baadaye, alijiunga na vijana wenzake kufuata masomo ya muda mfupi yaliyokuwa

    yakitolewa kijijini hapo.

    Masomo hayo yaliwalenga vijana wote waliokuwa wamemaliza masomo yao ya
    shule za sekondari na yalilenga kuwawezesha kuandaa miradi midogo midogo
    ya kujiendeleza na jinsi ya kuifanikisha. Masomo hayo yaliwafurahisha vijana
    wengi na Masengesho aliyasoma kwa makini; jambo lililokuwa desturi yake.

    Masengesho alikuwa msichana mwenye mawazo na mtazamo imara wa maisha
    kiasi kwamba watu walishangaa kutokana na tabia na mienendo yake. Mafunzo
    yalifanyika kwa muda wa mwaka mzima akapewa cheti katika fani ya maandalizi
    na utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo. Mwezi mmoja uliofuata, Taasisi ya
    Maendeleo ya Rwanda ilihitaji kuajiri vijana waliokuwa wamemaliza masomo yao
    ili wasaidie katika kazi za ukalimani na uongozaji wa watalii kwenye vivutio vya
    utalii. Masengesho alipeleka ombi lake na baada ya muda mfupi akaitwa kwa
    mtihani na kuufaulu. Kazi ilipoanza, aliifanya kwa bidii kiasi kwamba watalii wengi
    walifurahia huduma yake, wakampenda kwa uwezo wake wa kuzungumza lugha
    tofauti na bidii aliyokuwa akionyesha kazini.

    Alifungua akaunti kwenye benki moja na kuanza kuhifadhi sehemu ya mshahara
    wake. Alipoona akaunti yake ilikuwa na pesa za kutosha, aliamua kuomba mkopo
    ili aweze kuzalisha mali katika shamba lake kubwa ambalo mpaka wakati huo
    lilikuwa halijatumiwa vizuri. Shamba hili lilikuwa kwenye mwinuko wa mlima na
    lilikuwa likiharibiwa na mmomonyoko wa ardhi. Kwa kupambana na tatizo hili,
    alitengeneza mifereji ya maji na kupanda miti mbalimbali karibu na shamba hilo.

    Aliandaa vizuri mradi wa kilimo na ufugaji, akajenga vibanda vya mifugo yake,
    akawaajiri baadhi ya vijana waliokuwa pamoja katika mafunzo ya muda ule mfupi,
    kila mmoja akapewa jukumu lake. Pamoja na kazi yake ya ukalimani, Masengesho
    alifuata vizuri mradi wake akanunua vifaa vilivyohitajika pamoja na gari lililokuwa
    likitumia umeme. Alinunua gari hili ili apunguze moshi unaochafua mazingira.

    Mwaka mmoja baadaye, alikuwa ameishapata mali nyingi na kuanza kujulikana
    nchini kote kwa uwezo wake wa kufanya mambo mengi kwa muda mfupi na kwa
    ukamilifu.

    Serikali ya Rwanda ilipotoa tuzo kwa watu waliochangia kubadilisha maisha
    ya watu wengine, Masengesho alikuwa miongoni mwa watu waliochangia
    kuyaboresha maisha ya majirani zao. Kila mtu katika kijiji chetu aliitikia mwaliko
    wake na wengi tulikuwa tunajivunia kuwa na kijana mwerevu kama yeye. Kwa
    sasa ameanza kuendelea na masomo yake katika Chuo kikuu cha Rwanda
    ambapo anatarajia kupata shahada yake ya kwanza katika uwanja wa Ukalimani.

    Masengesho amekuwa mfano mzuri kwa vijana wengine wengi ambao
    wanapoyakumbuka maisha yake, huyaamini yaliyosemwa na wahenga kwamba”
    Mchumia juani hulia kivulini” na “mvumilivu hula mbivu”. Wema kwa kila mtu,
    utulivu na upendo ni baadhi ya sifa zinazomtambulisha kijana huyu ambaye

    amewashangaza wengi wanaofahamu alipotoka.

    Maelezo muhimu kuhusu mnyambuliko wa maneno

    Katika mada ya kwanza tuliona kuwa mnyambuliko au uambishaji ni mbinu ya

    kuzalisha maneno mapya kutoka maneno mengine. Mbinu hii hufanyika kwa

    kuongeza kwenye sehemu fulani (viini, mizizi au mashina) za maneno hayo

    viambishi mbalimbali mwanzoni au mwishoni. Katika sarufi ya lugha ya Kiswahili

    kuna:

    -- Mnyambuliko wa vitenzi

    -- Mnyambuliko wa nomino

    -- Mnyambuliko wa vielezi

    • Mnyambuliko wa vitenzi

    Mnyambuliko wa vitenzi ni uundaji wa vitenzi kutoka maneno mengine. Tunaweza

    kupata :

    -- Vitenzi kutoka vitenzi

    -- Vitenzi kutoka majina

    -- Vitenzi kutoka vivumishi

    -- Vitenzi kutoka vielezi

    Vitenzi kutoka vitenzi

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kuongezea viambishi mbalimbali katika mzizi

    wa kitenzi. Viambishi hivi vinaweza kuja mwanzoni au mwishoni mwa mzizi huu.

    Mifano: Kucheza: wanacheza- mtachezea-ulichezwa-litachezeshwa

    Kupenda: wanapendana-unapendwa-zilipendwa-yanapendeza

    • Vitenzi kutoka majina

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kuongezea viambishi mbalimbali katika shina la

    jina. Viambishi hivi vinaweza kuja mwanzoni au mwishoni mwa shina hilo.

    Mifano: Haya: kutahayari-wametahayarishwa-tulitahayaria-vilitahayarika

    Dhuluma: kudhulumu-walidhulumiwa-hawakudhulumiwawatadhulumiana

    • Vitenzi kutoka vivumishi

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kuongezea viambishi mbalimbali vya shina la

    kivumishi. Viambishi hivi vinaweza kuja mwanzoni au mwishoni mwa shina hilo.

    Mifano: Laini: kulainisha-vililainishwa-mtalainisha-yamelainika

    Pana: kupanua-vilipanuka-mlipanua-yalipanuliwa-pamepanuliwa

    • Vitenzi kutoka vielezi

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kuongezea kielezi au sehemu ya kielezi viambishi

    mbalimbali. Viambishi hivi vinaweza kuja mwanzoni au mwishoni mwa mzizi huu.

    Mifano: Sawa: kusawazishwa-kumesawazishwa-watasawazishianahayakusawazishika

    Karibu: Kukaribiana-watakapokaribishwa-tulipokaribishwa-yanavyokaribiana

    • Mnyambuliko wa majina

    Mnyambuliko wa majina/nomino ni uzalishaji wa majina mapya kutoka maneno

    mengine. Tunaweza kupata :

    -- Majina kutoka majina mengine

    -- Majina kutoka vivumishi

    -- Majina kutoka vitenzi

    -- Majina kutoka vielezi

    • Majina kutoka majina

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kubadilisha ngeli za kawaida za majina. Jambo

    hili linaweza kufanyika kwa kutia jina katika umoja au wingi, kwa kulidunisha,

    kulikuza au kulitia katika dhana ya dhahania.

    Mifano:


    • Majina kutoka vivumishi
    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kupachika kiambishi ngeli mbele ya shina la

    kivumishi.

    Mifano: -embamba : wembamba

    -- rembo: urembo

    -- ovu: ovu, maovu, uovu

    -- hodari: uhodari

    • Majina kutoka vitenzi

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kutia viambishi ngeli vya majina mbele ya mzizi

    wa kitenzi na viambishi tamati (viambishi vya kauli, viishio) nyuma ya mzizi huo.

    Viishio vinavyotumiwa ni –a, -e, -o, -i, -u na -aji

    Mifano: - dunda: mdundo

    -- lima: mkulima-kilimo-kilimio

    -- pika: mpishi-upishi

    -- andika: mwandishi-wandikaji- uandishi

    • Majina kutoka vielezi

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kupachika kiambishi ngeli mbele ya kielezi.

    Mifano: Sawa: usawa

    Mbali: umbali

    Karibu: ukaribu

    • Mnyambuliko wa vielezi

    Mnyambuliko wa vielezi ni uzalishaji wa vielezi kutoka maneno mengine. Tunaweza

    kuwa na :

    -- Vielezi kutoka majina

    -- Vielezi kutoka vivumishi

    • Vielezi kutoka majina

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kupachika kiambishi ki- mbele ya shina la

    nomino. Vielezi hivi ni vya namna.

    Mifano: Mume: kiume (Ijapokuwa alipata shida alijikaza kiume.)

    Mke: kike (Kabarisa anapenda kuvaa nguo za kike.)

    Upuuzi: kipuuzi (Usitamke mambo ya kipuuzi mbele ya watu wazima.)

    Marekani:kimarekani (Vitabu hivi vilinunuliwa kwa dola hamsini za

    kimarekani)

    • Vielezi kutoka vivumishi

    Mnyambuliko huu hufanyika kwa kupachika viambishi ki- na vi- mbele ya shina la

    kivumishi. Vielezi hivi ni vya namna au vya kiasi.

    Mifano: - dog: kidogo- Kutokana na homa anatamka kidogo (namna).

    Mwaka huu tumepata mvua kidogo (kiasi).

    -- zuri: vizuri- Amefanya vizuri katika mtihani.

    -- vyake: kivyake - Kila mtu anaelewa mambo kivyake.

    -- gumu: vigumu – Kwa kuwa ana masikio mazito yeye anasikia vigumu.

    SOMO LA 7: INSHA ZA KUBUNI


    7.1. Kusoma na Ufahamu: Kioja katika Mbuga ya
    Mwangaza
    Soma kifungu kifuatacho, kisha ujibu maswali yaliyotolewa hapo chini
    Siku ya mazishi ya Mzee Ngedere ilikuwa siku tukufu kwa wanyamapori wote wa
    Mbuga ya Mwangaza. Waliamua asindikizwe kwa sherehe maalum kwa sababu
    mbili. Kwanza, alikuwa mpatanishi wao mwenye busara. Mizozo ilipokuwa ikizuka
    mbugani alikuwa akiitatua bila kupendelea upande wowote. Pili, Mzee Ngedere
    alikuwa muuguzi bingwa wa kienyeji aliyeheshimika sana.

    Baada ya kifo cha Mzee Ngedere, umoja wa Wanyama ulivunjika. Baadhi yao
    walikuwa wakipendekeza mganga huyu arithiwe na Bwana Chui na wengine

    wengi wakimpendekeza Bi Tembo. Siku hii ya mazishi, Mfalme Simba aliamua

    kulifumbia jicho jambo hili la urithi wa uganga ili Marehemu asisindikizwe kwa
    zogo na vurumai.

    Waombolezaji walimiminika kwa wingi: wafalme na raia kutoka mbuga jirani,
    viongozi wa kidini na raia wa Mbuga ya Mwangaza kwa ujumla. Wanyama walijaa
    uwanjani hata pasipatikane nafasi ya kuweka sindano. Kila raia wa Mwangaza
    alijiandaa kila iwezekanavyo kuifanikisha siku hiyo. Lakini wote walifanya hivi
    nyoyo zikisumbuka kwa majonzi ya kumpoteza mshauri na mganga wao.

    Kabla ya sala ya wafu kuanza, waombolezaji walijipanga kwa mstari mrefu
    na kumuaga mpatanishi na tabibu wao kitamaduni kwa kuimba nyimbo za
    kuomboleza na kubeba mikoba yake ya utabibu pamoja na mgwisho wake wa
    uungwana. Gunia lenye maiti lilibebwa kutoka nyumba ya Mzee Ngedere hadi
    kaburi lililokuwa karibu na kasri la Mfalme Simba.

    Baada ya msafara huo, mpanga ratiba, ambaye ni Binti Sungura alimkaribisha
    Kasisi Nyati kuongoza sala. Wasemaji wote waliopewa fursa walikariri sifa za
    marehemu. Kipindi cha sifa kilipomalizika, jua lilikuwa likiwaka sana. Kila kiumbe
    kilikuwa kikitokwa na jasho. Wakati wa kufundisha Neno la Bwana ulipofika,
    kasisi wa Mbuga ya Mwangaza, Mzee Nyati, alichukua fursa akamsifu Mungu na
    kuwaomba wanyama wamshukuru Mungu wao. Yeye alisimama, akivaa miwani
    sawasawa na kufungua jarida la karatasi. Baada ya kusafisha koo lake alianza
    kuzungumza. Alizungumza na kuzungumza hadi wanyama wengine waanze kuota
    mizizi kwa sababu ya kukaa na wengine kusimama kwa muda mrefu. Bwana Chui
    alimwamrisha Kasisi Nyati kumaliza maneno yake wakamzike Mzee Ngedere.

    Bwana Chui alisema haya huku akipanga kumrithi Mzee Ngedere kwa sababu
    alikuwa makamu wake. Aliposikia hayo, Bi Simba alilia kwa kwikwi huku
    akimwomba Mungu amrudishe mpatanishi wao kwa sababu Bwana Chui
    alikuwa akiogopwa na wanyama wengi kwa ukatili wake. Alikuwa hawapokei
    vizuri walipokuwa wakimpelekea malalamiko yao.

    Kimya kizito kilitawala kati ya wanyamapori. Kitambo, wingu jeusi lilipita na
    kuwatisha wote waliokuwa hapo. Kunguru moyo ulimdundadunda na kujitayarisha
    kukimbia akisema kuwa shetani kapita. Kusikia hayo Mfalme Simba alimshauri
    kutowatisha kwa kusema mambo ya kishenzi.

    Mara gunia lilianza kutikisika na kuonyesha dalili ya kuwa ndani mlikuwamo
    kiumbe hai. Kasisi Nyati alipoona hayo alianza kutokwa na jasho kubwa hadi mwili
    mzima ukalowa maji. Lo! Wanyama wengi walitimuka na kutawanyikia vichakani
    na porini. Kasisi Nyati naye hakuweza kuhimili kioja hicho. Bila ya kuvua joho lake
    naye alitimka mbio na kufuata wafuasi wake. Mfalme Simba na Bwana Chui
    walijizatiti na kubaki pale ili wajionee kilichokuwa kikijili hapo huku wakiwashauri

    wenzao kutokimbia.

    Baada ya muda mfupi walimwona Mzee Fuko, mke na watoto wake wawili
    wakijitokeza chini ya gunia wakidai kuja kumzika Mzee Ngedere. Bi Fuko
    alipotaka kujua sababu iliyowafanya wanyama kutimuka, alielezwa kwamba
    labda walidhani kwamba Mzee Ngedere amefufuka. Bada ya hapo, Bwana
    Chui alitumwa kuwarudisha wanyama kwa sababu kulikuwa hakuna jambo la
    kuwafanya wakimbie.

    Baada ya kupata taarifa, wanyama walirudi na kumzika mganga na mpatanishi
    wao mpendwa. Mazishi yalipomalizika, Bi Tembo alichaguliwa kuwa mpatanishi.
    Nafasi ya makamu akapewa Binti Sungura. Bwana Chui alipotaka kuzusha ghasia
    alionywa kuwa angefunguliwa mashtaka kwa kosa la uchochezi wa ghasia. Kwa
    kusikia hayo, aliomba msamaha, akaahidi kugeuka mzalendo mwema. Aliwaambia
    wafuasi wake kutimiza masharti ya Mfalme Simba. Tangu siku hiyo hali ya utulivu

    ilirudi. Upendo na amani ikatawala katika Mbuga ya Mwangaza.

    Maelezo muhimu kuhusu mnyumbuliko

    Soma maelezo yafuatayo kisha ujibu maswali ya hapo chini
    Mnyumbuliko wa kitenzi ni mbinu ya kurefusha kitenzi. Mbinu hii hufanyika kwa
    kuongezea mzizi wa kitenzi viambishi tamati. Kiambishi tamati ni mofimu yoyote
    inayokuja baada ya mzizi wa kitenzi. Viambishi tamati vinavyotumiwa katika
    mnyambuliko ni viambishi tamati vya kauli. Viambishi tamati vya kauli ni viambishi
    vinavyoongezea mzizi wa kitenzi maana mpya yenye kauli fulani. Kuna:

    • Kauli ya kutendea: -il-






    Maelezo Muhimu kuhusu Insha za Kubuni
    Insha za kubuni ni aina ya insha ambazo hutungwa kuhusu mawazo yanayozuliwa
    na ambayo si matukio ya kawaida.

    Kama insha nyingine, insha ya kubuni huwa na kichwa cha habari cha insha
    ambacho ni maneno machache, takribani matano, ambayo ndiyo jina la insha.

    Kichwa cha habari huandikwa juu, sehemu ya katikati kwenye ukurasa wa kwanza
    wa insha. Mara nyingi, huandikwa kwa herufi kubwa na hubeba wazo kuu la
    insha. Insha ya kubuni huwa na utangulizi ambao ni sehemu ya mwanzo yenye
    urefu usiozidi aya moja. Utangulizi hudondoa kwa ufupi kabisa kile kinachoelezwa
    kwenye insha.

    Kiini cha insha ya kubuni ni sehemu tunayoweza kusema kwamba ni insha
    yenyewe. Kwenye kiini ndipo ufafanuzi wote hutolewa. Ufafanuzi huu hupangwa
    katika aya moja au zaidi. Hapa ndipo mwandishi hubainisha mawazo yake,
    huthibitisha, hushawishi, huhimiza na hufafanua. Baada ya kiini, huja hitimisho,
    yaani sehemu ya mwisho wa insha ya kubuni ambayo haizidi aya moja. Katika
    sehemu hii, mwandishi anaweza kurejea kwa ufupi sana yale aliyozungumzia
    kwenye insha yake. Anaweza kuonyesha msimamo wake, anaweza kutoa

    mapendekezo, au kuwahimiza walengwa wake kuchukua hatua fulani.

    Insha za namna hii humhitaji mwandishi kujiweka kimawazo katika hali fulani ya
    kubuni na kutunga insha katika hali hiyo. Kwa hivyo, ili mwandishi afaulu katika
    uandishi wake, ni sharti awe na uwezo wa kubuni mawazo kwa undani na pia
    kuweza kuyaeleza mawazo hayo kwa njia ya kuaminika kwa wasomaji.

    Tanbihi: Kuwepo kwa insha za kubuni hakuondoi ukweli unaosema kwamba
    insha zote hutokana na ubunifu wa mwandishi. Hivi ni kwa sababu aina zote
    za insha huwa zinaandikwa kwa mawazo yanayobuniwa na akili ya mwandishi.

    Jibu maswli yafuatayo:
    1. Kifungu cha habari ulichosoma hapo juu kuhusu Kioja katika Mbuga ya
    Mwangaza ni aina gani ya insha? Kwa sababu gani?
    2. Ni jambo gani mwandishi wa insha ya kubuni anapaswa kuzingatia kabla
    ya kuandika?

    3. Ni mambo gani yanayojitokeza katika insha ya kubuni na insha nyingine?

    

    MADA YA 2 UTUNGAJI WA BARUA RASMIMADA YA HOTUBA 4 HOTUBA