• MADA YA 2 UTUNGAJI WA BARUA RASMI

    • Malengo ya ujifunzaji:
    -- Kueleza maana ya barua rasmi,
    -- Kutaja sehemu kuu za barua rasmi,
    -- Kubainisha mahali tofauti pa kutumia barua rasmi,
    -- Kuonyesha umuhimu wa barua rasmi,

    -- Kutambua nafasi ya kiwakilishi rejeshi -po- katika kitenzi.

    SOMO LA 3: MWONGOZO WA KUTUNGA BARUA
    RASMI/KIKAZI

    3.1. Kusoma na Ufahamu: Baruaya Kuomba Kazi


    Tovuti:Tovuti: www.gisagara.gov.rw

    Barua pepe: gisagaradistrict@minaloc.gov.rw

    Ndugu,

    KUH. OMBI LA KAZI YA KUFUNDISHA

    Napenda kutuma ombi langu la kazi ambayo nimeitaja kwenye kichwa cha habari

    cha hapo juu.

    Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka kumi na nane. Nimemaliza masomo yangu

    mwaka 2019 katika chuo cha Ualimu cha Save na kupewa cheti cha ualimu wa

    ufundishaji wa lugha ya Kiswahili katika shule za sekondari.

    Barua pepe: gisagaradistrict@minaloc.gov.rw
    Ndugu,

    KUH. OMBI LA KAZI YA KUFUNDISHA
    Napenda kutuma ombi langu la kazi ambayo nimeitaja kwenye kichwa cha habari
    cha hapo juu.
    Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka kumi na nane. Nimemaliza masomo yangu
    mwaka 2019 katika chuo cha Ualimu cha Save na kupewa cheti cha ualimu wa
    ufundishaji wa lugha ya Kiswahili katika shule za sekondari.
    Natuma ombi langu la kazi ya kufundisha kwako ili niwe mmoja kati ya wale
    watakaofikiriwa kupewa kazi ya kufundisha katika Wilaya ya Gisagara.
    Nyaraka zote zinazohitajika nimeziambatisha kwenye barua hii kama viambatisho.
    Ni matumaini yangu kuwa ombi langu litakubaliwa.

    Wako mtiifu,
    Uwamwiza

    UWAMWIZA Zawadi



    Maelezo muhimu kuhusu matumizi ya kiambishi –po-

    Kiambishi rejeshi –po- kinaweza kutumiwa kwa njia mbili. Njia ya kwanza –poinarejelea
    mahali. Kwa njia ya pili –po- huonyesha wakati.

    • Matumizi ya –po- ya mahali
    Kiambishi -po- kikisimamia mahali kinakuwa –o rejeshi iliyotumiwa katika ngeli
    ya PA-M-KU. Kinapotumiwa ndani ya kitenzi kinasimamia maneno “mahali
    ambapo.” Ni kusema kuwa –po- hii inapatikana tunapoondoa “amba” katika
    sentensi.

    Mifano:
    -- Mahali ambapo anaishi ni pazuri: Mahali anapoishi ni pazuri.
    -- Pale (Mahali) ambapo palijengwa panatisha: Pale palipojengwa
    panatisha.
    -- Mahali ambapo tutapanda miti ile ni pale milimani: Mahali tutakapopanda
    miti ile ni pale milimani.
    • Matumizi ya –po- ya wakati
    Kiambishi –po- kikionyesha wakati hutumiwa kwa kuonyesha tendo hutendeka,
    lilitendeka au litatendeka na kufuatwa na jingine.

    Mifano:
    -- Mvua iliponyesha tulikimbia.
    -- Mvua nyingi inaponyesha watu wengi huogopa.

    Tanbihi:
    • Katika wakati ujao kiambishi –po- huenda pamoja na kiambishi –ka-.
    Mifano:
    -- Atakapofika tutampokea vizuri.
    -- Nitakapopewa kazi ya kufundisha nitafundisha ipasavyo.
    • Kuna kiambisi –po- kinachotumiwa pamoja na –si- tukikanusha vitenzi
    vyenye kiambishi ki- na –takapo-.

    Mifano:

    i) Maana ya Barua
    Barua au waraka ni maandishi yaliyopangwa kwa utaratibu na mtiririko maalum
    kwa minajili ya kuwasilisha ujumbe fulani. Barua ni risala au mjumbe mwepesi
    anayemwakilisha mtungaji wake kwa mtu mwingine na kuwasilisha taarifa yake
    kwa mtu huyo.
    Barua huandikwa kwa madhumuni mbalimbali kama kuarifu, kuomba kitu kama
    vile kazi, ruhusa; kuagiza bidhaa, n.k.

    ii) Aina za barua
    -- Barua za kirafiki: ni zile ambazo huandikiwa na mtu au watumbalimbali
    walio na uhusiano wa karibu na anayeandika; k.v. rafiki, mzami, ndugu, n.k.
    -- Barua za mwaliko zenye lengo la kumwalika mtu katika sherehe au
    sikukuu fulani
    -- Barua rasmi/ za kikazi zenye madhumuni ya kazi. Kwa kawaida
    barua rasmi huandikwa kwa makusudi mbalimbali kama vile, kutoa
    taarifa za tukio fulani, kuomba kazi, kuagiza vifaa au vitu, kumwalika
    kiongozi katika shughuli maalumu, kutoa taarifa ya kushindwa kufika
    mkutanoni na kadhalika. Barua hizi zina utaratibu wa kuziandika.

    iii) Sehemu za barua rasmi
    Sehemu za baruwa rasmi zinakaribia kufanana na zile za barua ya kirafiki lakini
    kuna tofauti kidogo. Ifuatayo ni mifano wa mipangilio ya barua za kuomba kazi.

    *Barua ya kuomba kazi kwa mara ya kwanza

    iv) Maelezo
    1. Anwani ya ya mwandishi na tarehe

    Anwani hii huandikwa upande wa juu mkono wa kulia wa barua na chini yake
    kunawekwa tarehe.

    2. Anwani ya mwandikiwa
    Anwani hii inaandikwa upande wa kushoto wa karatasi chini kidogo ya anwani
    ya mwandishi. Katika sehemu hii jina la mwandikiwa haliandikwi isipokuwa cheo
    chake; hata ikiwa mnazoeana kwa kiasi fulani ni lazima kuandika cheo chake.

    3. Kichwa cha habari
    Hili ni kusudi la barua. Kichwa cha habari huwa chini ya anwani ya mwandikiwa.
    Kichwa hicho huandikwa kwa herufi kubwa na kupigiwa mstari chini.

    4. Ujumbe wa barua
    Ujumbe wa barua huandikwa chini ya kichwa cha barua. Katika barua za kikazi
    ni mambo muhimu yanayoandikwa tu. Ujumbe huu unatanguliwa na sentensi
    inayorejerea kwenye kichwa cha habari.
    Tanbihi:
    -- Uandishi wa barua za kikazi unahitaji uangalifu sana na lugha iliyo wazi kwa
    sababu kama kuna matatizo barua hiyo huwa ni shahidi wako na inaweza
    kukuokoa au kukuponza.
    -- Hakuna sehemu ya salamu kwa mwandikiwa katika barua hizi. Mambo
    hayo ya salamu ni ya barua za kirafiki.

    5. Hitimisho la barua
    Hitimisho/Mwisho wa barua huwa ni tamko la heshima la kumalizia barua. Mara
    nyingi mwisho unaotumika katika barua rasmi ni kama vile :
    -- Wako mtiifu,
    -- Wako mwaminifu,
    -- Wako katika ujenzi wa taifa,
    -- Wako katika kazi,
    -- Na kadhalika.

    6. Sahihi na jina la mwandikaji
    Jina la mwandishi huandikwa likifuata sahihi yake. Jina huwekwa chini ya sahihi

    si juu yake.

    TANBIHI:
    Kama barua rasmi inatoka ofisi ikienda nje au inatoka nje ikingia ofisini, kuwa
    sehemu nyingine zinazoweza kuonekana kwenye barua hiyo. Sehemu hizo ni
    kama kumbukumbu namba, kupitia kwa na nakala.

    1. Kumbukumbu namba
    Kumbukumbu namba zinaandikwa mara nyingi kwenye upande wa kushoto wa
    karatasi. Kumbukumbu hii husaidia kurahisisha kutafuta barua katika majalada.
    Kwa hiyo ni muhimu kutaja kumbukumbu namba ya barua unapojibu na kuandika
    barua iliyo na uhusiano nayo. Zaidi ya kumbukumbu namba, barua nyingine
    zinakuwa na namba ya simu chini yake.

    2. Kupitishwa kwa (kwa kifupi: KK)
    Kuna wakati mwandishi wa barua hupitisha barua yake kwa kiongozi mwingine
    kabla ya kuifikisha kwa mwandikiwa. Inapojitokeza haja hiyo, huandika KK
    chini kidogo ya anwani ya mwandikiwa na chini yake cheo cha huyo kiongozi,
    ukitarajia kwamba atatia saini yake kuhakikisha kwamba amekuwa wa kwanza
    kujua maombi yako.
    Kwa mfano, iwapo mwandishi wa barua ameajiriwa na anaandika barua binafsi
    kwa mkuu mwingine wa kazi ili kuomba kazi, kuuliza mambo ya kikazi na kadhalika,
    inambidi apitishe barua hiyo kwa mkuu wake wa kazi mahali anapofanyia kazi.

    3. Nakala mbalimbali
    -- Iwapo kuna watu zaidi ya yule unayempelekea barua ambao unataka
    wapashwe habari ya jambo uliloandika, basi ni lazima kuwatumia nakala
    ya barua hiyo unayoandika. Jambo hilo pia litamjulisha mwandikiwa kuwa
    barua hiyo inasambazwa kwa watu wengi.
    -- Orodha ya watu wanaopelekewa nakala ya barua huonyeshwa upande wa
    kushoto wa karatasi. Kichwa cha nakala hulingana na sahihi ya mwandikaji.

    Jibu maswali yafuatayo:
    1. Barua rasmi huandikwa kwa minajili ipi ?
    2. Barua rasmi hutofautiana vipi na barua ya kirafiki ?

    3. Taja sehemu muhimu ziundazo barua rasmi

    KUH: KUOMBA RUHUSA YA KUPUMZIKA
    Kichwa cha habari cha hapo juu chahusika. Ninaandika barua hii ili kuomba
    ruhusa ya kukosa kuhudhuria masomo yote ya leo.

    Jana sikuweza kuja chuoni kwa sababu niliamka nikijihisi mgonjwa. Mama
    alinipeleka hospitalini ambapo nilipata matibabu. Walipopata vipimo waligundua
    kuwa ninaugua malaria. Nilipata dawa lakini bado sijapata nafuu. Ninaomba
    uniruhusu siku tatu nimalize dawa kisha nikipata nafuu nitarejea shuleni.

    Samahani sana kwa kutosema hili mapema.

    Ninaambatisha na ripoti ya daktari.
    Ninatumai ombi langu litakubaliwa.
    Asante.
    Wako mwaminifu,
    marym

    Mary Mutoni

    Barua rasmi zipo za aina nyingi, lakini zote zinapatikana kulingana na minajili
    yake. Barua hizo zinaweza kuwa:
    -- Barua ya kuomba kazi
    -- Barua ya kutoa taarifa
    -- Barua ya kuomba ruhusa
    -- Barua ya huduma
    -- Barua ya kuomba nafasi katika shule fulani
    -- Barua ya kuomba msamaha
    -- Barua ya shukrani
    -- Barua ya malalamiko
    -- Barua kwa mhariri
    -- Barua ya mapendekezo
    -- Barua ya uteuzi
    -- Barua za kuagiza au kupokea bidhaa/vitu
    -- Barua ya kusimamisha kazi

    -- Barua ya kusimamishwa au kufutwa kazi

    YAH: NAFASI YA MASOMO
    Kichwa cha habari cha hapo juu chahusika. Ninakuandikia barua hii kuomba
    nafasi ya kujiunga na Chuo kikuu cha Rwanda chenye sifa na umaarufu mwaka
    wa masomo ujao.

    Kwa mintarafu ya masomo yangu, mimi nilisoma katika Chuo cha Ualimu cha
    Byumba, wilayani Gicumbi. Nilimaliza masomo yangu mwaka jana na nikafaulu
    vizuri sababu kiasi kwamba nilipewa zawadi na serikali ya kuchagua chuo
    chochote kile nipendacho ili niendeleze masomo yangu.
    Ni matumaini yangu kwamba utanipa fursa ya kusajiliwa ili nithibitishe uwezo na
    ukakamavu wangu.

    Vitambulisho vyangu pamoja na matokeo ya mtihani wa taifa utayasoma kwenye
    stashahada yangu iliyoambatishwa kwenye barua hii.
    Asante sana !
    Wako mwaminifu,
    karemjon
    KAREMERA Joni
    Nakala:
    -- Waziri wa Elimu
    -- Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Elimu
    Jibu maswali yafuatayo:
    1. Ni madhumuni gani yanayoweza kumfanya mtu aandike barua rasmi.
    2. Ni nini tofauti, katika mpangilio, iliyoko baina ya barua ya kuomba ruhusa

    na barua ya kuomba nafasi ya masomo.

    4.5. Kusikiliza na Kuzungumza




    MADA YA 1 UFAHAMU NA UFUPISHOMADA YA 3 UTUNGAJI WA INSHA