MADA YA 4: KISWAHILI NA TEKNOLOJIA
Uwezo mahususi
Kutumia kwa ufasaha msamiati maalum katika uwanja wa teknolojia
Malengo ya Ujifunzaji
-- Kubainisha vyombo vitumiwavyo katika mawasiliano ya kiteknolojia;
-- Kujadili faida na hasara za mawasiiliano ya kiteknolojia;
-- Kutunga barua mbalimbali za mawasiliano ya kiteknolojia kwa kutumia
msamiati maalum
-- Kutunga sentensi sahihi kwa kutumia viambishi vya masharti: -nge- -ngelina-ngali-
KIDOKEZO
Toa maoni yako kuhusu maswali yafuatayo:
1. Ni vyombo vipi vya kiteknolojia vinavyoweza kutumiwa
katika mawasiliano?2. Je, vyombo hivyo vina faida au hasara gani?
SOMO LA 7: MAWASILIANO YA KITEKNOLOJIA
KAZI 1
Tazama kwa makini picha hapa juu. Jadili moja kwa moja matumizi yake.7.1. Kusoma na ufahamu: Tahadhali vijana!
Amina na Simeon ni wanafunzi wa Shule ya Ualimu wilayani Gatsibo.
Wanazungumzia jinsi teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) huweza
kurahisisha mawasiliano na kupotosha akili ya watumiaji wake.
KAZI 2
Maswali ya ufahamu
Chagua jibu sahihi
1. Wahusika wanaozungumziwa ni:
a) Amina na Simeon.
b) Watumiaji wa vyombo vya mawasiliano ya kiteknolojia.
c) Amina, Simeon pamoja na mpenzi wake Amina.d) Hakuna jibu sahihi
2. Amina ameleta simu ya mkononi shuleni kwa sababu ya:
a) kuwasiliana na mpenzi wake aliyeko ugenini.
b) kutupia jicho wakati wa jaribio na mtihani.
c) kupakua maelezo ya somo la Biolojia na Jiografi.
d) burudani kwa mawasiliano na mpenzi wake pamoja na kuitupia jichowakati wa jaribio na mtihani.
3. Amina alipata anwani ya mpenzi wake kupitia:
a) Watisapu.
b) Fesibuku.
c) Tovuti.
d) barua pepe.
4. Mpenzi wake Amina alimpelekea Amina simu ya mkononi kwa ajili ya:
a) kurahisisha mawasiliano kati yao.
b) kuendeleza hali ya teknolojia ya habari na mawasiliano barani Afrika.
c) kumwondolea mpenzi wake aibu.
d) Majibu mengine ni sahihi isipokuwa b.
5. Simu ya mkononi hairuhusiwi shuleni kwani:
a) inaweza kutumiwa katika vitendo tofauti vya upotovu.
b) ni chombo cha bei ghali.
c) inaweza kuleta fujo darasani.
d) husababisha gharama nyingi.
6. Wakati una mabawa maana yake ni:
a) Ningekuwa na mabawa nigeruka mpaka Marekani.
b) Wakati wa jambo kutendeka ni huu.
c) Utakuwa na mabawa lini?d) Majibu yote ni sahihi.
7.2. Matumizi ya msamiati
KAZI 3
Jaza sentensi zifuatazo kwa kutumia msamiati huu: kupekua,
tovuti, kupiga marufuku, kutia aibu, ana kwa ana, kubakwa,
uasherati, barua pepe.
1. Kufeli mtihani wa taifa ni jambo la..........................kwa mwanafunzi
binafsi na kwa wazazi wake.
2. ...............huanzwa na https://www.
3. Watu wengi hu.................picha kwa kutumia Youtube.
4. ......................ni vitendo vya uzinifu, yaani kufanya mapenzi nje ya
ndoa. Vitendo hivyo ni vya........................kwa ajili ya kupigana dhidi ya
ugonjwa wa UKIMWI.
5. .......................ni njia ya kuwasilisha ujumbe kwa mtu aliye mbali au
karibu bila kuangaliana..............................
6. Wakati wa mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi nchini Rwanda
wanawake pamoja na wasichana wengi waliumizwa na vitendo vya.......................
7.3. Sarufi: Matumizi ya kiambishi cha masharti –nge-
KAZI 4
Eleza dhana ya kiambishi –nge- katika sentensi zifuatazo:
i) Ungejua athari ya mienendo mibaya hiyo kwa maisha yako,
usingeendelea kupotoshwa na uongo wa mawasiliano kutoka
mitandao ya intaneti au tovuti mbalimbali.ii) Nisingekuwa na simu ya mkononi, nisingekuwa kama nilivyo leo.
MAELEZO YA KUZINGATIA
Nge hutumika kuonesha uwezekano au majuto, yaani hutumika kuonyesha
kwamba kitendo fulani hakijafanyika na kwa hiyo jambo fulani halijatokea lakini
kuna uwezekano wa kufanya kitendo hicho na jambo hilo litokee.
Mfano:
1. Ningejua umuhimu wa elimu, ningewafundisha watoto wangu.
→ Sentensi hii inaonesha majuto: Sikujua umuhimu wa elimu, kwa hiyo
sikuwafundisha watoto wangu.
2. Ningekuwa na mchumba, angeninunulia simu ya mkononi aina ya Nokia.
→ Sentensi hii inaonyesha uwezekano: Bado sina mchumba wala simu ya
mkononi aina ya Nokia, lakini nikimpata mchumba ataweza kuininunulia.
Tanbihi: Katika hali kanushi nge hutanguliwa na kikanushi –si-
Mfano:
Nisingekuwa na simu ya mkononi, nisingekuwa kama nilivyo leo.
KAZI 5
Eleza ikiwa kiambishi -nge- kinaonyesha uwezekano au majuto.
a) Angefanya bidii, asingeshindwa mtihani wa taifa.
b) Wangewapatia watoto wao maadili, wangefaidika na matokeo mazuri.
c) Tungejua kuwa mvua itanyesha leo, tungeleta miavuli.
d) Mngetimiza wajibu wenu kazini, msingefukuzwa.
7.4. Matumizi ya lugha: Vyombo na njia mbalimbali katika
teknolojia ya habari na mawasiliano
KAZI 6
Zungumzia kuhusu vyombo vinavyotumiwa pamoja na njia za
kuwasilisha ujumbe
MAELEZO YA KUZINGATIA
A. Vyombo vya uwasilishaji wa habari na mawasiliano.
Kuna aina mbalimbali za vyombo ambavyo hutumiwa katika teknolojia ya habari
na mawasiliano kama vile:
• Redio.
• Runinga au televisheni.
• Simu.
• Tarakilishi au kompyuta.
• Posta.
• Satalaiti, n.k.
B. Njia za uwasilishaji wa habari na mawasiliano
• Fesibuku
• Watisapu
• Twita
• Skaipu
• Faksi
• Barua pepe
• Tovuti
• Telegramu• Instagramu
KAZI 7
Husisha ishara zifuatazo na maana yake
7.5. Kusikiliza na Kuzungumza
KAZI 8Igiza mazungumzo kati ya Amina na Simeon.
7.6. Kuandika
KAZI 9Tunga kifungu cha habari chenye aya tatu kuhusu faida za TEHAMA.
SOMO LA 8: MAWASILIANO KWA NJIA YA SIMUYA MKONONI
KAZI 1
Tazama kwa makini mchoro hapo juu. Unadhani watu hawawanashughulikia nini? .
Maswali ya ufahamu
KAZI 2
Chagua jibu sahihi
1. Wahusika wanaozungumza ni:
a) Mkuu wa shule na Mkuu wa masomo.
b) Viongozi wa shule.
c) Fisto, Mkuu wa shule na Angela, Mkuu wa masomo.
d) Majibu yote ni sahihi.
2. Kifungu cha habari kinazungumzia:
a) Mkuu wa shule na Mkuu wa masomo.
b) Kupata hati kutoka tarakilishi kwa ajili ya mkutano.
c) Matumizi ya simu ya mkononi.
d) Kubonyeza vidude kwenye tarakilishi.
3. Angela amepata matatizo ya:
a) Kutomudu matumizi ya kompyuta.
b) Kukatika kwa simu.
c) Kufiuka kwa simu.
d) Mtandao wa simu, kusanidi kicharazio na kielekezi pamoja na kusabidikichapishi.
4. Kabla ya kuzima tarakilishi inatubidi:
a) Kuchapisha nakala.
b) Kuhifadhi mabadiliko.
c) Kusasaisha.d) Kubonyeza vidude.
8.2. Matumizi ya msamiati
KAZI 3
Jaza sentensi zifuatazo kwa kutumia msamiati huu: kubonyeza
vidude, kusasaisha, nakala bayana, kumemeka, kicharazo,
kusanidua, kuamilisha, nakala laini.
1. Hati iliyohifadhiwa katika kompyuta bila kuchapishwa huitwa...................
wakati ambapo nakala iliyochapishwa huitwa...................
2. Zoezi la kwanza kwenye kompyuta ni ...................................
3. Unaweza .............programu matumizi za simu ya mkononi au tarakilishi
wakati ambapo zinaonekana kama siyo muhimu.
4. Ili uweze kuandika kwenye kompyuta ni lazima utumie .........................
....................
5. Baada ya muda mrefu .hati kuhifadhiwa katika kompyuta inatubidi ....
..........................................
6. Simu ya mkononi haiwezi ..................................bila kuchajiwa.
7. Inatubidi ......................kingavirusi katika kompyuta zetu ili kulinda hatizetu dhidi ya virusi.
8.3. Sarufi: Matumizi ya kiambishi cha masharti –ngeli- au–ngali-
KAZI 4
Eleza dhana ya kiambishi –ngeli- au –ngali- katika sentensi
zifuatazo:
-- Ningelikuwa na kingavirusi, ningeliiamilisha katika tarakilishi yako ili
kuepuka uharibifu wa hati.-- Ningalifuata maonyo ya wazazi wangu, nisingalipata cha mtemakuni.
MAELEZO YA KUZINGATIA
Ngeli au ngali mara nyingi hutumiwa katika wakati uliopita kuonesha uwezekano
au majuto, yaani hutumika kuonesha kwamba kitendo fulani hakijafanyika na kwa
hivyo jambo fulani halijatokea lakini kuna uwezekano wa kufanya kitendo hicho
na jambo hilo litokee.
Mfano:
Ningelikuwa na kingavirusi, ningeliiamilisha katika tarakilishi yako ili kuepuka
uharibifu wa hati.
Ningalifuata maonyo ya wazazi wangu, nisingalipata cha mtemakuni.
Tanbihi:
1. Ni kosa la kisarufi kuchanganya ngeli na ngali katika sentensi moja. Ikiwa
kipande cha kwanza kimetumia ngeli, ni lazima ngeli itumiwe pia katika
kipande cha pili n.k
2. Katika hali kanushi ngeli au ngali hutanguliwa na kikanushi –si-Mfano: Ningalifuata maonyo ya wazazi wangu, nisingalipata cha mtemakuni.
KAZI 5
Weka sentensi hizi katika hali yakinishi au kanushi.
a) Nisingelisoma, nisingeliwafundisha watoto wangu.
b) Wangalihifadhi mazingira yao, wangaliishi kwa usalama.
c) Mngeliepuka tabia ya uzinifu, msingeliambukizwa ugonjwa wa ukimwi.d) Ungalishughulikia kazi za ujasiliamali, ungalijiendeleza kiuchumi.
8.4. Matumizi ya lugha: Vyombo na njia mbalimbali katikateknolojia ya habari na mawasiliano.
KAZI 6
Kwa kutegemea mchoro, onyesha vipengele muhimu vyakompyuta au tarakilishi
8.5. Kusikiliza na Kuzungumza
KAZI 7Igiza mazungumzo kati ya Fisto na Angela.
8.6. Kuandika
KAZI 8
Tunga kifungu cha habari chenye aya angalau tatu kuhusu hasaraza TEHAMA.
Tathmini ya mada
I) Taja vyombo angalau vitano vya TEHAMA na kueleza matumizi yake.
II) Chagua jibu sahihi:
1. Ili ujumbe kutoka Fesibuku uwasilishwe ni lazima kuwe na vifaa
vifuatavyo isipokuwa:
a) tarakilishi au simu ya mkononi.
b) mtandao wa intaneti.
c) anwani ya mtumaji na mpokezi wa ujumbe.
d) meza ya kuwekea tarakilishi pamoja na kiti cha kukalia.
2. Mawasiliano kwa njia ya Watisapu huwezekana iwapo kuna:
a) simu ya mkononi iliyounganishwa kwenye mtandao wa intaneti.
b) simu kadi pamoja na chaji.
c) simu ya mkononi pamoja na mtumiaji.
d) simu ya mkononi iliyounganishwa kwenye mtandao wa intaneti pamoja
na mtumiaji.
3. Google ni aina ya:
a) mtandao.
b) tovuti.
c) barua pepe.
d) tarakilishi.
4. Youtube hutumiwa:
a) kupelekea mtu barua pepe.
b) kubonyeza vidude.
c) kupakua picha.
d) kutangaza habari.
5. Kielekezi kazi yake ni:
a) kuonesha nafasi ya kuandikia kwenye tarakilishi.
b) kufuta maandishi.
c) kuchapisha nakala.
d) kusanidua nakala laini.
6. Badilisha sentensi zifuatazo kwa kutumia kiambishi –nge-, -ngeli- au–ngali-.
a) Sikununua chai kwa sababu nilikosa pesa.
b) Nikifanya kwa bidii sitafeli mtihani wa taifa.
c) kama hukujua umuhimu wa kuhifadhi mazingira hukupanda miti karibuna nyumba yako.
MAREJEO
Waititu, F. na Wenzake (2008): Kiswahili Fasaha. Kitabu cha Mwanafunzi.
Kidato cha Tatu. Oxford University Press, East Africa Ltd, Nairobi, Kenya.
TUKI (2004): Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Toleo la Pili. Oxford University Press.
Bakhressa, S.K. na Wenzake (2008): Kiswahili Sanifu. Kitabu cha Mwanafunzi.
Darasa la Saba. Oxford University Press, East Africa Ltd, Elgon Road, Upper
Hill, Nairobi, Kenya.
Nkwera F.M.V. (1978): Sarufi na Fasihi Sekondari na Vyuo. Tanzania Publishing
House, Dar Es Salaam.
HARERIMANA, F. (2017): Tujivunie Lugha Yetu. Kitabu cha Mwanafunzi, Kidato
cha 5. MK Publishers (R) Ltd. Kigali, Rwanda.
Ndalu, A. E. (2016): Masomo ya Kiswahili Sanifu. Kitabu cha Mwanafunzi.
Kidato cha 2. Moran (E.A) Publishers Limited.
Bakhressa, S.K. na Wenzake (2008): Kiswahili Sanifu. Kitabu cha Mwanafunzi.
Darasa la 8. Oxford University Press, East Africa Ltd, Elgon Road, Upper Hill,
Nairobi, Kenya.
Ntawiyanga, S. na Wenzake (2017): Kiswahili kwa Shule za Rwanda. Mchepuo
wa Lugha, Kidato cha 5. Longhorn Publishers (Rwanda) Limited. Kigali, Rwanda.
Kenya Literature Bureau (2006): Kiswahili kwa Darasa la Nane. Kitabu cha
Wanafunzi. Kenya Literature Bureau, Nairobi, Kenya.
Ntawiyanga, S. na Wenzake (2017). Kiswahili kwa Shule za Rwanda. Mchepuo
wa Lugha, Kidato cha 6. Longhorn Publishers (Rwanda) Limited. Kigali, Rwanda.
Niyirora, E. na Ndayambaje, L. (2012): Kiswahili Sanifu kwa Shule za Sekondari.
Kitabu cha Mwanafunzi Kidato cha Tano. Tan Prints (India) Pvt. Ltd.
Massamba, D.P.B. na Wenzake (2009): Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu,
Sekondari na Vyuo. Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam, Tanzania.
Massamba, D.P.B. na Wenzake (2012): Sarufi Maumbo ya Kiswahili Sanifu,
Sekondari na Vyuo. Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam, Tanzania.
Nkwera, F.M.V. (1979): Sarufi na Fasihi, Sekondari na Vyuo.Tanzania PublishingHouse, Dar es Salaam,Tanzania.