• MADA YA 3 :MIDAHALO

    Uwezo mahususi

    Kushiriki vilivyo katika midahalo, kuongoza na kutoa hoja kwa kutetea au

    kupinga mawazo yaliyotolewa.

    • Malengo ya ujifunzaji
    -- Kutoa maana ya mdahalo
    -- Kubainisha sifa za mdahalo mzuri
    -- Kuonesha mbinu au taratibu za mdahalo
    -- Kueleza umuhimu wa mdahalo
    -- Kutaja masuala mtambuka mbalimbali yaliyozungumziwa katika midahalo.
    -- Kueleza maana ya viambishi rejeshi

    -- Kuorodhesha viambishi rejeshi

    KIDOKEZO
    Tazama mchoro ufuatao kisha ujibu maswali yaliyo hapo chini yake
    x

    Maswali

    1. Elezea yale unayoyaona kwenye mchoro

    2. Watu hawa wanafanya nini?

    SOMO LA 5. MAANA YA MDAHALO
    5.1. Kusoma na ufahamu: Utekelezaji wa elimu ya

    kujitegemea kwa vijana
    Soma mdahalo ufuatao wenye mada “ Utekelezaji wa elimu ya
    kujitegemea kwa vijana wa leo ni dhaifu zaidi kuliko ule wa vijana wa
    miaka iliyopita ”, kisha ujibu maswali yaliyotolewa hapo chini.


    Mwenyekiti (anasimama
    ): Waheshimiwa mabibi na mabwana mliokusanyika
    hapa hivi leo, hamjambo? Mada ya mdahalo wetu wa leo ni kama mnavyoiona
    ubaoni ni“Utekelezaji wa elimu ya kujitegemea kwa vijana wa leo ni dhaifu zaidi
    kuliko ile ya vijana wa miaka iliyopita.”

    Mimi jina langu ni Kabatesi, mwenyekiti wa mdahalo. Niko pamoja na Gahizi

    kama katibu wa mdahalo wetu pamoja na Uwase atakayechunga muda. Vilevile
    tuna pande mbili hapa. Timu moja inatetea mada na nyingine inapinga mada.
    Bila ya kuchelewa Napenda kumkaribisha bwana (anataja jina lake) ambaye ni
    msemaji mkuu wa kwanza upande wa utetezi ili atoe hoja zake kuhusu mada
    yetu ( anakaa).

    Msemaji wa 1 (Utetezi):
    Mheshimiwa mwenyekiti na washiriki wote, ni wazi
    kabisa kwamba hali ya elimu ya kujitegemea si dhaifu kwa vijana wa leo kama
    mada isemavyo vijana wa leo wameenda shule, wameanza wakiwa wadogo,
    wameendelea na masomo hadi chuo kikuu na kuhitimu itakiwavyo kiasi kwamba
    wanaweza kufanya kazi katika nyanja mbalimbali zinazohitajika katika harakati za
    kulijenga taifa. Vijana wa leo wana mishahara minono. Mheshimiwa Mwenyekiti,
    waheshimiwa wote mnaoshiriki katika mdahalo huu; haya ni baadhi ya mambo
    mengi yanayoweza kututhibitishia kwamba vijana wa leo hushiriki vizuri katika
    kutekeleza elimu ya kujitegemea.

    Mwenyekiti:
    Naam, wasikilizaji washiriki. Nafikiri baada ya kusikiliza hoja za
    msemaji mkuu

    wa kwanza upande wa utetezi, sasa ningependa kumkaribisha msemaji mkuu

    wa kwanza upande wa upinzani naye atowe hoja zake. Karibu!

    Msemaji wa 1 (Upinzani): Asanteni sana mwenyekiti na wasikilizaji washiriki.
    kwa kunipa fursa hii. Sikubaliani na hoja za mtetezi wa mada hii. Msemaji
    aliyetangulia alisema kwamba vijana wa leo wanaanza kusoma wangali wadogo
    na kufikia viwango vikubwa na kupewa shahada za hali ya juu pamoja na
    mishahara minono kuliko wa miaka iliyopita. Vijana wa miaka iliyopita walikuwa
    na namna yao ya kufanya kazi walikuwa wanajituma na walifanya kazi bila
    usimamizi au unyampala, walikuwa si wavivu, vijana wa leo baadhi yao ni wavivu
    kazi haiwezi kufanyika bila kuwa na mtumishi nyumbani kwao, ambapo vijana wa
    miaka iliyopita walijituma kwa shughuli yoyote ile iliyohitaji ujenzi wa taifa, kama
    kuwinda, kwenda vitani, pia kuliwasidia wale wasiojiweza, n.k Nashukuru sana
    kwa kunisikiliza.

    Mwenyekiti:
    Naam! Mambo yameanza kupamba moto. Baada ya kusikiliza
    hoja za wasemaji wakuu wa kwanza kutoka pande zote mbili ningependa
    kumkaribisha msemaji mkuu wa pili kwa upande wa utetezi ili naye atoe hoja
    zake.

    Msemaji wa 2 (Utetezi)
    : Asante sana mwenyekiti, wenzangu watetezi na
    mahasimu wangu wapinzani pamoja nanyi wasikilizaji-washiriki. Ni wazi kwamba
    utekelezaji wa elimu ya kujitegemea kwa vijana wa leo ni dhaifu zaidi kuliko ile
    ya vijana wa miaka iliyopita. Hili ni kwa sababu vijana wa leo hawawezi kufanya
    kazi bila kulazimishwa. Lakini vijana wa zamani walikuwa wakijituma katika
    kutekelza kazi zote ili kuendeleza nchi. Kazi hizo hasa zilikuwa za kilimo, ujenzi
    na kazi nyingine za mikono. Vijana wa leo wao huogopa kutumia mikono yao. Je
    tutaendeaje? Haviwezekani. Asante sana.

    Mwenyekiti:
    Naam! Wapinzani mmekubali? Au mtashikilia shindano? Msemaji
    wa pili, fursa kwako!

    Msemaji wa 2 (upinzani):
    Asante sana mwenyekiti na nyinyi nyote ambao
    mmekusanyika hapa leo hii. Sisi wapinzani hatukubaliani na maoni ya watetezi
    hata kamwe! Je? Mnasema kuwa vijana wa leo hawafanyi kazi lakini siku hizi
    ndipo unaona kuwa kazi mpya zinabuniwa ilhali hapo zamani mtoto alikuwa
    akifuata kazi ya wazazi wake. Kama wahenga walivyosema “Mtoto wa mhunzi
    asiposana huvukuta”. Vilevile hapo zamani vijana waliokuwa wakitoka shuleni
    walikuwa wakisuburi kazi kutoka kwa serikali. Lakini leo mambo ni kinyume.
    Hatusubiri kazi za ofisini tunabuni nyingine mpya na kuajiri vijana wenzetu. Je
    huo si utekelezaji thabiti wa elimu ya kujitegemea? Asante sana.

    Mwenyekiti:
    Mambo yamekuwa shamrashamra kweli! Lakini ninaona kwamba
    muda hauturuhusu kusonga mbele. Hoja nzuri zimetolewa kwa kila upande
    lakini tunahitaji mshindi wa leo. Kwa hiyo ningependa kumkaribisha katibu
    aje atupigishe kura ili tujuwe mshindi wa leo. (Katibu anasimama na kuomba
    wanaotetea wanyoshe mikono na wanaopinga wafanye hivyo baadaye na
    kuhesabu kura).

    Katibu: Upande wa utetezi umepata kura kumi na tano. Upande wa upinzani
    umepata kura ishirini na moja. Kwa hiyo washindi wa mdahalo wa leo ni upande
    wa upinzani. (Wasikilizaji washiriki wanawapigia makofi.)

    Mwenyekiti
    : Mabibi na mabwana, baada ya matokeo haya sina budi kuwaambia
    kuwa huu ni mwisho wa mdahalo wa leo. Tukutane wakati ujao panapokuwa

    majaliwa ya Mungu.

    KAZI 1

    Maswali ya ufahamu
    1. Andika kichwa cha mada ya hapo juu.
    2. Ni pande gani zinazoonekana katika mdahalo huu?
    3. Eleza hoja za mtetezi wa kwanza katika mdahalo huu.
    4. Eleza jinsi vijana wa miaka iliyopita walivyoweza kujituma.

    5. Kwa sababu gani wapinzani walishinda ?

    5.2. Msamiati kuhusu mdahalo

    KAZI 2

    Unganisha maneno ya safu A na maana yake katika safu B

    kutokana na jinsi yalivyotumika katika kifungu cha habari .

    d

    KAZI 3

    Tunga sentensi zenye maana kamili kwa kutumia maneno
    yafuatayo yaliyotumika katika kifungu cha ufahamu:
    1. Kutetea
    2. Kujituma
    3. Katibu
    4. Mwenyekiti

    5. Kusikiliza

    5.3. Sarufi: Matumizi ya viambishi rejeshi kulingana na

    ngeli za majina

    KAZI 4

    Angalia mifano ya sentensi zifuatazo kisha ueleze viambishi
    vilivyopigiwa mistari.
    1. Mwenyekiti aliyeongoza mdahalo wa jana alikuwa msomi.
    2. Wanafunzi- walimu watakaoshinda vizuri watazawadiwa.
    3. Vijana waliokuwa wakitoka shuleni walikuwa wakisubiri kazi kutoka
    kwa serikali.
    4. Kazi nyingi zilizobuniwa ni za vijana.

    • Viambishi vilivyopigiwa mistari ni virejeshi au viambata.
    Maelezo muhimu kuhusu virejeshi/viambata

    Kirejesh
    i ni kiambishi kinachotiwa katika kitenzi ili kurejerea tendo kwa

    mtendaji. Ni kusema kuwa kirejeshi hujulisha kwamba jina/kiwakilisha
    kilichotajwa ndicho kilichofanya/kinachofanya/hufanya/kitakachofanya au
    kilichofanyiwa’kinachofanyiwa/hufanyiwa/kitakachofanyiwa jambo fulani. Jina/
    kiwakilishi kinachorejelewa hutangulia kitenzi.

    Isipokuwa kwenye ngeli ya A-WA katika umoja mahali ambapo kirejeshi huwa –

    ye mahali pengine kirejesshi ni –o kikabadilika kulingana na ngeli za majina kama

    jedwali lifuatalo linavyoeleza :

    x

    KAZI 5

    Jaza kwa kutumia kirejeshi kilicho mwafaka
    1. Kitabu uli…nipa kimenifurahisha.
    2. Mwendo una…kwenda utakuponza.
    3. Jino daktari ataka…ng’oa ni hili bovu.
    4. Saa ili------tundikwa ukutani imeanguka.

    5. Mwenyekiti ataka…ongoza mdahalo amefika.

    5.4. Matumizi ya Lugha: Maana ya Mdahalo

    KAZI 6

    Soma maelezo muhimu yafuatayo kisha ujibu maswali ya hapo
    chini
    Mdahalo ni majadiliano baina ya watu wengi juu ya jambo moja maalumu.
    Kuna mada inayozungumziwa, wazungumzaji wakuu wanaotetea mada
    (upande wa utetezi) na wazungumzaji wakuu wengine wanaopinga mada
    (upande wa upinzani). Aghalabu huwa wazungumzaji wakuu wawili kwa kila
    upande.

    Mwenyekiti wa mdahalo ana wajibu wa kufungua na kuendesha mdahalo,

    kuwapa wasemaji nafasi ya kuzungumza, kupigisha kura na kufunga mdahalo.

    Katibu wa mdahalo ndiye huandika hoja zinazotolewa na wazungumzaji

    mbalimbali, kufanya na kusoma muhtasari wa hoja zilizotolewa na pande
    mbili mwishoni mwa mdahalo na kutangaza matokeo ya kura zilizopigwa.
    Mdahalo ukifanyiwa darasani, mwalimu atatoa maoni yake juu ya mdahalo.

    Mdahalo mzuri unaonesha namna ya kuchagua mada inayoleta hoja nyingi

    tofauti (mada hii inapaswa kuwa ile inayoleta mchango fulani katika maisha
    ya jamii, uongozi mzuri wa mwenyekiti na umahiri wa wanaozungumza katika
    utafutaji na utoaji wa hoja ndivyo baadhi ya vipengele vinavyochangia katika
    kuboresha mdahalo.

    Jibu maswali yafuatayo:

    1. Ni lipi jukumu la mwenyekiti wa mdahalo?
    2. Katibu ana jukumu lipi katika mdahalo?
    3. Kuna aina ngapi za wazungumzaji katika mdahalo? Zitaje

    4. Ni zipi sifa za mdahalo mzuri?

    5.5. Kusikiliza na Kuzungumza
    KAZI 7
    Andaa mdahalo kisha uwasomee wenzako msimamo wako kuhusu

    mada isemayo:

    «Kazi za ofisini ndizo zinazoendeleza uchumi wa nchi yetu. »

    5.6. Kuandika
    KAZI 8

    Tunga mdahalo kuhusu mada ifuatayo :

    “Usawa wa jinsia ndiyo njia sahihi ya kuendeleza nchi yetu”

    SOMO LA 6: MWONGOZO WA MDAHALO

    v

    KAZI 1
    Tazama mchoro hapo juu kisha ujadili unayoyaona yakitendeka kwenye
    mchoro husika.


    6.1. Kusoma na ufahamu: Tutokomeze dawa za kulevya

    Soma mdahalo ufuatao kisha ujibu maswali ya ufahamu.

    “Wazazi wana wajibu mkubwa katika kutokomeza dawa za kulevya

    zinazoharibu vijana.”
    Mwenyekiti: Waheshimiwa wote mabibi na mabwana mliokusanyika hapa,
    kwanza ninataka niwakaribisheni kwenye mdahalo usemao kuwa “Wazazi wana
    wajibu mkubwa katika kutokomeza dawa ya za kulevya zinazoharibu
    vijana.” Karibuni sana nyote na bila kupoteza muda, ninamkaribisha mshiriki

    upande wa utetezi kutoa mchango wake.

    Msemaji wa 1 (Upande wa utetezi): Ninawashukuru sana viongozi,
    wasikilizaji na washiriki wenzangu. kuniruhusu kuzungumzia mada isemayo
    Wazazi wana wajibu mkubwa katika kutokomeza dawa za kulevya
    zinazoharibu vijana.
    ” Kama inavyojulikana elimu ya kwanza ya mtoto huanzia
    nyumbani. Nyumbani ndipo mtoto anapopata malezi ya msingi ambayo huanzia
    uimarishaji wa msingi wa malezi. Malezi haya ya kwanza ambayo hupatikana
    nyumbani humsaidia na kumuimarisha mtoto katika kufanikiwa katika maisha
    yake. Kwa hiyo wazazi wakitoa malezi bora vijana wataepukana na utumiaji wa
    madawa ya kulevya.

    Mwenyekiti
    : Asante sana kwa mazungumzo mazuri. Kama mlivyosikia, msemaji
    huyu ameeleza kwamba wazazi ndio wenye jukumu la kuwapatia watoto wao
    uimalishaji imara wa elimu ya mtoto kutokana na haya ndio wenye wajibu mkubwa
    katika kutokomeza madawa ya kulevya. Sasa ebu nitoe fursa kwa mshiriki wa
    upande wa upinzani.

    Msemaji wa 1 (Upande wa upinzani)
    : Asante sana kiongozi kwa fursa hii ya
    kuniruhusu kutoa mchango wangu. Kwa maoni yangu, ni kweli kwamba wazazi
    wana nafasi kubwa kwa watoto wao na hasa wale walio wadogo kuanzia
    chekechea . Lakini, kwa wale walio wakubwa kuna matatizo makuu ambayo
    wazazi hawawezi kutilia mkazo kwani watoto hao hawashindi na wazazi wao,
    wengine wako shule za sekondari wengine wanajipangia nyumba zao za kuishi
    wakati wa kusoma shule; kwa hiyo naona jukumu kubwa ni la walimu katika
    kutokomeza madawa ya kulevya yanayoharibu vijana. Hili ni kwa sababu walimu
    ndio wanaoshinda na watoto hao muda mrefu. Kwa hiyo walimu wakiwafuatilia
    karibu wanaweza kuepukana na madawa hayo nao wakatoa mchango wao
    katika kuendeleza nchi.

    Mwenyekiti:
    Ninamshukuru sana mshiriki upande wa upinzani. Ameelezea
    kwamba jukumu

    kubwa katika kutokomeza madawa ya kulevya yanayoharibu vijana ni kazi ya

    walimu ambao huwa na vijana hawa muda wote wa masomo. Hebu, tumsikilize
    pia mshiriki aliyenyosha mkono pale upande wa utetezi .

    Msemaji wa 2 (Upande wa utetezi):
    Ninawashukuru Mheshimiwa
    kiongozi,wasikilizaji na washiriki wenzangu. Watu ambao wako karibu sana
    na watoto ni wazazi wao ambao wana mchango wa kwanza katika malezi ya
    watoto hao. Wazazi huwatunza watoto wao, tangu wanapozaliwa na wakati
    wa kwenda shule unapofika, wao ndio wanapiga hatua ya kwanza kuwapeleka
    shuleni. Wajibu wa kila mzazi ni kupeleka mtoto wake shuleni kwani anapata
    mwenendo mwema utakaomsaidia maishani mwake. Watoto wanapofika
    shuleni, ni vyema wazazi wao wawajibike kufuatilia malezi, nidhamu na matendo
    ya watoto wao kwa kuwashauri, kuwafundisha kuwa na mienendo mizuri.
    Waheshimiwa wasikilizaji, kama mnavyoelewa, bila mchango wa wazazi, vita hivi
    dhihi ya dawa za kulevya vitatushinda. Je mtoto anapokuwa likizoni, atampata
    wapi mwalimu wa kumkanya? Au anapotoka shule jioni na kuelekea nyumbani
    mwalimu atamsindikiza? Tunaposema mzazi hatusemi yule aliyemzaa mtoto tu!
    Hapa tunataka kusema kila mtu mzima anayekutana na mtoto huyu. Akimwona
    katika matendo maovu vizuri amkanye. Wazazi wakifanya haya visa vile vya
    wizi, madawa ya kulevya, utovu wa nidhamu hautakuwepo kwa sababu wazazi
    watakuwa wakiwafuatilia karibu watoto wao. Asante sana kwa kunitega sikio,
    hayo ndiyo maoni yangu.

    Mwenyekiti:
    Baada ya kusikiliza hoja za msemaji mkuu wa pili kwa upande
    wa utetezi, ningependa kumpa fursa msemaji wa pili upande wa upinzani. Karibu
    ndugu!

    Msemaji wa 2 (Upande wa upinzani)
    : Asante sana mwenyekiti kwa kunipa
    fursa hii. Mimi sina mengi ya kusema kwa kuwa msemaji wa kwanza mwenzangu
    amesema mengi. Na ninafikiri kuwa yanatosha. Asante sana.

    Mwenyekiti
    : Naam! Baada ya kusikiliza hoja za wasemaji wakuu wa pande
    zote mbili yaani upande wa utetezi na upande wa upinzani, tutafanya uchaguzi ili
    tuone ni upande upi ambao umeshinda safari hii. Tutapiga kura kwa kunyoosha
    mikono kisha katibu atahesabu kura.

    Katibu
    : Upande wa utetezi umepata kura kumi na tano (aandike 15 ubaoni).
    Upande wa upinzani umepata kura kumi (anaandika 10 ubaoni).
    Mwenyekiti: Mabibi na mabwana, baada ya matokeo haya kura zinaonyesha
    kuwa ushindi katika mdahalo huu umeangukia upande wa utetezi (ukumbi
    uliwapigia makofi washindi na mwalimu wa somo akatoa maoni yake juu ya
    mdahalo huo. na ukawa mwisho wa mdahalo)

    KAZI 2
    Maswali ya ufahamu

    1. Taja mada inayozungumziwa katika mdahalo.
    2. Kuna makundi ya aina ngapi katika mdahalo huu ?
    3. Mtetezi wa pili alieleza kuwa mzazi ni nani ?
    4. Ni upande gani ulioshinda? Kwa sababu gani?
    5. Mdahalo ulimalizika kivipi?

    6.2. Msamiati Kuhusu mdahalo
    KAZI 3
    Tunga sentensi sahihi kwa kutumia maneno yafuatayo:
    -- Wajibu
    -- Kutokomeza
    -- Jukumu
    -- Mienendo
    -- Ukumbi

    6.3. Sarufi: Matumizi ya viambishi rejeshi kulingana na
    ngeli za majina
    .
    KAZI 4
    Chunguza sentensi zifuatazo kisha ueleze mabadiliko
    yanayojitokeza
    1. Mwenyekiti ambaye aliongoza mdahalo wa jana alikuwa msomi.
    2. Mwenyekiti aliyeongoza mdahalo wa jana alikuwa msomi.
    3. Binadamu ambao huishi kwa amani na wenzao pamoja na mazingira
    yao husifika.
    4. Binadamu waishio kwa amani na wenzao pamoja na mazinira yao
    husifika.

    Maelezo muhimu

    Kirejeshi ni kiambishi kinachotiwa katika kitenzi ili kurejerea tendo kwa mtendaji.
    Ni kusema kuwa kirejeshi hujulisha kwamba jina lililotajwa ndilo lililofanya au
    lililofanyiwa jambo fulani.

    Tunapotumia
    amba- haturuhusiwi kutumia kirejeshi hii ni kwa sababu ambainasimama
    sawasawa na kirejeshi. Kwenye vishirikishi vipungufu na kwenye
    kitenzi katika wakati wa mazoea, kirejeshi huja mwishoni.

    Mifano

    1. Mkufunzi ambaye alitufundisha Kiswahili mwaka jana amehama.
    2. Mkufunzi aliyetufundisha Kiswahili mwaka jana amehama.
    3. Mvua ambayo hunyesha kila siku si nzuri.
    4. Mvua inyeshayo kila siku si nzuri.
    5. Ni huku ambako tulikuwa tukizungumzia.
    6. Huku ndiko tulikokuwa tukizungumzia

    KAZI 5
    Ondoa amba- katika sentensi zifuatazo:

    1. Gari ambalo tulisafiria lilikuwa na hitilafu.
    2. Mchuzi ambao tulikunywa ulipikwa kwa ustadi.
    3. Amani ambayo sisi Wanyarwanda tunayo tuyatunze vyema.
    4. Nyumba ambazo tutazijenga ziwe na viwango vya kujengea nyumba.
    5. Mazingira ambayo tunastahili kuishi ndani ni yale yenye hewa safi.

    6.4. Matumizi ya lugha: Mwongozo na utekelezaji wa
    mdahalo
    KAZI 6
    Soma maelezo muhimu hapo chini kisha ujibu maswali yanayofuata:
    Maandalizi ya mdahalo

    a) Kuchagua mada ya kuzungumzia katika mdahalo: uchaguzi huu
    hufanyika kwa kupiga kura.
    b) Kumchagua mwenyekiti wa mdahalo: mwenyekiti huchaguliwa kwa
    kupiga kura na atakayechaguliwa ni yule mwenye uwezo wa kuongoza
    na kuendesha mdahalo.
    c) Kumchagua katibu wa mdahalo: mhusika huyu pia huchaguliwa, yeye
    ana wajibu wa kuandika na kuwasomea hadhira muhtasari na matokeo
    ya mdahalo.
    d) Kumchagua mtunzawakati: huyu ana jukumu la kuchunguza kwamba
    kila mhusika anatumia muda aliopewa katika kutoa hoja zake.
    e) Kupanga wahusika kwa upande wa utetezi na upande wa upinzani
    kama wasemaji wakuu wa pande hizo.
    f) Kupanga namna ya kukaa kwa wahusika wa mdahalo upande wa
    utetezi na upande wa upinzani na wasikilizaji pia. Kitendo hiki huweza
    kufanywa kwa kupanga watetezi na wapinzani kwenye pande mbili
    (upande wa kulia na upande wa kushoto) ambapo watabadilishana
    mawazo kwa urahisi.
    g) Kupanga muda utakaotumiwa na wahusika wa pande hizo mbili.

    • Mambo ya kuzingatia katika utekelezaji wa mdahalo :

    a) Kutumia vizuri muda uliopangwa.
    b) Kuepuka fujo, kelele na usumbufu wowote.
    c) Kutoa sauti inayosikika unaporuhusiwa kutoa hoja yako.
    d) Kutoa maoni kuendana na mada inayozungumziwa.
    e) Kutumia lugha rahisi na yenye adabu au heshima.
    f) Kuheshimu mawazo ya watu wengine wanapoongea
    g) Kuwa na mpangilio mzuri wa mawazo wakati wa kuzungumza
    h) Kukumbuka kuwa mdahalo ni mchezo si pambano.

    Jibu masali yafuatayo:

    1. Mtunzawakati ana jukumu gani?
    2. Mwenyekiti anapaswa kuwa na sifa gani?
    3. Jadili mambo mawili ya kuzingatia katika uandalizi wa mdahalo.

    4. Kwa sababu gani tunasema kuwa mdahalo si pambano?

    6.5. Kusikiliza na Kuzungumza
    KAZI 7
    Chunguza mada ifuatayo kisha utafute hoja za kuitetea na za
    kuipinga hatimaye uwasilishe darasani:

    “Nidhamu ya vijana wa leo ni bora kuliko nidhamu ya vijana wa zamani.”

    6.6. Kuandika
    KAZI 8
    Tunga mdahalo juu ya mada ifuatayo:
    “Madawa za kulevya hazina umuhimu katika maisha ya binadamu.”
    Tathmini ya mada
    1. Toa maana ya mdahalo.
    2. Eleza baadhi ya mambo ya kuzingatia katika utekelezaji wa mdahalo.
    3. Taja sifa za mdahalo mzuri.
    4. Eleza mambo ya kujiepusha katika mdahalo.
    5. Mdahalo huongozwa na nani? Anafanya kazi gani?
    6. Kwa sababu gani tunasema kuwa mdahalo si pambano?
    7. Taja masuala mtambuka yanayopatikana katika midahalo tuliyoona hapo juu.
    8. Jaza nafasi kwa kutumia kirejeshi kilicho mwafaka:

    i) vyakula viandaliwa-----vitafurahisha kila mtu.

    ii) Nguo wazishona ------ ni za bei nafuu.
    iii) Aisifu------ imemnyea.
    iv) Zimwi likujua------- halikuli likakwisha.
    v) Hamna hamna ndi----- mliwamo.

    9. Ondoa amba- katika sentensi zifuatazo:

    i) Mbunge ambaye hutuwakilisha bungeni atatutembelea kesho.
    ii) Kazi ambazo serikali inatuhamasisha kuunda ni zile zinazojenga nchi.
    iii) Vyakula na vinywaji ambavyo sisi hutumia huwa na viwango vya ubora.
    iv) Dawa za kupunguza ukali wa UKIMWI ambazo atapewa zitamsaidia sana.

    v) Umoja ambao sisi Wanyarwanda tunao tuulinde usije ukavunjika tena.

    MADA YA 2: UTUNGAJI WA BARUA RASMIMADA YA 4: KISWAHILI NA TEKNOLOJIA