• MADA YA 2: UTUNGAJI WA BARUA RASMI

    Uwezo mahususi
    Kuandika barua rasmi kwa ufasaha

    Malengo ya Ujifunzaji

    -- Kubainisha sehemu kuu za barua rasmi;
    -- Kutunga barua rasmi kwa ufasaha;
    -- Kutunga sentensi sahihi kwa kutumia kirejeshi – po - .

    SOMO LA 4: TARATIBU ZA KUTUNGA BARUA RASMI 
    KIDOKEZO
    n


    4.1. Kusoma na ufahamu: Barua ya kuomba kazi
    m
    n
    Maswali ya ufahamu
    KAZI 1

    Soma kifungu cha habari hapo juu na ujibu maswali ya ufahamu
    yafuatayo:
    1. Mwandishi wa barua hii ni nani?
    2. Mwandishi huyu anaishi wapi?
    3. Amemwandikia nani?
    4. Nini lengo la barua yake?
    5. Mwandishi amemshawishije mwandikiwa?

    KAZI 2
    Chagua jibu lililo sahihi kuliko mengine

    1. Mwandishi ana tajiriba ya:
    a) Miaka miwili
    b) Cheti cha ualimu
    c) Kuomba kazi
    d) Miaka miwili ya kufundisha katika shule za msingi.

    2. Baadhi ya vitambulisho vilivyoambatishwa kuna:

    a) Ombi la kazi
    b) Cheti cha ualimu pamoja na nakala ya kitambulisho cha uraia
    c) Kitambulisho cha mwajiri wa mwisho
    d) b na c ni sahihi

    3. Mwombaji kazi anaamini kuajiriwa kwa sababu:

    a) alijifunza ualimu.
    b) ana tajiriba ya kutosha katika ualimu na uwezo wa kutumia kompyuta.
    c) ana tajiriba katika ualimu katika shule za msingi pamoja na uwezo wa
    kutumia kompyuta.
    d) ana mbinu nzuri za kutimiza kazi yoyote.

    4. Kweli au uongo/sikweli

    a) Bila shaka Ndizeye ataajiriwa kwenye Shule ya Msingi Mukingi.
    b) Ndizeye ni mwalimu mwerevu sana na mwenye uwezo sana.
    c) Atakapoajiriwa kwenye alipoomba kazi wanafunzi wote watafaulu
    mitahani yao.
    d) Cheti cha ualimu ni kitambulisho pekee kinachofaa kupata ajira ya ualimu.
    e) Kufaulu mitihani kwa wanafunzi hutegemea jinsi mwalimu anavyotumia
    vizuri mbinu shirikishi za ujifunzaji na ufundishaji.

    4.2. Matumizi ya msamiati
    KAZI 3
    Jaza sentensi zifuatazo kwa kutumia msamiati huu: kuhitimu,
    uthibitisho, tarakilishi, kutimiza, feli, nakala

    1. Wanafunzi wanaombwa kufanya bidii ili wasi.............................majaribio
    na mitihani yao.
    2. ...............................ni kifaa cha kiteknolojia kinachorahisisha leo kazi ya
    mawasiliano kwa kupitia njia ya maandishi.
    3. Unapoomba kazi ni lazima kutoa ...................za vyeti na vitambulisho
    vingine muhimu vya..............................
    4. Katika barua yake ya kuomba kazi, Ndizeye aliahidi...........................
    wajibu wake ipasavyo.
    5. Baada ya .......................masomo yake ya ualimu, Ndizeye alipata kazi
    kwenye Shule ya Msingi Mukingi.

    4.3. Sarufi: Matumizi ya kirejeshi – po -
    KAZI 4
    Eleza matumizi ya mofimu yenye wino uliokolea
    i) Mahali tunapoishi ni pasafi.
    ii) Mahali ambapo panapatikana mbu ndipo panapoweza kuhatarisha
    maisha ya binadamu.
    iii) Mahali walipokaa palikuwa na utulivu.
    iv) Mahali wezi hujifichapo hapajulikani.

    MAELEZO MUHIMU

    - Po – ni kiambishi rejeshi cha mahali. Kwa kawaida hujihusisha na majina ya
    ngeli ya PA-M-KU na kutumiwa kama ifuatavyo:
    -- Katikati ya kiambishi nafsi cha kitenzi na mzizi wa kitenzi.
    -- Kwenye mzizi wa amba- na ndi-.
    -- Mwishoni mwa kitenzi.
    Tanbihi: Katika wakati ujao, kirejeshi –po- husababisha kiambishi –ka-.
    Mfano: Utakapofika utanipigia simu.
    Wakati wowote mtakapokata tamaa mtafeli mitihani yenu.

    Mifano mingine:

    i) Mahali nitakapoajiriwa nitafanya bidii.
    ii) Mahali ambapo panapatikana mbu panaweza kuhatarisha maisha ya
    binadamu.
    iii) Nipo tayari kuwasili wakati wowote nitakapohitajika.
    iv) Hapa ndipo patakapopandwa miti kwa ajili ya kuhifadhi mazingira.
    v) Mahali nitakapoajiriwa nitafanya bidii.
    vi) Mahali ambapo panapatikana mbu panaweza kuhatarisha maisha ya
    binadamu.
    vii) Nipo tayari kuwasili wakati wowote nitakapohitajika.
    viii) Hapa ndipo patakapopandwa miti kwa ajili ya kuhifadhi mazingira..,

    KAZI 5
    Unganisaha sentensi zifuatazo kwa kutumia kirejeshi –poi)

    Tunakaaa mahali pengi. Mahali papo ni penye raha.
    ii) Mahali pale panajulikana kama Eldorado. Ni pazuri sana.
    iii) Tulitembelea mahali penye mbugaza wanyama.
    iv) Walijenga nyumba mahali penye harufu nzuri.

    4.4. Matumizi ya lugha: Mwongozo wa kutunga barua
    rasmi

    Maelezo muhimu
    a) Maana ya barua rasmi:
    Barua rasmi au barua za kiofisi ni barua ambazo zinahusu mambo ya kiofisi kama
    vile taarifa za mikutano, kuomba kazi, kuagiza vifaa vya shughuli nyingine rasmi.

    b) Aina za barua rasmi

    Barua rasmi zipo za aina nyingi lakini zinaweza kugawanyika katika makundi au
    mafungu matatu makubwa yafuatayo:
    1. Barua za taarifa
    2. Barua za maombi mbalimbali
    3. Barua za upokeaji vifaa.

    c) Mtindo wa barua rasmi:

    Barua rasmi huandikwa kuelezea ujumbe maalumu, kwa hiyo huhitaji kuandikwa
    kwa uangalifu na umakini wa kutosha. Ni muhimu kuandika jambo husika waziwazi
    na kuepuka maelezo yasiyo muhimu, kama vile salamu na kadhalika. Mwandishi
    analazimika kuandika kwa ufupi na lugha nyepesi. Barua rasmi huwa na sentensi
    chache tena fupi, na ni lazima kufuata taratibu za uandishi, sentensi ziwe kamili.

    d) Lugha ya barua rasmi:

    Tofauti na lugha ya barua ya kirafiki, barua rasmi hutumia lugha fupi
    na mwandishi hulenga mada mara moja bila kuzungukazunguka. Kwa mfano,
    kama minajili yako ni kuomba hela za kulipa karo ya shule kama barua hii ya
    EssayVikings, hutazungukazunguka. Utayataja madhumuni ya barua mara moja.
    Lugha yenyewe huwa nyepesi kuelewa na haina misimu. Unapoandika barua
    ya kirafiki, waweza kutumia misimu ambayo mwandikiwa ataelewa kwa sababu
    ni rafiki yako. Katika barua rasmi, hili halifanyiwi. Mwandikiwa si rafiki yako na
    huenda ikawa humjui. Pia yafaa usome barua yako vizuri kabla ya kuituma ili
    isiwe na makosa ya tahajia au lugha.

    e) Mtindo wa barua rasmi:

    Barua rasmi huandikwa kueleza ujumbe maalumu, kwa hiyo huhitaji kuandikwa
    kwa uangalifu wa umakini wa kutosha. Ni muhimu kuandika jambo husika
    waziwazi na kuepuka maelezo yasiyo muhimu, kama vile salamu na kadhalika.
    Mwandishi analazimika kuandika kwa ufupi na lugha nyepesi. Barua rasmi huwa
    na sentensi chache tena fupi, na lazima kufuata taratibu za uandishi, sentensi
    ziwe kamili.

    f) Lugha ya barua rasmi: Tofauti na lugha ya barua ya kirafiki, barua
    rasmi hutumia lugha fupi na mwandishi hulenga mada mara moja bila
    kuzungukazunguka. Kwa mfano, kama minajili yako ni kuomba hela za
    kulipa karo ya shule kama barua hii ya Essay Vikings, hutazungukazunguka.

    Utayataja madhumuni ya barua mara moja. Lugha yenyewe huwa nyepesi

    kuelewa na haina misimu.

    Unapoandika barua ya kirafiki, unaweza kutumia misimu ambayo mwandikiwa

    ataelewa kwa sababu ni rafiki yako. Katika barua rasmi, hili halifanyiki. Mwandishi
    si rafiki yako na huenda ikawa humjui. Pia, yafaa usome barua yako vizuri kabla
    ya kuituma ili isiwe na makosa ya tahajia au lugha.

    KAZI 6
    Jadili muundo wa barua rasmi

    Muundo wabarua rasmi

    Anwani
    ya mwandishi huandikwa katika barua yake juu, kwenye pembe ya
    upande wa kulia wa karatasi.

    Tarehe
    : hii huandikwa upande wa kulia wa karatasi katika mstari uleule
    wa kumbukumbu namba ya barua kama ipo; tarehe iwe chini ya anwani ya
    mwandishi

    Kumbukumbu namba:
    hii ni namba ambayo huwa kama kitambulisho cha
    barua; mara nyingi huwa na tarakimu pamoja na herufi, kwa mfano: SRB MD 05.

    Anwani ya mwandikiwa
    : hii hutangulia na cheo cha mwandikiwa na huandikwa
    katika mkono wa kushoto, chini ya namba ya kumbukumbu.

    Mwanzo wa barua
    : huandikwa chini ya anwani ya mwandikiwa; mara
    nyingi neno ndugu hutumika kama salamu au mwanzo wa barua.

    Kichwa cha barua
    : Hutangulizwa na maneno kama vile KUHsadkuhusu),
    MINTsadmintarafu). Ni sharti kiachwe kiandikwe kwa herufi kubwa na kipigiwe
    mstari. Kichwa kinapaswa kuwa kifupi na kinachoelezea mada ya barua
    kiukamilifu.

    Barua yenyewe
    : hii huandikwa mambo yote muhimu kuhusu barua yenyewe,
    barua iwe fupi na taarifa muhimu tu.

    Mwisho wa barua
    huwa ni kimalizio cha barua: ni tamko la heshima la kumalizia
    barua; mara nyingi miisho ambayo hutamkwa ni kama vile, “wako mtiifu”, “wako
    katika kazi”, “wako katika kujenga taifa”, “wako mwanachama”.

    Saini au jina la mwandishi: baada ya kimalizio cha barua mwandishi atie
    saini yake, kisha jina lake kwa ukamilifu.

    Cheo cha mwandishi
    : mwisho wa barua, chini ya jina la mwandishi huandikwa
    cheo cha aliyeandika barua; cheo chaweza kuwa ni mwombaji, mwalimu wa
    darasa, mwanafunzi, kiranja mkuu, waziri wa elimu, mjumbe wa tawi, n.k.

    4.5. Kusikiliza na Kuzungumza
    KAZI 7
    Fikiria barua moja rasmi uliyowahi kuisoma na kuizungumzia
    hadharani.

    4.6. Kuandika
    KAZI 8
    Rejelea hapa chini mfano wa barua rasmi. Bainisha makosa ya
    kimuundo na kuyasahihisha.


    12/12/2019.

    GATETE, S.L.P. 2345,                                                                                   PAUL
    SIMU +2507345621876, KIGALI.
    Kumb.Nb 003
    KWA MKURUGENZI MKUU,
    SHAMBA LA MIKAHAWA LA USANASE, S.L.P. 3000,
    RUHANGO.
    Kwa Bi. Ituze,

    MINT: Kuomba Nafasi ya kuwa meneja wa uzalishaji kahawa


    Narejelea tangazo kutoka Gazeti la Mkulima Bora, toleo la siku ya Ijumaa

    tarehe 6, Desemba, 2019, kuhusu kuwepo kwa nafasi niliyotaja hapo juu
    nikiomba nizingatiwe. Mimi ni Mnyarwanda na ninapenda sana kilimo hasa
    cha mikahawa. Kwa miaka zaidi ya kumi, nimekuwa nikijihusisha katika
    kuwahamasisha wanakijiji kuhusu mbinu bora za kuimarisha kilimo cha
    mikahawa. Kwa sasa, kijiji chetu kinaongoza katika uzalishaji wa mikahawa
    mingi yenye thamani ya juu zaidi.
    Nimefanya utafiti kuhusu mbinu za kisasa za kuimarisha uzalishaji wa
    mikahawa na ninatumai kuwa maarifa niliyonayo yatakufaidi katika kukuza
    uzalishaji wa kahawa.

    Natazamia mawasiliano kutoka kwako wakati wowote.

                                                                                          wako mwaminifu,
                                                                                          Paul Gatete.
                                                                                          Saini
    KAZI 9
    Rejelea mfano wa barua rasmi kuhusu ombi la kazi ya hapo juu. Tunga barua

    yako kwa Waziri wa Elimu kwa ajili ya kuomba kuendendelea na masomo
    katika Chuo Kikuu cha Ualimu.

    Tathmini ya mada
    7. Nini maana ya barua rasmi?
    8. Jadili muundo wa barua rasmi.
    9. Zungumzia aina za barua rasmi.
    10. Andika barua rasmi kwa mkuu wa shule kuhusu ombi la maandalizi
    ya mazoezi ya ufundishaji.
    11. Tunga sentensi angalau mbili mbili kwa kila nafasi ya matumizi ya
    kirejeshi –po-, yaani katikati ya kiambishi nafsi cha kitenzi na mzizi
    wa kitenzi, kwenye mzizi wa amba- na ndi – pamoja na mwishoni
    mwa kitenzi.



    MADA YA 1: UANDISHI WA BARUA ZA KIRAFIKI, MWALIKO NA MATANGAZOMADA YA 3 :MIDAHALO