• MADA YA 1 UFAHAMU NA UFUPISHO

    Uwezo mahususi
    Kufupisha matini zenye urefu wowote kulingana na kanuni zinazohusika.

    Malengo ya ujifunzaji:
    -- Kueleza mbinu za kufahamu kifungu cha habari fulani,
    -- Kuonyesha dhamira kuu au kiini cha habari kinachozungumziwa,
    -- Kupanga mawazo muhimu yaliyozungumziwa katika matini,
    -- Kubainisha mbinu au taratibu za ufupisho,
    -- Kubainisha sifa za ufupisho,
    -- Kuonyesha umuhimu wa ufupisho,
    -- Kufupisha matini mbalimbali za Kiswahili kulingana na taratibu au mbinu
    za ufupisho,

    -- Kuambisha maneno ya Kiswahili.



    SOMO LA 1: UFAHAMU
    1.1. Kusoma na Ufahamu: Miti

    Soma kifungu kifuatacho, kisha ujibu maswali yaliyotolewa hapo chini
    Miti ina faida nyingi. Si kwa binadamu tu bali hata kwa wanyama, ndege, wadudu
    na viumbe wa baharini. Kuna miti inayotoa vyakula kwa watu na kwa wanyama.
    Miti hiyo ni kama michungwa, mipapai, milimau, mipea, mikanju, miwa, fito na
    kadhalika. Miti mingine hutupatia vifaa vya kukidhi mahitaji yetu. Vifaa hivyo ni
    kama samani yaani meza, makabati, viti, madawati na vifaa vingine kama vinu,
    michi, mipini ya majembe na mashoka, mivure na kadhalika. Miti hiyo ni kama
    mivule, mikalitusi, misonobari na mikangazi. Baadhi ya miti hutupa dawa za
    kutibu magonjwa mbalimbali.

    Halikadhalika, miti hutupa mvua na kutuepusha na jangwa. Miti pia ni kuni na
    makaa ya kupikia vyakula. Na miti hutumiwa kwa kujengea mapaa ya nyumba.
    Vilevile, miti ni mapambo ya mazingira.

    Kwa kuona faida na umuhimu wa miti, watu duniani walitenga siku maalum,
    kila mwaka, ya kupanda miti. Nchi yetu nayo haikubaki nyuma kama mkia bali
    nayo hushiriki kikamilifu katika shughuli ya upandaji wa miti. Mbali na siku hiyo
    maalum, serikali yetu inahamasisha raia kupanda miti. Jambo hili, hufanyika katika
    misaragambo au katika hafla mbalimbali. Kulingana na jambo hili Wanyarwanda
    wana msemo usemao “Ukikata mmoja (mti), panda miwili.” Isitoshe, serikali ya
    Rwanda ilitunga sheria za kuzuia uharibifu wa misitu. Uharibifu huu unahusiana
    na ukataji wa miti kwa kutafuta kuni, kuchoma makaa na hata kuchoma misitu na
    vichaka kwa utafutaji wa malisho ya mifugo. Ikumbukwe kuwa misitu ni makazi
    ya ndege na wanyama wa porini. Misitu hii ikiharibika kutokana na ukataji wa miti
    ndege na wanyama hawa watakosa vyakula na mahali pa kuishi.

    Miti ikiendelea kukatwa ovyo bila ya kupanda mingine ama misitu ikiendela
    kuharibiwa, mazingira yetu hayatakuwa safi. Nchi yetu Itakosa mvua na hata
    dunia nzima itageuka jangwa. Ni wajibu wetu wa kulinda mazingira kwa kupanda
    miti na kutoikata ovyo ili tusikumbane na madhara yatakayotokana na kuchafuka
    kwa hali ya hewa. Sababu ni kwamba miti ina umuhimu mkubwa katika maisha

    ya hapa duniani.


    1.2. Msamiati kuhusu Kifungu



    1.3. Sarufi: Uambishaji wa Maneno


    Maelezo muhimu kuhusu uambishaji
    Uambishaji ni mbinu ya kuzalisha maneno mapya kutoka maneno mengine. Mbinu
    hii hufanyika kwa kuongeza kwenye sehemu fulani (viini, mizizi au mashina) za
    maneno hayo viambishi mbalimbali mwanzoni au mwishoni. Mbinu hii huitwa
    tena mnyambuliko. Katika sarufi ya lugha ya Kiswahili kuna :
    -- Uambishaji wa vitenzi
    -- Uambishaji wa nomino
    -- Uambishaji wa vielezi

    • Uambishaji wa vitenzi
    Uambishaji wa vitenzi ni uundaji wa vitenzi vipya kutoka maneno mengine. Kuna :
    -- Uambishaji wa vitenzi kutoka vitenzi vingine
    -- Uambishaji wa vitenzi kutoka majina
    -- Uambishaji wa vitenzi kutoka vivumishi

    -- Uambishaji wa vitenzi kutoka vielezi

    i) Uambishi wa vitenzi kutoka vitenzi vingine
    Uundaji huu wa vitenzi vipya hufanyika kwa kuongezea mzizi wa kitenzi viambishi
    tamati vya kauli au vya hali. Ni kusema kuwa tunachukua kitenzi katika kauli ya

    kutenda na kukitia katika kauli nyingine.

    Mifano:



    ii) Uambishaji wa vitenzi kutoka majina
    Uundaji wa vitenzi kutoka majina hufanyika kwa kuongeza kwenye shina la jina
    kiambishi awali ku- na viambishi tamati (viambishi vya kauli na viishio).

    Mifano:



    iii) Uambishaji wa Vitenzi kutoka Vivumishi
    Uundaji wa vitenzi kutoka vivumishi hufanyika kwa kuongezea shina la kivumishi

    kiambishi awali ku- na viambishi tamati (vya kauli na viishio).


    i) Uambishaji wa vitenzi kutoka vielezi
    Uambishaji wa aina hii hufanyika kwa kuongeza kwenye kielezi au sehemu ya

    kielezi kiambishi awali ku- na viambishi tamati (viambishi vya kauli na viishio).


    1.4. Matumizi ya Lugha: Maelezo Muhimu kuhusu Ufahamu


    Ufahamu ni neno ambalo linatokana na kitenzi “kufahamu.” Yaani kujua, kutambua
    na kuelewa unachosoma au unachoambiwa. Ufahamu ni dhana inayolenga
    kujua na kulielewa jambo kwa usahihi ili kuweza kulieleza upya bila kupotosha
    maana yake ya awali. Ufahamu ni somo la kupata mbinu zote za kuelewa mambo
    tunayosikia au tunayosoma.

    Ufahamu unaweza kufanyika kwa kusikiliza yanayosemwa au kwa kusoma
    yaliyoandikwa. Kwa hiyo, kuna aina kadhaa za ufahamu: ufahamu wa kusoma,
    ufahamu wa kusikiliza, ufahamu wa kutazama na kusikiliza (runinga au filamu) na
    ufahamu wa kutazama tu (picha za filamu au video ambazo hazina sauti).

    Tunapozungumza au tunaposoma maandishi fulani ni lazima tuelewe na
    kuelewana. Kuelewa mambo yanayosemwa na mtu mwingine ni hatua ya kwanza.
    Hatua ya pili ni kuweza kupata ukweli wa yale yanayosemwa na kuyakubali au
    kuyakana. Hatua ya tatu ni kujenga uhusiano na uelewano kati ya hao wawili
    wanaozungumza.

    Ili mtu aweze kufahamu anayoambiwa au anayoyasoma, au tunayoyatazama
    kuna mbinu anazopaswa kutumia. Mbinu hizo ni hizi zifuatazo:

    a) Kujua ujumbe wa maandiko mazima au mazungumzo. Hili hufanyika kwa
    kusoma vizuri kwa kuzingatia matumizi ya alama za vituo. Katika mazungumzo
    msikilizaji anapaswa kusikiliza vizuri kwa kuzingatia matamshi ya msemaji.

    b) Kuelewa maana za maneno na misemo tofauti: msomaji au msikilizaji anatakiwa
    kubaini maana ya maneno hayo ili kuelewa vema maana ya maneno aliyoyatumia
    mwandishi au msimuliaji.

    c) Kuchunguza mawazo makuu na yale madogo madogo katika maandiko
    hayo au masimulizi hayo kwa kujenga ujumbe.

    d) Kuelewa utanzu anaousoma au anaousikiliza: Anapokuwa na makini kuhusu
    utanzu anaousoma au anaousikiliza, ndipo msomaji au msikilizaji anaelewa vizuri
    jambo analolisoma au analolisikiliza.

    Ufahamu una umuhimu mkubwa kwa kuwa ni fursa njema ya kupanua msamiati.
    Kutokana na kuwa mwandishi au msemaji hutumia hasa maneno na misemo
    mbalimbali ambayo hutuongezea ujuzi wa lugha.

    Jibu maswali yafuatayo:
    1. Ufahamu ni nini?
    2. Kuna aina gani za ufahamu?
    3. Ni hatua zipi zinazofuatiliwa katika kufahamu?
    4. Taja mbinu za kutumia ili uweze kufahamu unayoyasoma au unayoyasikiliza.

    5. Ni nini umuhimu wa ufahamu?


    SOMO LA 2: UFUPISHO


    2.1. Kusoma na Ufahamu: Hotuba

    Soma hotuba ifuatayo, kisha ujibu maswali yaliyotolewa hapo chini.
    Hotuba: Jifya Moja Haliinjiki Chungu

    Mheshimiwa Mkurugenzi wa Masomo hapa shuleni,
    Mheshimiwa Mkuu wa Nidhamu hapa shuleni,
    Waheshimiwa Walimu,

    Na wanafunzi wote hamjambo?

    Tumekutana sote hivi leo, viongozi, walimu na wanafunzi wa shule yetu
    ya Mwangaza ili tuzungumze kwa kawaida yetu kuhusu mada ya “Ndi
    Umunyarwanda.” Asubuhi hii ningependa tuzungumzie waziwazi juu ya umuhimu
    wa ushirikiano baina yetu sote iwapo tunataka maendeleo mazuri ya shule yetu.
    Wahenga walisema: “Ngozi ivute ingali mbichi”. Tupo mwanzoni mwa mwaka.
    Ndiyo maana nimewaita hapa ili tuanze safari ya mwaka huu. Hii ni safari ndefu
    na ngumu na msafiri ni aliye bandarini.

    Madhumuni ya kuwataka viongozi, walimu na wanafunzi kushirikiana ni kwa
    sababu matokeo mazuri yanategemea ushirikiano wetu sisi sote pamoja. Jifya
    moja haliinjiki chungu. Kitu ambacho ningependa kusisitiza ni kwamba wanafunzi
    wote ni sawa. Wawe wavulana, wawe wasichana. Hatuwezi kusema wanafunzi
    wa aina fulani huzaliwa wajinga na wengine wa aina nyingine huzaliwa werevu.

    Mungu hakupanga hivyo kwani hana moyo wa kupendelea jinsia hii wala kuonea
    jinsia nyingine. Suala tunalokumbana nalo ni hili lifuatalo: «Kwa nini shule fulani
    tu ndizo zenye matokeo na maendeleo mazuri kila kukicha? » Ukaona kuwa
    wanafunzi wao hushinda vizuri, shule ina usafi na mengineyo. Jibu ni kwamba
    wanafunzi wote wa shule hizo huungana pamoja wavulana kwa wasichana.

    Mtanisamehe, leo, hakuna kufichana. Wahenga walisema “Mficha uchi hazai.”
    Tuambiane ukweli ili tuweze kuyatatua matatizo tunayokumbana nayo. Katika
    shule hii unaona kuwa wavulana wameanza kujenga makundi yao na wasichana
    wakajenga yao. Ati hamwezi kusoma pamoja, msichana hawezi kuwa kiranja,
    mvulana hawezi kupiga deki au kufagia na mambo mengine mengi ya utovu wa
    nidhamu. Leo ninawahamasisha walimu kufuatilia karibu mambo hayo ili tuweze
    kwenda pamoja. “Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.” Kazi anayoweza
    mvulana na msichana anaweza kuifanya au mvulana akafanya kazi zinazodhaniwa
    kuwa za kisichana. Mshikamano huu ndio utakaotuwezesha kuwa Wanyarwanda
    kindakindaki.

    Kwa upande wa masomo wanafunzi nawakumbusha kwamba, “Mtaka cha
    uvunguni sharti ainame.” Matokeo mazuri yatatokana na ustahamilivu, jitihada,
    mshikamano na kujitolea. Na wenzenu kutoka shule nyingine ndivyo wafanyavyo.
    “Ukiona vyaelea, vimeundwa.” Shule yetu ina vifaa vya kutosha na walimu wazuri.
    Mimi nina imani kwenu na ninatumaini kwamba mtaweza kwa kuwa uwezo mnao
    na nguvu mnazo. Kuanzia asubuhi hii tupate uamuzi mmoja wa kushikamana
    sote vilivyo na sisi wenyewe tutavuna matunda yatakayotufurahisha. Na shule
    yetu na hata nchi yetu zitazidi kusonga mbele.

    Nawashukuru kwa kunisikiliza na ninadhani kuwa maneno yangu hayajapita sikio

    hadi sikio. Asanteni.

    Kulima ni kitenzi
    • Mkulima, kilimo: nomino zinazotoka kwenye kitenzi kulima.
    • Mtoto ni jina.
    • Kitoto, toto, utoto: ni majina yanayotoka kwenye jina mtoto.
    • Usafi: ni jina linalotoka kwenye kivumishi safi.
    • Kitoto: ni kielezi kinachotoka kwenye jina mtoto.

    Maelezo muhimu kuhusu uambishaji wa maneno
    Katika somo la kwanza tulizungumzia kwa kina uambishaji kama mbinu ya
    kuzalisha maneno mapya kutoka maneno mengine. Mbinu hii hufanyika kwa
    kuongeza kwenye sehemu fulani (viini, mizizi au mashina) za maneno hayo
    viambishi mbalimbali mwanzoni au mwishoni. Katika somo hilo tuliona uambishaji
    wa vitenzi yaani uzalishaji wa vitenzi kutoka maneno mengine.
    Katika somo hili tutaona:
    -- Uambishaji wa majina

    -- Uambishaji wa vielezi

    • Uambishaji wa majina
    Uambishaji wa majina ni uundaji wa majina kutoka maneno mengine. Kuna:
    -- Uambishaji wa majina kutoka majina mengine
    -- Uambishaji wa majina kutoka vitenzi
    -- Uambishaji wa majina kutoka vivumishi
    -- Uambishaji wa majina kutoka vielezi

    i) Uambishaji wa majina kutoka majina mengine
    Uambishaji wa majina kutoka majina mengine hufanyika kwa kuweka katika hali/
    dhana fulani. Hali/dhana hizo ni umoja, wingi, udogo, ukubwa na dhahania.
    Kwa kawaida jina huundwa na sehemu mbili: kiambishi ngeli na shina. Kiambishi
    ngeli ni mofimu inayoonyesha ngeli ya jina. Viambishi ngeli vya majina ni mu-
    (vitu vyenye uhai), wa-, mu- (vitu visivyo na uhai), mi-,ji-/Ø-, ma-, ki-,
    vi-, n-, n-, u-, u-, ku-, pa-, mu-, ku-.

    Mifano:


    TANBIHI: Hakuna majina kwenye ngeli ya mu- na ku-. Kwa hiyo, katika lugha
    ya Kiswahili tunapachika kiambishi –ni nyuma ya majina ya kawaida.
    Mifano:
    -- Mezani kuna usafi.
    -- Chumbani mna usafi.
    a) Hali ya umoja na wingi
    • Katika umoja viambishi ngeli ni mu-, mu-, ji-/Ø-, ki-, n-, u-, u-, ku-,
    pa-, mu-, ku-.

    • Katika wingi viambishi ngeli ni wa-, mi,-ma-, vi-, n-/Ø, ku-, pa-.

    Mifano:


    b) Hali ya udogo (Kudunisha)
    Uundaji wa majina ya hali ya udogo hufanyika kwa kupachika viambishi ki- na

    vi- mbele ya mashina ya majina ya kawaida.


    TANBIHI:
    • Majina yenye mashina ya silabi moja huchukua ji- nyuma ya
    ki- na vi-.
    Mifano:

    Mtu: kijitu- vijitu
    Mto: Kijito- vijito
    • Mashina yanayoanzwa na irabu huchukua ji- nyuma ya ki- na
    vi-.
    Mifano:
    Mwana: Kijana- vijana
    Mume: kijiume- vijiume
    • Majina ya ngeli ya Ki-/Vi- huchukua ji- nyuma ya ki- na vi-.
    Mifano:

    Kitabu: Kijitabu- vijitabu
    Kiboko: kijiboko- vijiboko
    c) Hali ya ukubwa (Kukuza)
    Uundaji wa majina ya hali ya ukubwa hufanyika kwa kupachika viambishi ji-/Øna
    ma- mbele ya mashina ya majina ya kawaida.
    TANBIHI:
    • Kwa majina yenye mashina ya silabi moja ji- hurudi katika
    wingi.

    Mifano:


    • Majina yenye silabi mbili au zaidi huchukua kiambishi Ømbele

    ya shina katika umoja na ma- katika wingi.

    Mifano:


    • Majina ya ngeli ya Li-/Ya- huchukua ji- katika umoja na wingi.

    Mifano:


    • Majina yenye mashina yanayoanzwa na irabu huchukua jikatika

    umoja na ji- hii ikarudi katika wingi.

    Mifano:


    Tahadhari: Wanafuzi wawe makini na matumizi ya dhana za udogo au ukubwa
    katika mawasiliano rasmi. Kwani ukubwa au udogo unaojitokeza hapa mara
    nyingine huwa sio wa kupendeza.

    d) Hali ya dhahania
    Uundaji wa majina ya hali ya dhahania hufanyika kwa kupachika kiambishi umbele
    ya mashina ya majina ya kawaida. Majina haya hayana wingi

    Mifano:



    ii) Uambishaji wa majina kutoka vitenzi
    Uundaji wa majina kutoka vitenzi hufanyika kwa kupachika viambishi ngeli mbele
    ya mizizi au mashina ya vitenzi na viishio nyuma ya mizizi au nyuma ya mashina.
    Viishio vinavyotumiwa ni aji-, u-, e-, i-, o- na a-

    Mifano:
    -- Kufuga: mfugaji, ufugaji
    -- Kutenda: tendo, utendaji
    -- Kusoma: msomi, somo, msomaji
    -- Kufa: kifo, mfu

    -- Kupinda: pindo, upinde


    iii) Uambishaji wa majina kutoka vivumishi
    Uundaji wa majina kutoka vivumishi hufanyika kwa kupachika viambishi ngeli

    mbele ya mashina ya vivumishi.

    Mifano:
    -- safi: usafi
    -- refu: mrefu, urefu
    -- pana: upana
    -- nene: unene, mnene

    -- zuri: uzuri

    iv) Uambishaji wa majina kutoka vielezi
    Uundaji wa majina kutoka vielezi hufanyika kwa kupachika viambishi ngeli mbele
    ya vielezi.
    Mifano:
    -- Sawa: usawa

    -- Mbali: umbali

    • Uambishaji wa vielezi

    Uambishaji wa vielezi ni uzalishaji wa vielezi kutoka maneno mengine. Kuna:
    -- Uambishaji wa vielezi kutoka majina
    -- Uambishaji wa vielezi kutoka vivumishi.

    i) Uambishaji wa vielezi kutoka majina
    Uambishaji wa vielezi kutoka majina hufanyika kwa kupachika kiambishi ki- mbele

    ya shina la jina. Vielezi vinavyoundwa kwa namna hii ni vielezi vya namna.

    Mifano:


    ii) Uambishaji wa vielezi kutoka vivumishi
    Uambishaji wa vielezi kutoka vivumishi hufanyika kwa kupachika viambishi ki- na
    vi- mbele ya shina la kivumishi. Vielezi vinavyoundwa kwa namna hii ni vielezi vya
    namna na vile vya kiasi.

    Mifano:



    Maelezo muhimu: Maana ya ufupisho

    Ufupisho ni taaluma ya kufanya muhtasari wa habari iliyoandikwa au iliyosimuliwa
    bila kupotosha wazo au mawazo ya awali ya msemaji au mwandishi. Ufupisho ni
    hali ya kufanya muhtasari au kupunguza urefu.
    Ili mtu aweze kufanya ufupisho vizuri anapaswa kuzingatia taratibu zifuatazo:
    -- Kusoma habari au kusikiliza habari husika zaidi ya mara moja ili kuweza
    kuielewa.
    -- Ni lazima kuzingatia mawazo makuu na kuyaandika.
    -- Kuchagua au kuteua mambo muhimu au kiini cha habari huku tukijiepusha
    na maelezo ya ziada, mifano, vielezi au tamathali za usemi.
    -- Hakikisha kwamba maneno yote ya maana yaliyokusudiwa na makala au
    habari ya awali yamebaki.
    -- Hakikisha pia kwamba ufupisho wako una urari au mfuatano mzuri wa
    mawazo.
    -- Zingatia urefu wa muhtasari unaohitajika.
    -- Kuandika kwa mtiririko mambo muhimu uliyoyateua.
    -- Usiige lugha ya mwandishi au msimuliaji. Ni kusema kuwa unapaswa
    kutumia maneno yako unapofanya ufupisho.
    Ufupisho mzuri hauna budi kuwa na sifa zifuatazo:
    -- Unapaswa kuwa na mawazo makuu yanayoeleweka.
    -- Unapaswa kuwa si zaidi ya theluthi moja ya kifungu cha habari chote au
    habari uliyosikia.
    -- Lugha inayotumiwa ni lazima iwe lugha fasaha.
    -- Unaweza kuwa katika aya moja au nyingi.
    -- Unapaswa kumwezesha msikilizaji au msomaji kupanua msamiati.

    Jibu maswali haya :
    1. Unadhani ni kwa sababu gani ufupisho hutegemea sana mbinu za
    ufahamu?

    2. Ni nini umuhimu wa ufupisho?




    MADA YA 2 UTUNGAJI WA BARUA RASMI